Kaunga
JF-Expert Member
- Nov 28, 2010
- 12,529
- 13,502
Kama mmoja wa UKAWA nasema hivyo kwa uhakika nikimlinganisha Yakobo jinsi alivyoupata uzaliwa wa kwanza kwa njia 'zisizo haki' lakini mapenzi na mpango wa Mungu ukaendelea kutimilika kupitia yeye. Lowassa kupokwa ushindi ni kama Essau kutapeliwa uzaliwa wa kwanza.
Njia za Mungu hazichunguziki, na tunashukuru kwa ajili ya Magufuli maana anatekeleza yale ambayo ukawa tumekuwa tukiyapigia kelele.
Na hii inazidi kunikumbusha ile sala ya Bwana.....mapenzi yako yatimie; na pia sala ya Yesu kwa Baba yake....kikombe kiniepushe ila si kwa mapenzi yangu...
Go Magufuli, changamoto bado unazo sana na ushakuwa unpopular kwa chama chako.
Njia za Mungu hazichunguziki, na tunashukuru kwa ajili ya Magufuli maana anatekeleza yale ambayo ukawa tumekuwa tukiyapigia kelele.
Na hii inazidi kunikumbusha ile sala ya Bwana.....mapenzi yako yatimie; na pia sala ya Yesu kwa Baba yake....kikombe kiniepushe ila si kwa mapenzi yangu...
Go Magufuli, changamoto bado unazo sana na ushakuwa unpopular kwa chama chako.