The US Presidential Elections-2012

The US Presidential Elections-2012

do not debate on your anniversary day!............leo Obama alionekana ana hasira hasira hivi.......kuna sehemu akasema lets move on to the next part.....that ilionyesha weakness yake........nyingine Obama akampa adui yake silaha ya medicare ya Massachussets......mwenzie akaitumia hiyo hiyo .......kumpa "upper cut"......duuh!

....leo dogo Nyani Ngabu ............ "true substance of life"!!

The game is on.....I know Obama will bounce back i the next debates...........
 
Last edited by a moderator:
THUBUTU!! Mwenyekiti wa MAGAMBA ana "UBAVU" huo? Si atatafuta safari hata kama ni ya msiba kuliko akutane na Kamanda Mbowe?



..toeni majibu bwana sio mnamlinganisha mwanajeshi na mpiga disco yaani DJ,watu wengine vipi bwana, shame on you
 
Wana JF,

Leo alfajiri kulikuwa na mdahalo kati ya wagombea wenye nguvu kubwa katika siasa za Marekani, Mitt Romney wa Chama cha Republican na Barack Obama wa Chama cha Democrat. Mada kuu ilikuwa kuongelea sera zao za ndani ya nchi, hususani katika masuala ya Uchumi, Afya, Elimu, Nishati na Ulinzi. Katika mdahalo huo ulioanza mishale ya saa kumi na dakika tano na kuisha saa kumi na moja kasorobo alfajiri ya kuamkia leo, ni wazi kuwa mgombea urais kwa tiketi ya Republican Gavana Mitt Romney alionyesha kutulia huku akielezea sera za Chama chake kwa ufasaha na kujiamini zaidi na kujibu maswali yaliyoelekezwa kwake kwa weledi wa hali ya juu. Kwa upande mwingine, Rais anayetetea kiti hicho Barack Obama wa Democrat ameonyesha kutomudu vyema mdahalo huo huku akiongea kwa kutojiamini na kushindwa kumudu vyema maswali yaliyoelekezwa kwake kama ambavyo alivyokuwa mzungumzaji mzuri na mahiri wakati wa kampeni za Mwaka 2008. Kwa mdahalo huu wa leo, naamini hata kiwango cha kukubalika cha Mitt Romney kitaongezeka na hivyo kumpa wakati mgumu sana mtetezi wa kiti hicho Barack Obama.


Nini maoni yenu wadau?
 
Nasi hapa bongo tuandae mdahalo kati ya NAPE na MNYIKA
 
Nashauri iwe Mukama na Dr Slaa..makatibu wakuu wa vyama..
 
Hii ni kutokana na umakini wa wenzetu kuchagua candidate wenye uwezo mkubwa. Huwa hakuna uchaguzi rahisi Marekani, na watu wao huwa wanafatilia sana midahalo ili kuwapima watu watakaowapa ridhaa yao. Sisi huku bado tumejikita kwenye Fulana, Kanga, Kofia na ubwabwa. Kweli tuna safari ndefu sana bado.
 
Hapa kwetu tuandae mdahalo wa namna ya kutumia RASILI MALI ZETU KWA FAIDA YA UMMA kati ya CCM Vs CHADEMA
 
Uzi huu upo jukwaa la kimataifa,na umeandika muda wa uongo wa kumaliza mdahalo.nikweli Romney kafanya vizuri
 
Here we go!
obama-vs-romney-debate.jpg 😛oa
 
Laana ya kuunga mkono ushoga inamwandama. Aliniboa sana katika hili. Sikutegemea kauli kama ile itoke kwa mtu mweusi tena mwenye asili ya Afrika Mashariki kama yeye.
 
Wana JF,

Leo alfajiri kulikuwa na mdahalo kati ya wagombea wenye nguvu kubwa katika siasa za Marekani, Mitt Romney wa Chama cha Republican na Barack Obama wa Chama cha Democrat. Mada kuu ilikuwa kuongelea sera zao za ndani ya nchi, hususani katika masuala ya Uchumi, Afya, Elimu, Nishati na Ulinzi. Katika mdahalo huo ulioanza mishale ya saa kumi na dakika tano na kuisha saa kumi na moja kasorobo alfajiri ya kuamkia leo, ni wazi kuwa mgombea urais kwa tiketi ya Republican Gavana Mitt Romney alionyesha kutulia huku akielezea sera za Chama chake kwa ufasaha na kujiamini zaidi na kujibu maswali yaliyoelekezwa kwake kwa weledi wa hali ya juu. Kwa upande mwingine, Rais anayetetea kiti hicho Barack Obama wa Democrat ameonyesha kutomudu vyema mdahalo huo huku akiongea kwa kutojiamini na kushindwa kumudu vyema maswali yaliyoelekezwa kwake kama ambavyo alivyokuwa mzungumzaji mzuri na mahiri wakati wa kampeni za Mwaka 2008. Kwa mdahalo huu wa leo, naamini hata kiwango cha kukubalika cha Mitt Romney kitaongezeka na hivyo kumpa wakati mgumu sana mtetezi wa kiti hicho Barack Obama.


Nini maoni yenu wadau?
Mkuu nakushauri pia ufuatilie na wachambuzi wa kimataifa wanasemaje kuhusu huo mdahalo.
wachambuzi wengi wanasema Obama alimudu vema kuliko mpinzani wake.
Na mpaka sasa kwa mdahalo ule Obama ana 48% na Romney ana 46%
sasa nani hapo amegalagazwa?
 
Mkuu nakushauri pia ufuatilie na wachambuzi wa kimataifa wanasemaje kuhusu huo mdahalo.
wachambuzi wengi wanasema Obama alimudu vema kuliko mpinzani wake.
Na mpaka sasa kwa mdahalo ule Obama ana 48% na Romney ana 46%
sasa nani hapo amegalagazwa?

Sasa sisi tusiojua kidhungu tumwamini nani? Mara Romney mara obama,kwa mama naomba Obama ashindwe mpaka kwenye uchaguzi,sizipendi sera zake kabisa hasa kwa africa na mashariki ya kati
 
Mkuu nakushauri pia ufuatilie na wachambuzi wa kimataifa wanasemaje kuhusu huo mdahalo.
wachambuzi wengi wanasema Obama alimudu vema kuliko mpinzani wake.
Na mpaka sasa kwa mdahalo ule Obama ana 48% na Romney ana 46%
sasa nani hapo amegalagazwa?
Ndibalema, wachambuzi wa kimataifa na sisi wa kitaifa wote tuna haki ya kutoa maoni. Ndiyo maana glasi iliyojaa maji nusu kwa mwingine anaweza kusema iko nusu tupu! Maoni ni maoni tu, lakini hata hivyo kwa maoni yangu Romney alifanya vizuri zaidi. Wachambuzi wa BBC World News nao wanalitambua hilo. Wewe je?
 
Back
Top Bottom