The Second Door (Tamthilia)

The Second Door (Tamthilia)

Ipigie kura simuizi hii

  • Nzuri Sana

    Votes: 9 56.3%
  • Inafaa Kusomwa

    Votes: 5 31.3%
  • Yakawaida

    Votes: 0 0.0%
  • Sijaisoma

    Votes: 2 12.5%

  • Total voters
    16
Me najitolea kuwa mhamasishaji wa kuchangia hadithi hii.....Kama unajijua unapita hapa kujiburudisha iwe live au Kimya Kimya plssssss weka chochote kwenye mamba tajwa. Kumbukeni mhusika anatumia muda na akili kuhakikisha tunaburudika

Kwa kuwa umeamua kujitolea kuhamasisha, unaonaje nikipitishia mchango kwako
Weka namba yako hapa basi tukutumie:eyebrows::eyebrows:
 
Mchango mchango mchango,..... Jamii Forum weka namba tena ya mpesa na tigo pesa. Usiendelee na sehemu nyingine km hakuna kilichoingia kwenye namba
 
Last edited by a moderator:
The Second Door- Episode 11

SmartPress ndio shoo iliyopo hewani hivi sasa, kwa udhamini wa kam…. Oops! Sory nimejichanganya hii ni The second Door Tamthilia inayoelezea mkasa wa kuburudisha, kuelimisha na wakati mwingine kusikitisha kabisa huku mkasa huu wa kipekee ukikuacha na mafunzo mbalimbali katika maisha yetu ya kawaida. Msamiati ndio mwandishi ninaekuletea simulizi hii uipendayo na kwa namna ya kipekee kabisa nikukaribishe katika episode no 11 ya simulizi hii.
Kabla hatujaendelea, kwa dhati kabisa naomba niwatake radhi sana kwa mistake nyingi za uchanganyaji majina zilizokuwa zimejitokeza katika episode iliyopita, lilikuwa ni tatizo lililotokana na kuandika episode ndefu, hivyo ikapelekea nikashindwa kufanya uhariri kwa makini.

Tunaendelea… katika episode ya 10 tuliishia kwa kumuona Robi akishindwa kuwahadaa wale maafisa wa gereza ambalo amefungwa Tarick, kisha aliamua kuondoka na kurudi nyumbani. Leo asubuhi na mapema, Roby akiwa anamalizia kujiandaa kwa ajili ya kuendelea na pilika pilika za kutwa nzima, Roby anapoke simu kutoka hospitali alipokuwa amelazwa Brenda na kuambiwa kulikuwa na taarifa za mgonjwa wake hivyo anaombwa afike hapo mapema. Taarifa hizi zinamshtua kidogo roby akidhani kuwa pengine hali ya Brenda inaweza kuwa imebadilika ghafla au inawezekana amepoteza maisha. Asubuhi hiyo licha ya Roby kupata taarifa za hospitali, Roby anaamua kuziweka kando na kuwahi gerezani ambako leo amedhamiria kumfikia Tarick mapema kabisa hata kabla wafungwa wanaokwenda mahakamani hawajachukuliwa. Roby anatoka nyumbani kwake mapema kabisa akiwa amewahi moja kwa moja kuelekea Gerezani.

Ndani ya siku hiyo, familia ya Brenda inakubaliana kuwa Dada yake aende akakae nyumbani kwa Brenda kwaajili ya usalama wakati wakisubiria siku tano walizokuwa wameahidiwa na Rweyemamu zikamilike. Ikiwa ni siku moja tu tangu atoke kumuona mwanae, mama yake na Tarick anashtushwa na kitendo cha kutokumuona Frank kwa siku mbili sasa, anapata hofu zaidi akifikiria kuwa zimesalia siku 2 tu kabla ya siku kumi ambazo raisi alikuwa amesitisha shughuli zote za magereza. Mama anaumiza kichwa na kuwaza kuwa ni kitu gani anaweza kufanya, ilia pate picha kamili ya maendeleo ya kesi ya kipenzi chake Tarick. Ni kweli kwamba, kutokana na Frank kuwa alimuhakikishia mama huyu kila kitu kitakwenda sawa ingebidi atulie na kusubili matokeo, lakini uchungu wa mwana aujuae mzazi, mbali na matumaini na imani kubwa aliyokuwa nayo juu ya Frank, kimuhemuhe alichokuwa nacho mama huyu hakikuwa cha kawaida.

Gerezani alipofungwa Tarick, Huku maafisa wa zamu gerezani hapo wakiwa wanaendelea kuweka weka mazingira ya ofisi zao vizuri mara anaingia mchungaji, wote wanamshangaa kwani walikuwa hawamjui na haikuwa kawaida ya mchungaji kufika hapo mida kama hiyo, ilikuwa tayari imefikia saa tatu kamili. Maafisa wanaompokea mchungaji huyo wanamsalimia kwa heshima na nidhamu ya hali ya juu, kisha mmoja wao anamuuliza, "Ndio Baba mchungaji, Naomba nikusikilize tafadhali..", mchungaji yule anajibu kwa sauti ya ukalimu,"Nimempokea mwenzangu leo kuja kufanya maombi kwasababu hali yake ya kiafya sio nzuri" wote wanapatwa na mshtuko na kutazamana. Mpendwa rafiki, Mchungaji huyu wa dharura alikuwa ni Roby, na ameamua kutumia mbinu hii ili kuona kama anaweza kufikisha ujumbe kwa Tariki kabla hajaja kuchukuliwa. Lakini mbinu hii ya Tariki ilikuwa ya kukurupuka kwani hakuwa akijua hata taarifa moja kuhusiana na Mchungaji aliekuwa akienda pale gerezani kufanya maombi.

Upande wa pili, Mh Profesa Rweyemamu, baada ya kutoa ahadi ya kumpata Brenda akiwa hai, huku akiwa na malengo ya kujisafishia nyota kwa wakwe, lakini pia akiwa na nia ya dhati ya kutaka kulitia mikononi tunda na kipenzi cha moyo wake Brenda, safari hii anaamua kutumia jitihada binafsi bila kuwashirikisha wafanyakazi wake ambao alikuwa akiwatumia kila siku, wala kushirikisha polisi. Rweyemamu anaingia makubaliano ya kuidhamini kampuni ya ulinzi, ili iweze kuwasaka na walio muweka Brenda mafichoni na kumrudisha msichana huyo mikononi mwake akiwa mzima. Kampuni hiyo iliyokuwa imesajiliwa kama kampuni ya ulinzi ilikuwa ikimilikiwa na afisa mstaafu wa jeshi la kujenga taifa. Rweyemamu akiwa kwenye mazungumzo, licha ya kuzungumza mengi na viongozi wa juu wa hiyo kampuni, hakusahau kuwaeleza juu ya mtu anaemchezesha kindumbwendumbwe, akiwa anaelezea hayo anasema, "Nina nguvu kubwa sana kwenye jeshi zima la polisi, ila nimeamua kutumia kampuni binafsi kumtafuta huyu binti kwasababu kubwa moja, mtu aliemuweka kizuizini sio mtu wa kawaida", akiwa anazungumza maneno hayo huku viongozi hao wakimsikiliza kwa makini anaendelea kwa kusema, "Yupo imara sana, na kwa jitihada nilizozifanya kwa kutumia jeshi la polisi, ingekuwa tayari nimesha mtia mikononi ila……mmm mmm mmm huyo mtu ni hatari" Rweyemamu anaongea maneno hayo kwa msisitizo mkubwa lakini viongozi wa kampuni hiyo wakionesha kutojali hata kidogo wanasema, "Proffesa, ndani ya kampuni yetu tumejipanga kuliko kawaida, tunaweza kupambana na uhalifu wa aina yoyote ile, Hata kama huyo jamaa anaweza kupigana kama marehemu bruce, tuna kikosi maalimu kinaitwa Blockline Ninjas kikiongozwa na Don-Ju ninja wa kikorea, moto wa kuotea mbali yaani hakuna kinachoshindikana". Kusikia maneno hayo Rweyemamu anatikisa kichwa na kuongea taratibu akisema, "Sikumaanisha hivyo, Huyo mtu hajui hata ngumi inavyokunjwa…" kabla Rweyemamu hajaendelea mmoja anamkatisha na kumuuliza, "Kumbe kitu gani cha kumuhofia!?" Rweyemamu anajibu swali hilo haraka haraka kwa kusema, "Anafikiria kama Computer! Na amini usiamini wakati mwingine anatumia uchawi, ninauhakika kabisa atakuwa anatumia ushirikina, unapo mtaiti kabisa ili umkamate anaweza kuporonyokea hata kwenye ukuta". Bila kujua kuwa Frank Tayari alikuwa ameshaaga dunia Rweyemamu anaendelea kuwatahadharisha viongozi wa kampuni hiyo juu yake.

Mpenzi msomaji, katika hatua nyingine Rweyemamu anaendeleza mfululizo wa makosa kwani sasa anajiandaa kutumia nguvu kubwa zaidi akidhani anaenda kupambana na Frank, kumbe Brenda alikuwa mikononi mwa dokta Roby.

Dokta Roby akiwa pale gerezani Maafisa wote wanapigwa na butwaa kusikia kuwa amekaimu nafasi ya mchungaji aliekuwa akifika gerezani hapo kwa ajili ya kuombea wafungwa. Dokta Roby bila ya kujua kuwa, mchungaji huyo alikuwa akifika hapo sikumbili tu za week ambazo zilikuwa ni jumatatu na alhamisi yeye aliendelea kuwaondoa hofu wale askari kwa kusema, "Hakuna shida… kwasababu nimejiandaa kufanya sala kwa wafungwa wawili watatu tu…". Kauli, vitendo na maneno ya dokta Roby hatimae vinawafanya askari washindwe kabisa kumwamini, hivyo ili kuondoa ghasia askari mmoja anamwambia kama dharura kama hiyo imetokea basi ni vyema makao makuu ya kanisa waandike Barua kwa mkuu wa gereza, kwaajili ya kutoa taarifa. Kichwa kinamgonga dokta Roby akijuta kukosa maarifa ya kumfikishia Tarick ule ujumbe. Akiwa hana jinsi anawaaga na kuanza kutoka eneo hilo, mara anamsikia askari mmoja akisema, "Bonge kaondoka na gari iliyopeleka wafungwa mahakamani kisutu, nimemuagiza atakuja na karatasi zingine…." Maneno hayo yanamstua Roby, anaganda kidogo huku akiwaza. Kumbe Roby hakujua kuwa gari inayochukuwa wafungwa huwa inafika hapo saa 2 kamili. Na ndani ya muda huo Tayari ilikuwa imefika hapo na kuondoka. Baada ya kugundua hilo Roby anajipiga kichwa kwa hasira, anawaza mpaka anafikiria kuwa afadhari Frank andekuwepo muda huu tayari angekuwa ametoa wazo nini cha kufanya, anajidharau na kujiona mjinga.

Dokta Roby anakosa cha kufanya ila kabla hajaamua kukata tamaa kabisa anaamua kwenda kumalizia kazi yake mahakamani kujaribu kufatilia ni nani waliemchukuwa kwa jina ambalo Frank alikuwa amelibadilisha taarifa na za Tariki. Roby anaondoka na kuelekea moja kwa moja Kwenye mahakama ya kisutu, anafika eneo na kuamua kukaa kwa nje kidogo ilifikirie nini alitakiwa kuuliza au kusema mahakamani hapo. Akiwa hapo nje, kutoka ndani Roby anamsikia Hakimu ndani ya mahakama akisema. "Baada ya Mahakama kusikiliza ushahidi uliotolewa na wananchi mbali mbali, mahakama hii imejiridhisha na kukukuta na mashitaka sugu ya wizi wa mifugo midogo midogo ya majumbani, hususan ni kuku na Bata. Hivyo kwanza mahakama hii inakupa Ndugu Lucas Shehiza onyo la kuacha tabia hiyo mara moja, pia inakupa adhabu ya kifungo cha miezi sita jela au fine ya kiasi cha shilingi laki tano". Jina la Lucas Shehiza linalotajwa kwenye hukumu hiyo linamfanya Roby asimame na kuingia ndani yajengo la mahakama.

Ndani ya kipindi hicho, proffesa Rweyemamu alikuwa amefika gerezani kwaajili ya shughuli za kikazi, kama kawaida yake anaamua kwenda kumdhihaki adui yake Tarick. Kufika katika Eneo alilokuwa amefungwa Tarick, Rweyemamu anashtuka kuona eneo hilo halina mtu, anaita askari aliekuwa karibu yake na kumuuliza, "Kaamishiwa wapi huyu!? " yule askari anajibu kwa nidhamu, "Ni siku yake ya mahakamani mheshimiwa, amechukuliwa asubuhi". Rweyemamu ana uliza kwa mshangao, "What!". Rweyemamu anakimbia mpaka ofisi kubwa ya utawala, anafika na kuwauliza, "mfungwa wa chemba no 216 yupo wapi" dada mmoja anatizama kwenye computer na kujibu, "ni siku ya kesi yake leo amechukuliwa na watu wa mahakama." Reyemamu anakunja mdomo kwa hasira na kusema, "Acheni upumbavu, chumba namba 216, ni Tarick abdul Gaidi aliehukumiwa kifo, mmempeleka kusikiliza kesi gani?", Askari mwingine wa kiume anajibu, "Samahani mheshimiwa, chumba namba 216 hakuwa Tarick Abdul bali ni Lucas Shehiza" Rweyemamu anasogea kwa kasi mbele ya ile kompyuta na kuoneshwa jina na picha, Rweyemamu anakuna kichwa kwa hasira na kusema, "Nani kaliweka hili jina hapa? Mwenye hii picha ni Tarick Abdull !, nani kaweka hili jina la Lucas Hapa!? Mnacheza na Dolla!?" yule kaka anajibu na kusema, "Mheshimiwa… Database ya Profile za wafungwa inasimamiwa na Wizara sisi hatuna access kabisa wala uwezo wa kufanya mabadiliko yoyote". Frank anaganda ghafla na kuduwaa, kisha anasema taratibu kwa sauti ya upole na utulivu, "Toa taarifa wamzuie huyo mtu sasa hivi wasithubutu hata kumshusha kwenye gari". Rweyemamu anawaacha wale maafisa magereza wakihaha kupiga simu ili kutoa taarifa za kumzuia Tarick, Kisha yeye anaondoka kwa kasi kuelekea mahakamani ili kuwahi isije ikafanyika mistake Tarick akaachiwa au akawatoroka.

Roby nae pale mahakamani baada ya kuingia ndani anagundua kuwa yule aliekuwa akisomewa hukumu alikuwa ni Tarick. Mpenzi msomaji hapa mpango wa marehemu Frank ulikuwa umefanikiwa kwa asilimia mia moja. Kwani timu ya askari iliyokuwa ikizungukia magereza na kuchukua wafungwa wa kuwapeleka mahakamani ilifika pale gerezani na kumchukua Tariki kwa kufananisha picha yake na namba ya kizimba alichokuwa amefungwa. Mara ya kwanza wakiwa ndio wanaenda kumtoa gerezani Tarick alijua kuwa safari ya kuelekea isanga Dodoma ndio ilikuwa imewadia, lakini kitendo cha kushushwa Kisutu Tarick aliona ni mauzauza tu na hakuwa na nafasi ya kuzungumza chochote mpaka anasomewa hukumu ya wizi wa kuku. Kitendo cha hakimu kuuliza tu kama kuna ndugu yake yoyote atakae mlipia fine, Roby anajitokeza, kisha anaongozana na askari kwenye ofisi za Mahakama kwa ajili ya kufanya malipo ya fine hiyo. Muda wote huu Tarick alikuwa akiduwaa bila kuzungumza chochote, huku akiwa haelewi wala haamini kinachoendelea, anakuwa kama simu iliyopoteza network, nimtu ambae anahisi yupo ndotoni ndani ya gereza. Inamchukua dk 7 tu Roby kufanya malipo yote, kisha bila kuchelewa anampakia Tarick kwenye gari na kupotea nae maeneo hayo.

Wakiwa njiani, Roby anamwambia Tarick, "Pole Tarick… Hawatakuona tena", Tarick anajibu, "Ahsante nashukuru… Lakini.. wewe ni nani!? Na nini kinaendelea!?" Roby akiwa anaendesha gari kwa kasi anasema, "Utafahamu kila kitu tufike nyumbani" tariki anasema, "Naomba nipeleke kwa mama yangu, anione kama nipo nje ya gereza" Roby anamwambia tarick, "Sio salama, na pamoja kuwa uponje ya gereza haupo huru". Huku wakiendelea kuzungumza maneno yasiyokuwa na uelekeo maalum wanajikuta wamefika nyumbani kwa Roby. Roby anamuandalia maji Tarick na kumwambia akaoge kisha abadilishe nguo. Tariki anaoga vizuri kisha dokta Roby anaanza kushughulikia majeraha na maumivu mbali mbali aliyokuwa nayo, huku akisema, "Tarik karibu sana jisikie upo nyumbani", Tarick anaitikia, "Inshallah, Wewe ni nani na imekuwaje mpaka mimi niko hapa!" Roby anajibu, "Ndugu yako Frank ndie aliyekusaidia" Tarick kusikia kauli hiyo anamkatisha Roby na kuuliza,"Yupo wapi Frank!?" Roby anasita kidogo na kuonesha kuwa hakutarajia swali kama hilo, kisha anajibu, "Utamuona… Pole sana mwili wako unaonesha umeteseka. Na hivi…. ni nini kinachoendelea kati yako na Brenda?" Frank anajibu swali hilo kwa kusema, "Ni mwanamke shetani sana, yeye ndie iliefanya mipango yote mpaka mimi kutiwa hatiani na kuhukumiwa, Ni msichana ambae alijifanya ananipenda sana, siku zote nilimkatalia kabisa kuwa na mahusiano nae kwasababu nilikuwa nikifahamu uhusiano wake na Mheshimiwa mmoja hivi.., baadae alinipa tenda ya kuwa mpiga picha wake kwenye shughuli zake za uwanamitindo akajenga mahusiano ya karibu sana na mimi, na mipango yake ilipotimia akaniomba nimsindikize Arusha huko ndiko wakanibambika hiyo kesi". Roby anasema, "Pole sana Tarick. Mungu amesaidia umefanikiwa kutoka, Sasa kimebaki kibarua kimoja cha kufanya wasikuone tena. Frank aliniambia nikusaidie kutoroka kabisa nje ya Tanzania ili usikamatwe, ninajamaa zangu wapo Botswana nimezungumza nao itabidi keshokutwa tufanye mpango wa safari ukafanye maisha yako huko".
Kule Mahakamani Baada ya Rweyemamu kufika na kukuta Tarick akiwa ameachiwa na mahakama kwa fine ya laki tano. Bila kuchelewa Rweyemamu anatoa taarifa kwa viongozi wote wa vyombo vya ulinzi na usalama, na taarifa hizo zinamfikia mpaka waziri wa ulinzi. Maramoja waziri huyo anaitisha kikao dharura kitakacho jumuisha viongozi wote wa taasisi za ulinzi na usalama.
Roby baada kumpa huduma ya kwanza Tarick na kumuacha huku akimwambia asijaribu kutoka kabisa hata iweje. Roby anatoka nyumbani kwake kukimbilia hospitali, ili akafahamu nini kilichokuwa kimejiri juu ya hali ya Brenda. Anafika mpaka hospitali lakini kwa bahati nzuri kunakuwa hakuna taarifa mpya ila madaktari waliokuwa wakimshughulikia Brenda wanamwambia kuwa ubongo wa Brenda ulikuwa na mabaki ya kemikali za sumu, ambazo kwa teknolojia yetu hatuwezi kuzisafisha hivyo ili aweze kurudisha akili yake kama awali inabidi asafirishwe kwenda kumalizia matibabu yake nje. Hili linakuwa zoezi lisilowezekana kabisa kwa Roby kwani kitendo cha kujaribu kufanya hivyo, kinaweza kumfanya akakamatwa na Brenda kisha akaingia kwenye matatizo makubwa, kutokana na mawazo haya Roby anaamua kufanya mpango wa kumrudisha Brenda kwa Rweyemamu.

Baada ya pilika pilika hizo Robi anaamua kumalizia siku yake kwa kwenda kumtoa mdogo wake polisi. Ndani ya gari akiwa anamrudisha nyumbani Roby hakutaka kuongea nae chochote, lakini Zubery anasema, "Roby naomba unisamee Bro, nakuahidi hili halita jirudia tena, Nipeleke kwa Frank nikamuombe radhi", Roby huku bado akiwa na hasira na machozi yakimlenga anasema, "Na hilo ndio litakuhukumu mtu ambae ungemuomba samahani ameshakufa", Zubery kwa mshangao anasema, "Frank Amekufa!?" Mshutuko huo unamfanya Roby amjibu kwa ghdhabu, "Mnafki mkubwa wewe, wakati unamuitia polisi wenye masiraha kiasi kile ulitegemea nini?". Mazungumzo hayo yanaendelea, na mpaka wanafika nyumbani kunakuwa hakuna maelewano njia nzima.
Baada ya kumrudisha Mpaka nyumbani, Roby anarudi kwake kwaajili ya kujiandaa na mazishi ya Frank.

Hatimae Tarick Amefaulu kutoka Gerezani, Vitengo vyote vya ulinzi na usalama vinakutana kwa dharura ili kujua ni jinsi gani wataweza kulitia gaidi hilo nguvuni mapema iwezekanavyo kabla hata halijasababisha Athari zozote wala halijatoka nje ya mipaka ya nchi. Roby anataka kumrudisha Brenda kwa Rweyemamu na kumtorosha Tarick mbali kabisa nje ya nchi. Je Huu ndio mwisho wa hisia kali za kimapenzi za Brenda dhidi ya Tarick, Bado ni kizungumkuti kikubwa usikose kufatilia Episode namba 12 ya tamthilia hii ya the Second Door.

Kwa kumalizia, niseme tu kuwa kuna vitu viwili vinavyoniumiza kichwa, Sijui idadi ya watu wanaofatilia tamthilia hii, I real want to know my readers, lakini pia nataka kujua ni kiasi gani tamthilia hii inawavutia na jinsi gani mnaithamini fanya nijue, unaweza kufanya yote haya kwa kuchangia hata 500 tu kupitia namba ninazotoa, yaani katika watu 8000+ waliopitia hakuna aliyechangia hata 200 tu!? Kama Tamthilia haivutii coment hapa chini, mimi nitafanyia kazi kila comment kama nilivyofanya tangu awali, na kama itaendelea hivi kufikia episode 12 nitaisimamisha Tamthilia hii na kuanza nyingine nzuri zaidi itakayo wafurahisha. Tukutane kwenye episode no12.

 
Huo ni mwisho wa Episode No 9 namba 10 inakuja Juma 5. Mwisho bado kabisaaaaaa naziona kama Episode 50 hivi mbele.
Nilikua nabadilisha tu jinsi ya kumaliza Story. nashukuru kuona hii stori inasomwa na maprofessional wengine kama mizambwa I appreciating you kaka jaribu pia kuni advice how Can I Improve.

everlenk
,
Mrembo by Nature
Gunda66
Khantwe

na wasomaji wangu wote nawapenda sana.

Unaweza sababisha mtu akafa hivihivi kwa presha, maana hujui he imeishaje tarick hajanyongwa au hajatoka jela?, vp kuhusu blenda na jambazi kuu la tamthiria yetu.
 
Mchango mchango mchango,..... Jamii Forum weka namba tena ya mpesa na tigo pesa. Usiendelee na sehemu nyingine km hakuna kilichoingia kwenye namba

Mimi binafsi toka mwanzo ni mdau wake ila napata shida kidogo majina yetu halisi yatajulikana,sijui tufanyeje juu ya hili?
 
Last edited by a moderator:
JamiiForum forum usikate tamaa mwanzo mgumu ila usichoke mbona matunda ya kazi yako utakula tu,tupe muda
 
Last edited by a moderator:
Mimi binafsi toka mwanzo ni mdau wake ila napata shida kidogo majina yetu halisi yatajulikana,sijui tufanyeje juu ya hili?

Sidhani sababu hata kama jina halisi litajulikana still bado identity yako ya humu ndani haitojulikana
 
Salamu za Nusu mwaka

Hallow my Beautiful Readers, Iam more than happy kutambua kuwa mola amenijalia kuingia ngwe ya pili ya mwaka huu(2014) nikiwa hai pamoja na wasomaji wangu wote. sijui kama ni utaratibu wa kawaida, ila naamini ni nidhamu na adabu yakipekee, kumshukuru mwenyezi mungu kwa kutuwezesha kumaliza nusu ya mwaka tukiwa salama. Amini usiamini kama watu wangepiga kura kuwa nani atangulie mbele za haki kati yako na Marehemu Director George Tyson, safari yako ingeishia mwezi mei, ila kwa kuwa anayeamua hatma ya kila mmoja ni Mwenyezi Mungu, muamuzi wa haki na asiyekuwa na mshauri, This is another opportunity given to you, Mwenyezi Mungu anajua nini unataka kufanya na ameona nyota kubwa ndani yako, ndio maana amekupa fulsa hii. Kwakuwa Mungu amekuthamini mpaka kufikia hatua ya kutoa fursa hii kwako, sasa unatakiwa kudhihirisha kuwa umestahili fulsa hii. Haijalishi hata kama bado vikwazo ni vingi mpaka kutimiza malengo yako mwaka huu, amini aliyekupa fulsa ya wewe kuendelea kuwepo ameona kwamba utavishinda vikwazo vyote na havita kuangusha. Usijihoji kwa kasi ndogo ya kuelekea kutimiza malengo yako ya mwaka, Jihoji kwa mazuri machache ambayo umeshayafanikisha na mipango madhubuti ya kupasua mepesi yaliyobaki kabla mwaka haujakatika, Usitizame vikwazo vilivyotingisha mahusiano yako kwasabau umepewa fulsa kubwa zaidi ya kuyaimarisha. Usijihukumu kwa nafasi ulizozipoteza kwani nafasi na fulsa ulizonazo sasa ndizo zilizokuwa zinahitajika kwenye mafanikio yako.Ungana na mimi kuamini usemi wa mwanafalsafa mmoja unaosema "Kama umeweza tamabaa Basi unaweza tembea". Mungu alieona ukubwa wa ndoto zako ndani ya mwaka huu, na uwezo wa ajabu ulio nao wa kutimiza Malengo yako yote, ana nguvu kuliko Bosi aliyekunyima kazi, kuliko adui anaekuwekea vikwazo, kulikojirani anaekutabilia mabaya, Kuliko Rafiki anaekuletea uadui. Fumba macho kisha uitazame picha kubwa aliyoiona Mwenyezi Mungu picha ya malengo yako ya mwaka huu yakiwa yametimia, Mwenyezi Mungu ameiona na kuiwezesha taswira hiyo ndio maana amekutunuku kuingia nusu ya pili ya mwaka huu.

Mwisho fikiria kuingia mwaka 2015 bila upinzani kwa kushiriki katika kuifanya dunia iwe sehemu salama na yenye amani kwa maisha ya wanadamu. Usiwe kikwazo cha aina Yoyote wala Usisababishe Maumivu ya makusudi kwa kiumbe chochote. Toa Zaidi, Penda Zaidi, Jali Zaidi, Saidia Zaidi na Mwenyezi Mungu Atafanya Badala Yako Zaidi.
Nawatakia Mafanikio Mema. NAWAPENDA SANA.
 
Mi nimekutumia kwa Mpesa sema jina lililokuja huko huwezi lijua lipo tofauti na lililopo hapa ,

wengine nanyi tumeni basi apate muudi ya kuwasilisha mawazo yake
 
Mi nimekutumia kwa Mpesa sema jina lililokuja huko huwezi lijua lipo tofauti na lililopo hapa ,

wengine nanyi tumeni basi apate muudi ya kuwasilisha mawazo yake

Vizuri sana,nami nimemcheki kwenye T.pesa,wadau wengine changieni basi kijana aendeleze kipaji.
 
The Second Door Episode- 12

Mpendwa Rafiki, leo tunaendelea na Episode namba 12 ya Tamthilia hii nzuri kabisa ya The Second Door, Katika Episode ya 11 Tuliishia kuona Roby akiwa amefanikisha zoezi la kumtoa Tarick Gerezani Kwa kumlipia Fine.



Ikiwa ni siku mpya, alfajiri na mapema, Roby akiwa ndio anatoka kuamka anamalizia kujiandaa ili aende kazini huku akiwa na lengo la kwenda kutazama hali ya Brenda pamoja na kufanya utaratibu ikiwezekana leo wamzike Frank, kumbuka tu muda wote huu Roby alikuwa hajamtaarifu Tarick juu ya kifo cha Frank. Wakiwa pamoja Roby na Tarick wanakunywa chai, Tarick anasema, "Nashukuru sana kwa msaada wako dokta", Roby anatabasamu na kusema,"Usijali ilikuwa ni lazima nimalizie kazi hii kwa nguvu yeyote ile" Baada ya Roby kusema maneno hayo, Tarick anamuuliza Roby, "Lakini dokta leo si ninaweza kurudi nyumbani!?", Roby ananyamaza kidogo kisha kwa umakini mkubwa anasema, "Mashtaka yako ni makubwa sana, na tangu jana utoke, hatujajua polisi wapo katika hali gani. Naona ni vema tusubiri kwanza, lakini kwakuwa lengo kubwa ni kumuondoa mama hofu, mchana nitaenda kumfata aje uonane nae". Tarick anaridhika na ushauri wa Roby na kujibu, "inshalla nahisi hilo litakuwa jambo jema zaidi". Kimya kifupi kinatawala huku wakiendelea kunywa chai, Roby anaanza kusema, "Tarick! Frank amekupigania sana" Tarick anajibu kauli hiyo kwa kusema, "Ndio maana ninahamu isiyo kifani ya kumuona ndugu yangu, sijui nitafurahi kiasi gani, kwanini usiwasiliane nae tuone kama anaweza kufika hapa leo!". Kwambaali sana majonzi yanaanza kuonekana usoni kwa Roby, anajibu kwa upole na uchungu huku akijitahidi sana kuficha hisia zake, anasema, "Tarick! Usihofu tutaonana nae tu, Lakini Nasikitika sana kwamba hatutaweza kuwasiliana nae tena kwa sasa". Tarick akiwa ndio anamalizia chakula kauli ya mwisho inamfanya moyo wake unashtuka kama mtu mwenye presha anauliza kwa hofu, "Nini kimetokea!?" Roby anajibu,"Katika purukushani za kutetea uhai wako, Frank alipoteza maisha, hatunae tena". Taarifa hiyo inampa simanzi kubwa sana Tarick na kumfanya aangue kilio. Analia kwa uchungu huku akilaumu kwanini alifikia hatua ya kupoteza uhai wake wakati hukumu yake ilitokana na uzembe wake Mwenyewe.
Huku nyumbani mama yake na Tarick anahaha kumtafuta Frank kwenye simu ili apate taarifa za hukumu ya Tarick kwani alijua kuwa leo lazima angesafirishwa kuelekea Dodoma kwenye hukumu hiyo. Anapiga simu bila kukata tamaa lakini hakuna matumaini yoyote ya kupatikana simu hiyo. Baada ya mama kuitafuta simu ya Frank kwa muda mrefu bila mafanikio, anaamua kujiandaa ili aende kule gerezani kufatilia na kupata taarifa.


Huku kwa Roby mara baada ya Tarick kupewa taarifa za kifo cha Frank na mazingira yaliyopelekea mauti yake, Tarick analia mpaka uso wote unamvimba, analia kiasi kwamba Roby anaanza kuhofia afya yake na kujuta kwanini alimpa taarifa hizo mapema. Lakini haina jinsi, Robi anamuaga Tarick ili kafatilie mipango ya mazishi. Roby akiwa anatoka tu kwenye geti la nyumba yake, zinakuja Difender mbili kwa kasi na kufanya moyo wa Roby udunde kwa nguvu kutokana na hofu. Difender hizo zinakuja na kupita kwa kasi mbele ya nyumba hiyo huku zikipiga ving'ora. Kimoyo moyo Roby anasema "hii ndio ghasia ya kuishi kandokando ya barabara". Asubuhi hii Roby akiwa ndani ya gari lake anaendesha moja kwa moja mpaka hospitali kisha kabla hajaingia ofisini kwake anaenda kimtizama Brenda na kumjulia hali. Baada ya hapo anaweka mambo yake ya kiofisi sawa kisha anatafuta vijana na kuwapa hela waende wakaandae mazingira ya kuupumzisha mwili wa Frank. Vijana hao wanapokea hela ya kutosha na kwenda kufanya maandalizi yote kwenye makaburi yaliyopo kinondoni.


Mpenzi msomaji Desturi mbaya ya dokta Roby kutofatilia wala kujali kilichokuwa kikiendelea kwenye vyombo mbalimbali vya habari, safari hii inaweza kumgharimu, kwani magazeti yote ya siku hiyo yalikuwa yamepambwa na taarifa ya tukio la kutoweka kwa Tariki kutoka mikononi mwa jeshi la polisi, kwa upande mmoja swala hili linaripotiwa kama kashfa ya uzembe wa hali ya juu kwenye jeshi la polisi, na katika ripoti zingine tukio hili linaelezewa kwa makisio kuwa limefanikiwa kutokana na teknolojia ya hali ya juu inayotumiwa na mitandao wa kigaidi, lakini mwisho wa yote vyombo vyote vya habari vinaripoti, msako wa kihistoria dhidi ya gaidi hilo. Kama ilivyo kawaida magaazeti ya udaku nayo hayakuacha kupiga bao kwenye biashara ya taarifa hizo huku magazeti hayo yakiwa yamepambwa na habari tofauti tofauti, wakati mengine yakiandika "Gaidi la lililohukumiwa kifo laachiliwa kwa fain kwenye kesi ya kuku". Taarifa zote hizi pamoja na vipindi vyote kwenye maredio kulizungumzia swala hili kwa mitazamo tofautitofauti lakini Roby hakuweza kujua ukubwa wa tukio zima.
Bado Roby alikuwa na pilikapilika nyingi sana siku ya leo, lakini muda huu anautumia kuwasiliana na jamaa yake ambae alikuwa akiishi Botwsana kwa mara nyingine tena na kukamilisha mipango ya kumtorosha Tarick. Baada ya hapo, Roby anaamua kumaliza zoezi la kwenda kumchukua mama yake na Tarick ili ampeleke kumkutanisha na Tarick, kisha waongozane wote kwa pamoja kwenda kwenye mazishi. Roby anafunga safari kuelekea kwa mama lakina kabla ya hapo anamuagiza jamaa wa monchwari kuwa atatuma watu waje kuuchukuwa mwili wa Frank kwaajili ya kuelekea kwenye maziko. Dokta Roby anafunga safari kuelekea kwa mama, maelekezo mazuri na uzoefu wa kona mbali mbali za jiji zinafanya Roby kufika nyumbani kwa mama bila shida. Inakuwa kama bahati kwa Roby kwahi kufika nyumbani hapo kwani mama ndio alikuwa anatoka, kitendo cha mama kumpokea mgeni asiyemfahamu, kinapelekea avute subira kidogo na kumkaribisha ndani kwa ukarimu ili amsikilize.


Kama nilivyokwisha kuelezea, msako mkali wa jeshi la polisi, ambao ulianzia kwa kuimarisha ulinzi maeneo yote ya mipakani na kuhakikisha kuwa Gaidi wanalolitafuta halikatishi kwenda nje ya nchi, pia msako huu ulikuwa umepamba moto katika kona zote za ndani ya nchi. Lakini ndani ya muda huu kwa kutumia intelegencia ya hali ya juuu, jeshi la polisi likiamini kuwa lazima gaidi hili litataka kwenda kwa mama yake au kujaribu kufanya nae mawasiliano kwa njia yoyote, hivyo polisi hawa wanaamua kufanya uvamizi wa kushtukiza nyumbani kwa kina Tarick. Roby akiwa na mama, bila kupoteza muda, anamwambia, "mama, nimekuja kukupa taarifa za tarick", kauli hiyo inampa mshituko mama kisha anauliza kwa shauku kubwa,"Nashukuru mwanangu, niambie anaendeleaje, hapa nilikuwa sijui hata pa kuanzia ". Roby akiwa anataka kuanza kufunguka, mara wanasikia kundi la zaidi ya askari sita likiingia humo ndani. Kundi hilo linaingia mpaka sitting room kwa fujo, na kusalimia kisha wanamuuliza Roby, "unaweza kutumia dakika moja kutuambia Wewe ni nani na umefata nini hapa chap chap!", baada ya swali hilo mama anadakia na kujibu kwa hasira, "wajinga nyinyi, mnaacha kijitambulisha kwanza nyinyi ni wakina nani na mnataka nini hapa mnakimbilia kuhoji watu, washenzi nini!?" aliyekuwa akiongoza kikosi hicho, anasema, "mama! Tupo kazini utapata shida" kisha anamgeukia Roby na kumwambia, "umebakisha sekunde thelasini, hakikisha nakuelewa", japokuwa askari hawa hawakuwa na sare za polisi lakini Roby alikuwa ameshaelewa kilichokuwa kikiendelea anajibu, "mimi ni dokta Roby", nipo hapa kwa ajili ya kucheck afya ya mama. Yule askari anauliza, "nipe kitambulisho chako fasta!" Roby anatoa kitambulisho na kumkabidhi. Baada ya yule askari kusoma kile kitambulisho na kuthibitisha kuwa Roby alikuwa ni daktari, anamuamuru aondoke eneo hilo.


Tukio lililomkuta Roby pale kwa mama linamshtusha na kumuonesha kuwa hali haikuwa shwari kabisa muda huo, anarudi haraka mpaka nyumbani kwake na kukuta Tarick japokuwa alikuwa amepata nguvu lakini, bado sura yake ilikuwa na majonzi mazito ya kumpoteza Frank. Roby anampa salamu, kisha kabla ya kusema chochote, Tarick anasema, "Nilitegemea ungekuja na mama!" Frank huku akiwa anatembea taratibu kwenda kuwasha television anajibu, "Nimeenda kwa mama lakini nimeshindwa kuja nae", kauli hiyo inamshtua Tarick kisha anauliza kwa hofu kubwa, "kwanini!?", Roby anajibu, "mama amevamiwa na askari" taarifa hiyo inampa wasiwasi mkubwa Tarick huku akisimama anasema, "whaaaat!" kisha anaduwaa kwa sekunde chache lakini kabla hajaongea neno, taarifa ya habari inayorushwa kila baada ya saa moja na kituo maarufu inaripoti taarifa ya jeshi la polisi juu ya msako wa Tarick.


Katika taarifa hiyo anaoneshwa kamanda wa polisi kanda maalumu akisema,"Jeshi letu limejipanga vizuri kwaajili ya kuhakikisha tunalitia nguvuni gaidi hilo kabla halijatoka nje ya mipaka ya nchi yetu, na tuwaambia wananchi wote waendelee na shughulizao za kawaida bila hofu yoyote kwani tumesha imarisha ulinzi katika kila kona ya nchi hususan katika maeneo yenye mikusanyiko ya watu ili kuhakikisha gaidi hili halileti madhara kama yale ya Arusha. Na katika jitihada za awali tunahakikisha tunawakaba watu wake wote wa karibu ili walisaidie jeshi la polisi kwenye upelelezi". Kusikia taarifa hizo Tarick anakurupuka ili amkimbilie mama yake, Roby anamkamata na kumzuia kisha anamuuliza, "Unaenda wapi sasa!" Tarick anajibu kwa hasira, "Niachie nimuwahi mama yangu, hastahiri kupata shida yoyote kwa ajili yangu, hili linanihusu mimi wacha mimi ni wajibike na sio mama yangu". Roby anamjibu Tarick kwa msisitizo, "Acha ujinga, kwani ukifa wewe ndio utakuwa umemsaidia nini , mama yako?" Hoja hii inaonekana kumzidi nguvu Tarick anaanza kulia huku akisema, "Niache dokta watu wasiokuwa na hatia wataendelea kufa na kuteseka kwasababu yangu, nimeshampoteza ndugu yangu Frank, sasa hivi mama yangu mzazi nae yupo hatarini, hata kama nikisalimika mimi wao wakafa wote ndio nitakuwa nimefanyaje!?".


Mvutano mzito baina ya Tarick na Roby unaishia kwa Roby kufanikiwa kumtuliza Tarick na kumsihi atulize munkari, kisha anamuahidi kuwa yeye atahakikisha usalama wa mama yake. Ila Tarick anaapa kuwa endapo watamfanya chochote mama yake basi atafanya tukio kubwa zaidi ya lile walilompachika. Roby anampigia simu dereva wa pikap na vijana waliomuandalia sehemu ya kuzikia kisha anawaelekeza waende muhimbili wakachukuwe mwili wa Frank na kuupeleka makaburini. Baada ya hapo Tarick na Roby wanaongozana kutangulia kwenye eneo la makaburi japokuwa kutokana na ukaribu wa kutoka hospitali mpaka makaburini wangekuta maiti ya Frank imeshafika. Halikuwa jambo salama kwa Tarick kuingia uraiani muda huu lakini hamna jinsi kwani Roby asingeweza kwenda kuzika peke yake.


Wanaongozana mpaka makaburini, Nakatika tukio la kuhuzunisha kabisa Tarick anashiriki katika kuhitimisha safari ya mwisho ya ndugu na rafiki yake kipenzi Frank Rwambano. Wanakaa eneo hilo mpaka majonzi yanapungua kabisa kisha wakiwa wanavuta pumzi kwa ajili ya kurudi nyumbani, Roby anasema. "Tumekamilisha kazi ya muhimu, jiji sio salama kabisa kwako hivi sasa, kesho tutaanza safari ya kuelekea Botswana kupitia Lusaka Zambia" kitendo cha Roby kumaliza kusema maneno hayo Tarick anamjibu, "Sitaki kuondoka!", kauli hiyo inamchanganya Roby anamtizama Tarick na kumuuliza kwa mshangao, "hutaki kuondoka !? unamaanisha nini?" Tarick anajibu swali hilo kwa ujasili, "nataka kuishi karibu na adui yangu" Roby anajibu kwa mshangao kwa kusema, "Tarick! adui yako sio mtu wa kawaida, ni mtu mwenye nguvu na madaraka, kama unafikiria kulipa kisasi hautaweza, ni kheri uokoe nafsi yako" Roby anaongea maneno hayo kwa uchungu mpaka chozi linamdondoka, Tarick naye huku akiwa mwenye simanzi kiasi cha kuongea kwa majonzi mpaka mdomo unamtetemeka anasema, "dokta! …" Dokta Roby anageuka na kumtazama, kisha Tarick anaendelea, "Mimi ni mwislamu safi naapa mbele za mola wangu, nimemsamehe Rweyemamu kwa roho moja na kwa nia safi, lakini nafsi yangu inaniambia niishi naye karibu, na nakuomba tafadhari usinisaidie kutoroka, nisaidie niendelee kuishi hapa dar es salaam ili niishi karibu nae." Kwa maneno hayo ya Tarick wote wawili wanashindwa kuzuia hisia kali za majonzi wanakumbatiana kwa uchungu huku Roby akisema, "Haitakuwa salama kwako Tarick ".


Mpenzi msomaji na mfatiliaji wa mkasa huu. Frank anakataa kwenda kuishi Botswana, na madai yake ni kwamba, japokuwa amewasamehe kabisa wabaya wake wooote, lakini anataka kuishi nao karibu. Je nini maana yake? Na je! Ni swala litakalo wezekana ama ndio utakuwa mwisho wake kama jinsi ilivyokuwa kwa Frank! Na vipi kuhusu, Roby yeye ndie aliekuwa na dhamana ya kumtorosha Tarick ja ataweza kumsaidia ili frank aendelee kuishi jijini dar es salaam kwa amani? Usijinyime uhondo huu, ilikupata majibu mahususi ya maswali yote haya ungana na mimi katika episode no 13 ya tamthilia hii ya kepekee ya the second door.


COMENT HAPA KWA KUNIAMBIA UNAHISI NINI KITAFATIA!


Nashukuru sana na nimefurahi kuona baadhi ya wapenzi wa mkasa huu wakiwa wameonesha moyo wa kujitolea kuisapoti kazi hii kwa kuichangia, bado michango yenu inahitajika sana kwaajili ya kuboresha burudani hii, hivyo niendelee tu kuwahimiza kama umevutiwa na mkasa huu, usikose kuchangia kiasi chochote utakachoweza ili kuisapoti kazi hii. Mwisho nasema nawashukuru sana na Ahsanteni.

 
Yap! uhondo unaendelea na kuanzia Episode ya 14 au 15 nahisi ndio utakuwa mwanzo wa utamu kamili wa Tamthilia hii nashukuru wooooote kwa sapport. Lakini shukrani zangu za kipekee ziwafikie prospa, everlenk na beth ambao wamekuwa watu wa kwanza kutoa michango yao kwaajili ya kuisapot Tamthilia hii naamini wasomaji wangu wengine wanaonipa nguvu kubwa kabisa kwa kufatilia tamthilia hii wasomaji kama ram, xfactor,davidson689, Mrembo by Nature, Mbimbinho, Kyenju na wengine wengi sana zaidi ya 5000 siwezi kuwataja woote naamini pia wapo njiani kusapot kazi hii kwa kuichangia hata kidogo
 
Back
Top Bottom