The Second Door (Tamthilia)

The Second Door (Tamthilia)

Ipigie kura simuizi hii

  • Nzuri Sana

    Votes: 9 56.3%
  • Inafaa Kusomwa

    Votes: 5 31.3%
  • Yakawaida

    Votes: 0 0.0%
  • Sijaisoma

    Votes: 2 12.5%

  • Total voters
    16
Duh!! Si mchezo jaman! Naanza kuamini maneno ya Sheikh lakini Zuberi ataponaje? Nyota ya Frank itang'aa kweli? Asante JamiiForum kwa simulizi tamu, big up!!
 
Last edited by a moderator:
Ha ha ha najua watu wengi Wanafikiria huu mwanzo wa muvi, Badooo! The second Doa ni Mbele kuanzia Episode Ya 12 au 13. ndio itajulikana mbivu na mbichi. huu ni utangulizi tu everlenk.
kwani kufikia hapa Unaweza uka relate Jina La Tamthilia na Story yenyewe vinaendana?
 
THE SECOND DOOR- EPISODE 9

Habari gani wasomaji wangu woote mnao nipa nguvu na kunipa akili ya kuendeleza kisa hiki cha kipekee ndani ya Tamthilia ya The Second Door, I promise Bonge la zawadi kwa wasomaji wote wa simulizi hii ambao ni zaidi ya 5000, kutoka FaceBook, WattPad, ReverbNation, Kwenye Blog, na kwa namna ya pekee kabisa kutoka Jamiiforum, Kaeni mkao wa kula.

Katika Episode namba 8, Tuliona jinsi Frank na wenzie walivyofanikisha zoezi la kuwaponyoka makachero wa Rweyemamu, Lakini Zubery akiwa ameshafanikiwa kuwatoka askari hao, anaingia mikononi mwa askari wa usalama barabarani kwa kosa la kuendesha gari bila ya Leseni, muda huo ndio aliokuwa amepokea simu ya Roby na kumpa taarifa za kukamatwa. Lakini Zubery alitumia mbinu ya kuwadanganya wale Trafik kwa kuwaambia kuwa ilimbidi afanye hivyo ili kumuwahisha shemeji yake hospitali kwani alikuwa akisumbuliwa na kifafa cha ujauzito, pointi hiyo inapewa nguvu na Brenda ambaye alikuwa amelala kwenye siti ya nyuma bila fahamu. Askari wanamruhusu Zubery amuwahishe mgonjwa lakini hilo linafanikiwa kwa nguvu ya mlungula(Rushwa).

Zubery Baada ya kuwataarifu Frank na Roby kilichotokea wanapatana wakutane Keko kwaajili ya kuelekea kwenye Restaurant ya Wahindi ambako Frank alikuwa amelipia chumba kikubwa cha familia. Wanafanikiwa kukutana na kuelekea Kwenye huo mgahawa, wakiwa wanaingia ndani na mgonjwa wao mara Brenda anaanza kuhema, Frank anakuwa wa kwanza kugundua hilo, kwa mshtuko anasema,"anahema!" Roby ambae alikuwa hajagundua anamtizama haraka haraka, baada ya dokta Roby kumtizama na kugundua kuwa mapigo yake ya moyo yalikuwa yameongezeka kasi wanaongeza spidi na kumuingiza ndani. Roby anatoa vifaa vyake vya matibabu na kuanza kumtizama maramoja.

Tayari ilikuwa imeingia jioni Frank anamuaga Dk Roby, "Mahali hapa ni salama, ngoja nikuache kwa sasa nitakuja kesho mapema" Roby anamjibu, "Usijali frank nenda kapumzike" Kauli hiyo ya Roby inamfanya atoe tabasamu jepesi na kumjibu,"Bado mda wa kupumzika, ninajukumu linguine kubwa zaidi ya hili lina ningojea" Roby anasema,"ok! Nakutakia mafanikio" Kabla hajaondoka Frank anamtizama Zubery na kumwambia,"Nashukuru kwa msaada wako, umekuwa msaada mkubwa sana kufanikisha sisi kuwa hapa muda huu, pengine tungekuwa gerezani" Zubery na Roby wanacheka kisha Zubery anajibu,"Usijali kaka…". Baada ya kuagana Mbiombio Frank anarudi mpaka hotelini alikokuwa anakaa. Usiku wa leo Frank anaonekana akiutumia kupekua kila kurasa za mtandao wa internet wa Wizara ya ulinzi na usalama wa taifa, zoezi hilo haliishii hapo, Frank anakagua kila website ya wizara hiyo inayohusiana na magereza, zoezi hilo linamfanya Frank ashtukie tayari imeshafika alfajiri.

Siku hiyo, ikiwa ni siku moja tu tangu makachero wa Rweyemamu wachezeshwe kizungumkuti na baadhi yao kupewa kipigo kikali na Raia, Rweyemamu anafika hospitali kuwatizama watu wake waliokuwa mahututi, akiwa peke yake kwa wagonjwa hao ambao walikua wamelazwa hospitalini hapo, Rweyemamu anaumiza kichwa na kutafakari. Ndani ya kipindi hiki Rweyemamu tayari alikuwa amesha pata taarifa juu ya yote yaliyotokea kuanzia hosteli mpaka wakina Frank wanawaponyoka watu wake, akiwa bado anawaza kwa makini, anaingia lugano na wenzie, baada ya salamu Rweyemamu huku akitumia ishara ya kichwa na mikono anawaonesha wafanyakazi wake wale wagonjwa akimaanisha, mmeona? Lugano anasema, "walituzidi akili kidogo tu bosi, lakini tulishawatia nguvuni", kwa uchungu na msisitizo Rweyemamu anamkatisha na kusema,"I told you!", Kauli hiyo ya Rweyemamu inakatishwa kwa mwenzie na Bosco kuanza kutapatapa pale kitandani, kumbuka waliokuwa wameingia mikononi mwa raia ni Bosko na mwenzie aliekuwa akiitwa inspector Hashimu, aliyekuwa akitapatapa muda huu ni hashimu, daktari wao aliekuwa katengwa maalum kwa ajili ya kuwatazama anafika hapo mara moja na kuanza kumtizama, Hashimu anazidi kufurukuta kama mtu ambae anazama kwenye maji, anahangaika mpaka anamshtua Bosko ambae alikuwa amesinzia lakini hali yake ilikuwa na nafuu kidogo, Hatimae mwisho wa kuhangaika huko Hashimu anakata Roho papo hapo, Wote wanaumizwa sana na tukio hilo lakini, Bosko anaumia zaidi na kwakuwa yeye bado alikuwa anaumwa pale kitandani anaishia kumwagikwa na machozi kwa huzuni. Wengine nao wanashindwa kujikaza kwani Hashimu alikuwa ni mtu ambae walikuwa wameshafanya nae kazi kwa zaidi ya miaka 2, alikuwa ni mshirika mzuri katika kila jambo walilokuwa wakilifanya kwa pamoja, alikuwa na upendo kwa wenzie wote lakini alimjali na kumheshimu kila mmoja kipindi cha uhai wake. Rweyemamu anashindwa kuvumilia anatoka eneo hilo na kuwaacha wenzake wakiendelea kuomboleza.
Asubuhi hii Frank ameamkia, Unix Network, Kampuni kongwe ya maswala ya technologia. Frank anajitambulisha kama mteja, na kupokelewa na kitengo cha masoko kwenye kampuni hiyo, kitengo ambacho kinatangulia kwa kujimwagia sifa kibao na kumwelezea mambo mbalimbali wanayoshughulika nayo. Katika maelezo mengi wanayo yatoa wanafanya kosa kubwa kwa kuanza kuorodhesha baadhi ya wateja wao wanao wahudumia na hapo kwa sifa na kujinadi wanataja Taasisi za Serikali ikiwemo na Magereza, Mrembo Magret aliyekuwa amepewa jukumu la kuhakikisha mteja huyo hachomoki, anaifanya kazi yake vizuri, ila kitendo cha kutaja Taasisi ya magereza kinamfanya masikio yamsimame na kumuongezea nguvu frank akiamini yupo sehemu sahihi.

Bila kupoteza muda Frank anamuomba dada huyo amkutanishe na maengeneer wa kampuni hiyo ili aweze kupata taarifa za kitaalamu zaidi. Dada huyo anamuomba Frank asubilie kidogo na kwenda kwenye ofisi za waheshimiwa hao. Akiwa ndani anazungumza nao, wanaonesha kudharau baada ya kuambiwa aliekuwa akihitaji kuwaona ni mswahili, mmoja wao anasikika akisema, "Wasumbufu tu pengine website yake imefutika tu, sasa anaacha kujaza form huko aelezee tatizo lake anataka mpaka aonane na sisi". Yule dada Baada ya kuona maengeneer hao ambao walikuwa na asili ya kihindi wamedharau kumuona mteja, anaamua kurudi na kutumia Busara kwa kusema,"Samahani kwa kukuchelewesha.. Sasa…. Maengeneer wote wapo bize sana muda huu, lakini unaweza ukajaza form ya huduma yoyote unayohitaji halafu tukakuhudumia".
Frank anaoneshwa kutoridhishwa kabisa na maneno ya huyo dada, anajaribu kumsisitiza na kumwambia kuwa lazima awaone, na yule dada anajaribu kumsihi kuwa ukarimu kuwa kwa kufata utaratibu inabidi ajaze form ya huduma anayohitaji ili iwerahisi pia hata kuonana na mtu sahihi. Wakati majibishano hayo yakiendelea, General maneger anatoka ndani ya ofisi yake akiwa anataka kuelekea kwenye hoteli ya karibu kupata Breakfast. Kwenye chumba maalum cha mazungumzo ambacho kilikuwa kimezungushiwa na vioo, Bosi huyo anagundua kutokuwepo na maelewano kwenye mazungumzo yoa. Anahisi kuwa pengine Frank alikuwa ni mteja ambae alikuwa akilalamikia huduma aliyopewa.

Bosi huyo anaamua kuingia ndani ya chumba hicho anasalimia vizuri na kuuliza kama kulikuwa na tatizo lolote. Magret anapata hofu kidogo na kusita kujibu, Bosi huyo alikuwa anaongea kihindi na kingereza tu, hivyo frank bila kujali anasema. "mimi ni Frank Rwambano, natokea Vox Telecom SouthAfrica…", Huyo bosi anaonesha mshtuko kwa mbaali kisha anamtizama Frank usoni na kumkatisha halafu anasema,"Nioneshe kitambulisho chako?" Frank anatoa wallet na kumpa kitambulisho, Baada ya kukisoma anampa Frank mkono na kumkaribisha. Kitambulisho hicho kilikuwa kikionesha kuwa frank alikuwa ni Computer Forensic Expert Katika kampuni hiyo ya Vox Telecom, Lakini Bosi huyo alijikuta akimnyenyekea Frank ghafla kwani Kampuni yake inafanya kazi katika nchi zote za Africa mashariki kwa msaada mkubwa wa technology kutoka Vox Telecom southafrica. Lakini kunakitu kingine kinachomfanya afikie hatua ya kumuogopa Frank kwani kitengo cha forensic ndani ya kampuni ya kina frank ni kitengo kinacho ogopeka kabisa na kuheshimika katika nchi zote za kiafrica, hivyo kinakuwa kitu cha ajabu kabisa kuona frank ambae ni mtanzania ni miongoni mwa wafanyakazi wa kitengo hicho.

Tatizo limetatuliwa, Frank anakaribishwa ofisini kwa maneger huyo na kukabidhiwa kwa maengeneer hao kisha wanaambiwa wahakikishe wanamhudumia mpaka hatua ya mwisho bila kikwazo chochote na gharama za huduma zote Frank atakuja kuzifata ofisini kwake. Maengeneer hao baada ya kupewa wasifu wa frank hatimae wote wanaanza kumnyenyekea na mmoja anapewa kazi ya kusikiliza, Frank anadai kuwa anataka kusafirisha DataBase ya mteja wake kutoka Zimbabwe kuja hapa Tanzania hivyo anataka database hiyo ihifadhiwe kwao. Lakini Frank kabla ya kufanya hivyo frank anatoa ombi moja, kuwa kabla yakuanza process hizo anaomba afanye ukaguzi wa usalama wa network yao.

Maengeneer hao wanamsikiliza frank kwa heshima na adabu kwani wakati akizungumza nao alikuwa akizungumza na maneno mengine ambayo yalikuwa ya kitaalamu kiasi kwamba alikuwa akiwaacha njia ya panda. Frank anaagana nao na kuahidi kurudi siku ya Jumatatu kwani kesho itakuwa Jumapili siku ambayo sio ya kazi kabisa kwenye kampuni hiyo. Hivyo anaahidi kurudi Jumatatu kwa ajili ya kuanza ukaguzi wa njia zitakazotumika kupitisha Database hiyo kutoka Zimbabwe hadi Tanzania. Baada ya kazi hiyo frank anarudi moja kwa moja Restaurant na kukuta Roby akiwa anaendelea na matibabu ya mgonjwa, ambae muda huu alikuwa ametoa macho anatizama moja kwa moja bila kufumba wala kupepesuka(kupiga kope). Dokta anamwambia frank,"Hapo anaona, ila mifumo mingi ya fahamu mwilini mwake haifanyi kazi" Frank anauliza kwa hofu, "atapona?" dokta huku akionesha kutojiamini anajibu,"Aatapona Lakini sizani kama atarudi kama kawaida". Maneno hayo ya dokta yanamfanya frank ashushe pumzi.

Rweyemamu akiwa ameumia kweli kweli kumpoteza mfanyakazi wake anaamua kufanya mpango maalumu wa kumtokomeza Frank. Anaenda kwa Swaiba wake ambae ni kamanda wa vikosi vya usalama na ulinzi kanda maalum na kufanya nae kikao kifupi cha siri. Bosko pale hospitali alipokuwa amelazwa anapata nafuu kidogo kisha ndugu zake wanakuja kumchukua na kumrudisha nyumbani huku wakiwa na malengo ya kumpeleka kwenye maombi siku inayofata.Frank nae siku hiyo anarudi kwa mama kisha kama kawaida anamwambia mama kuwa kila kitu kinaenda sawa hivyo asiwe na hofu hata kidogo karibia Tarick atakuwa huru. Frank alifanya hivyo ili kumuondoa mama hofu, kwani presha ya mama huyo ilikuwa ikimpelekea kupoteza fahamu hivyo ingeweza kumletea madhara endapo angeendelea kuwaza sana kuhusiana na Tarick.

Kesho yake asubuhi Frank anaamkia kwa Brender, anakuta hali ya brender inatia matumaini kidogo ukilinganisha na awali pia ukizingatia kuwa hakuwa na fahamu kabisa kwa zaidi ya siku 7 sasa. Upande mwingine Bosko baada ya kudra za mungu kunusuru maisha yake, ndugu zake wanampeleka kanisani jumapili ya leo kwa ajili ya kufanyiwa maombi zaidi na kutoa shukrani mbele za mungu kwa fulsa nyingine tena ya kuendelea kuishi. Akiwa kanisani leo maneno ambayo mchungaji anaongea yanamchoma na kuigusa sana nafsi ya Bosko, mchungaji huku akiendelea kuhubiri anasema,"Sio mar azote shetani anafanya kazi katika njia tulizo zizoea………, wakati mwingine atamtumia mkeo………., wakati mwingine atamtumia mmeo kukutia katika dhambi…………, na shetani akikuta mwenzi wako katika ndoa yupo imara amesimama katika imani…, shetani atamtumia bosi wako, utajikuta unaingia katika majukumu yanayokutia katika dhambi ukizani unatekeleza majukumu ya kikazi, utajikuta unaingia kwenye uongo, unaingia kwenye dhulma, unaingia kwenye wizi, Amka sasa mtu wa mungu, na utizame kuwa hiyo sio kazi kukuletea kipato bali kukuletea hukumu ya milele katika jina la yesu, Amkaaaa…………". Maneno hayo makali na mazito yanamfanya Bosko ajutie sana kwani alinafahamu wazi kuwa, Tangu ahamishiwe kwenye kitengo maalum cha mwanasheria mkuu wa serikali akitokea makao makuu ya polisi, amekuwa akimtumikia Rweyemamu siku zote na sio Jamhuri ya muungano iliyo muajili, Bosko anajuta sana na hatimae anaadhimia kuacha kazi.

Jumatatu asubuhi, Frank akiwa anatoka hotelini alipokuwa anakaa, anakuta magazeti mengi yaliyokuwa katika meza mbalimbali asubuhi hiyo yakiwa na tangazo dogo kwenye kurasa za nyuma kuwa anatafutwa na polisi na ahadi kuwa donge nono inatolewa kwa yeyote atakae toa taarifa zozote zitakazo fanikisha kupatikana kwake akiwa mzima au amekufa, na makosa yaliyo orodheshwa kwenye matangazo hayo ni pamoja na kuteka nyara, ujasusi na mauaji.

MWISHO!
 
Mhhh!!! JamiiForum mbona leo umetuacha solemba??? Shauri yako wasomaji wako tuna presha kama mama yake Tarick!!!
 
Last edited by a moderator:
Huo ni mwisho wa Episode No 9 namba 10 inakuja Juma 5. Mwisho bado kabisaaaaaa naziona kama Episode 50 hivi mbele.
Nilikua nabadilisha tu jinsi ya kumaliza Story. nashukuru kuona hii stori inasomwa na maprofessional wengine kama mizambwa I appreciating you kaka jaribu pia kuni advice how Can I Improve.

everlenk
,
Mrembo by Nature
Gunda66
Khantwe

na wasomaji wangu wote nawapenda sana.
 
Huo ni mwisho wa Episode No 9 namba 10 inakuja Juma 5. Mwisho bado kabisaaaaaa naziona kama Episode 50 hivi mbele.
Nilikua nabadilisha tu jinsi ya kumaliza Story. nashukuru kuona hii stori inasomwa na maprofessional wengine kama mizambwa I appreciating you kaka jaribu pia kuni advice how Can I Improve.

everlenk
,
Mrembo by Nature
Gunda66
Khantwe

na wasomaji wangu wote nawapenda sana.

Tunakupenda piaaa....nilijua ndo mwisho...nimepataje hasira sasa...nikajuta kuifuatilia
 
Hongera sana kijana, kiendeleze kipaji chako, kwa mbaaali umenifanya nimkumbuke marehemu Ben Mtobwa. Jitahidi kuboresha uandishi, lakini pamoja na yote tanthilia yako ni nzuri.
 
Hongera sana kijana, kiendeleze kipaji chako, kwa mbaaali umenifanya nimkumbuke ndg Ben Mtobwa.

Nashukuru sana, Kaka nashukuru mna ni inspire kundelea kufanya utunzi kwani nilisha acha kabisa.
 
Huo ni mwisho wa Episode No 9 namba 10 inakuja Juma 5. Mwisho bado kabisaaaaaa naziona kama Episode 50 hivi mbele.
Nilikua nabadilisha tu jinsi ya kumaliza Story. nashukuru kuona hii stori inasomwa na maprofessional wengine kama mizambwa I appreciating you kaka jaribu pia kuni advice how Can I Improve.

everlenk
,
Mrembo by Nature
Gunda66
Khantwe

na wasomaji wangu wote nawapenda sana.

Pamoja sana,asante sana JamiiForum,tunakupenda pia,Mungu akupe afya umalize hadithi yetu salama salmini.
 
Last edited by a moderator:
Ukimaliza kuiweka yote, niite kwa kunimention, maana nimechoka kusoma mafungu mafungu.
 
Back
Top Bottom