The Second Door (Tamthilia)

The Second Door (Tamthilia)

Ipigie kura simuizi hii

  • Nzuri Sana

    Votes: 9 56.3%
  • Inafaa Kusomwa

    Votes: 5 31.3%
  • Yakawaida

    Votes: 0 0.0%
  • Sijaisoma

    Votes: 2 12.5%

  • Total voters
    16
Mimi naungana na wazo lako everlenk , mimi mchango wangu Jumatatu then Msamiati Useme bado kiasi gani kutimia, Tunaosoma second door tupo wengi sana zaidi ya 5000, hata tukichanga 200, 200 inatimia tumpenguvu kijana mbona tunanunua kwa shigongo 5000 hatuwezi kushindwa hata buku kwanza mimi naona hii inaquality kulikozile za jamaa. Mungu akutangulie akulinde na kila Baya
 
safi sana.... leo ndio angalau nimepata nafasi ya kusoma kidogo please naomba unimention niwezefwatilia kwa karibu japo muda unagoma
 
MAMBO VIPI MARAFIKI, NINAWATAKA RADHI SANA KUWATAARIFU KUWA NINASAFARI YA KUELEKEA TANGA KUANZIA J/3 AU J/4 KWA MUDA USIOZIDI WIKI MOJA HIVYO SITAKUWA NA NAFASI NZURI YA KUENDELEA KUANDIKA
RIWAYA HII. lAKINI NAAHIDI MUDA WOWOTE NIKIPATA KOMPUTER YOYOTE SAFARINI NA UPENYO WA
KUENDELEA KUANDIKA NITAIPOST KWANI SITAWEZA KWENDA INTERNET CAFE USIKU.
SITAKI MUDA MREFU UPITE BILA KUENDELEA KUWAPA BURUDANI HII.
NAOMBENI DUWA ZENU.


Mungu akutangulie mpendwa ktk safari yako, pamoja sana
 
mimi nimesha toa mchango wangu kwenye nambayako ya voda Msamiati. Jitahidi uwe unatoa updates za kiasi kilichopatikana ili tujue bado kiasi gani, wadau tujitahidi kuchangia tumuwezeshe mtunzi wetu, naamini akifanya kazi yake katika mazingira mazuri hata utamu wa Tamthilia utaongezeka.
 
THE SECOND DOOR- EPISODE 14

Habari gani Rafiki, ni wasaa mwingine tena unapoungana nami mwandishi wako Msamiati, katika kuwaletea mkasa wa kuburudisha ndani tamthilia hii ya the second door, na leo tunaenda kuendelea na episode no 14 ya mkasa huu.

"Kichwa kimestack kabisa... au wewe umepata wazo lolote?"Swali hili linaulizwa na Roby, kisha Tarick anajibu kwa kutikisa kichwa huku akisema, "Hapana sijapata jibu tutafanyaje". Kitendo cha Tarick kumaliza kauli yake hiyo ghafla mlango unasukumwa kisha anaingia Zubery huku akisema, "mimi ninajibu kaka…" Roby anasimama kwa mshutuko na kusema, "Zubery… ! mbona umekuja bila taarifa?" Zubery huku akijiamini, taratibu anawasogelea Roby na tariki wakati akiendelea kusema, "Roby, najua mpo katika wakati mgumu sana kaka yangu, na mimi ninawazo linaloweza kuwatoa katika sintofahamu hii". Zubery akiwa ametembea mpaka kwenye viti, huku wakitazamana na Roby wanakaachini kwa pamoja, kisha kwa msisitizo Roby anasema, "Zubery…! Nashukuru kwa wazo, lakini ninavyoongea hivi simama urudi nyumbani, na usijaribu tena kuja hapa bila kunipa taarifa." Tarick anaamua kuingilia mazungumzo haya kwa kusema, "Samahani dokta, sitaki kuingilia matatizo ya kwenye familia yenu, lakini… unahisi tofauti yenu inaweza kuwa muhimu kuliko wazo analotaka kulitoa!?" Baada hoja hiyo ya Tarick kila mmoja anakaa kimya, lakini kwa Roby ukimya wake unakuwa wa tofauti kwani unatokana na shaka kubwa ya kuweka maisha ya Tarick rehani kwa kuamua kumuamini tena Zubery, hata hivyo Roby hataweza kuzungumzia chochote juu ya kosa alilofanya Zubery kwani inaweza kuleta mtafaruku kati ya Zubery na Tarick. Baada ya kimya hicho kifupi Tarick anamalizia kwa kusema, "Wacha tumsikilize, Hata wazo lake likiwa na kasoro linaweza kutupa pa kuanzia" .

Zubery anadakia na kuanza kusema wazo alilokuwa nalo huku wote wakimsikiliza kwa makini, "Tarick anaweza kuendelea kuishi kwa uhuru na amani endapo atabadilisha kila kitu katika uhalisia wake, abadilishe, Jina, Wazazi, Vitambulisho, Pasport na Historia ya maisha yake". Maneno hayo ya Zubery yanaonesha kudharauliwa na kila mmoja, na kuona kuwa lilikuwa ni wazo la kitoto kabisa. Roby kwa kejeli anasema, "asante kwa wazo unaweza kwenda sasa!", Tarick anadakia na kusema, "Sikia Zubery, nitakapokamatwa vitambulisho feki havitaweza kunisaidia" Zubery anamkatisha Roby na kumwambia, "Hamjanielewa, Tarick anatakiwa akajipandikize kwenye familia nyingine na kuishi ndani ya familia hiyo kwa kutumia details zote za mtoto ambaye yupo kwenye hiyo familia". Roby anaonekana kuelewa alichokuwa akifikiria Zubery anamjibu kwa kumwambia, "Ok….. kwa wazo lako, Let Say Tarick anajipandikiza kwenye familia yetu kwa mfano na kutumia ID zako zote, kuanzia jina, historia ya kuzaliwa elimu na kila kitu, then how about you!?" Zubery anajibu Swali hilo kwa kusema, "Nina rafiki yangu ambaye kaka yake mkubwa alizamia south africa miaka kumi iliyopita na mpaka leo hana mawasiliano yoyote na familia yake, Tarick anaweza kujipachika kwa urahisi kwa kujifanya ndio yeye amerudi".
Roby na Tarick wanafikiria wazo la Zubery na kugundua kuwa lilikuwa ni wazo zuri, lakini lilikuwa gumu kuliingiza kwenye uhalisia. Kwakuwa wameshajadili kwa muda mrefu na sasa umesha kuwa usiku mnene, wanakubaliana kulala ili kesho wajaribu kulifanyia kazi wazo hilo.

Inaingia siku nyingine, Jumapili tulivu leo Tarick ameamka na wazo la kumpigia simu mama yake lakini Roby anamzuia na kumwambia kuwa kitendo cha kuwasiliana na mama kwenye simu kinaweza kutumiwa na askari kugundua mahali alipo, Tarick anaamua kusikiliza ushauri wa Roby. Baada ya hapo, Roby anajiandaa na kuwaaga kuwa kunashughuli za kikazi ambazo lazima akazimalizie weekend hii hivyo atawaacha hapo na kurejea kabla ya saa 8 mchana, Lakini anamwambia Zubery asiondoke mpaka yeye atakaporudi. Mara baada ya Rweyemamu, kugundua kuwa mtu aliyekuwa amempigia simu jana alikuwa na taarifa zinazohusiana na Tunda la moyo wake Brenda, Leo anaamua kusuka mpango kabambe wa kuhakikisha anamnasa mtu huyo na kupata taarifa zote zinazohusiana na Brenda . Rweyemamu anaita timu ya vijana wake, na kuwapa maagizo, kwa umakini na msisitizo mkubwa anasema, "Kuna mshenzi mmoja alinipigia simu jana, kauli yake ya mwisho inaonesha kuwa anataarifa za Brenda, sasa chukueni hii namba fanyeni juu chini mumpate huyu mtu, mnaweza kwenda hata TCRA wakawasaidia, hakikisha mnafanya kadri iwezekanavyo kutumia vizuri taaluma zenu ili kupata hizi taarifa. Jioni nataka jibu " baada ya Rweyemamu kutoa kauli hiyo na kuwakabidhi kazi hiyo kwa watu wake, anawaaga na kuelekea kwenye ofisi ndogo za bunge kwa ajili ya shughuli zake za kikazi.

Roby baada ya kutoka nyumbani kwake aliamua kuelekea nyumbani kwa wazazi wake ili angalau akawasalimie kwani zilikuwa zimepita siku kadhaa bila kuonana nao, kitendo cha Roby kupitia nyumbani kwa wazazi wake kinasababisha atumie zaidi ya masaa 4 jambo linalo mpelekea achelewe kwenda hospitali kama alivyokuwa amepanga. Lakini pamoja na kuchelewa Hii haiwezi kumfanya Roby aghairi safari hiyo, ambapo leo amepanga kujaribu kufikiria njia mbadala anayoweza kuitumia kumrudisha Brenda kwa Rweyemamu. Kwa Roby hili lilikuwa zoezi la nguvu kutokana na mawazo ya Rweyemamu ya kutumia upenyo huo kumnasa mtu aliyekuwa na Brenda, ambapo Rweyemamu aliamini kabisa kuwa atakuwa ni Frank, Bila kujua kuwa Frank tayari alikuwa ametangulia mbele za haki. Ni wakati huohuo makachero wake aliowatuma kufatilia ile namba ya simu walikuwa makao makuu ya mamlaka ya mawasiliano wakijaribu kuchonga mpango wa kumnasa aliyekuwa mmiliki wa namba hiyo.

Roby mara baada ya kutoka kwa wazazi wake sasa anaondoka moja kwa moja kuelekea hospitali, lakini akiwa njiani anapata wazo la kupitia supermarket angalau anunue chochote kwaajili ya Brenda. Kupitia supermarket na mlolongo wa foleni kwenye njia aliyopitia Roby, kwa pamoja vinapelekea Roby aingie hospitali saa nane mchana. Akiwa anakaribia kwenye geti la kuingia hospitali, Roby anapigiwa simu na mpenzi wake wa muda mrefu aliyekuwa akijulikana kama grace, binti huyu aliyekuwa na mwonekano rahisi na wakuvutia ni mwandishi wa habari katika television maarufu hapa nchini, simu hii aliyokuwa akimpigia baba watoto wake mtarajiwa ilikuwa na lengo la kumuomba ampitie nyumbani na kutoka nae kwa ajili ya mapumziko ya weekend. Kutokana na matatizo aliyokuwa nayo Roby anajaribu kuweka vikwazo kwenye ombi la grace, lakini sauti nyororo na ya ushawishi inamfanya Roby akubaliane na ombi hilo. Roby anakata simu na kuongeza umakini kwenye kupaki gari yake. Anapandisha vioo vyote vya gari yake na kuweka kila kitu sawa ndani ya gari. Kushuka tu nje ya gari Roby anazingirwa na jamaa watatu waliojazia mmoja wapo anatoa salamu na kusema, "Habari yako dokta!" Roby anapata mashaka juu ya watu wale lakini anaitikia kwa hofu kubwa, "Nzuri tu" Baada ya kuitikia salamu hiyo anajaribu kuwapotezea na kutaka kupita katikati yao ili aondoke, lakini njemba hizo za haja zina mzinga asipate njia na mmoja wao anatoa kitambulisho na kumuonesha Roby huku akisema, "Sisi ni maafisa usalama, tunaomba kuondoka na wewe muda huu kwaajili ya mahojiano mafupi kituoni".

Mpenzi msomaji, Makachero wa Rweyemamu walipofika kwenye ofisi za mamlaka a mawasiliano waliweza kupata msaada mkubwa kwani waliunganishwa na watu wa mtandao wa simu aliyotumia Roby kisha watu wa mtandao wakaweza kumtambua wakala aliyekuwa amesajili namba ile iliyotumiwa na Roby. Hivyo basi kwakuwa siku aliyosajili Roby ni watu watatu tu waliokuwa wamesajili laini siku hiyo kwahiyo haikumpa shida yule wakala kumkumbuka dk Roby. Wakala akawaelekeza polisi jinsi ya kumpata dokta Roby huku akiwaambia kuwa anawasiwasi kuwa yeye ndie alie sajili kwa jina lililokuwa likionekana kwenye utambulisho wa line ile. Huo ndo ulikuwa ujanja uliowawezesha askari kumnasa Roby. Sasa tuangalie pamoja na askari kumnasa Roby, Je wataweza kuthibitisha kuwa yeye ndiye aliyesajili laini na hatimaye kumtia hatiani? Hili linaweza kuwa baraa kubwa zaidi kwenye Tamthilia yetu kwani Roby akikutwa na Brenda ataingizwa kwenye mashtaka ya kushirikiana na Gaidi Most Wanted Frank Rwambano lakini pia anaweza hata kuhusishwa na Kupotea kwa Tarick, na hivyo kufanywa mshukiwa namba moja na kutakiwa kuisaidia polisi kuwatafuta watu hao. Nini kinataka kutokea!? Watch Out episode Number 15.



Nawashukuru sana kwa michango mnayofanya kwaajili ya kufanikisha kupata computer nzuri zaidi ya kuandalia kazi hii. Kama ambavyo Beth alikuwa amependekeza tayari watu wawili wameanza kuchanga kesho nitasemakiasi kilichopatikana. Sehemu nzuri ya simulizi hii bado sijaifikia kabisa tujitahidi kuchangia ili niboreshe uandishi wa tamthilia hii na nyingine nzuri zaidi zitakazokuja baada ya hii.

Lets Go Blaki Womani....
 
Mkuu safari njema na afya njema pia, ule machungwa kwa wingi upate nguvu ya kuandika tamthilia hii nzur sana
 
Duh! dokta Roby alivyo muoga sijui itakuwaje??? Frank alimuachia kibarua kizito sana, asante sana Msamiati kwa story tamu ila leo kalikuwa kafupiiiii!!!

Wadau tuendelee kuchanga zaidi mimi nimeongeza tena na nitachanga tena na tena,mwenye 500,1000,5000,10000 tuchange jamani,haba na haba hujaza kibaba,tumsaidie kijana atoke amethubutu na anaweza,kutoa ni moyo na wala si utajiri. Mungu awabariki sana pale mnapotoa apaongeze mara dufu.
 
Last edited by a moderator:
The Second Door- Episode 15

Habari gani marafiki, ni siku nyingine tulivu kabisa nikiwa ndani ya jiji la tanga na nafasi murua ya kuendeleza burudani hii ndani ya tamthilia ya the second door. Leo ni hatua nyingine katika Episode ya 15 ambapo tutaendelea na tukio la tarick kuchukuliwa na polisi kwa ajili ya mahojiano.


Baada ya kumuomba dokta roby kwa heshma na taadhima ili wakafanye nae mahojiano, dokta roby anakubaliana nao lakini anawaambia kuwa lazima aingie ofisini na kuweka mazingira ya kazi vizuri, itagharimu kama nusu saa hivi kisha wanaweza kuongozana. Askari walilazimika kufata matakwa ya dokta Roby kutokana na wadhfa wake katika hospitali hiyo ya taifa na hata angeamua kukataa kwenda nao wasingeweza kutumia nguvu. Lakini dokta Roby kwa kuwa hakuwa na uhakika kwamba nini kilikuwa kinaendelea basi hakuona umuhimu wa kuzozana nao wale askari. Roby anaweka mazingira ya ofisini kwake vizuri na kuondoka na kuondoka nao, wakiwa wanataka kuondoka wale polisi wanataka watumie gari yao pamoja na Roby lakini Roby anakataa na kuwaambia kuwa yeye atatumia gari yake wakutane kituo cha polisi Oysterbay sehemu ambayo walitaka kufanya nae hayo mahojiano.



Baada ya kufika kituoni hapo, Roby anaingizwa kwenye chumba cha upelelezi kisha askari wanaanza kumhoji kuhusiana na Laini ya simu iliyokuwa imesajiliwa siku tatu zilizopita kwa utambulisho wa Hemedi Razack. Roby anaonesha kushtushwa na mshangao mkubwa kutokana na kuhusishwa na line hiyo na kwenye majibu yake anasema, "Hivi nyinyi mnashindwa kutumia akili ! mimi sio Hemedi Razack!? na siku mnayodai hiyo line ilisajiliwa mimi nilikuwa na ratiba ya wagonjwa kutwa nzima nisingeweza kupoteza muda kuanza kusajili laini, tena kwa majina mengine, kwanza laini za kazi gani!? Wakati mimi nina laini za mitandao yote!" Baada ya kumaliza kuongea maneno hayo askari mmoja anamuuliza Roby, "Sawa dokta, lakini wewe ulifika kwenye ofisi za wakala wa usajili pale nje ya hospitali!", Roby anajibu swali hilo kwa kusema, "Yaaa nilifika! kisha nikanunua vocha na kuondoka haikuchukuwa hata dakika moja sasa nashangaa mnaponiambia kuwa nilifanya kazi ya kusajili lain". Pamoja na maswali mengi ya kumbana dokta Roby, majibu aliyokuwa akiyatoa kwa kujiamini kabisa yanapelekea askari wale waamini kuwa Roby hakuwa akifahamu chochote kuhusiana na ile lain. Askari wanaona kuwa hakuna haja ya kuendelea kumpotezea muda dokta Roby kwani hata yule kijana anayefanya kazi ya usajili wa line alishawaambia kuwa hakuwa na uhakika kuwa line ile ilisajiliwa na dokta huyo.


Roby anamaliza mahojiano na wale askari kisha anapanda kwenye gari lake na kurudi hospitali. Akiwa njiani Roby anampigia simu zubery na kumpa taarifa kuwa atachelewa kidogo kurudi hivyo aendelee kumsubiri. Roby anafika hospitali na kwenda kumtazama Brenda baada ya hapo anaacha maagizo kuwa kesho jumapili atakuja kumchukuwa. Muda wa kazi umepita sana, Roby anamua kufunga siku na kurudi nyumbani. Baada ya kufika nyumbani anapumzika kidogo kisha anakaa chini rasmi pamoja na Tarick na zubery kwa ajili ya kujadili ni jinsi gani Tarick anaweza kujipandikiza kwenye familia aliyokuwa akiizungumzia zubery. Baada ya kupanga kwa zaidi ya saa nzima mpango huo unaonekana kuwa kabambe japokuwa unaonekana kuwa na baadhi ya upungufu lakini mapungufu yake hayawezi kufanya usitekelezeke. Pamoja na kwamba walijadili mpango huu kwa undani kabisa lakini Roby na Zubery kila mmoja alikuwa na haraka ya kumaliza mazungumzo yale ili aingie kwenye starehe za weekend, kwani zubery nae alikuwa na appointment na Mchumba wake jioni ya leo kama ilivyokuwa kwa kaka yake Roby.


Mara tu baada ya kikao hicho kuisha zubery anakuwa wa kwanza kuaga na kuondoka. Baada ya hapo Roby anamwambia Tarick, "Tarick! Ukibaki peke yako utakua mpweke sana, Jiandae Twende wote…" Tarick anajibu huku akionesha furaha, "Usijali kawaida tu, mimi utanikuta" maneno hayo ya Tarick yanampa uhuru Roby wa kujiandaa haraka ili amfate mchumba, hata hivyo kitendo cha Tarick kukataa safari hiyo kinaonekana kuwa na faida kwa Roby kwani isingekuwa vizuri kuongozana na Tarick kisha wakifika Tarick abaki kumkodolea macho wakati akiwa kwenye starehe na mpenzi wake, japo kuwa kwa upande wa Tarick kukataa huko kulikuwa na maana kubwa zaidi ukiachilia mbali maadili ya kiimani aliyofunzwa kutoka kwenye familia yao. Roby anamaliza kujiandaa kisha anampigia simu msichana wake halafu anamtaarifu kuwa ajiandae kwani atampitia ndani ya dakika chache zijazo. Baada ya hapo Roby anaondoka na kumuacha Tarick akiwa peke yake. Muda huu tayari ilikuwa imehitimu saa moja na nusu, na giza lillikuwa limetanda japokuwa mataa yaliyokuwa kila kona ya jiji na kwenye mabarabara yanaendelea kuangaza na kutoa nuru inayowasaidia watu waliokuwa katika mizunguko mbali mbali ya weekend. Tarick Baada ya kuhakikisha kuwa Roby ameondoka kabisa sasa unakuwa ni muda muafaka wa kutekeleza lengo lake kubwa la kukataa kwenda na Roby.



Zubery nae akiwa na mpenzi wake aliekuwa anaitwa qeen, msichana ambaye zubery alikuwa akimpenda kiasi kwamba alikuwa tayari kufanya lolote kwa ajili yake. Wakiwa kwenye mahaba na starehe binti huyu anasema, "Sio kwamba sitaki kuolewa na wewe, ila baby… mimi sitaki maisha ya familia yetu yawe hapa Tanzania. Nakama tukishindwa kwenda kuishi Europe basi hata Johannesburg hapa hapa Africa" Sauti nyororo na ya kubembeleza aliyokuwa nayo qeen ilikuwa ikifanya maneno yake yaingie masikioni kwa zubery kama amri bila kufanyiwa upembuzi wowote, binti huyu aliyekuwa na mitego ya kila aina alifanikiwa sana kuwa na ushawishi kubwa kwenye maisha ya Zubery. Qeen anazidi kugongelea msumary kwenye maneno yake kwa kusema, "Baba yako wewe anauwezo, Dada yenu mkubwa yupo spain mwaka wanne huu kaka yako bosi mkubwa tu kwenye hospitali ya taifa, wewe ukiamua unaweza kuisha mahali popote duniani hapa, au haunipendi!?" Zubery anamtazama Qeen na kumjibu, "Usiniulize hilo swali Qeen utaniua!" Qeen anadakia na kusema, "Ndio maana yake!". Roby anasema, "Ok kuna ishu moja nimefikiria inabidi nifanye, nitapata pesa zakutosha. Mwisho wa mwezi huu tutaenda Johannesburg tutakaa mwezi mzima ili tuangalie kama itakuwa ni sehemu nzuri ya kuishi au tutafute mahali pengine" kauli hiyo ya Zubery inamfanya Qeen atoe tabasamu zito na kumkumbatia zubery kwa furaha, zubery anasema, "Mimi nipo tayari kuishi mahali popote ilimradi tu niwe na wewe malaika wangu" Qeen anajibu kwa kusema, "Zed K wangu… naomba usibadilishe mawazo ya kuwa na mimi tafadhari, nimesha kuwa mtumwa wa hisia kwenye penzi lako" Maneno hayo yanampa faraja ya kipekee Zubery, anajibu kwa bashasha ya hali ya juu akisema, "Usijali Malaika mimi ninaishi kwa ajili yako".



Msukumo mkubwa wa kutaka kuishi maisha ghari zaidi anaoupata Zubery kutoka kwa Qeen, unafungua milango mipya ya fikra za kutumia fulsa ya Zubery kumkamatisha Tarick kwa dau nono zaidi kutoka katika jeshi la polisi. Anajaribu kufikiria na kuwaza lakini anagundua kuwa hakuna kitakachoweza kumzuia kama ilivyotokea awali, na ukizingatia kuwa safari hii yeye ndie anaetegemewa kuweka sawa mchongo wa kumficha Tarick, hivyo anaweza akamkamatisha kiulaini bila kujulikana na mtu yoyote kama yeye ndie alie fanya mpango huo.



Roby naye akiwa na mrembo wake weekend hii, kwenye moja kati ya hoteli za kifahali jijini Dar es salaam, wakiwa wanapata vinywaji huku wanabadilishana mawazo ya hapa na pale, wakati wanaendelea kuongea Roby anaona cd kwenye mfuko wa Grace anafungua na kuitazama kisha anauliza, "Ni cd ya kitu gani hii?" Grace anajibu, "ni video ya hafla ya kuvalishana pete ya uchumba kati ya kaka yangu na mchumba wake" Roby anashangazwa na taarifa hiyo, kisha anauliza, "Hujawahi kuniambia kuwa una kaka!" Grace anajibu, "ni kweli, lakini kaka ninae japokuwa ni kama vile hayupo!" Roby anaendelea kuuliza, "Kwanini!?" Swali hili linamtia majonzi sana Grace, na kuonesha kuwa pengine jibu lake lilikuwa na taarifa zinazohuzunisha, anapiga kope na kuruhusu chozi lidondoke kwenye jicho lake la kushoto anafuta hilo na kusema, "Ni stori ndefu" majibu ya Grace na jinsi alivyokuwa akipokea yale maswali vinamfanya Roby atake kujua zaidi, anamuuliza, "Amekufa?" Grace anajikaza na kujibu, "Hapana ni mzima lakini hayupo pamoja na sisi. Alipomaliza tu chuo baada ya kumvalisha pete mchumba wake na kumleta nyumbani alipata dili la biashara kwenye migodi ya mwadui, tangu aondoke ni miaka miwili na nusu sasa hatuna taarifa zozote, tumesha mtafuta kwa kila njia imeshindikana tumeamua kumuachia mungu". Grace anamwambia maneno hayo Roby huku akiwa na majonzi mazito, hata hivyo majonzi ya Grace Hayakati shauku ya Roby kutaka kujua zaidi na zaidi juu ya shemeji yake huyo.Maswali mengi ya Roby yanaishia kwa kumuomba Grace ile cd ili akaitazame. Cd hiyo ilikuwa imerekodi matukio ya siku nzima iliyofanyika hafla ya uchumba, ilijumuisha picha za video zilizopigwa asubuhi, mchana, jioni kwenye hafla mpaka usiku huku mlengwa mkubwa kwenye video zote hizo akiwa ni kaka yake na Grace ambaye hajulikani alipo. Wakiwa wanaendelea na mazungumzo hayo huku mziki wa taratibu ukiendelea kupiga kwa sauti ya chini na kuwaruhusu waliokuwa na hamasa ya kucheza waendelee taratibu kwa mbaali Roby anamuona Rweyemamu naye akiwa eneo hilo.
Kumbe Rweyemamu nae weekend hii aliamua kumtoa out shemeji yake ambaye ni dada yake na Brenda na mahali walipokuwa wakiendelea kuburudika na muziki laini ndio hapa hapa alikuwa Roby na mpenzi wake.



Tukirudi kwa Tarick, yeye baada ya Roby kuondoka anaamua kutekeleza wazo lake la kwenda kumuaona mama yake ili kuhakikisha kuwa alikuwa salama, lakini pia angalau akamtoe hofu kuwa yeye bado ni mzima na yupo huru. Bila kujua kuwa nyumba yao yote ilikuwa imewekwa kama mtego wa kumnasia, anajiandaa na kufunga safari huku akiwa amepiga mahesabu kuwa safari hiyo haitamchukuwa zaidi ya saa moja. Safari ya Tarick inampeleka mpaka nyumbani kwao, kwakuwa alishaambiwa na Roby kuwa askari walikuwa hawakauki pale nyumbani kwao Tarick anaamua kusimama kwenye fance ya nyumba ya jirani ili aweze kutizama mazingira na kuangalia kilichokuwa kikiendelea kwenye nyumba yao. Wakati akiendelea kuangalia huku na huku kwa umakini mkubwa, anatokea askari kisha anamstua na kumpiga na kitako cha bunduki, sehemu ya juu ya jicho inachanika na kuanza kumwaga damu nyingi, yule askari anamshindilia Tarick na teke huku akisema, "Pumbavu mkubwa unanyata nyata nini hapa". Mara wanatokea askari wengine watatu na kumzingira Tarick, Polisi wanamburuza mpaka mbele ya mlango wa nyumba yao, kisha wanaanza kumpa kisago huku wakimsachi na kuchukua kila alichokuwa nacho, baada ya gumzo kuongezeka pale nje na Tarick kupiga kelele kutokana na maumivu makali. Mama yake akiwa ndani anasikia sauti ya kilio inayogonga kuta za moyo wake. Anatoka mbio mbio kuja kushuhudia kiichokuwa kikiendelea pale nje.


Kitendo cha mama kufika eneo lile macho yake yanagongana moja kwa moja na ya mwanae Tarick, Jicho linamtoka mama, mdomo unapatwa na ukakasi machozi yanamjaa machoni lakini anayadhibiti yasidondoke, kisha anaamua kujizuia kabisa baada ya kugundua kuwa askari walikuwa hawajamshuku kuwa waliyekuwa wanampiga ndie waliyekuwa wanamuwinda usiku na mchana. Askari mmoja anamchimbia mama mkwara na kumwambia, "We bibi ingia ndani". Baada ya mama kuambiwa kauli hiyo kwa ukali, anapiga hatua taratibu kurudi nyuma na kuingia ndani. Baada ya askari hao kufanya unyama wao kwa kumpiga na kumuibia Tarick huku wakisahau jukumu lao la kumsaka gaidi, wanaamua kumpakia Tarick kwenye Diffender na kuondoka nae. Baada ya kufika mbali kabisa wanamshusha na kumuacha aondoke zake.



Ok mimi niishie hapa katika episode hii ya 15. Ungana nami katika episode ya 16, ili uweze kujua kama jitihada za kumuwezesha tarick aendelee kuishi Nchini Bila kujulikana zitafanikiwa mbele ya Zubery. Episode hii nilianza kuiandika Dar na Nimeimalizia hapa Tanga. Sina computer huku lakini nitajitahidi niisogeze simulizi hii angalau hadi episode ya 17 au ya 18 kabla sijarudi dar.
Blaki Womani tunaendelea..........


Mwisho niwashukuru wapenzi wa tamthilia hii ambao wameamua kuchangia ili kufanikisha upaitikanaji wa computer nzuri itakayorahisisha uandaaji wa story hii na zingine zitakazokuja wamechangia watu 2 na imepatikana sh 25,000/=

Kama unafatilia simulizi hii jitahidi uchangie hata kidogo ili kuiwezesha

 
Hili li Zubery mbona limbea sana na lina tamaa??? Maskini Tarick naye mbishi huyu!! ila siyo yeye ni upendo alionao kwa mama yake.duh!! asante Msamiati,usijali haba na haba hujaza kibaba,Wadau tuchange tena na tena,kidogo kidogo kijana apate laptop,utafika tu japo utachelewa.....
 
Last edited by a moderator:
wamama kwa ubahili .....kumbe ni wawili tu mliochangia?
anyway big up msamiati na wote mnaompa moyo.....
huu ni ubunifu mzuri ingawa mimi sio mshabiki wa tamthilia
 
The Second Door- Episode 16

Baada ya pilika pilika na purukushani za weekend, tunaingia katika siku mpya, ikiwa ni jumapili tulivu waumini wa madhehebu ya kikristo wakiwa kwenye movement za hapa na pale kuelekea kwenye nyumba za ibada na wengine ambao jana walikesha kwenye maeneo tofauti tofauti ya kujirusha, wakiwa bado na uchovu unaotokana na starehe za usiku kucha. Bila kusahau waliojaribu kufanya majaribio hatari kama Tarick, yeye asubuhi ya leo anaamka huku sehemu ya juu ya jicho ikiwa imechimbika kabisa. Kwa mara ya kwanza anaonana na robi, asubuhi hii Roby anastaajabu kuona jeraha kubwa kiasi kile usoni kwa Tarick wakati jana alimuacha akiwa mzima. "Imekuwaje Tarick!?" Tarick anajibu, "ilikuwa usiku wakati naenda kujisaidia nikajigonga mlangoni" Roby anasogea ili kumuangalia kwa karibu na kugundua kuwa lile jeraha lilikuwa kubwa. Kabla ya kufanya chochote dokta Roby itabidi amshone na kumpa matibabu.

Baada ya kumaliza kushughulikia lile jeraha wanakunywa chai huku huku wakitazama cd ambayo Roby alikuwa ameichukuwa jana kwa Grace. Leo walikuwa na makubaliano kuwa Zubery angekuja na Details zote ambazo Tarick inabidi azitumie. Kwajinsi walivyopanga, ilibidi Tarick aanze maisha hayo mapya kuanzia jumanne, japokuwa hili lilikuwa jaribio la hatari kabisa na jaribio ambalo lingeweza kumkamatisha Tarick kiulaini, lakini kwasasa ndio njia pekee ambayo endapo ikifanikiwa basi Tarick ataendelea kuishi bila shida kama watu wengine. CD wanayotizama muda huu ni ndefu sana, hivyo Roby anamwambia Tarick aendelee kuitazama ili yeye aende akamalizie kibarua cha kumrejesha Brender kwa Rweyemamu.

Zubery nae akiwa amedhamiria kabisa kumuuza Tarick, lakini safari hii akitumia umakini mkubwa ili asije kuingia kwenye matatizo kama yaliyomkuta kwa Frank, leo amefanikiwa kupata mawasiliano ya secretary ofisi ya kamanda mkuu kanda maalum ya dar es salaam, wanapanga kukutana kwaajili ya mazungumzo yasiyokuwa ya kiofisi ili watizame ni jinsi gani wanaweza kushirikiana kutengeneza pesa kupitia biashara hiyo ya kumuuza Tarick. Wanafanikiwa kukutana, kisha yule secretary anamhakikishia zubery kuwa dili hilo linaweza kumuingizia zaidi ya shilingi milioni themanini bila wasi wasi wowote kwani mpaka muda huu serikali inapoteza mamilioni ya pesa kila kukicha kwaajili ya kulisaka gaidi hilo lililoponyoka kutoka kwenye hukumu ya kifo. Mazungumzo hayo yanafana, hatma yake wanaishia kwa kukubaliana kuwa Huyu secretary ataenda kuzungumza na jenerali mwamkonge ili kujua kama jeshi la polisi litakuwa tayari kutoa Shillingi million 100 kwa mtu atakae fanikisha kukamatwa kwa gaidi hilo. Mazungumzo hayo yanamalizika huku secretary akimuahidi Zubery kuwa, kama kweli anauhakika anaweza kufanikisha zoezi la kukamatwa kwa mhalifu huyo basi hizo pesa zisingekuwa tatizo kabisa kutolewa, kwani kunahofu kubwa kuwa kitendo cha gaidi hilo kuingia uraiani kunaweza kupelekea tukio la mauaji makubwa zaidi kuliko yale yaliyofanywa arusha.

Tukirejea kwa dokta Roby, yeye anaenda mpaka hospitali na kumchukuwa Brenda kisha kwa kutumia line nyingine kabisa anampigia Rweyemamu na kusema, "Kishoka naongea.. Tunaweza kufanya makubaliano?" Rweyemamu kusikia swali hilo anadharau na kukata simu. Lakini ndani ya sekunde chache anashtuka na kugundua kuwa ile ilikuwa ni sauti aliyo zungumza nayo mara ya mwisho, Rweyemamu anaamua kumpigia simu swaiba wake kamanda mwamkonge na kumpa taarifa, mwamkonge unaunganisha simu hiyo kwenye mtandao wa polisi na kuwapa oda ya kufatilia mazungumzo yote, kisha anamwambia Rweyemamu apige simu ya huyo mtu bila kukata simu yake. Rweyemamu anafanya hivyo. Wakati Roby akiwaza kitu cha kufanya mara simu yake inaita, anaipokea kisha Rweyemamu anamwambia, "samahani, naomba nikufahamu kisha uniambie ulikuwa unahitaji makubaliano gani na mimi", Roby anajibu, "Sina shida ya kufahamiana na wewe ila nataka kufahamu tu kama makubaliano ninayotaka yanaweza kukufaa" Rweyemamu anasema, "Ok, sema nakusikiliza…" bila kujua kuwa mazungumzo yao yalikuwa yakifatiliwa kwa makini na makao makuu ya jeshi la polisi, Roby anasema, "Kama utafanya kila nitakachokuelekeza, leo unampata Brenda, ukifanya kinyume ukajaribu kuleta ujanja wowote, utampata akiwa robo yake, na sehemu inayobaki hautaiona maisha yako yote" Roby anaamua kumtisha Rweyemamu ili asijaribu kushirikisha polisi kama alivyofanya awali, Roby anaendelea, "Kama unamtaka akiwa hai, fanya kama tutakavyokubaliana, ila kama kichwa chake ndio muhimu zaidi kwako jaribu kunizunguka" Rweyemamu anaanza kuogopa maneno ya Roby na kuhisi kuwa akifanya masikhara anaweza kupoteza uhai wa mpenzi wake, Rweyemamu anamkatisha Roby na kusema, "Nipo tayari kufata makubaliano yoyote tafadhari naomba nimpate akiwa mzima… hata kama unahitaji kiasi chochote cha pesa nipo tayari kukupatia" Roby anasikiliza kwa makini na kumwambia, "Hakuna kunizunguka!" kauli hiyo inamfanya Rweyemamu ajibu kwa kutetereka, "Naapa sitakuzunguka!" Roby nae bado hajiamini kabisa kwenye tukio analoenda kulifanya anasisitiza kwa kusema, "No trick no Game!" Rweyemamu kitete kinamzidi anaamua kumwambia Roby asubiri kwanza, kisha anakata simu ya generali mwamkonge na kusababisha kukatika kwa mawasiliano yaliyokuwa yakiunganisha mazungumzo hayo na makao makuu ya polisi. Baada ya hapo Rweyemamu anasema, "Sikia kishoka, I real need that girl alive" Baada ya Rweyemamu kuzungumza kauli hiyo, Roby hakutaka kuendelea na mazungumzo yoyote moja kwamoja anamwambia, "tukutane kwenye ufukwe wa msasani saa tisa kamili hakikisha unakuja peke yako utanikuta mbele ya soko la samaki".

Tukirudi nyumbani Tarick yeye alivutiwa sana na ile cd aliyoachiwa na Roby, akajikuta anaitizama kwa mara ya pili, wakati akiwa anamaliza kuitazama mara anaingia Zubery, wanasalimiana kwa furaha kisha Zubery anatoa picha za Ramson Sanga jamaa ambaye Tarick alitakiwa kujifanya ndio yeye. Zubery anaanza kumuelezea Tarick tabia na muonekano aliokuwa nao Ramson Sanga, Zubery anamuelekeza Tarick jinsi Ramson alivyokuwa akiongea, vitu alivyokuwa akipendelea, historia fupi ya maisha yake pia anamuelezea kuhusu ndugu na jamaa wa karibu waliokuwa wanamzunguka. Zubery anajitahidi kumpa Tarick details nyingi kadri awezavyo, hii yote ilikuwa ni katika kuhakikisha familia ya Ramsoni haimgundui Tarick kwa njia yoyote ile.

Upande wa pili mchezo wa makubaliano baina ya dokta Roby na Rweyemamu unaendelea. Hofu kubwa ya kumpoteza Brenda inampelekea Rweyemamu afanye kama anavyoagizwa na Roby, na katika kuhakikisha anatekeleza vizuri kabisa makubaliano yao Rweyemamu anaamua kumuacha mpaka dereva wake ambaye alikuwa akiongozana nae kila mahali na kuendesha gari mwenyewe. Kwa Roby yeye mambo yanakuwa tofauti kidogo, kama unavyojua mpenzi msomaji, Roby yeye siku zote amekuwa ni mwoga sana kuingia katika matatizo, hivyo saa zote woga wake umekuwa ukimpelekea awe mtu asiyemwamini mtu yoyote, na yeye alijiwekea kauli mbiu binafsi inayosema, kama imani inarisk hakuna sababu ya kumuamini mtu. Kwa kauli hii Roby alikuwa akimaanisha kuwa endapo ikitokea mazingira yatakayomtaka atumie imani, basi atamwamini mtu kama kitendo cha kumuamini hakitakuwa na risk yoyote lakini endapo imani hiyo itarisk basi hatamwamini mtu, kwa kutumia fikra na mawazo haya Roby anaamua kutoamini kuwa Rweyemamu hatamuwekea mtego hivyo anaamua kwenda mpaka kwenye ufukwe wa bahari ya hindi eneo la msasani, kandokando ya soko mahali ambapo walipatana na Rweyemamu kuwa wakutane, kisha kwa uangalifu mkubwa anamfikisha hapo Brenda na kumshikisha bahasha ya kaki ambayo ilikuwa na ujumbe wa Frank aliotakiwa kuupata Rweyemamu. Baada ya kuhakikisha ameweka mazingia vizuri kabisa Roby anaenda kujificha mbali kabisa na eneo hilo na kuendelea kuwasiliana na Rweyemamu. Saa tisa kamili kama walivyokuwa wamekubaliana Rweyemamu alifika eneo hilo kisha Roby anamuelekeza mpaka alipokuwa amekaa Brenda, Mara baada ya Rweyemamu kumuona Brenda akiwa amekaa kwenye lundo la mchanga wa ufukweni, anamkimbilia na kupiga magoti mbele yake, Rweyemamu anamtizama Brenda huku akiwa haamini kabisa kama ndio yeye, anashindwa kuamini kuona msichana mrembo aliyemliza akiamini tayari amepoteza maisha hatimaye anarudi mikononi mwake akiwa salama. Anajaribu kumuongelesha, lakini Brenda anaishia kumtazama tu na kumkodolea macho kama ndondocha. Rweyemamu anamkumbatia kwa furaha, furaha hiyo inazidi mpaka inapitiliza na kumfanya Rweyemamu aanze kulia. Wakati tukio hilo likiendelea katika hali isiyokuwa ya kawaida, wanatokea askari ambao walikuwa wakimfatilia Rweyemamu kwa siri ili kuhakikisha usalama wake, na hii ni amri ambayo ilikuwa imetolewa moja kwa moja kutoka kwa jenerali mwamkonge mara baada ya kuona Rweyemamu amekata simu na kuamua kufanya makubariano na gaidi. Intellejensia ya jenerali mwamkonge ilikuwa ikimuonesha kuwa Rweyemamu angeweza kukutwa na jambo lolote baya.

Rweyemamu anambeba Brenda kutoka pale chini, askari kuona mheshimiwa professa Rweyemamu akiwa anataka kuhangaika kumnyanyua Brenda wanataka kumsaidia lakini anawazuia. Bila kupoteza muda Rweyemamu anamchukuwa Brenda pamoja na ile bahasha kisha anaenda nae moja kwa moja mpaka kwenye hospitali binafsi ya SANITAS. Baada ya Rweyemamu kumfikisha Brenda kwenye hospitali hiyo madaktari wanaanza kazi ya kukagua afya yake mara moja wakiwa wanaendelea na zoezi hilo, Rweyemamu anaitaarifu familia ya Brenda kuwa amefanikiwa kutimiza ahadi yake ya kumpata Brenda na yupo nae hospitali ili kucheki kama kuna athari zozote za kiafya alizozipata. Roby baada ya kufanikisha zoezi la kumkabidhi Brenda bila shida anapiga dua kimoyo moyo na kuwaza kuwa zoezi moja tu lililo salia ambalo lilikuwa ni kumficha Tarick usoni kwa adui yake.

Huku nyumbani Tarick na Zubery wanahakikisha wamechambua vizuri kila Nyanja ya maisha mapya atakayoenda kuyaanza Tarick, na kuhakikisha Tarick anaelewa vizuri kila alichotakiwa kuelewa na kukariri kila alichokuwa anatakiwa kukariri ili mpango usije ukashindikana. Zubery anafanya jitihada zote hizi ili kuhakikisha kuwa itakaposfikia dakika ya mwisho ya biashara yake haramu anayotaka kufanya na jeshi la polisi, basi kaka yake asijue kama yeye ndiye aliyemuuza Tarick. Baada ya kuona muda umeenda sana na hakuna dalili ya Roby kutokea Zubery anaamua kuondoka na kuahidi kuwa atarudi kesho kwaajili ya kuweka sawa safari ya Tarick kuingia kwenye maisha mapya. Baada ya Zubery kutoka tu anapishana kidogo na kaka yake Roby kwani Roby naye ndio alikuwa anarudi. Zubery akiwa njiani kurudi nyumbani, anapokea simu ya secretary kisha anamwambia kuwa amesha zungumza na Generali na mchakato mzima upo sawa, kwahiyo wao upande wa polisi walikuwa wanamsikiliza yeye, ili awape muelekeo wa kumtia nguvuni gaidi anaesakwa usiku na mchana baadaya ya kuporonyoka hukumu ya kifo.

Roby anaingia nyumbani kwake kwa furaha, nakumkuta Tarick naye akiwa na furaha ya kwenda kuishi kwenye maisha mapya ya uhuru na amani. Tarick anamsimulia Roby kuwa Zubery alikuja, lakini pia anamsimulia hatua waliyofikia kwenye zoezi la kujibadilisha. Hatua nzuri waliyofikia haioneshi kumfurahisha sana Roby, baada ya kugundua hilo Tarick anamwambia Roby, "Kama unahisi kunatatizo ni vyema ukasema dokta ili mpango huu usije ukashindikana baada ya kupoteza nguvu nyingi". Roby anamtazama kwa umakini Tarick na kusema kwa msisitizo, "Hakuna shida yoyote Tarick, Lakini mimi simuamini kabisa Zubery".

Oooooookey wasomaji wangu wapendwa, huu ndio mwisho wa Episode ya 16 ya tamthilia hii ya the second Door. USIKOSE kufatilia Episode ya 17 na ya MWISHO kwenye SEASON 1 ya Tamthilia hii ya kuvutia, Ambapo tutaenda kuona hatma ya Brenda na Tarick.

Mwisho niwashukuru wapenzi wa tamthilia hii ambao wameamua kuchangia ili kufanikisha upaitikanaji wa computer nzuri itakayorahisisha uandaaji wa story hii na zingine zitakazokuja wamechangia watu 2 na imepatikana
sh 25,000/=


TigoPesa: 0712494761.
MPesa: 0754955566.
Kama unafatilia simulizi hii jitahidi uchangie hata kidogo ili kuiwezesha.


 
UPDATES:

Niwashukuru wapenzi wa tamthilia hii ambao wameamua kuchangia ili kufanikisha upaitikanaji wa computer nzuri itakayorahisisha uandaaji wa story hii na zingine zitakazokuja wamechangia watu 3 na imepatikana
sh
45,000/=


TigoPesa: 0712494761.
MPesa: 0754955566.
Kama unafatilia simulizi hii jitahidi uchangie hata kidogo ili kuiwezesha.

 
Back
Top Bottom