The Second Door (Tamthilia)

The Second Door (Tamthilia)

Ipigie kura simuizi hii

  • Nzuri Sana

    Votes: 9 56.3%
  • Inafaa Kusomwa

    Votes: 5 31.3%
  • Yakawaida

    Votes: 0 0.0%
  • Sijaisoma

    Votes: 2 12.5%

  • Total voters
    16
kuna kitu kinagoma katika maisha ya uhalisia! prof ryeyemamu ni mwanasheria mkuu hivi kwa akili ya kawaida mtu hadi aufikie uprof na kuwa mwanasheria mkuu wa serikali atakuwa na miaka mingapi? wakati huo huo baba yake still ni mwanasiasa maarufu

najiuliza hawa baba na mwana wanatofauti ya umri gani?
 
kuna kitu kinagoma katika maisha ya uhalisia! prof ryeyemamu ni mwanasheria mkuu hivi kwa akili ya kawaida mtu hadi aufikie uprof na kuwa mwanasheria mkuu wa serikali atakuwa na miaka mingapi? wakati huo huo baba yake still ni mwanasiasa maarufu

najiuliza hawa baba na mwana wanatofauti ya umri gani?

Samahani sana Bosi nilifanya Typing Error! Baba yake ni mtu aliekuwa mwanasiasa maarufu siku za nyuma.
 
Dah!! Kiongozi hii story ni nzuri mno!! Hongera sana kwa kutambua kipaji chako!! Big up mkuu....
 
Habari gani marafiki, ni wakati maridhawa kabisa tunapoenda kuendelea na Episode Namba sita ya simulizi yako uipendayo ya The Second Door. Na ukumbuke tu kuwa katika Episode namba sita tuliwaona jamaa wawili kutoka kwenye kundi la Rweyemamu wakiwa upande wa ndani wa geti la kuingilia kwenye eneo hilo la kanisa, wakiwa kama watu ambao walikua wakifanya doria hivi. Jamaa hawa wawili walikua wametangulizwa eneo hilo ili kuthibitisha na kuyazoea mazingira kabla wenzao hawajafika na kuingia kwenye mishen Rasmi. Wenzao ilikuwa wafike mapema tu lakini Foleni iliyokuwa imetokana na msafara wa viongozi wa kitaifa iliwafanya wachelewe kidogo.
Frank naye kipindi alichotoka ndani ya supermarket moyo wake ghafla ulijawa na hofu kubwa, ambayo ilitokana na kuhisi kwamba kundi la Rweyemamu linaweza kufika pale Hosteli na kuleta shida. Tatizo kubwa la Frank lilikuwa ni kwa yule daktari wake,Frank aliamini endapo wangemkuta na Brenda basi lazima wangemtia hatiani na kumbambikia makesi kama jinsi ilivyokuwa kawaida yao. Mpenzi msomaji Kwa upande mwingine Jambo ambalo lilipelekea frank ahakikishe Brenda anapona, ilikuwa ni kutokana na kuamini kuwa, Lazima Brenda alikuwa na taarifa muhimu zinazoweza kumsaidia afahamu ni kitu gani ambacho anaweza kukifanya kwa haraka haraka ili amuokoe Tarick. Mbali na hayo kutokana na mazingiza aliyoyakuta kwa Brenda siku ile ya tukio, Frank aliamini moja kwa moja kuwa kunamtu ambae alikuwa akifanya harakati za kumuangamiza Brenda na harakati hizo alihisi moja kwa moja ziliwezeshwa na Profesa Rweyemamu na pengine ilikuwa kwa lengo la kumzuia Brenda asiweze kudhihirisha kuwa Tarick hakuwa na hatia.
Kutokea Super market Frank alitumia Pikipiki kuelekea Hostel, Hivyo akawa amefika kama dk5 hivi nyuma ya kikosi cha Rweyemamu kilichokuwa kikisubiriwa ili waingie kufanya tukio. Akiwa anapita kwenye geti pekee la kuingilia na kutokea, Frank anakuta mazingira yakiwa yametulia na hali ni shwari kabisa. Baada ya kulipita geti kwa hatua kama 10 hivi Frank anamuona kaka mmoja wa makamo aliekuwa nadhifu na mtanashati, mahali aliposimama kaka huyo ndio njia aliyokuwa anapita Frank kuelekea kwenye jengo La hosteli. Macho ya frank yanagongana na ya kaka huyo, Hakuna anaeonesha kuwa na shaka na mwenzie, hukuakiwa anakatisha mbele yake Frank anamsalimia, "Kristo……?" kwa mshtuko kaka huyo anajibu, "aa…. Amina, ndugu" Frank anapita bila kujali huku akitabasamu na kuonesha kufurahishwa na uitikiaji wa yule jamaa. Ndani ya eneo hilo Frank alikua amesha zoea kila anaekutana nae Salamu ni, Kristo… na jibu ni, tumaini letu….. sasa kwa mara ya kwanza anashangaa kukutana na mtu ambaye yupo ndani ya eneo hilo na hajui kuitikia salamu hiyo. Ghafla Tabasamu la frank Linakatika na kuoneshwa Kushtushwa na Jambo. Huku akiwa bado anaendelea kutembea, Taswira ya yule jamaa aliekutana nae njiani inamjia na kukumbuka kuwa ilikuwa ni sura aliyoiona sikuile aliyoenda ofisini kwa Rweyemamu.
Frank anaongeza mwendo zaidi, huku akikimbuka sikuile iliyoenda ofisini kwa Rweyemamu, akiwa amesimama kwenye meza ya secretary anazungumza nae, kilitoka kikundi cha watu kama 7 hivi ofisini kwa Rweyemamu na mmojawao ali simama pale na kumtania yule Dada, mtu huyo ndio huyu ambae amempita sekunde chache zilizopita. Ndugu na Rafiki yangu kipenzi, Amini usiamini kama isingekuwa yule jamaa kushindwa kuitikia ile salamu basi Frank asingeweza kumstukia, kitendo chake cha kushindwa kuitikia ile salamu ndio kilifanya kichwa cha Frank kitafakari kwa haraka kuwa jamaa alikua mgeni kabisa maeneo hayo. Frank anagundua kuwa tayari walikuwa wamesha vamiwa eneo hilo, Kwa haraka zinamjia picha kichwani kuwa inawezekana kule ndani tayari wamemtia pigu dokta Roby, Zinamjia picha kuwa Dokta robi kashachezea kichapo na muda huu atakuwa anavuja damu. Sijui nimuelezee vipi Frank ili uweze kupata picha alikuwa ni mtu wa aina gani, yaani ni mtu ambae kichwa chake kinaweza kugenerate possible solution for each possible obstacles, kwani ndani ya sekunde hizi chache alikuwa ameshawaza mpaka uwezekano wa kuwahonga maaskari atakao wakuta ndani, na kichwa chake kilikuwa kimesha piga mahesabu kiasi cha pesa alichokuwa nacho bank na uwezekano wa kuwahonga, ikibidi kuwazidi akili wakati anaenda kuwatolea hela benk.

Frank akiwa hajiamini kabisa kwa kuhisi pengine na yeye Alikua ameshanasa mtegoni, huku akiwa ameongeza kasi anazungusha macho yake huku na kule, ghafla kwa mara nyingine tena macho yake yana gongana na yule jamaa. Kitendo cha kuongeza kasi, nakugeuka kwa mara ya pili kinamfanya hu kaka shtuke lakini mshtuko wake unamwambia kuwa Frank alikuwa mshamba flani alietoka kijijini na kuja kutumikishwa kwenye shughuli za kanisa hivyo kilicho mfanya ababaike ni kumuona mwanaume shababi na mtanashati anang'aa utasema kashuka kutoka uswiz sekunde kumi zilizopita, jamaa kiwa anawaza hayo anasema,"Utajigonga kwenye miti….. mjinga wewe!" wakati macho yake yakimtizama Frank akiwa anakatakona kuingia kwenye jengo la Hosteli, anashtushwa ghafla na Randcluser inayoingia ndani ya geti hilo kwa mbwembwe na fujo. Ilikua ni RandCluser mpya ya jeshi la polisi, inatimua vumbi nakupaki kisha wanashuka watu sita, akiwemo na askari ambae alikuwa ameshikiria mtutu wa Bunduki, askari huyu aliekuwa ameongezwa na Rweyemamu ilikuongezea nguvu, alikuwa ni mtu mwenye sifa ya kuwa na Roho mbaya kweli kweli, kiasi kwamba hata wenzie walikua wakihofia vitendo vyake, yeye alijulikana kama pengo kwakuwa kila mtu aliamini idadi ya meno yaliyobongonyoka mdomoni mwake ni kubwa kuliko yaliyosalia, hakuna mtu alie kuwa na uhakika na idadi ya meno yaliyokuwa kinywani mwake, na hii ilitokana na tabia yake ya kutokuwa na maneno mengi wala kutocheka kabisa na hata alipotaka kuongea, alizungumza Taratibu.

Frank anatembea Taratibu na kwa umakini mkubwa kuelekea ndani, anafika mpaka kwenye chumba alichokuwa Brenda na dokta, lakini anagundua kuwa walikuwa peke yao. Dokta anamuona frank akiwa anaingia, kisha anamuuliza, "vipi mbona unanyata?". Frank anajibu huku akiwa na haraka ya kuondoka eneo hilo haraka iwezekanavyo, "Sikia Roby, inatakiwa tuondoke hapa haraka iwezekanavyo" kunakundi la mashushushu wa Rweyemamu wamezunguka hili jengo", taarifa hiyo inampa hofu kubwa na woga dokta Roby, anauliza kwa hofu, "Jesus! Tutasalimika kweli?" Frank anamtazama na kumwambia ngoja tuone.

Bila kupoteza muda, Frank anambeba begani Brenda, Dokta anachukua briefcase yake iliyokuwa na vifaa vya matibabu, kisha wanatoka kwa kasi mle ndani. Ilikuwa ni ghorofa moja juu, kabla ya kushuka ngazi kulikuwa na eneo la kubwa la mapumzika ambalo lilitengwa kwaajili ya kupumzika na wanafunzi waliokuwa wakiishi humo ndani. Frank anafika kwenye viti vya eneo hilo nakumlaza Brenda, kisha anasegea mbele kulikokuwa na ngazi za kushuka chini ili akaangalie mazingira jinsi yalivyo, anatoka na kumuacha Roby akiwa amesimama na briefcase na baadhi ya nguo za kike alizokuwa amezibebelea. Hofu kubwa imemtanda dokta Roby, anahisi huu ndio mwanzo wa kuelekea gerezani. Hofu ya Roby inakuwa kubwa kiasi kwamba inaweza ikaathiri zoezi zima la kuwatoroka makachero wa rweyemamu.

Frank anashuka mpaka chini na kuelekea kwenye mlango wa kutokea kwenye jengo hilo la Hosteli. Anafika mlangoni na kuchungulia kwenye geti kubwa la kutokea nje, kabla macho yake hayajafika mbali analiona kundi la maofisa nane likiwa linakuja kuingia ndani ya jengo hilo, Moyo wa Frank unaenda mbio, anatamani kule juu kungekuwa na mlango mwengine wa kutokea, lakini uhandisi wa jengo hilo ulikuwa umesha kamilika bila kuona umuhimu wa wazo hilo, Frank anaona huu sio muda wa kuendelea kufikiri vitu visivyowezekana. Anarudi kwa kasi kule juu alipomuacha dokta Roby. Hawa mashushushu nao wanaongeza kasi ya kuelekea kule juu. Anamaliza tu kupandisha ngazi ya mwisho. Nyayo za majamaa hao zinasikika kwanguvu nao wakiwa wanapanda ngazi.

Frank anatizamana na Roby uso kwa uso, Frank akiwa kama hatua ishirini hivi kabla ya kumfikia Roby, Roby anauliza kwa ishara ya mikono akiashiria, vipi kupo sawa huko? Frank akiwa ametoa macho na kumkazia Roby bila kutizama kokote, hajibu swali la Roby, ila nyayo zilizokuwa zikisikika kupandisha ngazi zinampa jibu Robi kuwa wamesha nasa. Frank anafika mpaka pale kwa Roby kisha anamtua lile briefcase na kuchukua kitambaa kikubwa ilichokuwa amekibeba Roby anamfunika nacho Brenda huku akimwambia Roby,"Wanakuja, Adapt plan B". Baada ya kusema maneno hayo, kinachofata sasa ni zoezi la kujalibu zali la kuwapumbaza wale makachero kwa frank kujifanya mtumishi wa mungu anawaombea roby na Mke Wake. Roby ameduwaa huku hofu na wasiwasi ukiwa umemtinga moyoni kwake, ndani ya sekunde hiyo hiyo askofu msaidizi mzee Pita Kamatula anatoka ndani ya ofisi yake ambayo ilikuwa hatua kumi tu kutoka. Walipokuwa wakina Frank, muda huo Frank alikua ameshaanza kuomba kwa msisitizo wa hali ya juu na tayari alikuwa ameingia kwenye ulimwengu bandia wa kiroho. Askofu kuona hivyo anaamua kuongeza nguvu na yeye anaanza kuangusha duwa.

Wale makachero wanatokeza eneo lile na kuona watu wakiwa wanapambana na nguvu za ibirisi, wote wanasimama na kutizama tukio lile kwa makini. Frank anakazana kwa kusema,"Tizama wanaume hawa wamezingirwa na minyororo ya shetani…. Angalia Wababa hawa wanalilia huruma yako ee Mungu……. Nyosha mkono wako mfalme wa wafalme, Rudisha nguvu kwa wanaume hawa mungu wa Rehema". Kundi la Rweyemamu likiwa linaangalia mchezo ule, pengo, yule askari niliemuelezea hapo mwanzo anaona kwamba lile lilikua gozi gozi. Anapiga Hatua kusogea eneo lile. Wenzake wote wanaona kuwa pengo anataka kuanza kuleta Laana zake bila kujali kuwa hilo ni eneo la kanisa. Kabla hajaliacha kundi la wenzie anataka kupita Mbele ya Lugano, Lugano ana mkinga kwa mkono. Na kumwambia,"Iam in charge of this mission". Baada ya kusema hivyo lugano anatizama namba za kwenye milango ya vyumba vilivyopo pale kisha huku akionesha ishara ya mkono anasema,"This way".

Mashushushu hawa wanaenda mpaka kwenye chumba walichukuwa anakaa Anatumia Brenda na Roby na kukuta hakuna mtu. Lakini dalili zote zinaonesha walikua wametoka sekunde chache zilizopita. Kila mmoja anaonesha hofu yake nay ale maombezi yaliyokuwa yakiendelea pale nje. Wanarudi mbio mbio mpaka eneo lile wanakuta maombezi hakuna na wala hakuna mtu eneo hilo. Wanakimbia mbio mbio kushuka chini wanakuta dokta Roby ndio anaingia ndani ya gari yake aina ya RangeRover Discovery, wanakimbia kwa kasi kumuwahi , lakini ujuzi na ustadi mkubwa wa dokta huyo kwenye kugeuza gari unawazidi maarifa wale makachero na kuwaacha wameduwaa. Kitendo bila kuchelewa wanapanda gari ya RendCruser Prado iliyokuwa na pret namba za jeshi la polisi na kuanza kuwafukuza.

Ndani ya gari waliyokuwa wakina Frank walikuwa na mdogo wake dokta Roby aliekuwa anaitwa Zuberi. Zuberi yeye alikua iliipeleka hiyo gari kwenye service hivyo wakati anairudisha tu na yeye anajikuta akiingia katika kasheshe hilo. Wakati wakiendelea kufukuzana Rendcruser inaonekana kushindwa kuyahimili mashimo vizuri hivyo kasi yake inapungua na kufanya wakina Frank wasogee mbali kidogo. Wanakaribia kuingia kwenye Rami, Kwa mshtuko dokta Roby anamuuliza mdogo wake, "Zuberi! Gari haina mafuta?.......... " zubery anajibu ,"mimi sikuangalia".
Waswahili tunasema Bwawa limeingia Luba! Hizi zinaonekana kuwa mbio za sakafuni zinazoishia ukingoni. Hatimae Gari ya kina frank inaishiwa mafuta. Mafuta yaliyobaki yanaweza kukata muda wowote. Ok nadhani huu unafaa kabisa kuwa mwisho wa Episode hii ya 7, usikose sehemu ya saba Ya Tamthilia hii, ambayo naamini itakuwa nzuri kuliko Episode zote, Mpaka wakati mwingine,

Nawapenda Sana !
 
kuna kitu kinagoma katika maisha ya uhalisia! prof ryeyemamu ni mwanasheria mkuu hivi kwa akili ya kawaida mtu hadi aufikie uprof na kuwa mwanasheria mkuu wa serikali atakuwa na miaka mingapi? wakati huo huo baba yake still ni mwanasiasa maarufu

najiuliza hawa baba na mwana wanatofauti ya umri gani?

hii ni hadith kaka haina uhalisia ndo maana unaangalia filamu ya masaa matatu mtu anazaliwa anakua na anaoa au kuolewa ndan ya masaa matatu.
 
hii ni hadith kaka haina uhalisia ndo maana unaangalia filamu ya masaa matatu mtu anazaliwa anakua na anaoa au kuolewa ndan ya masaa matatu.

unakosea sanaa haipo hivyo! hata hizo filamu unazosema sio kwamba mtoto anazaliwa na kuolewa ndani ya umri wa utoto lazima waonyeshe alikuwa ndipo akaolewa hivyo no matter what suala la uhalisia kwenye sanaa ni la umuhimu sana
 
View attachment 159724

Unataka kujua Zimebaki Masaa mangapi kutoa Episode Inayofata? Click Picha Hiyo, ili utembelee magicHand Official Blog

Utasoma, utasikiliza na Kuburudika.

Bonyeza Picha
 
Hongera sana JamiiForum ni bonge la story,unanifanya nami nahangaika hapa nilipo kama Frank,dah! Sijui watapona kweli?

Vipi kuhusu dripu ya maji kwa Brenda alitembea nayo au? maana Frank alipokuwa supermarket ndo dokta Roby alikuwa akimwekea dripu Brenda. Correction kidogo Land Cruiser Prado badala ya Rend Cruser Prado. Hongera sana kwa improvement naona sasa itasomwa na wengi zaidi, big up!!!
 
Last edited by a moderator:
The Second Door- Episode 6


”simamisha gari”, Roby anastushwa na kauri hiyo ya Frank, huku akiwa mtu mwenye hofu anauliza kwa mshangao, “Unasemaje!” Kisha anacheka kwa kejeli,”Hee heee, Jinsi tulivyo watoroka, wakitushika hapa, tutaenda kupata fahamu gerezani huku kila mmoja wetu, akiwa kapoteza lita mbili za Damu”, Frank anaongeza msisitizo kwa kusema, “sikia Roby Tukisimamisha gari wenyewe inamaanisha tutakuwa na Plan nyingine ya nini cha kufanya, na tusipofanya hivyo litaishiwa mafuta na kusimama lenyewe, then tutashikwa kiulaini kabisa”.


Dk 40 tu zimesalia kabla ya sehemu ya 8 ya Tamthilia yetu ya The Second Door Kutoka, Gari imeisha mafuta, frank anatoa ushauri wa kushuka wakati askari wanakuja kwa kasi nini kitataokea? kaa mkao wa kula.
 
Hongera sana JamiiForum ni bonge la story,unanifanya nami nahangaika hapa nilipo kama Frank,dah! Sijui watapona kweli?

Vipi kuhusu dripu ya maji kwa Brenda alitembea nayo au? maana Frank alipokuwa supermarket ndo dokta Roby alikuwa akimwekea dripu Brenda. Correction kidogo Land Cruiser Prado badala ya Rend Cruser Prado. Hongera sana kwa improvement naona sasa itasomwa na wengi zaidi, big up!!!

Ha ha haaaa everlenk utajibeba! mbona mambo ndio kwanza yanaanza? kunapart mimi mwenyewe naifikiria mpaka naogopa kuandika. Drip itakuwa ilichomolewa tu kutokana na imegency iliyotokea, lakini kusema kweli nilisahau kufinalize hiyo ishu ya drip.
 
JamiiForum Endelea basi hizo dk 40 ni nyingi sana,difenda la Rweyemamu lishatukaribia bana!!!
 
Last edited by a moderator:
The Second Door- Episode 8

Habari gani marafiki namshukuru mwenyezi mungu kwa kuweza kuniweka salama mpaka wakati huu, Lakini pia kwa kutuwezesha kufikia Episode ya nane kwenye Tamthilia hii.
Kwenye episode namba saba tuliweza kuona jaribio la Frank na dokta Roby kuwatoroka Makachero waliokuwa wametumwa na Rweyemamu, na tukaishia mahali ambapo jaribio hilo liliingia dosari kwa gari waliyokuwa wakitumia kutorokea ambayo ilikuwa ya dokta Roby Kuishiwa mafuta.
Baada ya wakina Frank kugundua kuwa gari yao imeishiwa mafuta, kila mmoja anaonekana kuingiwa na hofu hususan Zuberi mdogo wake na dokta Roby, Frank anatizama nyuma kwambali anawaona wale makachero wakija kwa kasi, Frank anamtizama Roby na kumuuliza, "mafuta yaliyobaki yanaweza kutufikisha umbali gani ?" Roby anajibu, "kama mita 300 tu! Tutafanyaje?" umbali ambao Roby ameusema ni sawa na urefu wa viwanja vitatu vya mpira wa miguu, Frank anasema, "simamisha gari", Roby anastushwa na kauri hiyo, huku akiwa mtu mwenye hofu anauliza kwa mshangao, "Unasemaje!" Kisha anacheka kwa kejeli,"Hee heee, Jinsi tulivyo watoroka, wakitushika hapa, tutaenda kupata fahamu gerezani huku kila mmoja wetu, akiwa kapoteza lita mbili za Damu", Frank anaongeza msisitizo kwa kusema, "sikia Roby Tukisimamisha gari wenyewe inamaanisha tutakuwa na Plan nyingine ya nini cha kufanya, na tusipofanya hivyo litaishiwa mafuta na kusimama lenyewe, then tutashikwa kiulaini kabisa". Wakati Frank anamaliza kuzungumza hayo, Zubery ana dakia na kusema, "nimepata wazo!" kauli ya Zubery inafanya kila mmoja amsikilize kwa makini, Zubery anasema,"Simamisha Gari, kisha Nyinyi mshuke na kukimbia", Robi anamkatisha na kusema,"Halafu wewe na Brenda?" Zubery anajibu, "Simple! Mimi nitaangalia tension yao, kama wakishuka na kuwafukuza nyinyi sisi tutakua salama" Roby anahoji, "na what if wasipo tufata sisi wakaja kwenye Gari?". Zubery anaonesha kukwama, Frank ananyanyua mdomo kujibu, Gari inazima Ghafla, Frank anaghairi kile alichataka kusema kisha anauliza,"yamekata?" Zubery anajibu, "hapana mafuta hayajaisha imezima tu, nyinyi shukeni……." Frank na Roby wanatizamana kisha Frank anasema, "Tushuke" Roby anamtazama Zubery na kumwambia, Be Carefull". Roby anataka kushuka Frank anamvuta na kumwambia apite kwenye siti za nyuma kisha ajifanye kama mgonjwa ajitundike kitambaa ambao walikua nacho kutoka Kule hosteli, Frank akapita na kutokea mlango wa Dereva, kisha kwa kasi anazunguka na kumshika Roby ambae nae anatembea kama mgonjwa aliezidiwa kisha wanaingia kwenye mitaa. Huku nyuma wanamuacha Zubery akiwa ameinama chini kabisa. Wanapo potea tu ndani ya nyumba za watu wanazindua marathon.

Mpenzi msomaji mbinu hiyo ya Frank inafanikiwa kwani wale makachero wana shuka kwenye gari yao kwa kasi na kuanza kuwafukuza kwa kupita njia tofauti tofauti kwa lengo la kuwazunguka. Makachero wanaonesha kuwa hawana wasi wasi kwani waliamini kuwa mmoja wao kati ya wale waliokuwa wakiwakimbiza alikuwa mgonjwa, hivyo hawawezi kufika mbali na watawashika bila shida.

Askari saba kati ya wale nane walio kuwa ndani ya gari wanaungana kuwafukuza na kumuacha mmoja akiwa eneo lile. Zubery anachungulia na kumuona yule askari mmoja, yule askari anakusogea kwenye lile gari taratibu mara simu yake inaita, anapokea simu na kuanza kuongea, aliekuwa akimpigia askari huyo alikuwa ni shangingi mmoja aliekuwa akimtoa njia kuu askari huyo, hivyo askari huyo analegea ghafla na mawazo ya kikazi zaidi yanabadilika na kuwa mawazo ya kimahaba.

Zubery huku akijua kuwa ni wazi kabisa kwamba akimaliza kuongea na simu askari huyo atamfata, anatumia muda huo kukaa kwenye Stering. Wale askari waliokuwa wakimkimbiza frank na Roby wanachanganywa na vichochoro vya uswahilini na kujikuta wakizunguka hapo hapo. Lugano anamwambia Bosko arudi ili akakague gari waliyoiacha, wakati wao wakiwa wanaendelea kuwasaka, huku mmoja wao akisema, "Yule mwanamke bado mgonjwa anachechemea kabisa, hawajaenda mbali watakuwa wapo eneo hili hili". Wanazungumza maneno hayo,kumbe Frank na Roby walikuwa wamejibana ndani ya maliwato ambayo uswailini inajulikana kwa jina maarufu la PasportSize, wakati huyo askari akizungumza maneno hayo, kwa sauti ya chini Frank ansema,"akili zenu mbovu ndio zinachechemea". Huku kwa Zubery anaingia kwenye mtihani mpya kwani gari ambayo aliamini ingewaka kutokana na jinsi alivyoizoea sasa inamgomea kuwaka. Na kitendo cha kupiga stata kinamfanya yule jamaa aliekuwa akizungumza na simu ashtuke kuwa kwenye hiyo gari bado kunamtu.

Anakata simu maramoja na kuikimbilia ile gari, mungu si Athmuni akiwa anashika kitasa tu afungue mlango, Zuberi anafanikiwa kuiwasha hiyo gari na kumuacha huyo askari. Askari huyo anaamua kurudi kwa kasi mpaka kwenye gari yao na kufungua mlango wa gari kisha anaingia ili amfukuze, lakini inakuwa bahati mbaya kwani fungo walikuwa wameondoka nazo wale walioenda kumkimbiza Frank na Roby. Anashuka kwa kasi ili awapigie simu, na kujaribu kuwaangalia kwenye maeneo ya mitaa hiyo, mara anatokea Bosco akiwa na funguo. Huyu askari anamwambia,"Twende kunamtu kwenye gari". Wanaingia kwa kasi ndani ya gari hiyo na kuanza kuifukuza ikiwa bado haijafika popote na wanaiona mbele yao. Bosco akiwa kwenye Stering anaitoa gari kwa kasi eneo lile, kasi ambayoilikuwa ni mara 3 ya ile ambayo walitumia awali safari hii wakiwa wamechukia zaidi kwa kindumbwendumwe walichokuwa wakichezeshwa kama watoto.
Chichi Dusk Down, ni jina ambalo alikuwa amepewa na watu wa mtaa huo, mara baada ya kushindwa kutamka jina la movie maarufu ya From the Dusk till down wakati akihojiwa na kipindi maarufu cha Television, huku jina lake halisi likiwa ni chichi Ramadhani. Mtoto wa umri wa miaka kama mitano hivi, ambae alikuwa akipendwa sana na jamii nzima ya mtaa huo, wakati akiwa ametumwa dukani na mama yake kununua mafuta ya kupikia, anakutana uso kwa uso na Randcluser iliyokuwa ikiendeshwa na inspector Lugano. Ngao ya mbele ya gari hilo, inambamiza kwanguvu mtoto huyo maeneo ya kifuani na kumtupia kwa mbele kabla ya tairi la kushoto la gari hilo kuburuzika juu ya mguu wake wa kulia na kuusaga saga wakati Bosco akijaribu kufunga Breack. Ni sauti moja tu ya mbiu kubwa iliyosikika na kumwita mama yake mzazi aliyekuwa akikuna nazi nyumba ya tatu kutoka eneo la tukio.

Sauti kali ya mtoto chichi inakusanya Raia wa kike na wakiume waliokuwa na jazba ya kuona damu ya mtoto mdogo ikimwagwa na mikono ya watu wanaojihisi kuwa wako juu ya sharia. Kauli kali na zilizoambatana na hasira, kwa uchungu zilisikika zikisema,"Huu ni uvunjaji wa sharia, mwendo kasi wa gari yoyote hata iwe ya msafara wa raisi kwenye makazi ya watu ni chini ya km 50 kwa saa, hawa ni washenzi tu wameshaona fasheni kumwaga damu za watu kila kukicha, Leo tutawaonesha…….". Kilichokuwa kikifatana na kauli hizo kilikuwa ni sawa na kiama Bosco na mwenzie walijifungia kwenye gari, wakihofia raia, kisha wakawapigia simu wenzao ambao walikua mbali kidogo na eneo hilo, hata hivyo simu zote zinakuwa hazipatikani.
Huku wananchi hao wakifanya vurugu kubwa ili kuwashusha wakina Bosco kwenye gari, mama mmoja aliekuwa na uchungu kupitiliza anatoka huko mkuku mkuku huku akiwa na mchi mkubwa wa kinu, kisha anapiga gari hilo kwanguvu kwenye kona ya juu ya mlango, na huo unakua uzinduzi rasmi wa kulibongonyoa bongonyoa gari lote na kuwashusha watuhumiwa wao, kilichofata hapo kilikuwa ni kipigo kisichokuwa na formula, wananchi wenye hasira kali na wasiokuwa na hasira kabisa wote wanaungana kutoa hukumu kwa maafisa hao, kwani wanaami hakuna polisi haki. Kila siku wanalalamika vibaka wanaachiwa wakiwafikisha polisi, sembuse hao wenyewe kwa wenyewe? Mpenzi msomaji, kwakuwa sijaweka Tahadhari juu ya simulizi hii, nitazingatia itifaki hivyo sitaelezea jinsi wananchi walivyo wahukumu maafisa hawa.
Huku Frank na Roby Bado wanafatiliwa na askari, wanatokea kwenye mtaa ambao kuna kijiwe cha vijana waendesha pikipiki, wanazungumza nao na kukodi pikipiki mbili kisha wanatoweka eneo hilo. Maaskari hao wanafika hapo na kuwaona frank na Roby wakitokomea. Wanaamua kuwaweka chini ya ulinzi wale vijana. "------- nyinyi hapa mnakazi ya kufanya uharifu tu kila kukicha na haya mapikipiki yenu, mtaenda kuozea jera". Wanawasachi na kuwakamata vijana wawili waliokuwa na vipisi vya bangi, wanawafunga pingu na kuondoka nao.
Wanarudi mpaka walipoacha gari yao, nakukuta vurugu kubwa iliyokuwa imekosa muamuzi. Pengo anapiga risasi juu na kufanya wananchi wote watawanyike mbali kabisa na eneo hilo. Kama unavyojua mpenzi msomaji, dakika walizopata raia zilitosha kabisa kufanya hukumu kwa kiwango cha kuridhisha, lakini pia ziliwatosha kabisa vibaka kufungua Redio, Tairi, Milango, AirCondition, Taa na kila kilichokuwa cha thamani kwenye ile gari. Mara zinafika gari zingine za polisi na Kukuta Bosco na mwenzie wakiwa mahututi, Duniani hawapo, akhera wanatafutwa. Hilo linakuwa pigo la kipekee kwa kundi zima la makachero wanaofanya kazi chini ya mwanasheria mkuu wa serikali Mh Proffesa Rweyemamu.

Safari ya Frank na Roby inawapeleka mpaka sehemu salama, Huku wakifurahi na kuamini kuwa, mpango wao umefanikiwa, wanampigia simu Zubery ili wajue yupo wapi na Brenda. Roby anampigia simu Zubery kwa mbwembwe na furaha anasema,"Haloo Genius mpango wako umefanikiwa upo wapi?". Zubery anajibu, "Nimekamatwa nipo hapa central tazara" Frank akiwa anamtizama Roby wakati anaongea na simu anamsikia Roby akishtuka kwa mshangao,"what!?".
Pamoja na Furaha ya kuamini kuwa wamefanikiwa kuwatoroka mashushushu, taarifa ya kushangaza kuwa Zubery amekamatwa, inawafanya Roby na Frank wajione wajinga kabisa. Hofu na mashaka vinawajaa, nguvu kubwa na akili nyingi walizotumia mpaka kufikia hapa, zinaonekana kuwa sifuri kwani mwisho wa siku wataenda kujisalimisha wenyewe polisi. Mbali na yote, upande wa Frank zaidi ya kuwatoroka polisi, zaidi ya kuhakikisha anamlinda Brenda na kumfanyia matibabu mpaka ujue mwisho wake, Lakini Kibarua kikubwa zaidi na kilichomfanya atoke south Africa ni kumsaidia Rafiki na ndugu yake kipenzi Tarick dhidi ya Hukumu haramu na iliyozingatia manufaa ya kumapenzi zaidi kwa Rweyemamu kuliko usawa wa kisheria na Haki sawa kwa wote, Je Frank atasahau kilichomrudisha Tanzania? Au pilikapilika na vikwazo vinavyo tokea vinaweza kumchelewesha kumsaidia Tarick na hatimae akahukumiwa.

Tuishie Hapa kwenye Episode Hii ya 8. Ili kufahamu kitakacho endelea, usikose kuungana nami katika episode ya 9, na nimeweka njia Rahisi kabisa itakayokuwezesha kufahamu mpaka masaa yaliyo salia kabla ya kutoa Episode inayofata ni kwa kupitia Blog ya magichand. Ismagichand.blogspot.com. kwaheri.
 
Back
Top Bottom