The road towards 2010 Elections

The road towards 2010 Elections

Kati ya hawa nani atafaa kutuongoza 2010-2015?

  • Edward Lowassa

    Votes: 0 0.0%
  • Dr. Slaa

    Votes: 7 38.9%
  • Prof. Lipumba

    Votes: 0 0.0%
  • Mizengo Pinda

    Votes: 5 27.8%
  • Samwel Sitta

    Votes: 0 0.0%
  • Jakaya Kikwete

    Votes: 2 11.1%
  • Mark Mwandosya

    Votes: 2 11.1%
  • Harisson Mwakyembe

    Votes: 2 11.1%
  • None of The above

    Votes: 0 0.0%

  • Total voters
    18
  • Poll closed .
Ha ha ha sasa namchukia Kikwete eti kwa kusema kweli kwamba hakuweka mbele maslahi ya Taifa. Huu ni UNAFIKI WA HALI YA JUU. SITAPOTEZA MUDA WANGU KUJIBU MTU ASIYETAKA KUELEWA HALI HALISI YA NCHI YETU NA SASA UMEANZA KUNIZUSHIA KWAMBA NAMCHUKIA KIKWETE!!!! NIMCHUKIE KIKWETE KWA LIPI ALILONIKOSEA!!!!! KUSEMA KIONGOZI KASHINDWA KAZI NA USHAHIDI WA KUTOSHA KUTHIBITISHA HILI UPO NI KUMCHUKIA!!!! HA HA HA

Happy Good Friday

BAK inaelekea umemsoma MKR vibaya, soma tena katikati ya mistari!
 
Wana JF inachekesha sana kusikia watu wazima na akili zao wakiropoka kuwa JK awe mgombea pekee kama vile wamepoteza akili zao au kama vile wamesahau kuwa chama kinaongozwa na taratibu na katiba.

sikumbuki ni kipengele kipi cha katiba ya Chama au katiba ya jamhuri ya muungano, au muongozi wa rais unaomfanya yeye kuwa mgombea pekee wa Urais anapotaka kuingia kwenye kipindi cha pili. Kutokumbuka huku kunanifanya nione kuwa inawezekana JK akagombea nafasi hiyo akipingwa na wagombea wengine wanaoona kuwa wana haki au wanuwezo kuliko yeye.

Kuna kitu kama tacit agreement ndani ya chama kuhusu rais kuongoza kwa vipindi viwili, lakini hii ina base kwenye mambo ambayo ameonesha wakati wa kipindi cha kwanza. Tukiangalia katika kipindi hiki cha kwanza JK anastahili kuwa mgombea pekee? Je ametekeleza ilani ya uchaguzi ya chama? Je ameweza kuonesha uwezo wa uongozi wa taifa?

Inawezekana kuwa JK hatakiwi kupingwa lakini ni lazima saabu ziwekwe wazi ni kwanini yeye awe mgombea pekee. Sio kutaja jina lake bila kutaja sababu za kutaka awe mbombea pekee.

Na wanaotaka kugombea nafasi ya urais wasitaje majina yao tu, au wasioneshe nia tu ya kugombea kama wasindikizaji ni lazima waseme wanagombea kwanini, na wawe na hoja. Hakuna asiyejua kuwa nchi inatetereka, lakini kama wagombea ni weaker kuliko JK haitakuwa na maana kubadilisha, niafadhali kuwa na weak kuliko weaker.
 
Nadhani tunaanza kupotosha mada kwa kiasi fulani.

Sidhani kuwa tunazungumzia chuki kwa kiongozi yeyote. Kinachosisitizwa hapa ni kuwa, kila mwanachama wa CCM anayo haki ya kuomba kuchaguliwa na wenzake ili aongoze nchi. Endapo hakutakuwa na mtu mwingine zaidi ya kiongozi aliepo madarakani katika kuomba ridhaa hiyo, basi na aliepo awe mgombea pekee wa CCM. Kinachopingwa hapa ni dhana inayojengwa na baadhi ya watu ya kutaka wengine wote waache kuomba ridhaa hiyo (hata kama wanauwezo/hawanauwezo wa uchaguzi huo wa ndani ya chama). Kwangu, hii sio demokrasia halisi. Haikuwahi kutokea siku za nyuma kuwa mtu alinyimwa nafasi ya kuomba kuchaguliwa na wananchama wenzake. Utamaduni huu unatoka wapi leo?
 
Sijaona udhaifu wa kiasi cha kuwa tusimuamini tena kwa kipindi cha miaka mitano ijayo. Unajuwa kwanini? Sioni tofauti kubwa kati ya utawala huu na tawala zilizopita.

Ni matamshi kama haya yanayoniacha hoi nisiweze kuwaelewa watanzania wenzangu - kutafuta sababu yoyote ile kutetea udhaifu. Kwa mtaji huu sitashangaa nikimsikia Gozigumu akitetea klabu zetu za mpira kufungwa vibaya kwa kigezo kuwa hata huko nyuma tulikuwa tunafanya vibaya. Yaani mtu na akili yake timamu anatetea utendaji mbovu na kuuona kama hali ya kawaida. Ni yale yale ya kuishi kwenye uchafu halafu pamoja na kuathirika kiafya, hufikirii kutoka humo.

Inawezekana huko nyuma tuliwahi kuwa na tawala mbovu, lakini hii si sababu ya kuendelea kukumbatia hali hiyo. Maadamu sasa tumeamka na tunataka utawala bora na maendeleo, hatuwezi tena kumvumilia kiongozi asiyetupa matumaini - huyo hatufai. Unasema huoni tofauti kubwa kati ya utawala huu na tawala zilizopita, kwa hiyo ? Yaani hata sikuelewi ndugu yangu - hii ni karne ya 21 ya sayansi na teknologia, lakini asilimia kubwa ya watanzania bado ni kama wanaishi kwenye karne ya 19.

Wakati wa kuhitaji mabadiliko ni sasa na kiongozi tuliye naye hana uwezo wala ujasiri wa kutuongoza kwenye hilo. Kama hili wewe hulioni, kwa masikitiko hauko peke yako - uko pamoja na wezi, mafisadi, wahujumu na wavunja sheria wanaofumbiwa macho na utawala huu. Pamoja na hayo tutapambana nanyi kadiri ya uwezo wetu kwa kutumia silaha yetu kubwa ambayo ni haki na usawa. Ndani ya utawala bora kamwe hamuwezi kusitawi kwani toka lini giza likadumu kwenye mwanga ?
 
BAK inaelekea umemsoma MKR vibaya, soma tena katikati ya mistari!

Sina haja ya kumsoma yeyote anayetaka kunizulia kwamba namchukia Rais, hii ni tuhuma nzito sana na hana ushahidi wowote wa kuthibitisha tuhuma hii nzito dhidi yangu. Inanikumbusha Republicans walipokuwa wanawatuhumu wale wote waliokuwa wanapinga uvamizi wa Iraq au kumtuhumu Kichaka kwamba kaudanganya Ulimwengu katika uvamizi ule. Wote hawa Republicans walisema hawa patriotism dhidi ya nchi yao kitu ambacho hakikuwa na ukweli wowote.

Simchukii Kikwete na wala sina sababu yoyote ya kumchukia Kikwete, lakini kama Watanzania wale ambao hawaridhiki na utendaji wake kama Rais tangu aingie madarakani hawasemi hivyo kwa kuwa wanamchukia bali wana haki ya kusema hivyo kwa kuitakia mema nchi yao ili ipate kiongozi ambaye utendaji wake utaweka mbele maslahi ya nchi kuliko ilivyo sasa.
 
Bubu Ataka kusema na Recta,

Wakuu zangu vipi lugha inawapa shida?...
Hivi kweli hamfahamu matumizi ya neno a thin line between Love and Hate?..
Sikusema unamchukia JK ila nasema mapenzi yako yanaweza tafsirika kama Chuki kutokana na mtazamo wa upande huo -shilingi wakuu zangu, ina pande mbili..
Nitarudia kwa ufasaha zaidi..
Kikwete na Kundi lake wameacha kuwafikisha mahakamani Mafisadi kwa sababu wanahofia usalama wa nchi..
Fikra au maneno haya kwa mtazamo wao yanatokana na Mapenzi ya nchi yao ndiyo yanawasukuma kuona kwamba ni bora wamezee hili kuliko kuingia ktk vita ya ndani..On the other hand, mimi binafsi, nauchukia Ufisadi na naweza sema namchukia fisadi yeyote bila kificho kutokana na mapenzi ya nchi yangu na naomba kila siku Mafisadi wafikishwe mahakamani.. Fikra au imani hii inatokana na CHUKI (ya Ufisadi) hivyo, pia inaweza tafisrika kuwa ni chuki..na badala ya watu wa upande ule wa pili kutumia chuki yangu kwa vitendo vya Ufisadi wakaitumia jina au majina ya watu kupindisha ukweli - mathlan Mkandara anamchukia Rostam..(simchukii Rostam ila nachukia vitendo vyake)

Pili ktk vitendo vya Kikwete kuwaachisha kazi baadhi ya viongozi ni kutokana na mapenzi yake kwa nchi yetu lakini kuna baadhi ya watu watatazama hiyo kama chuki yake kwa watu hao..na matokeo ya migogoro yote ndani ya CCM inatokana na maneno haya mawili.. LOVE and HATE kutafsirika jinsi watu wanavyojisikia..

Wakuu zangu hawa jamaa wanalindana na sasa hivi wameamua kutoleana Uvivu - tumesikia wakisema fulani tumemsitiri kwa madhambi ya mkewe angekuwa akiozea Jela kama sio sisi..Maneno kama haya badala ya kujenga hoja ya wahusika hao ni lazima yatushtue toka usingizini kuhusiana na vitendo hivyo.. viongozi wa CCM sio kweli hawafahamu kwamba wanavurunda isipokuwa maadili yao yanawahimiza kulindana hata kama wakivunja sheria..now, Why hope something good itatoka huko! ndilo swali langu.

Jamani kwa miaka mitatu tumekuwa tukizingumza humu kuhusu utawala wa CCM, leo inashangaza sana watu mnafikiria kwamba tatizo sio CCM isipokuwa ni Kikwete wakati chama kizima kinampongeza kama alivyopongezwa Mwinyi na Mkapa.. haya madudu na akili ya kushikiwa itaisha lini?.. kwa nini msifikirie kumtafuta rais toka vyama vingine ambavyo kwa kauli zao wamesema watahakikisha Mafisadi wanafikishwa mahakamani!..

Utawala bora hauwezi kutanguliwa na kitu chochote ikiwa bado kuna watu Untouchbles, watu wanaopinga na kusherehekea Ufisadi au unafiki wa kuzungumzia ktk vijiwe wakati wanashindwa kusimama kupinga Ufisadi na watu kama Lowassa, Rostam, Karamagi wafikishwe mahakamani..Hawa Mafisadi bado wabunge, bado ni wana kamati wa chama tena wanaheshimika na kuabudiwa,leo mnafikiria kuna mtu ndani ya chama hiki anaweza kuifanya kazi kubwa aloshindwa baba lao Kikwete..

Bisides, Tuache reality, tuzungumzie mathlan kama kuna mtu ataweza kushindana na Kikwete na pengine kushinda..basi vita ya matokeo hayo sidhani kama kuna mtu hujmu ndani anayaombea, ndio hapo Usalama wa taifa utakuwa hatarini na nakuhakikishieni kwa lugha yenu na mtazamo wenu..Kama kweli kuna mtu huyo au nafasi hiyo ikitolewa - mgombea atakuwa Puppet wa Mafisadi!... And U all don't wanna that!
 
hao wazee mimi siwashangai kwa ajili kila mtu anayepinga ufisadi anasema anamuunga "mkono JK juhudi zake za kupambana na ufisadi" na wakati kila mtu anajua JK hapambani na ufisadi.

lazima waseme wanamuunga mkono, unazani wao wangeweza kusema vinginevyo, hawana ubavu? kinachoniuzi ni hao wazee wanavyoongea kana kwamba wanaubavu wa kusema hatumtaki kikwete, kitu ambacho wao wanakiweza ni kumsupport au kukaa kimya sio kinginecho.
 
Wakuu,kuna mambo ambayo yanaendelea yanayofanya mtu yeyote anayefikiria mustakabali wa nchi yetu kujiuliza swali kama JK anastahili kugombea kipindi kingine.

1. JK amekuwa mgumu kufanya maamuzi magumu kama vile kushughulika na mafisadi
2. Kutetea upindishaji wa sheria kama vile kutetea na kuwapongeza viongozi wa TAnesco kutofuata sheria ya manunuzi
3. KUtumia wazee wa CCM kuanza kumpigia chapuo na kuwatisha wale wote ambao wangetaka kugombea (na hivyo kuinyima fursa nchi kupata kiongozi bora zaidi yake) na mengine mengi.

JE UNADHANI JK ANASTAHILI KUGOMBEA KIPINDI CHA PILI?
 
Hastahili kugombea kabisaaaaaaaaaaa!!!!! Its a big NO
 
Hastahili kugombea kabisaaaaaaaaaaa!!!!! Its a big NO
Umewekewa sehemu ya kupigia kura. Kuna sehemu tatu chagua sehemu mojawapo ili baadaye tujue asilimia ngapi wanaunga mkono na wangapi hawaungi mkono. wa hiyo kazi kwetu wana JF kupiga kura. Shime na tupige kura
 
Umewekewa sehemu ya kupigia kura. Kuna sehemu tatu chagua sehemu mojawapo ili baadaye tujue asilimia ngapi wanaunga mkono na wangapi hawaungi mkono. wa hiyo kazi kwetu wana JF kupiga kura. Shime na tupige kura

Ipo wapi hiyo sehemu ya kupigia kura???

JK hafaiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii
 
Ipo wapi hiyo sehemu ya kupigia kura???

JK hafaiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii

Naomba basi huyo aliyeiweka, aiweke mahalipanapoonekana kirahisi. Amasivyo atoe maelekezo ya namna ya kuifikia sehemu ya kupiga kura. Kwa sasa mimi siwezi kuona maana nimeshapiga kura na inanionyesha asilimiaza waanaomkubali na wanaomkataa.
 
Hafaiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii kabisa.. Miaka 4 yajafanya cha maana tukimpa mingine 6 sindio atabolonga kabisa.
 
Anatutia aibu mno huyu mkulu wetu, hebu angalia alivyokaa kimya wakati Mama Anne Kilango alivyo kuwa anapigwa vita na mafisadi na wanaowaunga mkono, kisa tu mchango wake mkali kwenye suala la Richond na mapambano ya Ufisadi kwa ujumla. Lakini baada ya kuona wamarekani wampatia tuzo mama Kilango na yeye andakia eti kumpongeza!! ALIKWINA!?? mawili, anadakia ili awe sehemu ya mafanikio ya Kilango. Pili, watu waone na yeye anawaunga mkono wapinga ufisadi, basi tu hajitokezi.
Kama ingekuwa kwa wenzetu wenye demokrasia za kweli, tungekaa chini kwa uwazi kabisa, tuchague mmoja wetu mwenye uwezo wa kweli kabisa wa kutuongoza (bila kufanya hila za wanahabari kusifia vimeo!) tungepata tu... wapo watu weengi tu ambao kwa ukweli wanawezakuwa viongozi wetu wazuri tuu... wapo.
Tuachane na hawa walionunua ukuu.
 
Tumweke nani kati ya wapinzania wake wa sasa?


Wapo wengi tu mkuu, ambao hawana maswahiba mafisadi, wenye uwezo wa kukemea jambo baya waziwazi bila kuogopa kuwa wako kundi fulani, wenye nia ya dhati ya kutuletea maendeleo, wasiondekeza wasikaji wapo chungu nzima! wasiokuwa na makundi wapo tu mbona... mie naamini hata wewe unawe kama unasifa stahiki. Hivi kwani wapinzani wa mkulu ni kina nani?
 
Wakuu, mimi nafikiri tatizo kubwa sio JK bali ni mfumo mzima wa utawala na mentality ya viongozi/wabunge wetu.

Katiba ya nchi inasemaje kama rais ameshindwa wazi kabisa kutekeleza wajibu wake na kuchukua necessary and important decisions at crucial times? bunge lina wajibu gani? bunge lina nguvu gani? linaweza kuchukua wajibu wake? linaweza kudhubutu kufanya hivyo?

As long as mentality ya wabunge inasimama ilivyo sasa, katiba ile ile, rais wa nchi ndo mwenyekiti wa chama, rais kufadhiliwa na watu wakati wa kampeni, rais kuteua mawaziri etc, hata apewe nani urais, tunaweza kujikuta tupo pale pale
 
MNAPOSEMA HAFAI,mnatakiwa mpige kura mtu anaestahili.
sio mnasema hafai haafu mnampigia kura
 
Umewekewa sehemu ya kupigia kura. Kuna sehemu tatu chagua sehemu mojawapo ili baadaye tujue asilimia ngapi wanaunga mkono na wangapi hawaungi mkono. wa hiyo kazi kwetu wana JF kupiga kura. Shime na tupige kura

Kwa hiyo ukipiga kura hutakiwi kutoa maoni?
 
Wapo wengi tu mkuu, ambao hawana maswahiba mafisadi, wenye uwezo wa kukemea jambo baya waziwazi bila kuogopa kuwa wako kundi fulani, wenye nia ya dhati ya kutuletea maendeleo, wasiondekeza wasikaji wapo chungu nzima! wasiokuwa na makundi wapo tu mbona... mie naamini hata wewe unawe kama unasifa stahiki. Hivi kwani wapinzani wa mkulu ni kina nani?

Wapinzania wake ni wale wale wanaojitokeza kila uchaguzi... Kafu, Chadema, Tlp, Udp. Wengine mbadala naona hawajaamua kuongoza vinginevyo katika Wabongo milioni 40 hatuwezi kukoza mtu mwenye uwezo na nia nzuri na nchi yetu.

2010 sio mbali jitokezeni tutawapigia kura, vinginevyo kama yatakuwa yaleyale tusitegemee mabadiliko yoyote.
 
Back
Top Bottom