The road towards 2010 Elections

The road towards 2010 Elections

Kati ya hawa nani atafaa kutuongoza 2010-2015?

  • Edward Lowassa

    Votes: 0 0.0%
  • Dr. Slaa

    Votes: 7 38.9%
  • Prof. Lipumba

    Votes: 0 0.0%
  • Mizengo Pinda

    Votes: 5 27.8%
  • Samwel Sitta

    Votes: 0 0.0%
  • Jakaya Kikwete

    Votes: 2 11.1%
  • Mark Mwandosya

    Votes: 2 11.1%
  • Harisson Mwakyembe

    Votes: 2 11.1%
  • None of The above

    Votes: 0 0.0%

  • Total voters
    18
  • Poll closed .
That is JK using mengi to assert power which he does not have. He knows he's weak so he is trying to create a certain view in the Public eye kwamba chama bado kinamkubali.. anawazima wakina mwandosya kabla hawajaanza kumtishia ndani ya chama.. CCM is powerful but he is not..
 
Hata ukuu wa mkoa ni kumpendelea tu tena upendeleo wa wazi na hasa mkoa wenyewe ukiwa kama dar = chaos ... maana idadi ya watu ni zaidi ya mara tatu ya wale wanaomshinda kuwaongoza sasa, kwa hiyo inafaa kumuonea huruma na kumpumzisha kabisa, au kama anapenda sana madaraka awe mshauri wa mgambo... tosha

-----------
Tuna kazi ya kutafuta kazi


Mimi nadhani akiwa mshauri wa maskani ya michenzani atafaa sana
 
Nimesoma katika Maoni kuwa kazi aliyoianza Kikwete amalize!! thats bullshit kazi gani hiyo? akifa je? thats no sense.

Mabadiliko ya mkini yanahitajika vinginevyo kila siku Tanzania tutakuwa wapiga debe tu. we have potential people lakini ikifika wakati wa uchanguzi sijui tunapubazwa na nini!!!! tunachagua walewale the next day tunaanza kupiga kelele sijui ni shetani gani hili limeigubika nchi yetu na wana wake.

Sijui tatizo liko wapi. tunajua fika kuwa tunachagua mabomu wapiga domo still kila leo wamo mpaka wajiuzulu wenyewe!!!!! NO NO Tuliong'amuka lets spread mang'amuzi yetu kila pembe!!
 
Mkuu Sekenke... si wewe peke yako mwenye dukuduku. Hii nayo ni thread aliyoanzaisha BabaDesi
jamani naomba tuelewe kuwa CCM ni chaka la watu waliochoka kimawazo na wenye kuendekeza unafiki, fitina na majunguuu.... ujinga mtupu tunapowajadili hawa wazee wanaotoa mawazoo yaliyochokaaa...

nchi yetuu ni zaidii ya ccm na hivyoo tusongeee mbele kujadili mustakabali wa nchi yetu hasa jinsi ya kuondokanaa na umasikini wa kizembee, miundombionu ya umeme, maji, barabara, mawasiliano nk.. pia ni wakati muafaka wa kujenga uwezo wa kuongoza kwa ufanisi na tijaaa..

demokrasia changa tuliyo nayo tujitahidi kuboresha taasisi za kiungozi kama mahakama, bunge na utawalaaa...

mwamko wa kuweza kuhoji na kukosoaa serikali kwa mustakabali wa maendeleo yetuuu ni muhimu.

tuboreshe kwa kasi mpya ELIMU YETU ili kujenga taifa lenye uwezo wa kuchanganua na kujijengea ajira kwa rasilimali zilizopo.( hatuwezi kuendelea kulalamikia kuwa na utajiri usiotusaidia kwa sababu tuu ya ELIMU duni ya ujasiri wa kuzitumia rasilimali hizo).

TUBADILIKE KWA MAFANIKIOOOO...
 
Naungana na wajum,be wanaosema kuwa ni ujinga kujadili suala hili sasa. kwa kuwa utaratibu uko wazi kabisa. Si dhambi kuspeculate nani atamchallenge JK, au nani hataki awe challenged.

Incompetency iliyooneshwa kwenye hii miaka mitano lazima ifungue milango.
 
Naungana na wajum,be wanaosema kuwa ni ujinga kujadili suala hili sasa. kwa kuwa utaratibu uko wazi kabisa. Si dhambi kuspeculate nani atamchallenge JK, au nani hataki awe challenged. Incompetency iliyooneshwa kwenye hii miaka mitano lazima ifungue milango.


Wampe Mheshimiwa Magufuli awafundishe kazi! Kikwetele wao hana jipya na hafai kwa lolote!
 
Hawa unaowasikia wanampinga Karume ,maana Karume anatayarishwa kuchukua nafasi ya Kikwete ,ikiwa Kikwete ataamua kuachia ngazi ,ila wapo katika kutoa ishara kuwa hakuna sababu ya Kikwete kuachia ngazi, kama unakumbuka Mwinyi alipomaliza kuwa Raisi wa Zanzibar alipewa wa Tanzania na ndio hivyo hivyo ,kama unavyofahamu taratibu za CCM ,ili kujificha na ile dhana kuwa Zanzibar haipewi uongozi wa Tanzania ,ndio inaonekana kuwa Karume apishwe katika kipindi hiki au hata Kikwete akimaliza miaka kumi yake kama akiipata apewe Karume.Ni utaratibu wanaosema wamejipangia au wameamua kuurudisha ili kudumisha muungano.

Hiyo ndiyo CCM tunayoifahamu baadhi yetu. Mgombea mwingine ni 2015.
 
Hata kama hiyo ndiyo CCM mnayoifahamu, sasa kwa nini zinaanza kutumika nguvu kuhalalisha mgombea wa 2010? Kulikoni?

Hakuna nguvu yoyote inayotumika. Wengi wa unaowasikia wanasema ili Kikwete awasikie, awasamehe kwa yale ya 2005, ikibidi wakifa wazikwe kwa heshima zote za CCM.
 
Wampe Mheshimiwa Magufuli awafundishe kazi! Kikwetele wao hana jipya na hafai kwa lolote!

Sijui ni kwanini watanzania wana miyoyo thaifu kiasi hiki, nasema hivi kwa sababu kila mmoja anajua kuwa kwama ni uongozi ktk nchi hii kwa sasa hakuna anayeweza kumfikia MAGUFULI sasa kwanini tusimjaribu japo huyu tukaona,tatizo letu wana CCM hatumtaki kabisa kiongozi mkweli.mfano si mlishuhudia yaliyomtokea Agustino L Mrema?
 
Heshima Mbele

Habari nilizozipata hivi sana ni kuwa wzee wa CCM wamekaa na kukutana na waandishi wa habari na kusema kuwa hakunakiongozi mwingine ambaye ana sifa zinazofanana na kikwete.

Hivyo wmasema asijitokeze mtu mwingine wa kumpiga 2010

Mie nimepatwa na mshtuko sana.Inawezekana hakuna kiongozi mwenye sifa kama za JK?Yes ndiyo inawezekana kwa kuwa sifa alizonazo tunazijua.

Hawa wazee ni nja inayoswasumbua tu,yaani tumefika hapa kweli?

watu tunasupport mambo kwasababu ya utashi wetu?

Kwa kuwa ni wazee wa CCM?NO WAY

Huu ndiyo utu uzima??watu wanakuja tu na kusema mabo ambayo yanakataza haki za watu?Nchi hii kama ikiendelea hivi basi maendeleo tutayasikia kwa wenzetu tu


My Take:
Hao wazee wamechanganyikiwa na Siye kama wananchi tumerogwa!Haiwezekani Maisha ni magumu kama hivi sasa na hakuna suluhishi la mambo muhimu ya kiuchumu na kitaifa mtu anajitokeza na kuongea haya?

Tanzania yenye wazee wa aina hii Haiwezekani,Chukua hatua kwa kukataa mawazo mbaaya ya hawa wazee
 
Gembe,
Mkuu kwani Uongo?
Nani CCM anaweza kuwa bora kuliko Kikwete naomba sababu au vigezo vya mtu huyo ktk Uongozi bora..
 
wazee ndio wameiangusha hii nchi, mimi binafsi siwapendi halafu wanapenda ku blackmail vijana, sio wazee tuu hata mapadri na masheikh
 
Gembe,
Mkuu kwani Uongo?
Nani CCM anaweza kuwa bora kuliko Kikwete naomba sababu au vigezo vya mtu huyo ktk Uongozi bora..

Mkandara ndiyo maana nasema tumerogwa na ikiwezekana na wewe ni mmoja wao.

Tuna mawazo ya kuamini kuwa bila flani kitu flani hakiwezi kwenda!

Mie mpaka sasa siwezi kuamaini yeye ni bora,Asiyejua na mipango mizuri,asiye na vision!

Chaguo la Mungu!anapendwa na watu!

Go to hell,Hawa wazee wamechanganyikiwa...
 
Hao ni wazee wa CCM, na hiyo ndiyo siasa (ndani ya CCM) sasa kama wewe unaona JK ni kibonde nilitegemea ungefurahia maana ataangushwa na upinzani kwa urahisi, unless unauhakika kuwa lazima CCM itashinda 2010 au wewe mwenyewe ni kada wa CCM.

Sisi wa DP ya CCM wala hayatuhusu... Jamani vijana na wazee wa JK wameshaingia kazini, huu ndio wakati wao wa kutengeneza deal, kumbe wakale wapi mzee?

Kama alijenga ukuta 2005, 2010 ana nunua bati...
 
Habari nilizozipata hivi sana ni kuwa wzee wa CCM wamekaa na kukutana na waandishi wa habari na kusema kuwa hakunakiongozi mwingine ambaye ana sifa zinazofanana na kikwete.

Igawa mwandishi hakuweka wazi kuwa ni pamoja na kiongozi mwingine kutoka vyama vya upinzani,lakini nalazimika kujua kua amemaanisha ni kote,haya ni mawazo potofu sana ambayo hayatatusaidia chochote,hii mambo ya chama ndio inayotupeleka kaburini,cham chama chama,nakataa kuamini kuwa hamna mtu mwenye uwezo mkubwa kushinda muheshimiwa,na kama wakitaka tuamini hivyo pengine ni in comparative tu wao wazee .
 
Wacha wazee hawa wajikumbushe enzi zile za Ujamaa na Kujitegemea walipokuwa wanatoa candidate moja eti tunampigia kura alafu tunaambiwa ni demokrasia kwa vile tunapiga tu kura ....
leo hii hawana uwezo wa kumwambia mtu kitu. Kama mtu ataamua kugombea hiyo ni haki yake kama mwanachama, kama hawataki wamtimue... alafu tutaona watafika wapi na huyu Msanii wao JK.
 
Gembe,
Mkuu kwani Uongo?
Nani CCM anaweza kuwa bora kuliko Kikwete naomba sababu au vigezo vya mtu huyo ktk Uongozi bora..

huenda tukijikumbusha yaliyotokea Chimwaga kabla ya uchaguzi wa 2005 tunaweza pata jibu;

...Mkapa, aliwataka wana-CCM kuzingatia mambo matano muhimu katika kumchagua mgombea anayefaa ambayo ni pamoja na kujiuliza kama mgombea anakubalika na pande zote za muungano na katika ushindani wa vyama vingi, kuzingatia kuwa wapiga kura wengi ni vijana na wanataka nini toka kwa viongozi wao, kama mgombea amechipuka na kukulia kwenye chama na wachague mtu anayefahamu vizuri chama cha CCM.

Alisema chini ya uongozi wa kiongozi huyo ni lazima mapinduzi na muungano uimarike na Tanzania hiindele kuwa nchi yenye umoja. Aidha, kiongozi huyo asiwe na chuki, hasira

Aliwakumbusha wanachama wasichague mtu kwa kumpenda bali achaguliwe kwa sifa na kutoa mfano wa bangili kwamba hata ikiwa nzuri, lakini inapobana kwenye mkono haifai.
Rais Mkapa alisema kamwe mataifa ya nje hayawezi kuwachagulia Watanzania Rais na kuwataka wananchi wazingatie maslahi ya nchi.

Tujitahidi kutafuta mgombea mwadilifu kadri iwezekanavyo, mwenye dosari chache na asiyetumia madaraka yake vibaya, alisisitiza.
Aidha, aliwataka wanachama hao kukumbuka kuwa kabla ya kupiga kura wapunguze kujifikiria wao binafsi na kundi lao katika chama.

Aliwakumbusha kuwa Rais atakayechaguliwa atakuwa ni Amiri Jeshi Mkuu hivyo anahitaji kuheshimiwa na mtu mwenye msimamo thabiti asiyeyumbishwa.
Aliongeza kuwa hatutaki rais anayeyumbishwa, anayeanza kwa kuchechemea na anayefaa kwa wakati huu tu bali na ujao.
 
Back
Top Bottom