The road towards 2010 Elections

Kati ya hawa nani atafaa kutuongoza 2010-2015?

  • Edward Lowassa

    Votes: 0 0.0%
  • Dr. Slaa

    Votes: 7 38.9%
  • Prof. Lipumba

    Votes: 0 0.0%
  • Mizengo Pinda

    Votes: 5 27.8%
  • Samwel Sitta

    Votes: 0 0.0%
  • Jakaya Kikwete

    Votes: 2 11.1%
  • Mark Mwandosya

    Votes: 2 11.1%
  • Harisson Mwakyembe

    Votes: 2 11.1%
  • None of The above

    Votes: 0 0.0%

  • Total voters
    18
  • Poll closed .
Hebu wanaJF tujaribu kuliweka hili sawa dalili zote za muda wa CCM- Ku-expire zinaonekana hata kwa mtu wa kijijini ambaye alipewa kofia , kitenge, pilau na maneno mazuri ya kumtia imani kwamba ukali wa maisha utapungua kwa KAULI MBIYU ya Maisha Bora Kwa Kila Mtanzania, akalala nje kuchunga kura yake isipotee kapingwa na jua, vumbi kali sasa ndiyo wanaona makali yake ,makali ya kipindi cha kampani yalikuwa na nafuu kuliko sasa.

wachache waliaidiwa wao wamepata sisi tuliyo wengi walala hoi je?
 
Mhh.. 2010 ni karibu mno hakuna dalili za kuonesha CCM is collapsing na CHADEMA is so progressing.

Labda Utufafanulie, Uchungu na ukali wa maisha ndio huwa kila leo!
 
You know what kills Upinzani in Tanzania.
1. Poor and weak strategies
2. Greed and narrow mind point of view
3.Fight for top management while they don't establish there grass root strong
4.In adequate of leaders who are real motivated
5.Old fasion political game, (Only CHADEMA i see has new strategy)
can someone tell me, what make Lipumba to run for position over and over and how about Mrema? This people are greed.

Tanzanian don't need upinzani hewa, we want more wabunge, and when we start in the bunge we grow stronger, Don't think about presidential position while you have wabunge.
 
hii nimeisoma na kujiuliza maswali mengi sana:

jee kuna ukweli kuwa wako vigogo ndani ya CCM wanawafadhili wapinzani kwa pesa au njia nyengine ili kujiweka sawa 2010?

jee kuna wafanyabiashara ambao wanataka kuwania urais kwa kupitia umoja wa upinzani na sasa ndio wanaoufadhili upinzani kuzunguka nchi?

jee fedha inayotumika ikiwa suala A na B sio zinatokea wapi?
jee ni sahihi kutembea nchi nzima na kuwapandish hasira takatifu wananchi?

na baada ya kuwapandisha hasira jee kuna lipi ambalo laweza kutokea kutokana na hasira hizo?

jeee litakalotokea ni faida kwa taifa?

ni maswala ni mengi huenda na wenzangu mkisoma yataongezeka na pengine tutapata majibu ya haya na hayo

Wapinzani wadaiwa kufadhiliwa na 'mtu anayetaka urais 2010'



Mrema akana, asema yeyote ni mfadhili wao
Adai helikopta gharama rahisi kuliko shangingi
Waziri Chenge asema hawezi kujibu 'utumbo'


Na Reuben Kagaruki

VYAMA vinne vilivyoanzisha umoja wa kushirikiana vya Tanzania Labour Party (TLP) NCCR-Mageuzi, CHADEMA na Chama cha Wananchi (CUF) vinadaiwa kufadhiliwa na mfanyabiashara mmoja maarufu mwenye malengo ya kugombea urais mwaka 2010 ili viongozi wa vyama hivyo wazunguke nchi nzima kusaidia kumwekea mambo yake sawa.

Hata hivyo, Mwenyekiti wa TLP, Bw. Augustino Mrema, alipoulizwa kuhusiana na madai hayo kwa njia ya simu Dar es Salaam jana, alikana na kusisitiza kuwa wanafanya kazi hiyo ili kuamsha Watanzania wapate hasira 'takatifu' waondokane na undondocha unaowafanya wanyamaze kimya huku nchi ikitafunwa na kikundi cha wachache.

Alikana madai hayo huku kukiwa na taarifa kutoka vyanzo mbalimbali vya habari kuwa kuna mfanyabiashara anayefadhili vyama hivyo vianze kazi ya kumsafishia njia asiweze kupata shida ya kuingia Ikulu katika Uchaguzi Mkuu mwaka 2010.

Bw. Mrema alisema wao kazi wanayoifanya ni takatifu na mtu yeyote mwenye uchungu na nchi hii anaweza kuwasaidia kufanikisha lengo hilo.

"Lengo ni kuwahamasisha Watanzania wapate 'hasira takatifu' kwani wamezidi mno kuwa ndondocha wakati ufisadi unazidi kuwa mkubwa," alisema na kuwaomba watu waadilifu wakiwemo viongozi wa dini wajitokeze kusaidia vuguvugu la ukombozi dhidi ya watu walioamua kupora nchi.

Alisema mbali ya kutumia helikopta, ikiwezekana watatembea kwa miguu au mikokoteni kueneza hasira takatifu ili watu wagomee kigenge alichoita ni cha walaji wachache wanaoendeleza ufisadi huo.

Alipobanwa zaidi amtaje mfadhili wao alisema; "Ni mapema mno kusema kuna mfadhili. Sisi hatuna hela za rushwa, wala bangi, wala dawa zakulevya ...kama kuna mtu mwema ajitokeze atusaidie,".


Alipoulizwa kama hawana fedha wamepata wapi uwezo wa kukodi helikopta, Bw. Mrema alisema; "Nimegundua gharama za kuendesha shangingi ni kubwa kuliko helikopta. Mfano tulikwenda Sumbawanga (Rukwa) kwa saa. Tulitumia fedha kidogo kuliko tungetumia shangingi," alisema.

Alisema ni jambo la kusikitisha kusikia Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Abbas Kandoro, akihaha kutafuta sh. bilioni 10 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 822 wakati huo kuna watu hapa nchini wanajitangaza kwenye vyombo vya habari wanapata kipato zaidi ya fedha anazohitaji.

Alisema hayo wakati akirejea agizo la Bw. Kandoro kutaka wakazi wote wa Dar es Salaam kuchangia sh. bilioni 10 za ujenzi wa madarasa kwa ajili ya wanafunzi watakaomaliza darasa la saba mwaka huu watakaofaulu kwenda sekondari mwakani.

Wakati huo huo, Waziri wa Miundombinu, Bw. Andrew Chenge aliyekuwa Mwanasheria Mkuu katika Serikali ya awamu ya tatu aliyetajwa na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Wilbroad Slaa kama mmoja wa viongozi wanaotuhumiwa kwa ufisadi kwa kuishauri vibaya Serikali katika mikataba alisema hana muda kujibu 'utumbo huo'.

Akizungumza kwa simu na gazeti hili kutoka Sengerema, Mwanza aliko kwenye ziara, Bw. Chenge alisema kwa kifupi: "Mimi nakagua barabara huku bwana. Sina muda wa kujibu utumbo huo na kukata simu yake ya mkononi.

Bw. Chenge anakuwa mtu wa pili kujibu hadharani tuhuma zilizoelekezwa kwake na Dkt. Slaa. Wa kwanza alikuwa mwanasheria, Bw. nimrod Mkono.

Bw. Mkono juzi alikanusha tuhuma zilizoelekezwa kwake kwa kutoa vielelezo kutoka wakala wa Usajili wa Makamouni BRELA vinavyoonesha makampuni aliyodaiwa kuwa Mkurugenzi si yake na akachanganua malipo yake ya mabilioni ya fedha anayolipwa kihalali katika kesi ya Benki Kuu (BoT).

Source : majira
 
hii nimeisoma na kujiuliza maswali mengi sana:

jee kuna ukweli kuwa wako vigogo ndani ya CCM wanawafadhili wapinzani kwa pesa au njia nyengine ili kujiweka sawa 2010?

jee kuna wafanyabiashara ambao wanataka kuwania urais kwa kupitia umoja wa upinzani na sasa ndio wanaoufadhili upinzani kuzunguka nchi?

jee fedha inayotumika ikiwa suala A na B sio zinatokea wapi?
jee ni sahihi kutembea nchi nzima na kuwapandish hasira takatifu wananchi?

na baada ya kuwapandisha hasira jee kuna lipi ambalo laweza kutokea kutokana na hasira hizo?

jeee litakalotokea ni faida kwa taifa?

ni maswala ni mengi huenda na wenzangu mkisoma yataongezeka na pengine tutapata majibu ya haya na hayo

Wapinzani wadaiwa kufadhiliwa na 'mtu anayetaka urais 2010'



Mrema akana, asema yeyote ni mfadhili wao
Adai helikopta gharama rahisi kuliko shangingi
Waziri Chenge asema hawezi kujibu 'utumbo'


Na Reuben Kagaruki

VYAMA vinne vilivyoanzisha umoja wa kushirikiana vya Tanzania Labour Party (TLP) NCCR-Mageuzi, CHADEMA na Chama cha Wananchi (CUF) vinadaiwa kufadhiliwa na mfanyabiashara mmoja maarufu mwenye malengo ya kugombea urais mwaka 2010 ili viongozi wa vyama hivyo wazunguke nchi nzima kusaidia kumwekea mambo yake sawa.

Hata hivyo, Mwenyekiti wa TLP, Bw. Augustino Mrema, alipoulizwa kuhusiana na madai hayo kwa njia ya simu Dar es Salaam jana, alikana na kusisitiza kuwa wanafanya kazi hiyo ili kuamsha Watanzania wapate hasira 'takatifu' waondokane na undondocha unaowafanya wanyamaze kimya huku nchi ikitafunwa na kikundi cha wachache.

Alikana madai hayo huku kukiwa na taarifa kutoka vyanzo mbalimbali vya habari kuwa kuna mfanyabiashara anayefadhili vyama hivyo vianze kazi ya kumsafishia njia asiweze kupata shida ya kuingia Ikulu katika Uchaguzi Mkuu mwaka 2010.

Bw. Mrema alisema wao kazi wanayoifanya ni takatifu na mtu yeyote mwenye uchungu na nchi hii anaweza kuwasaidia kufanikisha lengo hilo.

"Lengo ni kuwahamasisha Watanzania wapate 'hasira takatifu' kwani wamezidi mno kuwa ndondocha wakati ufisadi unazidi kuwa mkubwa," alisema na kuwaomba watu waadilifu wakiwemo viongozi wa dini wajitokeze kusaidia vuguvugu la ukombozi dhidi ya watu walioamua kupora nchi.

Alisema mbali ya kutumia helikopta, ikiwezekana watatembea kwa miguu au mikokoteni kueneza hasira takatifu ili watu wagomee kigenge alichoita ni cha walaji wachache wanaoendeleza ufisadi huo.

Alipobanwa zaidi amtaje mfadhili wao alisema; "Ni mapema mno kusema kuna mfadhili. Sisi hatuna hela za rushwa, wala bangi, wala dawa zakulevya ...kama kuna mtu mwema ajitokeze atusaidie,".


Alipoulizwa kama hawana fedha wamepata wapi uwezo wa kukodi helikopta, Bw. Mrema alisema; "Nimegundua gharama za kuendesha shangingi ni kubwa kuliko helikopta. Mfano tulikwenda Sumbawanga (Rukwa) kwa saa. Tulitumia fedha kidogo kuliko tungetumia shangingi," alisema.

Alisema ni jambo la kusikitisha kusikia Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Abbas Kandoro, akihaha kutafuta sh. bilioni 10 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 822 wakati huo kuna watu hapa nchini wanajitangaza kwenye vyombo vya habari wanapata kipato zaidi ya fedha anazohitaji.

Alisema hayo wakati akirejea agizo la Bw. Kandoro kutaka wakazi wote wa Dar es Salaam kuchangia sh. bilioni 10 za ujenzi wa madarasa kwa ajili ya wanafunzi watakaomaliza darasa la saba mwaka huu watakaofaulu kwenda sekondari mwakani.

Wakati huo huo, Waziri wa Miundombinu, Bw. Andrew Chenge aliyekuwa Mwanasheria Mkuu katika Serikali ya awamu ya tatu aliyetajwa na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Wilbroad Slaa kama mmoja wa viongozi wanaotuhumiwa kwa ufisadi kwa kuishauri vibaya Serikali katika mikataba alisema hana muda kujibu 'utumbo huo'.

Akizungumza kwa simu na gazeti hili kutoka Sengerema, Mwanza aliko kwenye ziara, Bw. Chenge alisema kwa kifupi: "Mimi nakagua barabara huku bwana. Sina muda wa kujibu utumbo huo na kukata simu yake ya mkononi.

Bw. Chenge anakuwa mtu wa pili kujibu hadharani tuhuma zilizoelekezwa kwake na Dkt. Slaa. Wa kwanza alikuwa mwanasheria, Bw. nimrod Mkono.

Bw. Mkono juzi alikanusha tuhuma zilizoelekezwa kwake kwa kutoa vielelezo kutoka wakala wa Usajili wa Makamouni BRELA vinavyoonesha makampuni aliyodaiwa kuwa Mkurugenzi si yake na akachanganua malipo yake ya mabilioni ya fedha anayolipwa kihalali katika kesi ya Benki Kuu (BoT).

Source : majira

Wanafadhiliwa na dua na sala za walalahoi.Majira ni mouthpiece ya wanamtandao.
 
Sioni mtu yeyote huko CCM anayestahili kugombea 2010 hata 2015 naona mauzauza tu na viongozi uchwara walioweka mbele maslahi yao badala ya yale ya Watanzania.
 
Watuambie kwanza wao SISIEMU Fedha za kuendesha chama chao SISIEMU wanazitoa wapi?

Kabla ya 2010 lazima wafe Vingunge huko SISIEMU ili kutambikia Ufisadi, Ufisadi si tabia tu kwao ni Imani.

Inaelekea Kashfa zimetanda miili yao kama Siafu sasa wanatafuta mchawi ndani ya nyumba yao wenyewe.

SISIEMU mkome kulinga na fedha zenu Haramu.

Maisha yenu yote yanategemea Ufisadi

Watoto wenu wanasoma kwa fedha za Ufisadi.
Wake zenu wanavaa vizuri kweli kweli kwa fedha za Ufisadi
Uturi na Poda zote za wake zenu na vimada wenu ni juu ya fedha za Ufisadi.
Suti zenu za Pande tatu na za Haki Ya Mungu ni za kuficha Ufisadi.
Mahekalu yenu magari yenu na miradi yenu ni ya kifisadi
Heshima Utukufu na mamlaka yenu ni juu ya Ufisadi.
Mungu wenu ni ufisadi.
Imani na ulimwengu wenu usioonekana ni wa kifisadi.
Mnaheshimu fedha za Ufisadi kuliko Mama zenu na Baba zenu wazazi.
Mvi zenu zimejaa Ufisadi.
Hotuba zenu maongezi yenu na maandishi yenu yamejaa ufisadi.
Busara zenu Hekima zenu na njozi zenu zimejaa ufisadi.
kuamka kwenu Kula kwenu na kufanya kazi kwenu ni kwa kifisadi

Hata dhamanA ya kuongoza nchi mmeipata KIFISADI.
 
kama kweli yupo na aendelee kuwafadhili il kuwatoa watanzania katika 'undondocha', kwani wakishatoka huko sidhani kama atakuwa na nafasi ya kufanya ufisadi.
Na hakika ili aweze kuukwaa itambidi awe na rekodi safi kuliko mgombea mwenza wa CCM, kwani siasa ya kuchafuana itatawala, na katika hayo wananchi watafunuliwa zaidi.


Mungu Ibariki Afrika,
Mungu Ibariki Tanzania.
 
kama kweli yupo na aendelee kuwafadhili il kuwatoa watanzania katika 'undondocha', kwani wakishatoka huko sidhani kama atakuwa na nafasi ya kufanya ufisadi.
Na hakika ili aweze kuukwaa itambidi awe na rekodi safi kuliko mgombea mwenza wa CCM, kwani siasa ya kuchafuana itatawala, na katika hayo wananchi watafunuliwa zaidi.


Mungu Ibariki Afrika,
Mungu Ibariki Tanzania.

kasana nakubaliana nawewe ndugu,

Kama huyo mfadhili yupo MUNGU WETU AMBARIKI SANA NA AMZIDISHIE KWA KILE ATOCHO SABA MARA SABINI!
Hakika kazi yake ni ya kupongezwa sana kwani anawatoa wabongo katika usingizi mzito! Na usingizi ukisha toka upenyo wa kuongozwa na fisadi utakuwa mfinyo sana!

Na kama yupo, huyo ndo Mzalendo Namba moja kwani yuko tayali kutoa mali zake kwa ajili ya Ukombozi wa wengi!
 
Utumbo tu na kutaka wananchi wasahau habari za mafisadi na wahamie kuanza kumtuhumu Mengi.

Naona kipenzi changu Mrema kawa mjanja safari hii. Naona amecheza ngoma vizuri labda ndio uzee na experience vinamsaidia.
 
Kinachoendelea ni shughuli ya WAHANDISI wetu wa habari kutengeneza majungu. Hapa jungu linaivishwa dhidi ya REGINALD MENGI ambaye uasi wake kundini unaongezeka makali kila kukicha. Hivi sasa hata NIPASHE na GUARDIAN wamepewa go ahead ya kuandika kila kitu bila ya kusita wala kufinya macho.....

Tanzanianjema
 
Watamhadaa nani CCM? Hii habari ni matokeo ya upuuzi wa Rostam na wahariri wa Majira kutaka kubadilisha hoja. Tumeshamshtuki tangu zamani, yeye hajui tu. Sisi bado tunawatumbulia macho mafisadi. Pole pole watajua hasira za Watanzania maana yake ni nini.
 
Wakati huo huo, Waziri wa Miundombinu, Bw. Andrew Chenge aliyekuwa Mwanasheria Mkuu katika Serikali ya awamu ya tatu aliyetajwa na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Wilbroad Slaa kama mmoja wa viongozi wanaotuhumiwa kwa ufisadi kwa kuishauri vibaya Serikali katika mikataba alisema hana muda kujibu 'utumbo huo'.

Akizungumza kwa simu na gazeti hili kutoka Sengerema, Mwanza aliko kwenye ziara, Bw. Chenge alisema kwa kifupi: "Mimi nakagua barabara huku bwana. Sina muda wa kujibu utumbo huo na kukata simu yake ya mkononi.

Bw. Chenge anakuwa mtu wa pili kujibu hadharani tuhuma zilizoelekezwa kwake na Dkt. Slaa. Wa kwanza alikuwa mwanasheria, Bw. nimrod Mkono.

Bw. Mkono juzi alikanusha tuhuma zilizoelekezwa kwake kwa kutoa vielelezo kutoka wakala wa Usajili wa Makamouni BRELA vinavyoonesha makampuni aliyodaiwa kuwa Mkurugenzi si yake na akachanganua malipo yake ya mabilioni ya fedha anayolipwa kihalali katika kesi ya Benki Kuu (BoT).

Kiasi aute utumbo yeye si anakula nyama isyo na mifupa.....
 
Baada ya watu kunivumishia kwamba sitagombea mwaka 2010 kwa sababu ambazo wenyewe walitaka kuzisema natangaza rasmi kwamba nitasimama mwaka 2010.Huu ni uamuzi wangu mwenyewe na pia maombi makubwa toka Jimboni kwangu .Wazee wa Jimbo langu wamenifuta hapa nyumbani kwangu.Haya ni maneno ya Zitto mwenyewe ananieleza haya .Zitto anaendelea kusema kwamba anaamini mwaka 2010 kutakuwa na wabunge wengi zaidi vijana wa Upinzani so nataka kuwapo tuenmdelee kuitetea Tanzania yetu kwa ajili ya watoto wetu na vizazji vijavyo.Zitto anahitimisha kwa kusema mniombee kwa Mungu .


Mimi nasema Homgera Zitto kwa kutoa msimamo wako huo .
 
Hizi ni habari nzuri kama ni kweli amebadili mawazo yake, moto ambao Zito ameuwasha uendelee kwa kasi ili tuwamalize mafisadi wote na vibaraka wao.
 
Baada ya watu kunivumishia kwamba sitagombea mwaka 2010 kwa sababu ambazo wenyewe walitaka kuzisema natangaza rasmi kwamba nitasimama mwaka 2010.Huu ni uamuzi wangu mwenyewe na pia maombi makubwa toka Jimboni kwangu .Wazee wa Jimbo langu wamenifuta hapa nyumbani kwangu.Haya ni maneno ya Zitto mwenyewe ananieleza haya .Zitto anaendelea kusema kwamba anaamini mwaka 2010 kutakuwa na wabunge wengi zaidi vijana wa Upinzani so nataka kuwapo tuenmdelee kuitetea Tanzania yetu kwa ajili ya watoto wetu na vizazji vijavyo.Zitto anahitimisha kwa kusema mniombee kwa Mungu .


Mimi nasema Homgera Zitto kwa kutoa msimamo wako huo .

Hivi alivumishiwa kuwa hatagombea au alitangaza mwenyewe kuwa hatagombea?

I always take an extra care on whatever posted by Lunyungu, and I believe my worry will soon be substantiated.

Zitto might have change his mind and of course has the right to do so, but the words used by Lunyungu could easily been "inserted" by the reasons best known to poster!
 
Mimi nampongeza Zitto kwa kubadili uamuzi wake na kuamua kugombea tena ubunge 2010. Yeye sasa ni mtu muhimu kwenye siasa za upinzani kwahiyo kuondoka ingelikuwa pigo. Kwa kushirikiana na Dr. Slaa naamini watawasha cheche bungeni na kulifanya bunge liwe makini zaidi.

Ila tu kusema alivumishiwa ni uongo na kama Zitto mwenyewe ndio anasema hivyo, basi aje hapa JF tumpe data zake. Vinginevyo hii ni spinning nyingine yenye nia ya kuwadanganya Watanzania badala ya kutuambia ukweli.

Hivi lini mtaelewa kwamba siasa sio lazima mdanganye watu?
 
Masatu naomba kwanza uonyeshe mahala ambapo nimesha andika habari za uzushi ama uongo kabla hujaanza kuwapa watu tahadhali. Pili nasema sina sababu ya kumpamba Zitto ili niweze kubadilisha maneno yake . Nimefanya maongezi haya na Zitto na nime mweleza lazima nitasema kule Jamboforum na akasema ahadi yake inabakia kuwatumikia Watanzania.Zitto alidhani was time kwenda kusoma zaidi na anaamini kwamba Ubunge si mali yake kama walivyo wabunge wengi was CCM kama Kingumge , Malecela nk. Ubunge unatumikia na kuachia ukiona inatosha na si kugeuza Jimbo mali yako na familia yako .

Again nasisitiza Zitto kanieleza mimi licha ya kusema na wana Habari kwamba atasimama tena na ana mipango kabambe ya kwenda kuendeleza ujenzi wa Jimbo lake . Kazi iko pale pale na wewe nanihii acha majungu hapa .
 
Basi ni uamuzi mzuri sana.Hata hivyo tufikie mahali tuwe wakweli.Hivi Zitto hilo suala alivumishiwa? ok,yeye nakumbuka alisema aliongea na yule mwamndishi wa habari ila hakufanya press comference lakini mwandishi akaibeba kama alifanya nae press comference.Hata hivyo zitto atafanya jambo la maana sana kama safari hii atafanya press comference atangaze msimamo ili kuondoa comfussion na saije akashabihiana na CCM.Mzee zitto heshima yako mkuu,jaribu tu kuweka mambo clear mapena kwani kwa uzoefu wangu nadhani mabo kama haya yana madhara sana kisiasa
 
Back
Top Bottom