KakindoMaster
JF-Expert Member
- Dec 5, 2006
- 1,356
- 91
MwK'
Hili ni tatizo dogo na limekwishajulikana. Iliyobaki ni kwa wapinzani kuitangazia Tanzania yote kungali mapema kabisa kwamba upuuzi huu hauwezi kuendelea kuvumiliwa. Hayo yote na yaliyotokea Kiteto upinzani ni lazima wajiweke tayari kuyakabili kwa nguvu zote zinazowezekana. Wakati wa kulialia tu ili kuonewa huruma umepitwa na wakati.
Tatizo kubwa ni kuwaelimisha wananchi ili wawakatae CCM.
Aliyezungumzia suala la kiteto nafikiri kidogo hakujua ni jinsi gani CCM waliwekeza nguvu zao zote ambazo hazitaweza kuonekana wakati wa uchaguzi 2010. Hili lilitokea kwa sababu CCM yote, vyombo vyote vya dola vilielekezwa kiteto. Kwa njia hii hakukuwa na uwezo wowote wa kushinda.
Walio angalia uchaguzi uliopita vizuri watakubaliana nami kuwa CCM inashindika ni mikakati tu. Uchaguzi uliopita wabunge wengi wa CCM walipita siyo kwa kupendwa hila ilikuwa ni nguvu ya Kikwete na nguvu ya pesa alizokuwa nazo.
Watanzania walimchagua kikwete kwa pesa na ushawishi aliyokuwa amewaonyesha kuwa angeweza kufanya kazi na kuwaletea neema. Lakini kwa sasa ameingia uwanjani mpaka miaka mitano inaonekana tayari sina uhakika atajiteteaje kwa wananchi.
Labda tu kikwete ataweza kuwashawishi vizuri watanzania akiwatoa kafara rafiki zake(EL, RA, KAra, nk)ambalo pia haliwezekani. Vinginevyo wapinzania wanapoint nyingi sana za kuweza kufunika CCM kila mkoa.
Kikwete 2010 hatakuwa na influence yoyote ya kumrudisha mbunge wa CCM maana nayeye atakuwa hoehae. Kikubwa sana ambacho wapinzani wanatakiwa wafanye ni kuunda mkakati mapema sana.