Kubwajinga
JF-Expert Member
- Jan 23, 2008
- 2,193
- 299
Kubwajinga:
Una hoja sana kwenye posts zako. Lakini ambacho sijakupata ni kwa nini hasa wapinzani wasi-focus kwenye utais wakati uchaguzi unahusu urais, ubunge na madiwani? CHADEMA tuna uzoefu mzuri sana; chama chetu kimepata jina kubwa baada ya kusimamisha mgombea wa urais serious. Chama chetu pia kilipata idadi kubwa zaidi ya wabunge baada ya kuwekeza nguvu kubwa kwenye urais. Kwetu sisi, ushahidi tunao unaoonyesha a statistically significant correlation kati ya kusimamisha mgombea imara wa utais na kupata viti vingi vya ubunge.
Kitila,
Nafikiri wengi bado hawajanielewa. Ukisoma tena article yangu kwa utulivu utaona kuwa ninashauri kuwa Dr.Slaa aendelee kugombea ubunge na sio kuwa upinzani wasiwe na mgombea wa uraisi, kwani, sidhani kama Slaa ataweza kuing'oa CCM in 2010 akiwa kama mgombea wa CHADEMA pekee. CCM ina mizizi kila mahali, bila kuungana upinzani hawatawaweza.
Kama upinzani watajiunga pamoja na kuwa chama kimoja, hapo nitakubaliana na wazo la ku-sacrifice ubunge wa Slaa na kujaribisha uraisi. Bila ya hivyo, ni vema CHADEMA wakawa na uhakika wa kiti cha Slaa bungeni kuliko kuwapa nafasi CCM kukichukua.
Pia, akishindwa uraisi, mchango wake wa hivi sasa bungeni utakosekana na atakuwa non entity kama alivyo Mrema hivi sasa. Mrema angekuwepo bungeni, labda angekuwa ameibua mabomu mengi zaidi hasa ukitilia maanani kuwa yeye alikuwa mmoja wao.
Hii haina maana kuwa Chadema wasiwe na mgombea madhubuti, huyu anaweza kupatikana bila ku-sacrifice hizi nafasi zilizopo. Vigogo wa CCM ni moja kati ya wale wanaoweza kurubuniwa kujiunga hasa baada ya kukosa nomination za chama chao.
Kwa hiyo come 2010, kama upinzani bado watakuwa wamegawanyika, itakuwa jambo la busara kwa Chadema kumuacha Slaa katika ubunge na pia kutumia pesa yao zaidi katika chaguzi za wabunge. Wanaweza kusimamisha mgombea uraisi ambaye hana chance za kuwa mbunge au pia kutosimamisha kabisa kama ilivyofanya 2000.
Tatizo ni kuwa, tamaa ya madaraka iliyopo kwenye vyama, sidhani na maslahi mengine binafsi nafikiri yanawafanya iwe vigumu kwao kuungana maana kila kiongozi anaona ana-benefit zaidi wakibaki as they are.