The road towards 2010 Elections

The road towards 2010 Elections

Kati ya hawa nani atafaa kutuongoza 2010-2015?

  • Edward Lowassa

    Votes: 0 0.0%
  • Dr. Slaa

    Votes: 7 38.9%
  • Prof. Lipumba

    Votes: 0 0.0%
  • Mizengo Pinda

    Votes: 5 27.8%
  • Samwel Sitta

    Votes: 0 0.0%
  • Jakaya Kikwete

    Votes: 2 11.1%
  • Mark Mwandosya

    Votes: 2 11.1%
  • Harisson Mwakyembe

    Votes: 2 11.1%
  • None of The above

    Votes: 0 0.0%

  • Total voters
    18
  • Poll closed .
Nyani kwa maana hiyo mimi na wewe hatufai? Basi wengine kina Mtanzania na Mwafrika wa Kike wanafaa!
 
Unamwonea KadaMpinzani...! Usimwone kuwatetea ila facts zikija hata kama anazipinga zinamwingia sana akilini. Hawezi kuwa sawa na wao! Trust me, hapa tunafundana na nina imani kishajifunza mengi sana. He's a fast learner I assure you. That's KadaMpinzani

Kada ni mzuri sana kama kuna fact asemi chochote mfano thread ya Chenge akupost even a single posting mpaka watu wakamuuliza akasema awezi kupost kwa kuwa kila kitu ni fact na ndo maana wakati anasema haji tena JF nilimbembeleza hasichukue uamuzi huo kwa kuwa yeye ni muhimu hapa.
 
Nyani kwa maana hiyo mimi na wewe hatufai? Basi wengine kina Mtanzania na Mwafrika wa Kike wanafaa!

Kama vigezo vikiwa ni vya hali ya juu basi nakiri kwamba sitaweza ku-pass background check....sijui weye mwenzangu
 
Ila tuwe waangalifu na watu wanaotumia haya majina ya bandia humu ndani...wengine ni wanafiki tu....Ninayemuona anafaa ni Kitila Mkumbo peke yake...wengine ninaguna kidogo...

Hata mimi nakubaliana nawe katika hili ... Hawa wengine mpaka tuwajue kwa majina yao halisi ili tufanye upembuzi wa kina katika hili
 
Hata mimi nakubaliana nawe katika hili ... Hawa wengine mpaka tuwajue kwa majina yao halisi ili tufanye upembuzi wa kina katika hili
Mh!

Sasa hapo ndipo pabaya...! Mkuu Lunyungu anatumia jina lake la kweli. Then naye aaminiwe na atakapoomba ridhaa na ushirikiano wetu tumpe kila aina ya mchango aweze kutinga Bungeni mwaka 2010.

Itabidi watu waanze kujianika ikikaribia kipindi cha uchaguzi basi.
 
Mh!

Sasa hapo ndipo pabaya...! Mkuu Lunyungu anatumia jina lake la kweli. Then naye aaminiwe na atakapoomba ridhaa na ushirikiano wetu tumpe kila aina ya mchango aweze kutinga Bungeni mwaka 2010. Itabidi watu waanze kujianika ikikaribia kipindi cha uchaguzi basi.

Nakumbuka Mnyika alitoa wito hapa kwa wale wanaopenda kugombea kwa tiketi ya CHADEMA wawasiliane naye na baadhi ya watu walifanya hivyo.

Huu ni mwanzo na kama ikifanikiwa basi nchi yetu itakuwa na moto mpya wa maendeleo bungeni.
 
Naamini kabisa Dr. Slaa ndio mtu anaefaa kuwa Rais wa nchi yetu na mwenye uwezo mkubwa wa kulianzisha gurudumu la maendeleo nchini.
Back to the hoja,

Siamini kuwa Dr. Slaa anafaa kuwa rais! Naamini anafaa kuendelea kuwepo Bungeni. Think of it Geeque
 
Back to the hoja,

Siamini kuwa Dr. Slaa anafaa kuwa rais! Naamini anafaa kuendelea kuwepo Bungeni. Think of it Geeque


Dr Slaa anafaa sana kuwa nje kwa ajili ya balance and checks, ukiwa mtendaji unabanwa na majukumu so inabidi udelegate power, na hilo ndio tatizo kwa vile wanaoaminiwa na kupewa power mara nyingi hufanya ndivyo sivyo
 
Basi huu ni muda muafaka kwetu sote tukitumia nafasi ya kuongea na ndugu na jamaa zetu kule nyumbani kuwafahamisha jinsi gani CCM ilivyoharibu na inavyoendelea kuharibu Uchumi wa nchi yetu kila kukicha. Tutumie nafasi hizo wakati wanataka kutupiga mizinga au hata kabla ya kuwa-western union mambo fulani(joke) Tunahitaji mabadiliko na tusipokaza buti ndugu zangu tutabaki tukijilaumu wenyewe. CCM Has To Go, Kikwete Has To Go.

Unajua wakati mwingie nashangaa sana watu wa Tanzania, utakuta mtu analalamika kuwa ugumu wa maisha umeongezeka lakini baada ya dakika moja anaanza kummwagia misifa Kikwete. Yaani watu kama wamepumbazwa kwa kutoweza kuainisha shida zao na utawala wa CCM.
 
Basi huu ni muda muafaka kwetu sote tukitumia nafasi ya kuongea na ndugu na jamaa zetu kule nyumbani kuwafahamisha jinsi gani CCM ilivyoharibu na inavyoendelea kuharibu Uchumi wa nchi yetu kila kukicha. Tutumie nafasi hizo wakati wanataka kutupiga mizinga au hata kabla ya kuwa-western union mambo fulani(joke) Tunahitaji mabadiliko na tusipokaza buti ndugu zangu tutabaki tukijilaumu wenyewe. CCM Has To Go, Kikwete Has To Go.


CCM si rahisi kung'oka kirahisi kihiiiiivyo. Cha muhimu ni kuhakikisha kunakuwa na wabunge wengi wa upinzani, na ingawa rais atatoka ccm basi ushindi uwe kwa 51%, then 2015/20 upinzani unaweza kuchukua urais
 
Dr Slaa anafaa sana kuwa nje kwa ajili ya balance and checks, ukiwa mtendaji unabanwa na majukumu so inabidi udelegate power, na hilo ndio tatizo kwa vile wanaoaminiwa na kupewa power mara nyingi hufanya ndivyo sivyo

Kama sio Dr Slaa, je nani agombee?
 
Unajua Wanzania wenye integrity walishakata tamaa kujiingiza kwenye siasa na ndo maana wakabatiza kuwa siasa mchezo mchafu, na wasomi wachache waliojiingiza walijiingiza kwa masilahi binafsi, hakuna anayeingia kwenye siasa kutetea wananchi.

Wasomi wengi wakaishia nje ya nchi na kusahau kwao kwa sababu siasa zinawafrustrate, lakini i can the end of the tunel as siasa inaanza kubadilika na kuwa mtetezi wa wananchi, vichwa vitaanza kurudi kuja kutetea wananchi wao majimboni ili wapate barabara, umeme, zahanati na dawa sio majengo matupu, shule za msingi standard, shule za sekondari zenye walimu na maabara na vingine.

Kipato kitaongezeka maana babu yangu kule kata ya Rushwa Wilaya ya muleba, mkoa wa kagera ataweza kuuza mtama wake na uwele kwa wachaga wa moshi wakatengeneze mbege, kipato chake kitaongezeka atanunua bati na kuzeka nymba yake badala ya majani kama ilivyo sasa, atakuwa na uwezo wa kumlipia ada mjukuu mmoja atreast kwa mwaka kwenye shule ya kata yenye walimu wazuri na maabara inayokubalika.
Mbona mambo mengi, hayaishi.
 
CCM si rahisi kung'oka kirahisi kihiiiiivyo. Cha muhimu ni kuhakikisha kunakuwa na wabunge wengi wa upinzani, na ingawa atatoka ccm basi ushindi uwe kwa 51%, then 2015/20 upinzani unaweza kuchukua urais

Mama,

umesahau kuwa ccm wanatumia kila mbinu kushinda hata viti vya ubunge. Sasa hivi wanafanya kampeni ya kumtoa Chacha Wangwe kule Tarime. CCM wanauwezo wa kuchukua viti karibu vyote vya bara na Unguja kama wakipenda.

Katika hili tusidhani utani. CCM lazima inyang'anywe nguvu kubwa ya dola waliyonayo na ndipo wapinzani watapata hata hiyo asilimia 30 ya viti Bungeni. Umesahau alichofanya Mkapa kwa vyama vya upinzani kati ya 1995 na 2005? Alichukua karibu majimbo yao yote na kuvidumaza kabisaaaa
 
Mama,

umesahau kuwa ccm wanatumia kila mbinu kushinda hata viti vya ubunge. Sasa hivi wanafanya kampeni ya kumtoa Chacha Wangwe kule Tarime. CCM wanauwezo wa kuchukua viti karibu vyote vya bara na Unguja kama wakipenda.

Katika hili tusidhani utani. CCM lazima inyang'anywe nguvu kubwa ya dola waliyonayo na ndipo wapinzani watapata hata hiyo asilimia 30 ya viti Bungeni. Umesahau alichofanya Mkapa kwa vyama vya upinzani kati ya 1995 na 2005? Alichukua karibu majimbo yao yote na kuvidumaza kabisaaaa


Hapo ndio umuhimu wa katiba kubadilishwa unapokuja, katiba ya nchi bado imekaa kichama kimoja sana (mambo ya kushika hatamu).
 
Back
Top Bottom