The Rise and Fall of Augustine Lyatonga Mrema

The Rise and Fall of Augustine Lyatonga Mrema

oyaa!! Augustine Lyatonga Mrema atakumbukwa daima.
Ni wazi kila binadamu ana sehemu mbili chanya na hasi. Napenda kuongelea chanya za Lyatonga, huyu bwana ni mwanamageuzi wa kweli.wakati akiwa CCM na NCCR mageuzi niliwahi kuongea nae. Alikuwa na mipango madhubuti na alikuwa anajua anasema nini.Alifuata utashi wake na alitimiza wajibu wake.

Alipoingia NCCR alikuwa na mipango madhubuti ya kumkoma nyani, watu wa kulaumiwa ni akina Lamwai, Mabere na Ringo Tenga. Hawa watu walikuwa wasomi na ndio walikuwa wasanifu wa NCCR, niliwahi kuongea nao na nikiwauliza nini shida mnashindwa kuelewana marandu alinijibu kuwa Mrema anaakili nyingi sana huwezi cheza naye, nikimwuliza ninyi mlitengeza katiba kabla yake kwanini katiba yenu inawashinda, hakunijibu ila ukweli ni kwamba NCCR walitengeneza katiba ya kuwafaa viongozi ndio maana Mrema alipoanza kudili na katiba walishindwa kwani waanzilishi hawakuona mbali, kama vile itakavyotokea pale CCM itakaposhindwa na tume ya uchaguzi.

Mrema ana mengi sana ameyafanya ambayo hatuwezi kuyakataa, ni mwandemokrasia na mwana mapinduzi, alipigwa mishale mingi sana na CCM na kesi za kumwaga, alishaongelea sana matatizo ya tume ya uchaguzi, mgunduzi wa ufisadi wa serikali ya ccm ni chanzo cha kwanza cha kujiuzulu kwa mawaziri wa CCM, mbilinyi na mporogonyi. Mwiba wa mafisadi na wahamiaji maharamia. Mwiba kwa mama siti mwinyi kwenye wizi wa dhahabu. huyu jamaa alisaidia kupunguza wizi na ujambazi majambazi waliomba msamaha na kurjeesha silaha. ni huyu mrema aliye wahi kudhibiti matumizi mabovu ya magari ya serikali. ni huyu mrema aliyedhibiti unyanyasaji wa wanawake. Ni huyu mrema ambaye ameweza kuwa mbunge majimbo mawili moshi vijijini na temeke.

Hata kama kazeeka ni lazima akumbukwe kwa harakati zake za demokrasia tanzania, amepigwa mabomu ya machozi, amekamatwa na polisi na amefunguliwa kesi nyingi kuliko mtu yeyote. tutamkumbuka daima.
Mrema amekuwa mwiba tangia akiwa mbunge wa CCM amewahi kutishia kutoa shilingi kwenye mfumo wa chama kimoja alionyesha machungu na utetezi wa wanyonge hata pale ambapo alikuwa hana wala hapati umaarufu.

Ni lazima tukubali kujifunza kwa mashajaa wetu wa ukombozi wa demokrasia na watetezi wa wanyonge.
 
oyaa!! Augustine Lyatonga Mrema atakumbukwa daima.
Ni wazi kila binadamu ana sehemu mbili chanya na hasi. Napenda kuongelea chanya za Lyatonga, huyu bwana ni mwanamageuzi wa kweli.wakati akiwa CCM na NCCR mageuzi niliwahi kuongea nae. Alikuwa na mipango madhubuti na alikuwa anajua anasema nini.Alifuata utashi wake na alitimiza wajibu wake.

Alipoingia NCCR alikuwa na mipango madhubuti ya kumkoma nyani, watu wa kulaumiwa ni akina Lamwai, Mabere na Ringo Tenga. Hawa watu walikuwa wasomi na ndio walikuwa wasanifu wa NCCR, niliwahi kuongea nao na nikiwauliza nini shida mnashindwa kuelewana marandu alinijibu kuwa Mrema anaakili nyingi sana huwezi cheza naye, nikimwuliza ninyi mlitengeza katiba kabla yake kwanini katiba yenu inawashinda, hakunijibu ila ukweli ni kwamba NCCR walitengeneza katiba ya kuwafaa viongozi ndio maana Mrema alipoanza kudili na katiba walishindwa kwani waanzilishi hawakuona mbali, kama vile itakavyotokea pale CCM itakaposhindwa na tume ya uchaguzi.

Mrema ana mengi sana ameyafanya ambayo hatuwezi kuyakataa, ni mwandemokrasia na mwana mapinduzi, alipigwa mishale mingi sana na CCM na kesi za kumwaga, alishaongelea sana matatizo ya tume ya uchaguzi, mgunduzi wa ufisadi wa serikali ya ccm ni chanzo cha kwanza cha kujiuzulu kwa mawaziri wa CCM, mbilinyi na mporogonyi. Mwiba wa mafisadi na wahamiaji maharamia. Mwiba kwa mama siti mwinyi kwenye wizi wa dhahabu. huyu jamaa alisaidia kupunguza wizi na ujambazi majambazi waliomba msamaha na kurjeesha silaha. ni huyu mrema aliye wahi kudhibiti matumizi mabovu ya magari ya serikali. ni huyu mrema aliyedhibiti unyanyasaji wa wanawake. Ni huyu mrema ambaye ameweza kuwa mbunge majimbo mawili moshi vijijini na temeke.

Hata kama kazeeka ni lazima akumbukwe kwa harakati zake za demokrasia tanzania, amepigwa mabomu ya machozi, amekamatwa na polisi na amefunguliwa kesi nyingi kuliko mtu yeyote. tutamkumbuka daima.
Mrema amekuwa mwiba tangia akiwa mbunge wa CCM amewahi kutishia kutoa shilingi kwenye mfumo wa chama kimoja alionyesha machungu na utetezi wa wanyonge hata pale ambapo alikuwa hana wala hapati umaarufu.

Ni lazima tukubali kujifunza kwa mashajaa wetu wa ukombozi wa demokrasia na watetezi wa wanyonge.

NAKUKUBALI kinepi_nepi,keep it up.

NAKUKUBALI KWA DATA.
 
Mutungirei: Sifuati fedha TLP


ALIYEWAHI kuwa Katibu Uenezi Taifa wa chama cha Tanzania Labour (TLP), Benedicto Mutungirei amerudi katika chama hicho kinachoongozwa na Augustino Mrema.

TLP kimempa tena uanachama wa chama hicho miezi minne tangu kimfukuze kwa madai ya kuvunja Katiba ya chama hicho.

Katibu Mkuu wa chama hicho, John Komba, amesema leo kuwa, Halmashauri Kuu ya TLP kupitia Sekretarieti ya chama hicho ilipitisha uamuzi huo baada ya kubaini kuwa Mutungirei amejirekebisha.

Amewaeleza waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuwa, kwa mujibu wa Katiba ya chama hicho iwapo mwanachama aliyefukuzwa atajirekebisha sekretarieti ina uwezo wa kumrejesha iwapo itaridhika na marekebisho hayo.

"Kupitia kikao kilichofanyika Agosti 14, mwaka huu tunamrejesha Mutungirei na kumkabidhi kadi yake" amesema Komba.

Amesema kwa sasa chama hicho kimemrudishia uanachama wake na kwa kuwa ni mwanachama halali ana uwezo kuwania nafasi yoyote ya uongozi TLP na katika Uchaguzi Mkuu ujao.

Mutungirei amethibitisha kurejea katika chama hicho na kuongeza kuwa, mgongano uliokuwapo awali umekwisha.

Kwa mujibu wa mwanasiasa huyo,jambo la msingi kwake ni nafasi aliyonayo katika kukuza demokrasia.

"Nilisema kuwa sitaenda chama chochote na chama changu ni TLP, vyama vingi vimenifuata lakini sikwenda, lazima ikubalike kuwa siasa ina gharama yake na uvumilivu unahitajika, hapa sikufuata fedha hakuna hata hiyo fedha yenyewe lakini ningeenda kwingine kama CCM hata Ukuu wa wilaya ningepata," amesema.

Mutungirei amesema,msuguano ndani ya vyama si jambo zuri, na kwamba kilichotokea kwake ni suala la ushindani ambalo haliwezi kuwa kikwazo cha demokrasia kuchukua mkondo wake.

Amesema, wanachama wa chama wanapaswa kutambua kuwa hakuna tena mgongano ndani ya chama hicho.

Mutungirei alifukuzwa na chama hicho Aprili mwaka huu kwa tuhuma za kutoa taarifa za chama nje ya chama hicho jambo ambalo ni kinyume na Katiba ya chama hicho.

Hivi karibuni chama hicho pia kilimpa tena uanachama Naibu Katibu Mkuu Rajab Tao ambaye naye alifukuzwa kwa madai ya kukiuka Katiba ya TLP.
 
TLP kama chama cha siasa wamefanya jambo jema kuwarejesha wanachama wake waliofukuzwa kutokana na sababu mbali mbali.
Mara baada ya bwana W Lwakatare kujiunga kwa mbwembwe CHADEMA kuna mwajamvi mmoja alituletea habari kwamba kulikuwa na mpango wa kumpokea Bwana B Mtungurehi CHADEMA lakini hilo halikutokea.
Vyama vya upinzani yafaa kuacha kabisa mtindo wa kuibiana wanachama wenye kwa wenyewe.
Hongera Bwana Mtungurehi kwa uamuzi wako wa kukubali kumaliza matatizo ndani ya chama badala ya kuhamahama kama ilivyo desturi ya wanasiasa wenye njaa kali.
 
jamaa kafulia na utabiri wake.kwanza huyo mtungurei amesharudi tlp.na atagombea ubunge huko kwake kwa ticket ya tlp.hao chadema hata mrema akiwasema ni sawa tu maana hawana ushirikiano na vyama vingine.katika majimbo ya tarime,busanda,biharamulo na nk hawakuwapa nafasi wengine wanaokubalika kama cuf huko busanda.mrema nae atagombea ubunge huko vunjo.kama akishinda haiwezekani akarudi ccm.jus think about it.acheni assumptions
 
The only reason people are this nostalgic about the failure that is Mrema is the truism that we have a vacuum of leadership.

This vacuum is so fine that now people are entertaining elevating this joker Mrema. But I do not blame them entirely, in the middle of the Sahara, a dusty oasis may seem like pure cold mountain springwater.
 
Naona mzee Mrema angeiga mfano wa wenzake kama akina Mzee Mtei na Bob Makani. Asiwe kama mtu ambaye hawezi kupanda gari ambalo yeye siyo dereva. Angetoa mchango mubwa sana kama angebakia kwenye nafasi ya ushauri kwa TLP au hata kwa upinzani kwa jumla.
 
hakuna watu wanaoijua mahakama ya hakimu mkazi kisutu kama Mrema na Mtikila, duh jamaa walikua na kesi kila chumba!.
but atakumbukwa kwa mageuzi, si unakumbuka watu tulivyosukuma gari lake enzi zileee??, hata Nyerere haikutokea kabisa.
 
Mrema aheshimiwe kama kinara wa Upinzani Tanzania. Kama siyo yeye upinzani na hata watanzania wasingejua nini upinzani hadi leo na ingelitugharimu sana. Fikiria kamasi upinzani tungelijua juu ya EPA, Richmond, Kagoda, Kiwira n.k. Ila kama alivyowahi kusema ni kama muwindaji na kaambia wenye meno Kamata nyama na wanaendelea kutufaidisha na upinzani. Ushauri wangu ni kuwa Mrema sasa arudi SISIEMU. Akisharudi watatambua aliyoyafanya na kuyaenzi na wataweza kufikiria jinsi ya kumpunzisha kwa amani kama mpiganaji mahiri.
 
Siasa ina wakati wake,kupanda na kushuka Mzee wa Kiracharacha sasa kafulia bora apumzike asije kufa kwa kisukari.Inachekesha anakuwa wa kwanza kutoa ushauri kwa chadema.
 
Mrema pumzika kisukari kitakumaliza,kaa na wajukuu babu yetu,huo ndio ushauri wangu,kurudi CCM ni kula matapishi.
 
MWENYEKITI wa chama Tanzania Labour Party(TLP), Augustine Mrema amesema kitendo cha makada wa CCM kumlazimisha Rais Jakaya Kikwete kufanya maamuzi magumu ni sawa na kumuonea.

Mrema alisema kwamba kuonewa huko, kumetokana na baadhi ya makada wa siku nyingi ndani chama hicho kuwa na wivu binafsi na kiongozi huyo wa nchi.

"Sipo kwa ajili ya kumtetea au kumfagilia rais Kikwete, lakini si kweli kwamba hajafanya maamuzi, tayari amekwisha fanya hivyo na ndiyo maana alivunja baraza lake la mawaziri mara baada tua kujiuzulu kwa aliyekuwa waziri Mkuu, Edward Lowasa pamoja na mawaziri wawili, Ibrahimu Msabaha na Karamangi" alisema Mrema jana katika kipindi cha Kurunzi kinachorushwa na kituo cha televisheni cha Mlimani.

Mwenyekiti huyo ambaye tayari ametangaza nia yake ya kuogombea ubunge katika jimbo la Vunjo, alifafanua kwamba Rais Kikwete amekwisha dhihirisha kuwa amekwisha fanya maamuzi magumu na ndio maana katika utawala wake vigogo wengi wamefikishwa mahakamani.

'Hata ukiangalia katika serikali zote zilizopita huwezi kukutana idadi kubwa ya vigogo kama ilivyo sasa, ambao wamefikishwa mahakamani kwa tuhuma mbalimbali'

"Haya pia ni maamuzi magumu ambayo yamefanywa katika utawala huu, hivyo wanaosema kuwa hajafanya lolote ni watu wenye wivu na wanafiki" alisema Mrema.

Mrema alisema makada hao wanataka Rais Kikwete aendeshe nchi kwa ubabe, wakati ambapo hawezi kufanya hivyo kutokana kukua kwa utawala bora.

Hata hivyo alisema kwamba, Kama kweli makada hao wanaona Rais Kikwete anaendesha mambo kinyume na wanavyotaka, ni bora wangejiengua na kisha wakajiunga au kuanzisha chama chao cha upinzani.

"Mbona hawataki kutoka?" alihoji Mrema.

Alisema kwamba hata yeye wakati alipokuwa serikalini na kuona mambo hayaendi sawa alijiondoa na kujiunga na upinzani.

"Wakati nilipokuwa serikalini mara tu nilipogundua kuwa sipewi ushirikiano wa kutosha na wenzangu katika kupamba na vitendo viovu, nilijiengua na kujiunga na upizani", alisema Mrema.

Alisema kwamba anachokifanya Rais Kikwete kwa sasa ndicho alichokuwa akikifanya yeye wakati alipokuwa serikalini.

"Binafsi ninafarijika na jinsi utawala wa Rais Kikwete unavyopamba na vitendo vya ufisadi kwa kuwa sasa ni ajenda ya serikali na ya wananchi na haya ni muendelezo wa mapambano niliyokuwa nimeyaanzisha nilipokuwa serikalini," alisema.

Akizungumzia maamuzi ya kongombea ubunge katika jimbo la Vunjo ambalo kwa sasa linashikiriwa na mbunge Alyoce Kimaro(CCM), Mrema alisema; "Lengo langu ni kuwatumikia Watanzania katika ngazi zote na ndio maana nimefanya maamuzi haya"


MWANANCHI
 
Naombeni namba ya hawa TV ya mlimani sijui kama huwa wanapokea simu "live" maana naona wanaanza kuwa wabebaji ya sumu kali ya ulaghai wa kifikra..
 
Naombeni namba ya hawa TV ya mlimani sijui kama huwa wanapokea simu "live" maana naona wanaanza kuwa wabebaji ya sumu kali ya ulaghai wa kifikra..
.
MMKJJ, hii TV ya Prof. Mkandala hakuna 'live' yoyote, kila kitu ni recorded and for CCM. Kama ilivyo Redet na opinion polls zake.
 
huyu Mrema sasa hizi njaa, yaani Ubunge wa Moshi Vijijini ndo unampelekea kusema haya? au ndo zile fununu za kuwa siku zote yeye ni shushushu wa CCM anawazuga upinzani?
 
TV Mlimani nahisi ni extension ya Redet na ipo hapo kuganga njaa za Mkandala na wenzie wanaojipenkeza kwa CCM!!
 
huyu Mrema sasa hizi njaa, yaani Ubunge wa Moshi Vijijini ndo unampelekea kusema haya? au ndo zile fununu za kuwa siku zote yeye ni shushushu wa CCM anawazuga upinzani?
.
Mhh.Pumba hizi .
hayo ni maoni yake.Njaa hapo imetoka wapi?.Tusiwe kama kasuku.
 
Kama unampinga Mrema mpinge kwa hoja badala ya madongo yasiyokuwa na msaada kwa nchi na wana jamii!!.
 
Back
Top Bottom