KakindoMaster
JF-Expert Member
- Dec 5, 2006
- 1,356
- 91
Duuh! Sasa JF itafungiwa!
Suala la kufungiwa siyo suluhisho. Ni bora uweke sehemu ya kujua wananchi wako wanafikiria nini.
Unajua watu tumechoka kila siku MAFISADI, MAFISADI kila mahala. Na hao hao ndio viongozi tunaowategemea wawaondolee eti matatizo watanzania. Nafikiri hata ndani ya chama tawala wengi hawakubaliani na upuuzi huu.Kuna siku alipo tajwa, mzee John Marecela alishauliza bungeni kuwa wanataka kusema Chenge anayeheshimika anaweza kusainisha mikataba mibovu. Nafikiri Mzee John sasa atakuwa amepata majibu yake.
JK ambaye alipewa dhamana na watanzania kama ameshindwa kazi hakuna haja ya wananchi kugive up. Waziri Mkuu ameisha tamka kwamba Suala la UFISADI limeshindikana lakini hao hao kila kukicha wanapandisha gharama za maisha.
Sasa itafika wakati wananchi tujichukulie kasheria mkononi. Mtu kama Chenge nafikiri anawashinda viongozi wenzake lakini siyo watanzania au nguvu ya Umma. Watanzania wakiamua Chenge aondoke ataondoka tu.
Na kizuri chenge ni Mzito hawezi kuongea na wananchi wa kawaida hata siku moja nafikiri yeye itabidi atupishe tu aende kukaa na Lawyer wake huko USA maana makosa aliyo nayo ni mengi anaweza kuishia Segerea milele siku za usoni.
Kauli Mbiu ni kwamba: 'MAFISADI wataondoka Tanzania kwa nguvu ya Umma'