Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
This is a best story coming out of Tarime. Nimeonelea nianzishe maada si kuongelea Uchaguzi wa Tarme bali ni kuhusu CCM, Dola na Wananchi.
Nakumbuka enzi za enzi tulikuwa tunavisha Mbwa jezi za Simba wa Msimbazi. Hata siku moja sikuwahi kusikia kuwa Polisi pale Msimbazi, Polisi wilaya Ilala au Polisi mkoa Dar Es Salaam wakitafuta mchokozi aliyevisha mbwa fulana ya Simba!
Sasa huyu mbwa kavishwa jezi ya CCM, Serikali (yes Polisi ni Serikali!) ya CCM kupitia vyombo vya dola vimemkamata mwenye mbwa asaidie upelelezi kuelewa ni kwa nini mbwa alivaa vazi "tukufu" la nchi!
Mbwa huyu, masikini Bobi wa watu ameuawa, najiuliza kosa la Bobi lilikuwa nini wakati yeye alikuwa ni tarishi?
Labda upande mmoja, nitaelewa kwa nini Polisi wamkamate Mwenye mbwa kwa kuwa kitendo cha Bobi kutembea na fulana ya CCM, kilihatarisha usalama kwa kuchochea fujo.
Sasa swali langu ni hili kwenu ndugu Watanzania, inakuaje DOLA inafanya kazi kwa umakini kuilinda CCM au CCM ikiwa inahujumiwa lakini wengine na hata Taifa wakihujumiwa, DOLA hujivutavuta?
Hiza Tambwe katamba kuwa CCM ndicho chama chenye dola, ikiwa na maana ya Serikali na vyombo vyake hasa Mahakama, Polisi na Jeshi. Si mara ya kwanza kusikia Viongozi wa CCM na Serikali yake hasa nyakati za uchaguzi wakitanguliza vitisho vya kulinadi Jeshi la Polisi au nguvu za Serikali kupitia CCM.
Hivi Watanzania tu finyu wa upeo kudharau mambo na kuishia kughafilika kwa hasira za juu hata kutaka kutoa uhai? Hivi wangemvisha hiyo fulana kichaa, malaya au mwizi anayefahamika wakamtembeza barabarani kumtangaza kuwa CCM ni sawa na Kichaa, Malaya au Jambazi kama namna ya Fasihi, je wale wapenzi wa CCM wangefikia hatua ya kumuua bianadmu anayekidhalilisha Chama chao, badala ya kujibu mapigo ya ki itikadi hata kutunga taarabu au kumtumia John Komba aimbe angalau wimbo wenye kijembe kuwakebehi iwe Chadema, CUF au TLP?
Ni lini Mtanzania atapevuka na kuachana na hizi hisia mbovu za kujibu kebehi kwa hasira n a kukimbilia kutoa uhai?
Ni lini CCM wataacha kutishia kila mtu kuwa wao wanamiliki Polisi?
Je ilikuwa ni sahihi kwa Tambwe Hiza kutamka waziwazi kwenye jimbo la Marehemu Chacha Wangwe kuwa viongozi wakuu wa Chadema ndio watuhumiwa wa kifo cha Wangwe ambacho tuliambiwa ni ajali, lakini Hiza anatamkia umma kuwa kilikuw ani mauaji na wahusika (suspects) ni Viongozi wa Chadema?
Mbona yeye hakamatwi na Polisi kwa uchochezi? Polisi mko wapi kumkamata Tambwe kwa kuchochea vurugu?
Hivyo ni sahihi, kwa Tambwe na CCM kutoa kebehi na tuhuma chafu zisizo za kweli wala kuwa na ushahidi na za kichochezi, lakini kwa Wapinzani kuikebehi au kuituhumu CCM na serikali yake, rungu la dola linafanya kazi kwa mwendokasi wa mwanga na umahiri wa hali ya juu!
Tuliyaona Pemba, Kiteto na kweingineko, sasa yanajirudia Tarime!
Nakumbuka enzi za enzi tulikuwa tunavisha Mbwa jezi za Simba wa Msimbazi. Hata siku moja sikuwahi kusikia kuwa Polisi pale Msimbazi, Polisi wilaya Ilala au Polisi mkoa Dar Es Salaam wakitafuta mchokozi aliyevisha mbwa fulana ya Simba!
Sasa huyu mbwa kavishwa jezi ya CCM, Serikali (yes Polisi ni Serikali!) ya CCM kupitia vyombo vya dola vimemkamata mwenye mbwa asaidie upelelezi kuelewa ni kwa nini mbwa alivaa vazi "tukufu" la nchi!
Mbwa huyu, masikini Bobi wa watu ameuawa, najiuliza kosa la Bobi lilikuwa nini wakati yeye alikuwa ni tarishi?
Labda upande mmoja, nitaelewa kwa nini Polisi wamkamate Mwenye mbwa kwa kuwa kitendo cha Bobi kutembea na fulana ya CCM, kilihatarisha usalama kwa kuchochea fujo.
Sasa swali langu ni hili kwenu ndugu Watanzania, inakuaje DOLA inafanya kazi kwa umakini kuilinda CCM au CCM ikiwa inahujumiwa lakini wengine na hata Taifa wakihujumiwa, DOLA hujivutavuta?
Hiza Tambwe katamba kuwa CCM ndicho chama chenye dola, ikiwa na maana ya Serikali na vyombo vyake hasa Mahakama, Polisi na Jeshi. Si mara ya kwanza kusikia Viongozi wa CCM na Serikali yake hasa nyakati za uchaguzi wakitanguliza vitisho vya kulinadi Jeshi la Polisi au nguvu za Serikali kupitia CCM.
Hivi Watanzania tu finyu wa upeo kudharau mambo na kuishia kughafilika kwa hasira za juu hata kutaka kutoa uhai? Hivi wangemvisha hiyo fulana kichaa, malaya au mwizi anayefahamika wakamtembeza barabarani kumtangaza kuwa CCM ni sawa na Kichaa, Malaya au Jambazi kama namna ya Fasihi, je wale wapenzi wa CCM wangefikia hatua ya kumuua bianadmu anayekidhalilisha Chama chao, badala ya kujibu mapigo ya ki itikadi hata kutunga taarabu au kumtumia John Komba aimbe angalau wimbo wenye kijembe kuwakebehi iwe Chadema, CUF au TLP?
Ni lini Mtanzania atapevuka na kuachana na hizi hisia mbovu za kujibu kebehi kwa hasira n a kukimbilia kutoa uhai?
Ni lini CCM wataacha kutishia kila mtu kuwa wao wanamiliki Polisi?
Je ilikuwa ni sahihi kwa Tambwe Hiza kutamka waziwazi kwenye jimbo la Marehemu Chacha Wangwe kuwa viongozi wakuu wa Chadema ndio watuhumiwa wa kifo cha Wangwe ambacho tuliambiwa ni ajali, lakini Hiza anatamkia umma kuwa kilikuw ani mauaji na wahusika (suspects) ni Viongozi wa Chadema?
Mbona yeye hakamatwi na Polisi kwa uchochezi? Polisi mko wapi kumkamata Tambwe kwa kuchochea vurugu?
Hivyo ni sahihi, kwa Tambwe na CCM kutoa kebehi na tuhuma chafu zisizo za kweli wala kuwa na ushahidi na za kichochezi, lakini kwa Wapinzani kuikebehi au kuituhumu CCM na serikali yake, rungu la dola linafanya kazi kwa mwendokasi wa mwanga na umahiri wa hali ya juu!
Tuliyaona Pemba, Kiteto na kweingineko, sasa yanajirudia Tarime!