The Buzwagi Saga: Karamagi aenda kusaini Mkataba wa ULAJI London


Unategemea mchango gani kwa mwana mipasho wa vidole juu by proffesion....

Tutafika lakini safari ya peponi haiwezi kuwa rahisi kama tungelipenda iwe...

Tanzanianjema
 
Duh!! wamemfungia, Kwani huo mkataba ulisainiwa ama haukusainiwa? au ndio mambo ya nani ameshikilia mpini?
 
Leo sisemi kitu ila ni aibu tupu kwa TAIFA LETU.... WATANZANIA WATATUSHANGAA SANA

..kama wamezoea kuona wazungu wakipita kwenye 4*4 zao kuelekea kuchuma shambani kwao!

..wakiruka na ndege kwenye anga yao kuangalia shambani mwao mna nini ili wachukue!

..wameshazoe kuwahudumia wazungu kwa fedha walizozichuma kwa migongo yao wenyewe!

..wameshazoe kuishi kimungumungu!wasijue kesho kuna nini!

..washauzoe umasikini na kuukubali!

..watashangaa kitu gani!

..tushukuru hewa tunayovuta hamna anayewekeza na kufaidika nayo ama sivyo tungekufa wengi!
 
Ndg Icadon,
Mkataba umesainiwa na Ushahidi upo!,Mh.Zitto atakuja hapa nae atasema wazi nini kilichotokea huko Bungeni,Ikiwa ataingia hapa tujadili nini kimemleta, na sio kuuliza Vinginevyo! na kutaka kudhalilishana,tutoe nafasi ya kujadili masuala ya maana kwa jamii na sio kuwa kijiwe cha kujadili masuala binafsi!.Zitto pekee ndio mtu anayeweza kutupa ukweli kuhusu suala zima la Karamagi!!.Mh.Tuanaomba maelezo yako hapa.
 
Leo sisemi kitu ila ni aibu tupu kwa TAIFA LETU.... WATANZANIA WATATUSHANGAA SANA
 
Nashauri Zitto achukue muda wake kabla ya kujitosa katika bahari hii iliyojaa mamba na kenge kuzidi hata ule mtandao wetu...

Take your time kaka usije na ghadhabu zako hapa ukawapa watu faida...

Tanzanianjema
 
Mpaka hapo ZITO shujaa.Siku zote tunasema wabunge wa chama cha wenyewe sio wawakilishi wa waTz bali wa wao wenyewe.SHAME
 

kwa hiyo mwendo ni mabavu na kuonyesha who is the boss sio? ebwanae maslahi ya Taifa naona hayawekwi mbele kabisa siku hizi, alafu viongozi watajiuliza kwa nini watu wanapoteza Uzalendo taratibu?
 
Ndani ya Habari za TVT leo hii dakika kama 30 zilizopita nimepata mshtuko baada ya kuona wakitangaza kusimamishwa kuhudhuria na kushiriki vikao vya Bunge Mhe. Kabwe Zitto mpaka Januari kwa Madai ya kuudanganya Umma nafikiri kuhusiana na Masuala ya Madini na hivyo Mhe. Mudhihir Mudhihir kulingana na kipengele namba..... kinamruhusu MB kuomba kutolewa adhabu kali kwa Mbunge mwingine kama ikibainika amedanganya Umma.

Habari zaidi Kesho!
 


huju Mheshimiwa hata kama kakurukupa bado hawajathibitisha kuwa kasema uongo kwani madai yake hayajafanyiwa kazi, hapa ni kasumba ya kufata mkondo wa maji, nani kasema nini na ni mambo ya kichama zaidi. mheshimiwa Zitto amekuwa shujaa kwani hata alipoombwa kusema kama ana with draw statement yake akasema yeye ni mwanademokrasia na anaomba Bunge limjadili na kumpa adhabu kama kweli amesema uongo. Lakini still ukweli bado upo pale pale maamuzi haya kwa uono wangu ni ya kuzima moto kwani hawajathibitisha kama kasema uongo.
 
Star TV wamerekodi wataanza kuonyesha kuanzia saa nne usiku
 

Nadhani haya madai ya kusema "kamwe serikali isingeweza kuacha nafasi hiyo ipotee bure na ndiyo maana ikasaini mkataba huo mapema Februari kabla ya tarehe ya mwisho ya Machi mwaka huu" yanahitaji ufafanuzi.

  • Je serikali ndiyo iliyowaomba wawekezaji hawa, ambao waliweka masharti kuwa watawekeza tu ikiwa mkataba utasainiwa kabla ya mwisho wa Machi?
  • Lakini si wawekezaji wenyewe ni Barrick Gold Mines ambao wapo nchini tayari na walikuwa wanajua kuwa serikali inapitia upya taratibu za mikataba, nao walitaka waingie mkataba huo katika katika utaratibu wa zamani? Je hamuoni kuwa hata hii effort ya serikali "kuwashawishi" wawekezaji hawa kubadilisha vipengere kadhaa vya mikataba hiyo itapiga mwamba?
  • Kwa nini ripoti ya mazingira haikutiliwa maanani? Je wakati wa uchimbaji ikigundulika kuwa mradi huo ni hatari kwa mazingira serikali itasemaje wakati imeshainingia mkataba?

Je kama ripoti za mazingira zitaionyesha kuwa uchimaji huo utaharibu mazingira, serikali itafanya nini huku ikiwa imeshaingia mkataba?
 
Star TV wamerekodi wataanza kuonyesha kuanzia saa nne usiku
 
najitahidi kutafuta ile connection ya bure StarTv siipati...mwanakijiji naomba msaada wako..
 
Zitto aliwasilisha vizuri hoja yake nzito yenye vipengele muhimu kumi na moja. Karamagi akajibu kipengele kimoja baada ya kingine (kwa vijembe huku akinukuu vifungu mbalimbali vya sheria za madini na mapato alivyovitumia Zitto, akieleza jinsi Zitto alivyovitumia kulipotosha bunge). Na hapo ndipo alipowapiga bao wengi waliokuwa wanafuata mkumbo.

Kilichotokea ni kwamba majibu ya Karamagi yakawachanganya waliokuwa wamejiandaa kuunga mkono hoja kiasi kwamba wakabaki kuchanganyikiwa wakati wa kuchangia. Kungekuwa na uwezekano wa kujitoa, leo hii wabunge wengi wangemwomba spika aondoe majina yao. Hakuna mbunge hata mmoja aliyeweza kuoanisha hoja za Zitto na majibu ya Karamagi. Inaonyesha walikuwa wamekariri majibu, sasa baada ya Karamagi kumchambua Zitto wakabaki kujiumauma kiasi cha kufikia hatua ya kumwombea msamaha Zitto kwamba alikuwa anahitaji kueleweshwa (Maulida Komu). Wengine wakaanza kusoma vifungu vya Katiba vinavyompa mbunge kinga ya kutoshtakiwa kutokana na atakayochangia bungeni kana kwamba walishaamua kwamba Zitto kadanganya. .. walichanganyikiwa kweli kweli.

Hoja ikabadilishwa ikawa kwamba Kamati Teule iundwe ili kusafisha jina la Karamagi lililochafuliwa na tuhuma hizo. Hapo ndipo nikachoka kabisa. Aliyefurahisha zaidi ni Chacha Wangwe maana hakujua hata anachangia hoja ipi. Leo kwa kweli ilikuwa ni vichekesho tu bungeni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…