#COVID19 Teknolojia ya 5G na Chanzo cha Covid-19: Nadharia Njama (Conspiracy Theory) yenye maswali mengi

MUHTASARI
Mlipuko wa Covid-19 unasambaa ukiambatana na taarifa nyingi zisizo sahihi au za kupotosha. Taarifa hizi zinatengenezwa, ama kwa watu kukosa uelewa sahihi wa jambo wanalolizungumzia au kwa makusudi, kama “Nadharia Njama” (Conspiracy Theory). Mojawapo ni Nadharia Njama inayohusianisha mlipuko wa Covid-19 na tekenolojia mpya ya mawasiliano ya 5G. Nadharia hii inaenezwa na kuaminiwa kwa kasi sana hasa na baadhi ya makundi ya kiimani. Hii imetokana na baadhi ya watumishi kadhaa duniani “wenye majina” kuibeba na kuifanya sehemu ya mahubiri yao kipindi hiki cha taharuki. Kwenye makala hii, ninafafanua teknolojia ya 5G kwa kifupi, madhara yake, na kujaribu kuonesha mapungufu ya nadharia njama kuhusu uhusiano wa 5G na Covid-19. Lengo kuu ni kutoa mwanga kwenye jamii yetu kuhusu kinachosambazwa kupitia nadharia njama ya 5G na kuibua mjadala utakaotusaidia kuujua ukweli wa jambo hili tunapopambana na Covid-19. Kwa undani zaidi, soma makala nzima.

View attachment 1412217
Utangulizi.
Katika mapambano dhidi ya mlipuko wa Covid-19 kwenye nchi yetu na nyingi za Afrika, kuna eneo moja halijatazamwa kwa mapana yake. Eneho hilo ni ugonjwa huu kuhusianishwa na nadharia njama kadhaa na kupewa tafsiri za kiimani kuliko za kisayansi. Kwa kufanya hivyo, kuna hatari kwa baadhi ya watu kupuuzia mlipuko huu na hivyo kuhatarisha maambukizi kua makubwa. Pili, nadharia njama zinaongeza taharuki ya mlipuko na kuwapa watu madhara ya kisaikolojia kujiona wamezungukwa na hatari muda wote kutoka kwa watu wasiowajua. Ukifuatilia kwenye internet na vyombo vya habari vya kimataifa, utaona kuna kundi kubwa la watu hawaamini kama Covid-19 ni ugonjwa unaosababishwa na virusi ambao ni viumbe wa kawaida tulionao kwenye dunia hii. Kinyume chake wanaamini kuna njama, ama za kibaguzi, kibishara, au za kiimani zilizopelekea watu fulani wasiotajwa kutengeneza au kusababisha kutokea kwa ugonjwa wa Covid-19. Moja ya nadharia hizo ni ile inayoaminisha kwamba Covid-19 inasababishwa na teknolojia mpya ya mawasiliano ya 5G.

Je,5G ni kitu gani?
Teknolojia ya mawasiliano ya simu imekuwa ikipanuka na kuendelea siku hadi siku. Teknolojia ya mawasiliano ndio iliyokua kwa kasi zaidi katika historia ya kizazi chetu. Pamoja na mambo mengine, ukuaji wa teknolojia ya mawasiliano unapimwa kwa spidi/kasi ya kusafirisha data kati ya pande mbili zinazowasiliana. Kwa miaka mingi, spidi ya data imekuwa ikiboreshwa na kuongezeka kwa kuboresha miundombinu ya mawasiliano (hardware na software). Hivyo, tangu mwaka 1940, tumetoka kwenye teknolojia inayoitwa 0G (herufi “G” ikimaanisha Generation au kizazi) kwenda kwenye teknolojia inayoitwa 4G (4 generation au kizazi cha 4) tunayotumia sasa.

Kwa sasa, wavumbuzi wameibuka na teknolojia ya 5G ambayo ina spidi kubwa zaidi inayoweza kusafirisha zaidi ya 1 Gbit za data kwa sekunde. Kwa spidi hii kali, tunaweza kufanya kazi nzito zaidi ambazo teknolojia zilizopita haziwezi. Kwa mfano, teknolojia hii inaweza kutumika kwenye magari yanayojiendesha yenyewe (self-driving/autonomous cars); uwezo wa kuunganisha vitu mbalimbali katika mtandao kwa urahisi (Internet of Things); kuwa na miji yenye huduma za kijamii zilizojengwa na kuboreshwa kwa teknolojia ya mawasiliano (smart cities); kuongoza vyombo vya usafiri; vifaa vya burudani; nk. Teknolojia ya 5G inamwingiza binadamu kwenye aina mpya kabisa ya kuishi, na maisha yanatazamiwa kuboreshwa kwa sehemu kubwa. Lakini swali kubwa la kujiuliza hapa ni nini hasa kinatusukuma tunahamia 5G na tutapata faida au athari gani?

Ili kujua kwa nini dunia inaongelea 5G ni lazima uitazame kama kijiji kinachoendelea kwa kasi kubwa na hivyo kupelekea mabadiliko ya mahitaji mengi. Mathalani, kiwango cha data/taarifa kinachozalishwa katika dunia ni kikubwa mno. Ukichukulia mtandao wa Google pekee tuliouzoea, kila siku unazalisha takribani 20 petabytes (10PT) za data (Petabyte 1 ni sawa na Gigabyte (GB) milioni 1). Pia, sekta ya tamthilia (movie) inahama kwa kazi kutoka kutegemea video zinazouzwa kwa njia ya DVD au kaseti kuelekea kutazama tamthilia online kupitia mitandano kama Youtube na Netflix. Pia, utazamaji wa television unahamia kwenye Smart TV ambazo zinakupa uwezo wa kutazama television huku ukiwa unapata huduma nyingi kwa mtandao mithili ya matumizi ya kompyuta. Mahitaji haya ndiyo yalifanya wavumbuzi waanze kufikiria namna ya kuongeza uwezo wa kusafirisha data na kuibuka na 5G. Makampuni ya mawasiliano yanakimbilia kuwekeza katika teknolojia ya 5G kwa sababu ya faida nyingi ambazo wataje wao watapata. hata hivyo kuna changamoto kubwa mbili za 5G kimuondombinu.

  1. Teknolojia ya 5G inahitaji uwekezaji mkubwa wa miundombinu mipya ya mawasiliano kwa sababu inalazimisha kubadilisha ile iliyoko kwa sehemu kubwa. Hadi sasa kuna takribani nchi 35 (nyingi zikiwa tajiri) ambazo tayari zina miundombinu ya 5G na bado inajengwa. Ufungaji wa miundombinu hii kwa nchi nyingi umeanza mwaka 2019.

    Nchi zinazoongoza kuwa na miundombinu ya 5G kwenye miji mingi ni South Korea, China, na Marekani. Kwa miaka kama 2 iliyopita, utakua umesikia siasa za 5G kati ya mataifa makubwa hasa Marekani, Uingereza na China. Hii imetokana na ukweli kwamba kampuni ya Huawei ya wachina imekua mbele hatua kadhaa kiteknolojia na kuzifanya nchi nyingi zikiwemo za Magharibi kutumia teknolojia zake ikiwemo kuweka miundombinu ya 5G. Hii imewapa taharuki maadui zao kiuchumi hasa Marekani kwa hoja kwamba mitambo yao sio salama kwa kuwa inaratibiwa au kudukuliwa na serikali ya China (hili tuliachie hapa maana ni mjadala mwingine).


  2. Nyingine ni ukweli kwamba wateja watalazimika kuwa na vifaa vilivyotengenezwa kutumia teknoljia ya 5G, na hivyo kuingia gharama ya ziada/kubwa.
Pamoja na changamoto hizi na nyingine, bado 5G inatoa matumaini mapya ya maendeleo yatakayomwezesha binadamu kufanya shughuli nyingi ngumu kwa muda mfupi. 5G inafanikishwa mambo mawili makubwa. Moja ni kiwango cha data kinachoweza kusafirishwa, na mbili ni spidi/kasi ya data kusafiri kati ya kifaa kimoja na kingine.

Je, 5G ina madhara gani kiafya?
Nadharia njama ya 5G imejikita katika kile kinachoitwa madhara makubwa ya 5G kwa afya zetu. Kumesambaa habari nyingi duniani zilizoanzishwa na watu wachache na zimeshika kazi kama moto wa mabua kiasi kwamba zimeanza kuaminika kama ukweli. Hii imepelekea siku ya jana mtandao wa Youtube kuamu kuanza kufuta video zote kwenye mfumo wao zinazoongela nadharia njama ya G5 na uhusiano wake na Covid-19 (tazama hapa). Katika nchi za kiafrika ambapo kwa sehemu kubwa tumeturuhu watu wengine wafikirie na hata kuamua kwa niaba yetu, nadharia hii imeingizwa kwenye viunga vya kiimani na imeshakua ukweli kwa watu wengi maana huwa tunaogopa kuhoji mambo ya kiimani au wanachokisema watumishi.

Nimesikiliza na kusoma maelezo ya waanzilishi na wainjilisti wa nadharia njama ya 5G ili kuelewa msingi wa taharuki wanayoijenga. Mengi wanayoongea ni uongo, uzushi, ya kuungaunga, na hayana usahihi wowote kisayansi wala kiimani. Nadharia hii imeanzishwa na wataalamu wa nadharia njama (conspirancy theorists - wawili wakiwa ni waingereza) na kudakwa na baadhi ya watumishi “wenye majina” kama hoja ya mahubiri yao. Baadhi ya watumishi (hasa wa kikristo) hupenda kujionesha kua wao wana majibu au maelezo ya kila jambo duniani. Hivyo wamechukua hoja ya 5G na kuitumia kama ilivyo au kwa kuitohoa kujengea hoja za chanzo na malengo ya Covid-19. Nitaje kwa kifupi baadhi ya hoja zilizoko kwenye nadharia njama ya 5G.

  1. Taswira inajengwa kwamba kuna mkakati wa watu ambao wanaleta teknolojia ya 5G kwa lengo la kuitawala dunia na hasa kutufanya sisi wanadamu wote kuunganishwa kwenye mtandao mmoja ili kuweza kutaribiwa. Mkakati huu unapewa majina mengi lakini mojawapo ni mbinu ya kufanikisha kinachoitwa “New World Order (NWO)”. NWO ni nadharia njama inayodai kuna kundi la siri lenye nguvu kuliko mataifa yote litakaloitawala dunia nzima kibabe.
    UDHAIFU: wanaoaminisha nadharia hii hawataji watu hao ni kina nani, wako nchi gani, na iwapo ni wa dunia hii au sayari nyingine. Ukiachilia kutajwa kwa baadhi ya viongozi wakuu wa baadhi ya nchi na dini kubwa, nadharia hii inabaki kuwa yakufirika na imekuwepo kwa muda mrefu.


  2. Hoja inajengwa kwamba vifaa vya teknolojia ya 5G vina mionzi mikali yenye madhara kwenye miili yetu. Katika kupambana nayo, miili yetu inatengeneza virusi wa Corona.
    UDHAIFU: Moja, hakuna ushahidi wa kisayansi wowote juu ya hili. Pili, kama miili yetu inatengeneza virusi wa Corona tunapopigwa na mionzi ya 5G, kwa nini basi tusingekua tunaugua wote kwenye eneo lenye 5G? Tatu, kwa nini watu wanaoathirika wanapona?


  3. Wakati huohuo wanadai Covid-19 inasambazwa kwa watu kupitia vipimo tunavyofanyiwa kujua iwapo tuna maambukizi. Lengo kubwa la kuingiziwa virusi hivi ni ili dunia nzima iwe na maambukizi kisha kupitishwe taratibu/sheria inayomtaka kila mtu lazima apewe chanjo ya kumkinga na Covid-19. Kupitia chanjo hiyo tutaingiziwa “chip” ndogo ya mawasiliano kwenye miili yetu (mithili ya line ya simu yako) itakayowezesha watu hao wasiojulikana kutufuatilia kama vile mitambo ya kompyuta. Pia, mtu hataweza kupata visa kuingia nchi nyingine iwapo hajathibitisha kua na una kinga ya Covid-19.
    UDHAIFU: Moja, tuna ushahidi kutoka nchi nyingi watu kuambukizwa na kueonesha dalili (wengine hadi kufariki) kabla ya kupimwa. Pili, ili uweze kupachika chip ya kielekroniki ifanye kazi na kuweza kusafirisha data na mfumo wa mwili, ni lazima ipachikwe mahili maalumu na kuunganishwa na mfumo wa mawasiliano wa mwili. Wanaohubiri nadharia hii hawatuelezi ni kwa jinsi gani chanjo tutakayopewa (ama vidonge au kimiminika) itaingiza chip mwilini na ikafanye kazi.


  4. Wakristo wanatahadharishwa kwamba 5G ni mpango wa shetani na Covid-19 ni vita dhidi yao. Wengine wanakwenda mbali zaidi kudai Covid-19 imetengenezwa kwa lengo la kuangamiza waafrika ila waliotengeneza wamekosea ikawaathiri wao wenyewe.
    UDHAIFU: Hoja hii ni dhaifu kama zingine maana ni ya kufikirika.


  5. Katika kujenga hoja zao, baadhi ya manabii wa njama hii wanasema virusi sio viumbe halisia bali wanatengenezwa kwa malengo mabaya.
    UDHAIFU: Huu ni uongo ulioopitiliza kwani wanasayansi wa viorolojia wanatuambia kuna aina takribani 5,000 ya virusi wa asili duniani. Sifa kubwa ya virusi ni kutokua na uwezo wa kuishi wenyewe bila kuwa ndani au juu ya kiumbe kingine. Hivyo wanaweza kuishi kwa wanadamu, wanyama, ndege, samaki, mimea na hata viumbe vidogo kama bakteria. Hata hivyo wataalamu wa bayoteknolojia wanaweza kutengeneza virusi kwa njia za kimaabara kwa malengo mbalimbali.


  6. Wanajenga hoja kwamba kirusi cha Corona ni kipya na hajawahi kuwepo. Moja ya filamu ya kijapani iliyotengenezwa 2018 ina kipengele wanachotaja visuri wa Corona hivyo kipengele hiki kinatumika kuthibitisha kwamba Corona ni mkakati wa silaha za kibalojia.
    UDHAIFU: Hoja hii inadhirisha jinsi upotoshaji huu usivyo na mashiko. Virusi wanaosababisha Covid-19 (yaani SARS-CoV-2), ni kafamilia kamoja tu kati ya familia karibu 60 za ukoo wa Coronavirus. Wana dada yao anaitwa SARS-CoV-1 aliyesababisha mlipuko wa SARS kule China mwaka 2002/2004 lakini ukadhibitiwa. Pia wana binamu naitwa MERS-Cov aliyelipuka kule uarabuni 2012 na kudhibitiwa pia.
Uhalisia uko wapi?
Kuna uwezekano mkubwa wa teknolojia ya mawasiliano kuwa na madhara kiafya kama zilivyo teknolojia nyingi tunazotumia kila siku (magari, simu za mikononi, kompyuta, nk). Kwenye teknolojia ya mawasiliano, madhara yanahusishwa moja kwa moja na mionzi inayotumika kusafirisha data (kwa mfano simu zetu kuwasiliana na minara ya mawasiliano au na kifaa cha kupata mtandao wa intenet kwa njia ya upepo (WiFi)).

Kwa mfano, tafiti kadhaa zilizofanyika nchi kama India, Australia, Marekani, Ufaransa, nk, zimeonesha uwezekano wa madhara yatokanayo na matumizi ya simu za mikononi (sio za 5G). Ziko tafiti zimeonesha mionzi ya simu inaweza kusabanisha kansa, kuharibu mbegu za kiume, nk. Watafiti wanatoa tahadhari na kuwashauri watu kupuunguza mawasiliano ya simu za mikononi na kuzitaka kampuni zinazotengeneza simu kuwa wawazi kwa kuweka tahadhari wazi juu ya madhara mtu anayoweza kuyapata kwa kutumia simu. Wanashauri tuwazuie watoto kutumia simu na vifaa vingine vyenye WiFi ili kuzuia madhara ya mionzi ambayo imeonekana inaweza kusababisha kansa ya ubongo.

Kuna mjadala na mvutano mkubwa kati ya watafiti na watu walio kwenye sekta ya mawasiliano kuhusu ukweli wa madhara vifaa vya mawasiliano. Wanaopinga uwepo wa madhara wanasema hakuna ushahidi wa kutosha kuthibitisha yale yanayodaiwa [Hii ni mada ndefu hivyo kwa sasa niiachie hapa nirudi kwenye 5G].

Hivyo basi, kama simu ambazo tayari tunatumia zenye teknolojia ya 2G, 3G au 4G zimethibitika kwamba zinaweza kua na madhara yatokanayo na mionzi, ni wazi 5G inaweza kuwa na ina hiyohiyo ya madhara. Yanaweza yakawa ama nafuu zaidi kutokana na maendeleo ya teknolojia au makali zaidi kwa sababu hiyohiyo. Manabii wa nadharia njama ya 5G wanajenga hoja kwamba mionzi itokayo kwenye vifaa vya 5G ina nguvu isiyoweza kustahimilika na miili yetu.

Hata hivyo, lazima tutambue kwamba, wagunduzi wa mawasiliano nao ni binadamu na wanapotengeneza teknolojia mpya, wanazifanyia tafiti za kina kupima madhara yake kabla ya kuzipitisha kutumika. Pia, kila nchi (hasa zilizoendelea) zina taasisi za viwango, uratibu na udhibiti kwa lengo la kuthibitisha ubora na usalama wa mitambo ya mawasiliano kabla ya kutumika katika jamii (sisi tuna TCRA). Hakuna taifa/serikali hata moja duniani, iko tayari kufunga mitambo ya mawasiliano ambayo ina madhara kwa watu wake huku wakijua haitachagua nani wa kumdhuru.

Fursa inayotumiwa na wanaohubiri nadharia njama ya 5G
Baadhi ya manabii wa nadharia njama ya 5G ni watu wenye elimu kubwa na ufahamu mpana wa mambo. Wataalamu wengi wa nadharia njama wana akili nyingi na ni wasomi wazuri. Hivyo wanatumia nafasi hiyo kama njia ya kuonesha wanachokiongea kina ukweli. Kunahitajika uwezo mkubwa na uelewa wa mambo kung'amua yaliyo nyuma ya nadharia zao. Hata hivyo, miongoni mwao kuna wengi hawana kabisa uelewa wa teknolojia za mawasiliano na hawana uwezo wa kukuambia 5G ni kitu gani au hizo hatari zinatokeaje katika uhalisia. Ukiwasikiliza vema, wanatumia baadhi ya nadharia za mifumo ya teknolojia ya mawasiliano kwa kuungaunga kama namna ya kuonesha uhatari wa 5G. Wanataja maneno kama artificial intelligence (AI), Internet of Things (IoT) au Machine Leaning (ML) kujazia hoja zao bila kuelewa zinalenga nini hasa. Kwa mtu asiye na eleimu ya mambo haya (na hawa ni wengi kwenye jamii) akitajiwa mambo haya anapata picha inayotisha sana. Kama vile haitoshi, watu hawa hawana uelewa wa kutosha kuhusu epidemilojia ya magonjwa ya mlipuko. Ila, wanafanikiwa kwa kiasi kikubwa kupotosha kwa kua wanajua au kuamini kwamba wanaowasikiliza hawana uelewa wa mambo au elemu yao ni ndogo kuweza kung’amua ukweli au kutafuta usahihi wa wanachokisema.

Hitimisho na Ushauri
Nadharia njama ya 5G na nyingine zina hatarisha watu wengi kuambukizwa na Covid-19 kwani wanaozisambaza wanatoa maelezo yanayokanganya na kuwafanya wengi wasifuate maelekezo ya kisayansi ya ugonjwa huu na namna ya kukabiliana nao. Ndio mana utaelewa ni kwa nini juzi kule Abijan Ivory Coast wananchi wameandama na kwenda kuvunja jengo maalum linaloandaliwa kwa ajili ya kupimia wagonjwa wa Covid-19. Pia utaelewa ni kwa nini, baadhi ya “watumishi” wanahamasisha waumini wao waendelee kufanya ibada za pamoja kwa wingi zaidi wakiamini Covid-19 ni mbinu za mpinga Kristo na wanatakiwa kuamini haitawapata wao. Waliosambaza Covid-19 kwa wingi kule Korea ya Kusini walikua wakristo (walokole) waliopuuzia athari za ugonjwa huu. Waliambukizana kwa wingi na wakafanya karibu mji mzima kulemewa na maambukizi.

Kama nilivyosema kwenye moja ya makala zangu kuhusu janga la Covid-19 na kuziweka
hapa Jamii Forum, mlipuko huu umedhihirisha ni kwa kiasi gani sisi waafrika tulio wengi sio jamii inayoongozwa na elimu, maarifa, sayansi, na teknolojia. Imetuonesha namna tunavyofanya maamuzi yetu bila kutumia taarifa sahihi na tulivyo warahisi kuamini taarifa za uongo, za uzushi, na kutotaka kujishughulisha kutafuta ukweli na maarifa. Pia, imetuonesha namna mfumo wetu wa elimu usivyotuandaa na kutuwezeha kutumia uwezo wetu wa kufikiri, kufanya tafakuri tunduizi, na kuchambua mambo kwa lengo la kutafuta maarifa, ukweli au usahihi wa kile tunachosikia.

Kama vile haitoshi, mlipuko huu umetuonesha namna baadhi ya "watumishi wa dini zetu" wanavyotumia kila fursa wanayoipata kutuweka mbali na ukweli kwa makusudi na kwa manufaa yao binafsi. Hawataki tutumie akili zetu na elimu kutafuta majawabu ya maswali magumu yanatotukabili au suluhisho la changamoto tunazokutana nazo. Kila mara wanataka tutumie fikra za kiimani kama "shortcut" ambayo haitufikishi wanapotuahidi. Ifike mahali, wapendwa hawa wakubali kwamba wao sio miungu na hawana ufunuo wa kila jambo. Wao ni watumishi tu hivyo hawawezi kuwa na maelezo au majawabu ya kila swali au utata unaojitokeza kwenye jamii. Ni sahihi kabisa wakisema hawana maelezo au hawajui au bado wanamwomba wanayemtumikia kupata majawabu. Kukiri hivi hakuwapunguzii kitu katika nafasi yao ya utumishi. Pia kwa mambo ya kitaalamu/kisayansi, ni vema wakatafuta wabobezi wa eneo husika wakawapa mwanga wa kutosha wa kisayansi kabla ya kuyaongelea kwa umma katika muktadha wa kiimani. Hii ina msaada mkuwa sana na inawapa heshima hata nje ya waumini wao. Wana fursa kubwa ya kupata maelezo ya kitaalamu tena bure kutoka kwa makundi yao na hata wasio wa makundi yao.

Moja ya mambo yanayotuchelewesha waafrika kuendelea kwa kasi kama mataifa mengine tuyatazamayo kama vielelezo, ni kuhoji kila kitu kigeni kwa mtizamo wa kukiogopa au kukishuku huku tukiwa hatuna maelezo sahihi wala uthibitisho wa tunachoamini/kuaminishwa/kuwaaminisha wengine. Mbaya zaidi tunakua hatuna mbadala wa kuwapa tunaowajengea hofu. Unawaaminisha watu kuwa 5G ni hatari au ni shetani huku mfukoni una simu ya 4/5G na hotuba au mahubiri unayotoa unayarusha live kwa Youtube inayotumia teknolojia ya 5G kuweza kustahimili wingi wa watu wanayoitumia. Pia una accounts za mitandao ya kijamii ambayo kwa sehemu kubwa zinategemea teknolojia unayopambana nayo. Sasa tukuamini kwa lipi?


Zingatia
  1. Uchambuzi na maoni niliyoyatoa hapa, hayamaanishi kwamba ninaamini hakuna madhara yanayoweza kusababishwa na teknolojia ya 5G. Pia, hayamaanishi ninapinga watu kuhojia, kutafiti, au kuweka mashaka kuhusu usalama wa teknolojia hii. Hapana. Hoja yangu nya msingi ni kutofautina na upotofu unaonezwa na nadharia njama ya kuhusianisha Covid-19 na 5G. Tuhoji na kutafiti madhara ya 5G na mambo mengine (kama ni lazima) kwa kutumia ukweli na ushahidi wa kisayansi badala ya dhana za kufikirika na ndoto za abunuwasi.

    Sehemu kubwa ya Afrika tuko kwenye mkwamo kama jamii na mapokeo tuliyoletewa na waliotutawala (hasa imani) yanatuathiri kifikra na kimitazamo kuliko waliozinzisha. Hivyo tukimaliza hili la Covid-19, tuanze kuweka mikakati ya muda mrefu ya kujikwamua tulipokwama ili kurahisha maendeleo ya watu na vitu. Pamoja na bidii na imani zetu, tunahitaji elimu na maarifa sahihi ili tuweze kupiga hatua na kuleta maendeleo endelevu.


  2. Uchambuzi huu haujalenga kuwashambulia wakristo au "watumishi" kwani nami ni mmoja wao. Nimetaja ukristo (tena kwa tahadhari kubwa) maana ndio kundi nililoko na ninashuhudia jinsi baadhi yetu wanavyokazana kupotosha kuhusu Covid-19 na kinaathiri jamii kubwa.

  3. Neno "Nadharia Njama" sio rasmi katika viunga vya lugha ya Kiswahili bali nimelitohoa mimi mwenyewe baada ya kuketi na kamusi za Kiswahili nikiwa natafuta tafsiri/maana ya "Consipiracy Theory". Sifahamu tafsiri rasmi ya dhana hii kwa Kiswahili.

Mathew Togolani Mndeme (mmtogolani@gmail.com)
Mtafiti wa mifumo ya digitali kwenye ufuatiliaji na udhibiti wa magonjwa

  • Shukrani kwa classmate wangu Dr. Baraka Maiseli (Lecturer in Electronic and Telecommunications Engineering, UDSM) kwa ushauri kwenye ufafanuzi wa teknolojia ya 5G
The family secret at work
 
MUHTASARI
Mlipuko wa Covid-19 unasambaa ukiambatana na taarifa nyingi zisizo sahihi au za kupotosha. Taarifa hizi zinatengenezwa, ama kwa watu kukosa uelewa sahihi wa jambo wanalolizungumzia au kwa makusudi, kama “Nadharia Njama” (Conspiracy Theory). Mojawapo ni Nadharia Njama inayohusianisha mlipuko wa Covid-19 na tekenolojia mpya ya mawasiliano ya 5G. Nadharia hii inaenezwa na kuaminiwa kwa kasi sana hasa na baadhi ya makundi ya kiimani. Hii imetokana na baadhi ya watumishi kadhaa duniani “wenye majina” kuibeba na kuifanya sehemu ya mahubiri yao kipindi hiki cha taharuki. Kwenye makala hii, ninafafanua teknolojia ya 5G kwa kifupi, madhara yake, na kujaribu kuonesha mapungufu ya nadharia njama kuhusu uhusiano wa 5G na Covid-19. Lengo kuu ni kutoa mwanga kwenye jamii yetu kuhusu kinachosambazwa kupitia nadharia njama ya 5G na kuibua mjadala utakaotusaidia kuujua ukweli wa jambo hili tunapopambana na Covid-19. Kwa undani zaidi, soma makala nzima.

View attachment 1412217
Utangulizi.
Katika mapambano dhidi ya mlipuko wa Covid-19 kwenye nchi yetu na nyingi za Afrika, kuna eneo moja halijatazamwa kwa mapana yake. Eneho hilo ni ugonjwa huu kuhusianishwa na nadharia njama kadhaa na kupewa tafsiri za kiimani kuliko za kisayansi. Kwa kufanya hivyo, kuna hatari kwa baadhi ya watu kupuuzia mlipuko huu na hivyo kuhatarisha maambukizi kua makubwa. Pili, nadharia njama zinaongeza taharuki ya mlipuko na kuwapa watu madhara ya kisaikolojia kujiona wamezungukwa na hatari muda wote kutoka kwa watu wasiowajua. Ukifuatilia kwenye internet na vyombo vya habari vya kimataifa, utaona kuna kundi kubwa la watu hawaamini kama Covid-19 ni ugonjwa unaosababishwa na virusi ambao ni viumbe wa kawaida tulionao kwenye dunia hii. Kinyume chake wanaamini kuna njama, ama za kibaguzi, kibishara, au za kiimani zilizopelekea watu fulani wasiotajwa kutengeneza au kusababisha kutokea kwa ugonjwa wa Covid-19. Moja ya nadharia hizo ni ile inayoaminisha kwamba Covid-19 inasababishwa na teknolojia mpya ya mawasiliano ya 5G.

Je,5G ni kitu gani?
Teknolojia ya mawasiliano ya simu imekuwa ikipanuka na kuendelea siku hadi siku. Teknolojia ya mawasiliano ndio iliyokua kwa kasi zaidi katika historia ya kizazi chetu. Pamoja na mambo mengine, ukuaji wa teknolojia ya mawasiliano unapimwa kwa spidi/kasi ya kusafirisha data kati ya pande mbili zinazowasiliana. Kwa miaka mingi, spidi ya data imekuwa ikiboreshwa na kuongezeka kwa kuboresha miundombinu ya mawasiliano (hardware na software). Hivyo, tangu mwaka 1940, tumetoka kwenye teknolojia inayoitwa 0G (herufi “G” ikimaanisha Generation au kizazi) kwenda kwenye teknolojia inayoitwa 4G (4 generation au kizazi cha 4) tunayotumia sasa.

Kwa sasa, wavumbuzi wameibuka na teknolojia ya 5G ambayo ina spidi kubwa zaidi inayoweza kusafirisha zaidi ya 1 Gbit za data kwa sekunde. Kwa spidi hii kali, tunaweza kufanya kazi nzito zaidi ambazo teknolojia zilizopita haziwezi. Kwa mfano, teknolojia hii inaweza kutumika kwenye magari yanayojiendesha yenyewe (self-driving/autonomous cars); uwezo wa kuunganisha vitu mbalimbali katika mtandao kwa urahisi (Internet of Things); kuwa na miji yenye huduma za kijamii zilizojengwa na kuboreshwa kwa teknolojia ya mawasiliano (smart cities); kuongoza vyombo vya usafiri; vifaa vya burudani; nk. Teknolojia ya 5G inamwingiza binadamu kwenye aina mpya kabisa ya kuishi, na maisha yanatazamiwa kuboreshwa kwa sehemu kubwa. Lakini swali kubwa la kujiuliza hapa ni nini hasa kinatusukuma tunahamia 5G na tutapata faida au athari gani?

Ili kujua kwa nini dunia inaongelea 5G ni lazima uitazame kama kijiji kinachoendelea kwa kasi kubwa na hivyo kupelekea mabadiliko ya mahitaji mengi. Mathalani, kiwango cha data/taarifa kinachozalishwa katika dunia ni kikubwa mno. Ukichukulia mtandao wa Google pekee tuliouzoea, kila siku unazalisha takribani 20 petabytes (10PT) za data (Petabyte 1 ni sawa na Gigabyte (GB) milioni 1). Pia, sekta ya tamthilia (movie) inahama kwa kazi kutoka kutegemea video zinazouzwa kwa njia ya DVD au kaseti kuelekea kutazama tamthilia online kupitia mitandano kama Youtube na Netflix. Pia, utazamaji wa television unahamia kwenye Smart TV ambazo zinakupa uwezo wa kutazama television huku ukiwa unapata huduma nyingi kwa mtandao mithili ya matumizi ya kompyuta. Mahitaji haya ndiyo yalifanya wavumbuzi waanze kufikiria namna ya kuongeza uwezo wa kusafirisha data na kuibuka na 5G. Makampuni ya mawasiliano yanakimbilia kuwekeza katika teknolojia ya 5G kwa sababu ya faida nyingi ambazo wataje wao watapata. hata hivyo kuna changamoto kubwa mbili za 5G kimuondombinu.

  1. Teknolojia ya 5G inahitaji uwekezaji mkubwa wa miundombinu mipya ya mawasiliano kwa sababu inalazimisha kubadilisha ile iliyoko kwa sehemu kubwa. Hadi sasa kuna takribani nchi 35 (nyingi zikiwa tajiri) ambazo tayari zina miundombinu ya 5G na bado inajengwa. Ufungaji wa miundombinu hii kwa nchi nyingi umeanza mwaka 2019.

    Nchi zinazoongoza kuwa na miundombinu ya 5G kwenye miji mingi ni South Korea, China, na Marekani. Kwa miaka kama 2 iliyopita, utakua umesikia siasa za 5G kati ya mataifa makubwa hasa Marekani, Uingereza na China. Hii imetokana na ukweli kwamba kampuni ya Huawei ya wachina imekua mbele hatua kadhaa kiteknolojia na kuzifanya nchi nyingi zikiwemo za Magharibi kutumia teknolojia zake ikiwemo kuweka miundombinu ya 5G. Hii imewapa taharuki maadui zao kiuchumi hasa Marekani kwa hoja kwamba mitambo yao sio salama kwa kuwa inaratibiwa au kudukuliwa na serikali ya China (hili tuliachie hapa maana ni mjadala mwingine).


  2. Nyingine ni ukweli kwamba wateja watalazimika kuwa na vifaa vilivyotengenezwa kutumia teknoljia ya 5G, na hivyo kuingia gharama ya ziada/kubwa.
Pamoja na changamoto hizi na nyingine, bado 5G inatoa matumaini mapya ya maendeleo yatakayomwezesha binadamu kufanya shughuli nyingi ngumu kwa muda mfupi. 5G inafanikishwa mambo mawili makubwa. Moja ni kiwango cha data kinachoweza kusafirishwa, na mbili ni spidi/kasi ya data kusafiri kati ya kifaa kimoja na kingine.

Je, 5G ina madhara gani kiafya?
Nadharia njama ya 5G imejikita katika kile kinachoitwa madhara makubwa ya 5G kwa afya zetu. Kumesambaa habari nyingi duniani zilizoanzishwa na watu wachache na zimeshika kazi kama moto wa mabua kiasi kwamba zimeanza kuaminika kama ukweli. Hii imepelekea siku ya jana mtandao wa Youtube kuamu kuanza kufuta video zote kwenye mfumo wao zinazoongela nadharia njama ya G5 na uhusiano wake na Covid-19 (tazama hapa). Katika nchi za kiafrika ambapo kwa sehemu kubwa tumeturuhu watu wengine wafikirie na hata kuamua kwa niaba yetu, nadharia hii imeingizwa kwenye viunga vya kiimani na imeshakua ukweli kwa watu wengi maana huwa tunaogopa kuhoji mambo ya kiimani au wanachokisema watumishi.

Nimesikiliza na kusoma maelezo ya waanzilishi na wainjilisti wa nadharia njama ya 5G ili kuelewa msingi wa taharuki wanayoijenga. Mengi wanayoongea ni uongo, uzushi, ya kuungaunga, na hayana usahihi wowote kisayansi wala kiimani. Nadharia hii imeanzishwa na wataalamu wa nadharia njama (conspirancy theorists - wawili wakiwa ni waingereza) na kudakwa na baadhi ya watumishi “wenye majina” kama hoja ya mahubiri yao. Baadhi ya watumishi (hasa wa kikristo) hupenda kujionesha kua wao wana majibu au maelezo ya kila jambo duniani. Hivyo wamechukua hoja ya 5G na kuitumia kama ilivyo au kwa kuitohoa kujengea hoja za chanzo na malengo ya Covid-19. Nitaje kwa kifupi baadhi ya hoja zilizoko kwenye nadharia njama ya 5G.

  1. Taswira inajengwa kwamba kuna mkakati wa watu ambao wanaleta teknolojia ya 5G kwa lengo la kuitawala dunia na hasa kutufanya sisi wanadamu wote kuunganishwa kwenye mtandao mmoja ili kuweza kutaribiwa. Mkakati huu unapewa majina mengi lakini mojawapo ni mbinu ya kufanikisha kinachoitwa “New World Order (NWO)”. NWO ni nadharia njama inayodai kuna kundi la siri lenye nguvu kuliko mataifa yote litakaloitawala dunia nzima kibabe.
    UDHAIFU: wanaoaminisha nadharia hii hawataji watu hao ni kina nani, wako nchi gani, na iwapo ni wa dunia hii au sayari nyingine. Ukiachilia kutajwa kwa baadhi ya viongozi wakuu wa baadhi ya nchi na dini kubwa, nadharia hii inabaki kuwa yakufirika na imekuwepo kwa muda mrefu.


  2. Hoja inajengwa kwamba vifaa vya teknolojia ya 5G vina mionzi mikali yenye madhara kwenye miili yetu. Katika kupambana nayo, miili yetu inatengeneza virusi wa Corona.
    UDHAIFU: Moja, hakuna ushahidi wa kisayansi wowote juu ya hili. Pili, kama miili yetu inatengeneza virusi wa Corona tunapopigwa na mionzi ya 5G, kwa nini basi tusingekua tunaugua wote kwenye eneo lenye 5G? Tatu, kwa nini watu wanaoathirika wanapona?


  3. Wakati huohuo wanadai Covid-19 inasambazwa kwa watu kupitia vipimo tunavyofanyiwa kujua iwapo tuna maambukizi. Lengo kubwa la kuingiziwa virusi hivi ni ili dunia nzima iwe na maambukizi kisha kupitishwe taratibu/sheria inayomtaka kila mtu lazima apewe chanjo ya kumkinga na Covid-19. Kupitia chanjo hiyo tutaingiziwa “chip” ndogo ya mawasiliano kwenye miili yetu (mithili ya line ya simu yako) itakayowezesha watu hao wasiojulikana kutufuatilia kama vile mitambo ya kompyuta. Pia, mtu hataweza kupata visa kuingia nchi nyingine iwapo hajathibitisha kua na una kinga ya Covid-19.
    UDHAIFU: Moja, tuna ushahidi kutoka nchi nyingi watu kuambukizwa na kueonesha dalili (wengine hadi kufariki) kabla ya kupimwa. Pili, ili uweze kupachika chip ya kielekroniki ifanye kazi na kuweza kusafirisha data na mfumo wa mwili, ni lazima ipachikwe mahili maalumu na kuunganishwa na mfumo wa mawasiliano wa mwili. Wanaohubiri nadharia hii hawatuelezi ni kwa jinsi gani chanjo tutakayopewa (ama vidonge au kimiminika) itaingiza chip mwilini na ikafanye kazi.


  4. Wakristo wanatahadharishwa kwamba 5G ni mpango wa shetani na Covid-19 ni vita dhidi yao. Wengine wanakwenda mbali zaidi kudai Covid-19 imetengenezwa kwa lengo la kuangamiza waafrika ila waliotengeneza wamekosea ikawaathiri wao wenyewe.
    UDHAIFU: Hoja hii ni dhaifu kama zingine maana ni ya kufikirika.


  5. Katika kujenga hoja zao, baadhi ya manabii wa njama hii wanasema virusi sio viumbe halisia bali wanatengenezwa kwa malengo mabaya.
    UDHAIFU: Huu ni uongo ulioopitiliza kwani wanasayansi wa viorolojia wanatuambia kuna aina takribani 5,000 ya virusi wa asili duniani. Sifa kubwa ya virusi ni kutokua na uwezo wa kuishi wenyewe bila kuwa ndani au juu ya kiumbe kingine. Hivyo wanaweza kuishi kwa wanadamu, wanyama, ndege, samaki, mimea na hata viumbe vidogo kama bakteria. Hata hivyo wataalamu wa bayoteknolojia wanaweza kutengeneza virusi kwa njia za kimaabara kwa malengo mbalimbali.


  6. Wanajenga hoja kwamba kirusi cha Corona ni kipya na hajawahi kuwepo. Moja ya filamu ya kijapani iliyotengenezwa 2018 ina kipengele wanachotaja visuri wa Corona hivyo kipengele hiki kinatumika kuthibitisha kwamba Corona ni mkakati wa silaha za kibalojia.
    UDHAIFU: Hoja hii inadhirisha jinsi upotoshaji huu usivyo na mashiko. Virusi wanaosababisha Covid-19 (yaani SARS-CoV-2), ni kafamilia kamoja tu kati ya familia karibu 60 za ukoo wa Coronavirus. Wana dada yao anaitwa SARS-CoV-1 aliyesababisha mlipuko wa SARS kule China mwaka 2002/2004 lakini ukadhibitiwa. Pia wana binamu naitwa MERS-Cov aliyelipuka kule uarabuni 2012 na kudhibitiwa pia.
Uhalisia uko wapi?
Kuna uwezekano mkubwa wa teknolojia ya mawasiliano kuwa na madhara kiafya kama zilivyo teknolojia nyingi tunazotumia kila siku (magari, simu za mikononi, kompyuta, nk). Kwenye teknolojia ya mawasiliano, madhara yanahusishwa moja kwa moja na mionzi inayotumika kusafirisha data (kwa mfano simu zetu kuwasiliana na minara ya mawasiliano au na kifaa cha kupata mtandao wa intenet kwa njia ya upepo (WiFi)).

Kwa mfano, tafiti kadhaa zilizofanyika nchi kama India, Australia, Marekani, Ufaransa, nk, zimeonesha uwezekano wa madhara yatokanayo na matumizi ya simu za mikononi (sio za 5G). Ziko tafiti zimeonesha mionzi ya simu inaweza kusabanisha kansa, kuharibu mbegu za kiume, nk. Watafiti wanatoa tahadhari na kuwashauri watu kupuunguza mawasiliano ya simu za mikononi na kuzitaka kampuni zinazotengeneza simu kuwa wawazi kwa kuweka tahadhari wazi juu ya madhara mtu anayoweza kuyapata kwa kutumia simu. Wanashauri tuwazuie watoto kutumia simu na vifaa vingine vyenye WiFi ili kuzuia madhara ya mionzi ambayo imeonekana inaweza kusababisha kansa ya ubongo.

Kuna mjadala na mvutano mkubwa kati ya watafiti na watu walio kwenye sekta ya mawasiliano kuhusu ukweli wa madhara vifaa vya mawasiliano. Wanaopinga uwepo wa madhara wanasema hakuna ushahidi wa kutosha kuthibitisha yale yanayodaiwa [Hii ni mada ndefu hivyo kwa sasa niiachie hapa nirudi kwenye 5G].

Hivyo basi, kama simu ambazo tayari tunatumia zenye teknolojia ya 2G, 3G au 4G zimethibitika kwamba zinaweza kua na madhara yatokanayo na mionzi, ni wazi 5G inaweza kuwa na ina hiyohiyo ya madhara. Yanaweza yakawa ama nafuu zaidi kutokana na maendeleo ya teknolojia au makali zaidi kwa sababu hiyohiyo. Manabii wa nadharia njama ya 5G wanajenga hoja kwamba mionzi itokayo kwenye vifaa vya 5G ina nguvu isiyoweza kustahimilika na miili yetu.

Hata hivyo, lazima tutambue kwamba, wagunduzi wa mawasiliano nao ni binadamu na wanapotengeneza teknolojia mpya, wanazifanyia tafiti za kina kupima madhara yake kabla ya kuzipitisha kutumika. Pia, kila nchi (hasa zilizoendelea) zina taasisi za viwango, uratibu na udhibiti kwa lengo la kuthibitisha ubora na usalama wa mitambo ya mawasiliano kabla ya kutumika katika jamii (sisi tuna TCRA). Hakuna taifa/serikali hata moja duniani, iko tayari kufunga mitambo ya mawasiliano ambayo ina madhara kwa watu wake huku wakijua haitachagua nani wa kumdhuru.

Fursa inayotumiwa na wanaohubiri nadharia njama ya 5G
Baadhi ya manabii wa nadharia njama ya 5G ni watu wenye elimu kubwa na ufahamu mpana wa mambo. Wataalamu wengi wa nadharia njama wana akili nyingi na ni wasomi wazuri. Hivyo wanatumia nafasi hiyo kama njia ya kuonesha wanachokiongea kina ukweli. Kunahitajika uwezo mkubwa na uelewa wa mambo kung'amua yaliyo nyuma ya nadharia zao. Hata hivyo, miongoni mwao kuna wengi hawana kabisa uelewa wa teknolojia za mawasiliano na hawana uwezo wa kukuambia 5G ni kitu gani au hizo hatari zinatokeaje katika uhalisia. Ukiwasikiliza vema, wanatumia baadhi ya nadharia za mifumo ya teknolojia ya mawasiliano kwa kuungaunga kama namna ya kuonesha uhatari wa 5G. Wanataja maneno kama artificial intelligence (AI), Internet of Things (IoT) au Machine Leaning (ML) kujazia hoja zao bila kuelewa zinalenga nini hasa. Kwa mtu asiye na eleimu ya mambo haya (na hawa ni wengi kwenye jamii) akitajiwa mambo haya anapata picha inayotisha sana. Kama vile haitoshi, watu hawa hawana uelewa wa kutosha kuhusu epidemilojia ya magonjwa ya mlipuko. Ila, wanafanikiwa kwa kiasi kikubwa kupotosha kwa kua wanajua au kuamini kwamba wanaowasikiliza hawana uelewa wa mambo au elemu yao ni ndogo kuweza kung’amua ukweli au kutafuta usahihi wa wanachokisema.

Hitimisho na Ushauri
Nadharia njama ya 5G na nyingine zina hatarisha watu wengi kuambukizwa na Covid-19 kwani wanaozisambaza wanatoa maelezo yanayokanganya na kuwafanya wengi wasifuate maelekezo ya kisayansi ya ugonjwa huu na namna ya kukabiliana nao. Ndio mana utaelewa ni kwa nini juzi kule Abijan Ivory Coast wananchi wameandama na kwenda kuvunja jengo maalum linaloandaliwa kwa ajili ya kupimia wagonjwa wa Covid-19. Pia utaelewa ni kwa nini, baadhi ya “watumishi” wanahamasisha waumini wao waendelee kufanya ibada za pamoja kwa wingi zaidi wakiamini Covid-19 ni mbinu za mpinga Kristo na wanatakiwa kuamini haitawapata wao. Waliosambaza Covid-19 kwa wingi kule Korea ya Kusini walikua wakristo (walokole) waliopuuzia athari za ugonjwa huu. Waliambukizana kwa wingi na wakafanya karibu mji mzima kulemewa na maambukizi.

Kama nilivyosema kwenye moja ya makala zangu kuhusu janga la Covid-19 na kuziweka
hapa Jamii Forum, mlipuko huu umedhihirisha ni kwa kiasi gani sisi waafrika tulio wengi sio jamii inayoongozwa na elimu, maarifa, sayansi, na teknolojia. Imetuonesha namna tunavyofanya maamuzi yetu bila kutumia taarifa sahihi na tulivyo warahisi kuamini taarifa za uongo, za uzushi, na kutotaka kujishughulisha kutafuta ukweli na maarifa. Pia, imetuonesha namna mfumo wetu wa elimu usivyotuandaa na kutuwezeha kutumia uwezo wetu wa kufikiri, kufanya tafakuri tunduizi, na kuchambua mambo kwa lengo la kutafuta maarifa, ukweli au usahihi wa kile tunachosikia.

Kama vile haitoshi, mlipuko huu umetuonesha namna baadhi ya "watumishi wa dini zetu" wanavyotumia kila fursa wanayoipata kutuweka mbali na ukweli kwa makusudi na kwa manufaa yao binafsi. Hawataki tutumie akili zetu na elimu kutafuta majawabu ya maswali magumu yanatotukabili au suluhisho la changamoto tunazokutana nazo. Kila mara wanataka tutumie fikra za kiimani kama "shortcut" ambayo haitufikishi wanapotuahidi. Ifike mahali, wapendwa hawa wakubali kwamba wao sio miungu na hawana ufunuo wa kila jambo. Wao ni watumishi tu hivyo hawawezi kuwa na maelezo au majawabu ya kila swali au utata unaojitokeza kwenye jamii. Ni sahihi kabisa wakisema hawana maelezo au hawajui au bado wanamwomba wanayemtumikia kupata majawabu. Kukiri hivi hakuwapunguzii kitu katika nafasi yao ya utumishi. Pia kwa mambo ya kitaalamu/kisayansi, ni vema wakatafuta wabobezi wa eneo husika wakawapa mwanga wa kutosha wa kisayansi kabla ya kuyaongelea kwa umma katika muktadha wa kiimani. Hii ina msaada mkuwa sana na inawapa heshima hata nje ya waumini wao. Wana fursa kubwa ya kupata maelezo ya kitaalamu tena bure kutoka kwa makundi yao na hata wasio wa makundi yao.

Moja ya mambo yanayotuchelewesha waafrika kuendelea kwa kasi kama mataifa mengine tuyatazamayo kama vielelezo, ni kuhoji kila kitu kigeni kwa mtizamo wa kukiogopa au kukishuku huku tukiwa hatuna maelezo sahihi wala uthibitisho wa tunachoamini/kuaminishwa/kuwaaminisha wengine. Mbaya zaidi tunakua hatuna mbadala wa kuwapa tunaowajengea hofu. Unawaaminisha watu kuwa 5G ni hatari au ni shetani huku mfukoni una simu ya 4/5G na hotuba au mahubiri unayotoa unayarusha live kwa Youtube inayotumia teknolojia ya 5G kuweza kustahimili wingi wa watu wanayoitumia. Pia una accounts za mitandao ya kijamii ambayo kwa sehemu kubwa zinategemea teknolojia unayopambana nayo. Sasa tukuamini kwa lipi?


Zingatia
  1. Uchambuzi na maoni niliyoyatoa hapa, hayamaanishi kwamba ninaamini hakuna madhara yanayoweza kusababishwa na teknolojia ya 5G. Pia, hayamaanishi ninapinga watu kuhojia, kutafiti, au kuweka mashaka kuhusu usalama wa teknolojia hii. Hapana. Hoja yangu nya msingi ni kutofautina na upotofu unaonezwa na nadharia njama ya kuhusianisha Covid-19 na 5G. Tuhoji na kutafiti madhara ya 5G na mambo mengine (kama ni lazima) kwa kutumia ukweli na ushahidi wa kisayansi badala ya dhana za kufikirika na ndoto za abunuwasi.

    Sehemu kubwa ya Afrika tuko kwenye mkwamo kama jamii na mapokeo tuliyoletewa na waliotutawala (hasa imani) yanatuathiri kifikra na kimitazamo kuliko waliozinzisha. Hivyo tukimaliza hili la Covid-19, tuanze kuweka mikakati ya muda mrefu ya kujikwamua tulipokwama ili kurahisha maendeleo ya watu na vitu. Pamoja na bidii na imani zetu, tunahitaji elimu na maarifa sahihi ili tuweze kupiga hatua na kuleta maendeleo endelevu.


  2. Uchambuzi huu haujalenga kuwashambulia wakristo au "watumishi" kwani nami ni mmoja wao. Nimetaja ukristo (tena kwa tahadhari kubwa) maana ndio kundi nililoko na ninashuhudia jinsi baadhi yetu wanavyokazana kupotosha kuhusu Covid-19 na kinaathiri jamii kubwa.

  3. Neno "Nadharia Njama" sio rasmi katika viunga vya lugha ya Kiswahili bali nimelitohoa mimi mwenyewe baada ya kuketi na kamusi za Kiswahili nikiwa natafuta tafsiri/maana ya "Consipiracy Theory". Sifahamu tafsiri rasmi ya dhana hii kwa Kiswahili.

Mathew Togolani Mndeme (mmtogolani@gmail.com)
Mtafiti wa mifumo ya digitali kwenye ufuatiliaji na udhibiti wa magonjwa

  • Shukrani kwa classmate wangu Dr. Baraka Maiseli (Lecturer in Electronic and Telecommunications Engineering, UDSM) kwa ushauri kwenye ufafanuzi wa teknolojia ya 5G
Mathew Togolani Mndeme

Mwaka mmoja baadaye, hoja ya 5G na uhusiano wake na Corona haipo tena.
 
MUHTASARI
Mlipuko wa Covid-19 unasambaa ukiambatana na taarifa nyingi zisizo sahihi au za kupotosha. Taarifa hizi zinatengenezwa, ama kwa watu kukosa uelewa sahihi wa jambo wanalolizungumzia au kwa makusudi, kama “Nadharia Njama” (Conspiracy Theory). Mojawapo ni Nadharia Njama inayohusianisha mlipuko wa Covid-19 na tekenolojia mpya ya mawasiliano ya 5G. Nadharia hii inaenezwa na kuaminiwa kwa kasi sana hasa na baadhi ya makundi ya kiimani. Hii imetokana na baadhi ya watumishi kadhaa duniani “wenye majina” kuibeba na kuifanya sehemu ya mahubiri yao kipindi hiki cha taharuki. Kwenye makala hii, ninafafanua teknolojia ya 5G kwa kifupi, madhara yake, na kujaribu kuonesha mapungufu ya nadharia njama kuhusu uhusiano wa 5G na Covid-19. Lengo kuu ni kutoa mwanga kwenye jamii yetu kuhusu kinachosambazwa kupitia nadharia njama ya 5G na kuibua mjadala utakaotusaidia kuujua ukweli wa jambo hili tunapopambana na Covid-19. Kwa undani zaidi, soma makala nzima.

View attachment 1412217
Utangulizi.
Katika mapambano dhidi ya mlipuko wa Covid-19 kwenye nchi yetu na nyingi za Afrika, kuna eneo moja halijatazamwa kwa mapana yake. Eneho hilo ni ugonjwa huu kuhusianishwa na nadharia njama kadhaa na kupewa tafsiri za kiimani kuliko za kisayansi. Kwa kufanya hivyo, kuna hatari kwa baadhi ya watu kupuuzia mlipuko huu na hivyo kuhatarisha maambukizi kua makubwa. Pili, nadharia njama zinaongeza taharuki ya mlipuko na kuwapa watu madhara ya kisaikolojia kujiona wamezungukwa na hatari muda wote kutoka kwa watu wasiowajua. Ukifuatilia kwenye internet na vyombo vya habari vya kimataifa, utaona kuna kundi kubwa la watu hawaamini kama Covid-19 ni ugonjwa unaosababishwa na virusi ambao ni viumbe wa kawaida tulionao kwenye dunia hii. Kinyume chake wanaamini kuna njama, ama za kibaguzi, kibishara, au za kiimani zilizopelekea watu fulani wasiotajwa kutengeneza au kusababisha kutokea kwa ugonjwa wa Covid-19. Moja ya nadharia hizo ni ile inayoaminisha kwamba Covid-19 inasababishwa na teknolojia mpya ya mawasiliano ya 5G.

Je,5G ni kitu gani?
Teknolojia ya mawasiliano ya simu imekuwa ikipanuka na kuendelea siku hadi siku. Teknolojia ya mawasiliano ndio iliyokua kwa kasi zaidi katika historia ya kizazi chetu. Pamoja na mambo mengine, ukuaji wa teknolojia ya mawasiliano unapimwa kwa spidi/kasi ya kusafirisha data kati ya pande mbili zinazowasiliana. Kwa miaka mingi, spidi ya data imekuwa ikiboreshwa na kuongezeka kwa kuboresha miundombinu ya mawasiliano (hardware na software). Hivyo, tangu mwaka 1940, tumetoka kwenye teknolojia inayoitwa 0G (herufi “G” ikimaanisha Generation au kizazi) kwenda kwenye teknolojia inayoitwa 4G (4 generation au kizazi cha 4) tunayotumia sasa.

Kwa sasa, wavumbuzi wameibuka na teknolojia ya 5G ambayo ina spidi kubwa zaidi inayoweza kusafirisha zaidi ya 1 Gbit za data kwa sekunde. Kwa spidi hii kali, tunaweza kufanya kazi nzito zaidi ambazo teknolojia zilizopita haziwezi. Kwa mfano, teknolojia hii inaweza kutumika kwenye magari yanayojiendesha yenyewe (self-driving/autonomous cars); uwezo wa kuunganisha vitu mbalimbali katika mtandao kwa urahisi (Internet of Things); kuwa na miji yenye huduma za kijamii zilizojengwa na kuboreshwa kwa teknolojia ya mawasiliano (smart cities); kuongoza vyombo vya usafiri; vifaa vya burudani; nk. Teknolojia ya 5G inamwingiza binadamu kwenye aina mpya kabisa ya kuishi, na maisha yanatazamiwa kuboreshwa kwa sehemu kubwa. Lakini swali kubwa la kujiuliza hapa ni nini hasa kinatusukuma tunahamia 5G na tutapata faida au athari gani?

Ili kujua kwa nini dunia inaongelea 5G ni lazima uitazame kama kijiji kinachoendelea kwa kasi kubwa na hivyo kupelekea mabadiliko ya mahitaji mengi. Mathalani, kiwango cha data/taarifa kinachozalishwa katika dunia ni kikubwa mno. Ukichukulia mtandao wa Google pekee tuliouzoea, kila siku unazalisha takribani 20 petabytes (10PT) za data (Petabyte 1 ni sawa na Gigabyte (GB) milioni 1). Pia, sekta ya tamthilia (movie) inahama kwa kazi kutoka kutegemea video zinazouzwa kwa njia ya DVD au kaseti kuelekea kutazama tamthilia online kupitia mitandano kama Youtube na Netflix. Pia, utazamaji wa television unahamia kwenye Smart TV ambazo zinakupa uwezo wa kutazama television huku ukiwa unapata huduma nyingi kwa mtandao mithili ya matumizi ya kompyuta. Mahitaji haya ndiyo yalifanya wavumbuzi waanze kufikiria namna ya kuongeza uwezo wa kusafirisha data na kuibuka na 5G. Makampuni ya mawasiliano yanakimbilia kuwekeza katika teknolojia ya 5G kwa sababu ya faida nyingi ambazo wataje wao watapata. hata hivyo kuna changamoto kubwa mbili za 5G kimuondombinu.

  1. Teknolojia ya 5G inahitaji uwekezaji mkubwa wa miundombinu mipya ya mawasiliano kwa sababu inalazimisha kubadilisha ile iliyoko kwa sehemu kubwa. Hadi sasa kuna takribani nchi 35 (nyingi zikiwa tajiri) ambazo tayari zina miundombinu ya 5G na bado inajengwa. Ufungaji wa miundombinu hii kwa nchi nyingi umeanza mwaka 2019.

    Nchi zinazoongoza kuwa na miundombinu ya 5G kwenye miji mingi ni South Korea, China, na Marekani. Kwa miaka kama 2 iliyopita, utakua umesikia siasa za 5G kati ya mataifa makubwa hasa Marekani, Uingereza na China. Hii imetokana na ukweli kwamba kampuni ya Huawei ya wachina imekua mbele hatua kadhaa kiteknolojia na kuzifanya nchi nyingi zikiwemo za Magharibi kutumia teknolojia zake ikiwemo kuweka miundombinu ya 5G. Hii imewapa taharuki maadui zao kiuchumi hasa Marekani kwa hoja kwamba mitambo yao sio salama kwa kuwa inaratibiwa au kudukuliwa na serikali ya China (hili tuliachie hapa maana ni mjadala mwingine).


  2. Nyingine ni ukweli kwamba wateja watalazimika kuwa na vifaa vilivyotengenezwa kutumia teknoljia ya 5G, na hivyo kuingia gharama ya ziada/kubwa.
Pamoja na changamoto hizi na nyingine, bado 5G inatoa matumaini mapya ya maendeleo yatakayomwezesha binadamu kufanya shughuli nyingi ngumu kwa muda mfupi. 5G inafanikishwa mambo mawili makubwa. Moja ni kiwango cha data kinachoweza kusafirishwa, na mbili ni spidi/kasi ya data kusafiri kati ya kifaa kimoja na kingine.

Je, 5G ina madhara gani kiafya?
Nadharia njama ya 5G imejikita katika kile kinachoitwa madhara makubwa ya 5G kwa afya zetu. Kumesambaa habari nyingi duniani zilizoanzishwa na watu wachache na zimeshika kazi kama moto wa mabua kiasi kwamba zimeanza kuaminika kama ukweli. Hii imepelekea siku ya jana mtandao wa Youtube kuamu kuanza kufuta video zote kwenye mfumo wao zinazoongela nadharia njama ya G5 na uhusiano wake na Covid-19 (tazama hapa). Katika nchi za kiafrika ambapo kwa sehemu kubwa tumeturuhu watu wengine wafikirie na hata kuamua kwa niaba yetu, nadharia hii imeingizwa kwenye viunga vya kiimani na imeshakua ukweli kwa watu wengi maana huwa tunaogopa kuhoji mambo ya kiimani au wanachokisema watumishi.

Nimesikiliza na kusoma maelezo ya waanzilishi na wainjilisti wa nadharia njama ya 5G ili kuelewa msingi wa taharuki wanayoijenga. Mengi wanayoongea ni uongo, uzushi, ya kuungaunga, na hayana usahihi wowote kisayansi wala kiimani. Nadharia hii imeanzishwa na wataalamu wa nadharia njama (conspirancy theorists - wawili wakiwa ni waingereza) na kudakwa na baadhi ya watumishi “wenye majina” kama hoja ya mahubiri yao. Baadhi ya watumishi (hasa wa kikristo) hupenda kujionesha kua wao wana majibu au maelezo ya kila jambo duniani. Hivyo wamechukua hoja ya 5G na kuitumia kama ilivyo au kwa kuitohoa kujengea hoja za chanzo na malengo ya Covid-19. Nitaje kwa kifupi baadhi ya hoja zilizoko kwenye nadharia njama ya 5G.

  1. Taswira inajengwa kwamba kuna mkakati wa watu ambao wanaleta teknolojia ya 5G kwa lengo la kuitawala dunia na hasa kutufanya sisi wanadamu wote kuunganishwa kwenye mtandao mmoja ili kuweza kutaribiwa. Mkakati huu unapewa majina mengi lakini mojawapo ni mbinu ya kufanikisha kinachoitwa “New World Order (NWO)”. NWO ni nadharia njama inayodai kuna kundi la siri lenye nguvu kuliko mataifa yote litakaloitawala dunia nzima kibabe.
    UDHAIFU: wanaoaminisha nadharia hii hawataji watu hao ni kina nani, wako nchi gani, na iwapo ni wa dunia hii au sayari nyingine. Ukiachilia kutajwa kwa baadhi ya viongozi wakuu wa baadhi ya nchi na dini kubwa, nadharia hii inabaki kuwa yakufirika na imekuwepo kwa muda mrefu.


  2. Hoja inajengwa kwamba vifaa vya teknolojia ya 5G vina mionzi mikali yenye madhara kwenye miili yetu. Katika kupambana nayo, miili yetu inatengeneza virusi wa Corona.
    UDHAIFU: Moja, hakuna ushahidi wa kisayansi wowote juu ya hili. Pili, kama miili yetu inatengeneza virusi wa Corona tunapopigwa na mionzi ya 5G, kwa nini basi tusingekua tunaugua wote kwenye eneo lenye 5G? Tatu, kwa nini watu wanaoathirika wanapona?


  3. Wakati huohuo wanadai Covid-19 inasambazwa kwa watu kupitia vipimo tunavyofanyiwa kujua iwapo tuna maambukizi. Lengo kubwa la kuingiziwa virusi hivi ni ili dunia nzima iwe na maambukizi kisha kupitishwe taratibu/sheria inayomtaka kila mtu lazima apewe chanjo ya kumkinga na Covid-19. Kupitia chanjo hiyo tutaingiziwa “chip” ndogo ya mawasiliano kwenye miili yetu (mithili ya line ya simu yako) itakayowezesha watu hao wasiojulikana kutufuatilia kama vile mitambo ya kompyuta. Pia, mtu hataweza kupata visa kuingia nchi nyingine iwapo hajathibitisha kua na una kinga ya Covid-19.
    UDHAIFU: Moja, tuna ushahidi kutoka nchi nyingi watu kuambukizwa na kueonesha dalili (wengine hadi kufariki) kabla ya kupimwa. Pili, ili uweze kupachika chip ya kielekroniki ifanye kazi na kuweza kusafirisha data na mfumo wa mwili, ni lazima ipachikwe mahili maalumu na kuunganishwa na mfumo wa mawasiliano wa mwili. Wanaohubiri nadharia hii hawatuelezi ni kwa jinsi gani chanjo tutakayopewa (ama vidonge au kimiminika) itaingiza chip mwilini na ikafanye kazi.


  4. Wakristo wanatahadharishwa kwamba 5G ni mpango wa shetani na Covid-19 ni vita dhidi yao. Wengine wanakwenda mbali zaidi kudai Covid-19 imetengenezwa kwa lengo la kuangamiza waafrika ila waliotengeneza wamekosea ikawaathiri wao wenyewe.
    UDHAIFU: Hoja hii ni dhaifu kama zingine maana ni ya kufikirika.


  5. Katika kujenga hoja zao, baadhi ya manabii wa njama hii wanasema virusi sio viumbe halisia bali wanatengenezwa kwa malengo mabaya.
    UDHAIFU: Huu ni uongo ulioopitiliza kwani wanasayansi wa viorolojia wanatuambia kuna aina takribani 5,000 ya virusi wa asili duniani. Sifa kubwa ya virusi ni kutokua na uwezo wa kuishi wenyewe bila kuwa ndani au juu ya kiumbe kingine. Hivyo wanaweza kuishi kwa wanadamu, wanyama, ndege, samaki, mimea na hata viumbe vidogo kama bakteria. Hata hivyo wataalamu wa bayoteknolojia wanaweza kutengeneza virusi kwa njia za kimaabara kwa malengo mbalimbali.


  6. Wanajenga hoja kwamba kirusi cha Corona ni kipya na hajawahi kuwepo. Moja ya filamu ya kijapani iliyotengenezwa 2018 ina kipengele wanachotaja visuri wa Corona hivyo kipengele hiki kinatumika kuthibitisha kwamba Corona ni mkakati wa silaha za kibalojia.
    UDHAIFU: Hoja hii inadhirisha jinsi upotoshaji huu usivyo na mashiko. Virusi wanaosababisha Covid-19 (yaani SARS-CoV-2), ni kafamilia kamoja tu kati ya familia karibu 60 za ukoo wa Coronavirus. Wana dada yao anaitwa SARS-CoV-1 aliyesababisha mlipuko wa SARS kule China mwaka 2002/2004 lakini ukadhibitiwa. Pia wana binamu naitwa MERS-Cov aliyelipuka kule uarabuni 2012 na kudhibitiwa pia.
Uhalisia uko wapi?
Kuna uwezekano mkubwa wa teknolojia ya mawasiliano kuwa na madhara kiafya kama zilivyo teknolojia nyingi tunazotumia kila siku (magari, simu za mikononi, kompyuta, nk). Kwenye teknolojia ya mawasiliano, madhara yanahusishwa moja kwa moja na mionzi inayotumika kusafirisha data (kwa mfano simu zetu kuwasiliana na minara ya mawasiliano au na kifaa cha kupata mtandao wa intenet kwa njia ya upepo (WiFi)).

Kwa mfano, tafiti kadhaa zilizofanyika nchi kama India, Australia, Marekani, Ufaransa, nk, zimeonesha uwezekano wa madhara yatokanayo na matumizi ya simu za mikononi (sio za 5G). Ziko tafiti zimeonesha mionzi ya simu inaweza kusabanisha kansa, kuharibu mbegu za kiume, nk. Watafiti wanatoa tahadhari na kuwashauri watu kupuunguza mawasiliano ya simu za mikononi na kuzitaka kampuni zinazotengeneza simu kuwa wawazi kwa kuweka tahadhari wazi juu ya madhara mtu anayoweza kuyapata kwa kutumia simu. Wanashauri tuwazuie watoto kutumia simu na vifaa vingine vyenye WiFi ili kuzuia madhara ya mionzi ambayo imeonekana inaweza kusababisha kansa ya ubongo.

Kuna mjadala na mvutano mkubwa kati ya watafiti na watu walio kwenye sekta ya mawasiliano kuhusu ukweli wa madhara vifaa vya mawasiliano. Wanaopinga uwepo wa madhara wanasema hakuna ushahidi wa kutosha kuthibitisha yale yanayodaiwa [Hii ni mada ndefu hivyo kwa sasa niiachie hapa nirudi kwenye 5G].

Hivyo basi, kama simu ambazo tayari tunatumia zenye teknolojia ya 2G, 3G au 4G zimethibitika kwamba zinaweza kua na madhara yatokanayo na mionzi, ni wazi 5G inaweza kuwa na ina hiyohiyo ya madhara. Yanaweza yakawa ama nafuu zaidi kutokana na maendeleo ya teknolojia au makali zaidi kwa sababu hiyohiyo. Manabii wa nadharia njama ya 5G wanajenga hoja kwamba mionzi itokayo kwenye vifaa vya 5G ina nguvu isiyoweza kustahimilika na miili yetu.

Hata hivyo, lazima tutambue kwamba, wagunduzi wa mawasiliano nao ni binadamu na wanapotengeneza teknolojia mpya, wanazifanyia tafiti za kina kupima madhara yake kabla ya kuzipitisha kutumika. Pia, kila nchi (hasa zilizoendelea) zina taasisi za viwango, uratibu na udhibiti kwa lengo la kuthibitisha ubora na usalama wa mitambo ya mawasiliano kabla ya kutumika katika jamii (sisi tuna TCRA). Hakuna taifa/serikali hata moja duniani, iko tayari kufunga mitambo ya mawasiliano ambayo ina madhara kwa watu wake huku wakijua haitachagua nani wa kumdhuru.

Fursa inayotumiwa na wanaohubiri nadharia njama ya 5G
Baadhi ya manabii wa nadharia njama ya 5G ni watu wenye elimu kubwa na ufahamu mpana wa mambo. Wataalamu wengi wa nadharia njama wana akili nyingi na ni wasomi wazuri. Hivyo wanatumia nafasi hiyo kama njia ya kuonesha wanachokiongea kina ukweli. Kunahitajika uwezo mkubwa na uelewa wa mambo kung'amua yaliyo nyuma ya nadharia zao. Hata hivyo, miongoni mwao kuna wengi hawana kabisa uelewa wa teknolojia za mawasiliano na hawana uwezo wa kukuambia 5G ni kitu gani au hizo hatari zinatokeaje katika uhalisia. Ukiwasikiliza vema, wanatumia baadhi ya nadharia za mifumo ya teknolojia ya mawasiliano kwa kuungaunga kama namna ya kuonesha uhatari wa 5G. Wanataja maneno kama artificial intelligence (AI), Internet of Things (IoT) au Machine Leaning (ML) kujazia hoja zao bila kuelewa zinalenga nini hasa. Kwa mtu asiye na eleimu ya mambo haya (na hawa ni wengi kwenye jamii) akitajiwa mambo haya anapata picha inayotisha sana. Kama vile haitoshi, watu hawa hawana uelewa wa kutosha kuhusu epidemilojia ya magonjwa ya mlipuko. Ila, wanafanikiwa kwa kiasi kikubwa kupotosha kwa kua wanajua au kuamini kwamba wanaowasikiliza hawana uelewa wa mambo au elemu yao ni ndogo kuweza kung’amua ukweli au kutafuta usahihi wa wanachokisema.

Hitimisho na Ushauri
Nadharia njama ya 5G na nyingine zina hatarisha watu wengi kuambukizwa na Covid-19 kwani wanaozisambaza wanatoa maelezo yanayokanganya na kuwafanya wengi wasifuate maelekezo ya kisayansi ya ugonjwa huu na namna ya kukabiliana nao. Ndio mana utaelewa ni kwa nini juzi kule Abijan Ivory Coast wananchi wameandama na kwenda kuvunja jengo maalum linaloandaliwa kwa ajili ya kupimia wagonjwa wa Covid-19. Pia utaelewa ni kwa nini, baadhi ya “watumishi” wanahamasisha waumini wao waendelee kufanya ibada za pamoja kwa wingi zaidi wakiamini Covid-19 ni mbinu za mpinga Kristo na wanatakiwa kuamini haitawapata wao. Waliosambaza Covid-19 kwa wingi kule Korea ya Kusini walikua wakristo (walokole) waliopuuzia athari za ugonjwa huu. Waliambukizana kwa wingi na wakafanya karibu mji mzima kulemewa na maambukizi.

Kama nilivyosema kwenye moja ya makala zangu kuhusu janga la Covid-19 na kuziweka
hapa Jamii Forum, mlipuko huu umedhihirisha ni kwa kiasi gani sisi waafrika tulio wengi sio jamii inayoongozwa na elimu, maarifa, sayansi, na teknolojia. Imetuonesha namna tunavyofanya maamuzi yetu bila kutumia taarifa sahihi na tulivyo warahisi kuamini taarifa za uongo, za uzushi, na kutotaka kujishughulisha kutafuta ukweli na maarifa. Pia, imetuonesha namna mfumo wetu wa elimu usivyotuandaa na kutuwezeha kutumia uwezo wetu wa kufikiri, kufanya tafakuri tunduizi, na kuchambua mambo kwa lengo la kutafuta maarifa, ukweli au usahihi wa kile tunachosikia.

Kama vile haitoshi, mlipuko huu umetuonesha namna baadhi ya "watumishi wa dini zetu" wanavyotumia kila fursa wanayoipata kutuweka mbali na ukweli kwa makusudi na kwa manufaa yao binafsi. Hawataki tutumie akili zetu na elimu kutafuta majawabu ya maswali magumu yanatotukabili au suluhisho la changamoto tunazokutana nazo. Kila mara wanataka tutumie fikra za kiimani kama "shortcut" ambayo haitufikishi wanapotuahidi. Ifike mahali, wapendwa hawa wakubali kwamba wao sio miungu na hawana ufunuo wa kila jambo. Wao ni watumishi tu hivyo hawawezi kuwa na maelezo au majawabu ya kila swali au utata unaojitokeza kwenye jamii. Ni sahihi kabisa wakisema hawana maelezo au hawajui au bado wanamwomba wanayemtumikia kupata majawabu. Kukiri hivi hakuwapunguzii kitu katika nafasi yao ya utumishi. Pia kwa mambo ya kitaalamu/kisayansi, ni vema wakatafuta wabobezi wa eneo husika wakawapa mwanga wa kutosha wa kisayansi kabla ya kuyaongelea kwa umma katika muktadha wa kiimani. Hii ina msaada mkuwa sana na inawapa heshima hata nje ya waumini wao. Wana fursa kubwa ya kupata maelezo ya kitaalamu tena bure kutoka kwa makundi yao na hata wasio wa makundi yao.

Moja ya mambo yanayotuchelewesha waafrika kuendelea kwa kasi kama mataifa mengine tuyatazamayo kama vielelezo, ni kuhoji kila kitu kigeni kwa mtizamo wa kukiogopa au kukishuku huku tukiwa hatuna maelezo sahihi wala uthibitisho wa tunachoamini/kuaminishwa/kuwaaminisha wengine. Mbaya zaidi tunakua hatuna mbadala wa kuwapa tunaowajengea hofu. Unawaaminisha watu kuwa 5G ni hatari au ni shetani huku mfukoni una simu ya 4/5G na hotuba au mahubiri unayotoa unayarusha live kwa Youtube inayotumia teknolojia ya 5G kuweza kustahimili wingi wa watu wanayoitumia. Pia una accounts za mitandao ya kijamii ambayo kwa sehemu kubwa zinategemea teknolojia unayopambana nayo. Sasa tukuamini kwa lipi?


Zingatia
  1. Uchambuzi na maoni niliyoyatoa hapa, hayamaanishi kwamba ninaamini hakuna madhara yanayoweza kusababishwa na teknolojia ya 5G. Pia, hayamaanishi ninapinga watu kuhojia, kutafiti, au kuweka mashaka kuhusu usalama wa teknolojia hii. Hapana. Hoja yangu nya msingi ni kutofautina na upotofu unaonezwa na nadharia njama ya kuhusianisha Covid-19 na 5G. Tuhoji na kutafiti madhara ya 5G na mambo mengine (kama ni lazima) kwa kutumia ukweli na ushahidi wa kisayansi badala ya dhana za kufikirika na ndoto za abunuwasi.

    Sehemu kubwa ya Afrika tuko kwenye mkwamo kama jamii na mapokeo tuliyoletewa na waliotutawala (hasa imani) yanatuathiri kifikra na kimitazamo kuliko waliozinzisha. Hivyo tukimaliza hili la Covid-19, tuanze kuweka mikakati ya muda mrefu ya kujikwamua tulipokwama ili kurahisha maendeleo ya watu na vitu. Pamoja na bidii na imani zetu, tunahitaji elimu na maarifa sahihi ili tuweze kupiga hatua na kuleta maendeleo endelevu.


  2. Uchambuzi huu haujalenga kuwashambulia wakristo au "watumishi" kwani nami ni mmoja wao. Nimetaja ukristo (tena kwa tahadhari kubwa) maana ndio kundi nililoko na ninashuhudia jinsi baadhi yetu wanavyokazana kupotosha kuhusu Covid-19 na kinaathiri jamii kubwa.

  3. Neno "Nadharia Njama" sio rasmi katika viunga vya lugha ya Kiswahili bali nimelitohoa mimi mwenyewe baada ya kuketi na kamusi za Kiswahili nikiwa natafuta tafsiri/maana ya "Consipiracy Theory". Sifahamu tafsiri rasmi ya dhana hii kwa Kiswahili.

Mathew Togolani Mndeme (mmtogolani@gmail.com)
Mtafiti wa mifumo ya digitali kwenye ufuatiliaji na udhibiti wa magonjwa

  • Shukrani kwa classmate wangu Dr. Baraka Maiseli (Lecturer in Electronic and Telecommunications Engineering, UDSM) kwa ushauri kwenye ufafanuzi wa teknolojia ya 5G
RANGI ulizotumia ni mbaya mkuu,badilisha ili tukupe mawazo yetu.Naamini unayojua ni "in the box" not "out of the box."
 
Andunje Gwajima aliwafunga watu kamba sana kwa nadharia uchwara hadi alikuwa anabishana na wataalam.
 
MUHTASARI
Mlipuko wa Covid-19 unasambaa ukiambatana na taarifa nyingi zisizo sahihi au za kupotosha. Taarifa hizi zinatengenezwa, ama kwa watu kukosa uelewa sahihi wa jambo wanalolizungumzia au kwa makusudi, kama “Nadharia Njama” (Conspiracy Theory). Mojawapo ni Nadharia Njama inayohusianisha mlipuko wa Covid-19 na tekenolojia mpya ya mawasiliano ya 5G. Nadharia hii inaenezwa na kuaminiwa kwa kasi sana hasa na baadhi ya makundi ya kiimani. Hii imetokana na baadhi ya watumishi kadhaa duniani “wenye majina” kuibeba na kuifanya sehemu ya mahubiri yao kipindi hiki cha taharuki. Kwenye makala hii, ninafafanua teknolojia ya 5G kwa kifupi, madhara yake, na kujaribu kuonesha mapungufu ya nadharia njama kuhusu uhusiano wa 5G na Covid-19. Lengo kuu ni kutoa mwanga kwenye jamii yetu kuhusu kinachosambazwa kupitia nadharia njama ya 5G na kuibua mjadala utakaotusaidia kuujua ukweli wa jambo hili tunapopambana na Covid-19. Kwa undani zaidi, soma makala nzima.

View attachment 1412217
Utangulizi.
Katika mapambano dhidi ya mlipuko wa Covid-19 kwenye nchi yetu na nyingi za Afrika, kuna eneo moja halijatazamwa kwa mapana yake. Eneho hilo ni ugonjwa huu kuhusianishwa na nadharia njama kadhaa na kupewa tafsiri za kiimani kuliko za kisayansi. Kwa kufanya hivyo, kuna hatari kwa baadhi ya watu kupuuzia mlipuko huu na hivyo kuhatarisha maambukizi kua makubwa. Pili, nadharia njama zinaongeza taharuki ya mlipuko na kuwapa watu madhara ya kisaikolojia kujiona wamezungukwa na hatari muda wote kutoka kwa watu wasiowajua. Ukifuatilia kwenye internet na vyombo vya habari vya kimataifa, utaona kuna kundi kubwa la watu hawaamini kama Covid-19 ni ugonjwa unaosababishwa na virusi ambao ni viumbe wa kawaida tulionao kwenye dunia hii. Kinyume chake wanaamini kuna njama, ama za kibaguzi, kibishara, au za kiimani zilizopelekea watu fulani wasiotajwa kutengeneza au kusababisha kutokea kwa ugonjwa wa Covid-19. Moja ya nadharia hizo ni ile inayoaminisha kwamba Covid-19 inasababishwa na teknolojia mpya ya mawasiliano ya 5G.

Je,5G ni kitu gani?
Teknolojia ya mawasiliano ya simu imekuwa ikipanuka na kuendelea siku hadi siku. Teknolojia ya mawasiliano ndio iliyokua kwa kasi zaidi katika historia ya kizazi chetu. Pamoja na mambo mengine, ukuaji wa teknolojia ya mawasiliano unapimwa kwa spidi/kasi ya kusafirisha data kati ya pande mbili zinazowasiliana. Kwa miaka mingi, spidi ya data imekuwa ikiboreshwa na kuongezeka kwa kuboresha miundombinu ya mawasiliano (hardware na software). Hivyo, tangu mwaka 1940, tumetoka kwenye teknolojia inayoitwa 0G (herufi “G” ikimaanisha Generation au kizazi) kwenda kwenye teknolojia inayoitwa 4G (4 generation au kizazi cha 4) tunayotumia sasa.

Kwa sasa, wavumbuzi wameibuka na teknolojia ya 5G ambayo ina spidi kubwa zaidi inayoweza kusafirisha zaidi ya 1 Gbit za data kwa sekunde. Kwa spidi hii kali, tunaweza kufanya kazi nzito zaidi ambazo teknolojia zilizopita haziwezi. Kwa mfano, teknolojia hii inaweza kutumika kwenye magari yanayojiendesha yenyewe (self-driving/autonomous cars); uwezo wa kuunganisha vitu mbalimbali katika mtandao kwa urahisi (Internet of Things); kuwa na miji yenye huduma za kijamii zilizojengwa na kuboreshwa kwa teknolojia ya mawasiliano (smart cities); kuongoza vyombo vya usafiri; vifaa vya burudani; nk. Teknolojia ya 5G inamwingiza binadamu kwenye aina mpya kabisa ya kuishi, na maisha yanatazamiwa kuboreshwa kwa sehemu kubwa. Lakini swali kubwa la kujiuliza hapa ni nini hasa kinatusukuma tunahamia 5G na tutapata faida au athari gani?

Ili kujua kwa nini dunia inaongelea 5G ni lazima uitazame kama kijiji kinachoendelea kwa kasi kubwa na hivyo kupelekea mabadiliko ya mahitaji mengi. Mathalani, kiwango cha data/taarifa kinachozalishwa katika dunia ni kikubwa mno. Ukichukulia mtandao wa Google pekee tuliouzoea, kila siku unazalisha takribani 20 petabytes (10PT) za data (Petabyte 1 ni sawa na Gigabyte (GB) milioni 1). Pia, sekta ya tamthilia (movie) inahama kwa kazi kutoka kutegemea video zinazouzwa kwa njia ya DVD au kaseti kuelekea kutazama tamthilia online kupitia mitandano kama Youtube na Netflix. Pia, utazamaji wa television unahamia kwenye Smart TV ambazo zinakupa uwezo wa kutazama television huku ukiwa unapata huduma nyingi kwa mtandao mithili ya matumizi ya kompyuta. Mahitaji haya ndiyo yalifanya wavumbuzi waanze kufikiria namna ya kuongeza uwezo wa kusafirisha data na kuibuka na 5G. Makampuni ya mawasiliano yanakimbilia kuwekeza katika teknolojia ya 5G kwa sababu ya faida nyingi ambazo wataje wao watapata. hata hivyo kuna changamoto kubwa mbili za 5G kimuondombinu.

  1. Teknolojia ya 5G inahitaji uwekezaji mkubwa wa miundombinu mipya ya mawasiliano kwa sababu inalazimisha kubadilisha ile iliyoko kwa sehemu kubwa. Hadi sasa kuna takribani nchi 35 (nyingi zikiwa tajiri) ambazo tayari zina miundombinu ya 5G na bado inajengwa. Ufungaji wa miundombinu hii kwa nchi nyingi umeanza mwaka 2019.

    Nchi zinazoongoza kuwa na miundombinu ya 5G kwenye miji mingi ni South Korea, China, na Marekani. Kwa miaka kama 2 iliyopita, utakua umesikia siasa za 5G kati ya mataifa makubwa hasa Marekani, Uingereza na China. Hii imetokana na ukweli kwamba kampuni ya Huawei ya wachina imekua mbele hatua kadhaa kiteknolojia na kuzifanya nchi nyingi zikiwemo za Magharibi kutumia teknolojia zake ikiwemo kuweka miundombinu ya 5G. Hii imewapa taharuki maadui zao kiuchumi hasa Marekani kwa hoja kwamba mitambo yao sio salama kwa kuwa inaratibiwa au kudukuliwa na serikali ya China (hili tuliachie hapa maana ni mjadala mwingine).


  2. Nyingine ni ukweli kwamba wateja watalazimika kuwa na vifaa vilivyotengenezwa kutumia teknoljia ya 5G, na hivyo kuingia gharama ya ziada/kubwa.
Pamoja na changamoto hizi na nyingine, bado 5G inatoa matumaini mapya ya maendeleo yatakayomwezesha binadamu kufanya shughuli nyingi ngumu kwa muda mfupi. 5G inafanikishwa mambo mawili makubwa. Moja ni kiwango cha data kinachoweza kusafirishwa, na mbili ni spidi/kasi ya data kusafiri kati ya kifaa kimoja na kingine.

Je, 5G ina madhara gani kiafya?
Nadharia njama ya 5G imejikita katika kile kinachoitwa madhara makubwa ya 5G kwa afya zetu. Kumesambaa habari nyingi duniani zilizoanzishwa na watu wachache na zimeshika kazi kama moto wa mabua kiasi kwamba zimeanza kuaminika kama ukweli. Hii imepelekea siku ya jana mtandao wa Youtube kuamu kuanza kufuta video zote kwenye mfumo wao zinazoongela nadharia njama ya G5 na uhusiano wake na Covid-19 (tazama hapa). Katika nchi za kiafrika ambapo kwa sehemu kubwa tumeturuhu watu wengine wafikirie na hata kuamua kwa niaba yetu, nadharia hii imeingizwa kwenye viunga vya kiimani na imeshakua ukweli kwa watu wengi maana huwa tunaogopa kuhoji mambo ya kiimani au wanachokisema watumishi.

Nimesikiliza na kusoma maelezo ya waanzilishi na wainjilisti wa nadharia njama ya 5G ili kuelewa msingi wa taharuki wanayoijenga. Mengi wanayoongea ni uongo, uzushi, ya kuungaunga, na hayana usahihi wowote kisayansi wala kiimani. Nadharia hii imeanzishwa na wataalamu wa nadharia njama (conspirancy theorists - wawili wakiwa ni waingereza) na kudakwa na baadhi ya watumishi “wenye majina” kama hoja ya mahubiri yao. Baadhi ya watumishi (hasa wa kikristo) hupenda kujionesha kua wao wana majibu au maelezo ya kila jambo duniani. Hivyo wamechukua hoja ya 5G na kuitumia kama ilivyo au kwa kuitohoa kujengea hoja za chanzo na malengo ya Covid-19. Nitaje kwa kifupi baadhi ya hoja zilizoko kwenye nadharia njama ya 5G.

  1. Taswira inajengwa kwamba kuna mkakati wa watu ambao wanaleta teknolojia ya 5G kwa lengo la kuitawala dunia na hasa kutufanya sisi wanadamu wote kuunganishwa kwenye mtandao mmoja ili kuweza kutaribiwa. Mkakati huu unapewa majina mengi lakini mojawapo ni mbinu ya kufanikisha kinachoitwa “New World Order (NWO)”. NWO ni nadharia njama inayodai kuna kundi la siri lenye nguvu kuliko mataifa yote litakaloitawala dunia nzima kibabe.
    UDHAIFU: wanaoaminisha nadharia hii hawataji watu hao ni kina nani, wako nchi gani, na iwapo ni wa dunia hii au sayari nyingine. Ukiachilia kutajwa kwa baadhi ya viongozi wakuu wa baadhi ya nchi na dini kubwa, nadharia hii inabaki kuwa yakufirika na imekuwepo kwa muda mrefu.


  2. Hoja inajengwa kwamba vifaa vya teknolojia ya 5G vina mionzi mikali yenye madhara kwenye miili yetu. Katika kupambana nayo, miili yetu inatengeneza virusi wa Corona.
    UDHAIFU: Moja, hakuna ushahidi wa kisayansi wowote juu ya hili. Pili, kama miili yetu inatengeneza virusi wa Corona tunapopigwa na mionzi ya 5G, kwa nini basi tusingekua tunaugua wote kwenye eneo lenye 5G? Tatu, kwa nini watu wanaoathirika wanapona?


  3. Wakati huohuo wanadai Covid-19 inasambazwa kwa watu kupitia vipimo tunavyofanyiwa kujua iwapo tuna maambukizi. Lengo kubwa la kuingiziwa virusi hivi ni ili dunia nzima iwe na maambukizi kisha kupitishwe taratibu/sheria inayomtaka kila mtu lazima apewe chanjo ya kumkinga na Covid-19. Kupitia chanjo hiyo tutaingiziwa “chip” ndogo ya mawasiliano kwenye miili yetu (mithili ya line ya simu yako) itakayowezesha watu hao wasiojulikana kutufuatilia kama vile mitambo ya kompyuta. Pia, mtu hataweza kupata visa kuingia nchi nyingine iwapo hajathibitisha kua na una kinga ya Covid-19.
    UDHAIFU: Moja, tuna ushahidi kutoka nchi nyingi watu kuambukizwa na kueonesha dalili (wengine hadi kufariki) kabla ya kupimwa. Pili, ili uweze kupachika chip ya kielekroniki ifanye kazi na kuweza kusafirisha data na mfumo wa mwili, ni lazima ipachikwe mahili maalumu na kuunganishwa na mfumo wa mawasiliano wa mwili. Wanaohubiri nadharia hii hawatuelezi ni kwa jinsi gani chanjo tutakayopewa (ama vidonge au kimiminika) itaingiza chip mwilini na ikafanye kazi.


  4. Wakristo wanatahadharishwa kwamba 5G ni mpango wa shetani na Covid-19 ni vita dhidi yao. Wengine wanakwenda mbali zaidi kudai Covid-19 imetengenezwa kwa lengo la kuangamiza waafrika ila waliotengeneza wamekosea ikawaathiri wao wenyewe.
    UDHAIFU: Hoja hii ni dhaifu kama zingine maana ni ya kufikirika.


  5. Katika kujenga hoja zao, baadhi ya manabii wa njama hii wanasema virusi sio viumbe halisia bali wanatengenezwa kwa malengo mabaya.
    UDHAIFU: Huu ni uongo ulioopitiliza kwani wanasayansi wa viorolojia wanatuambia kuna aina takribani 5,000 ya virusi wa asili duniani. Sifa kubwa ya virusi ni kutokua na uwezo wa kuishi wenyewe bila kuwa ndani au juu ya kiumbe kingine. Hivyo wanaweza kuishi kwa wanadamu, wanyama, ndege, samaki, mimea na hata viumbe vidogo kama bakteria. Hata hivyo wataalamu wa bayoteknolojia wanaweza kutengeneza virusi kwa njia za kimaabara kwa malengo mbalimbali.


  6. Wanajenga hoja kwamba kirusi cha Corona ni kipya na hajawahi kuwepo. Moja ya filamu ya kijapani iliyotengenezwa 2018 ina kipengele wanachotaja visuri wa Corona hivyo kipengele hiki kinatumika kuthibitisha kwamba Corona ni mkakati wa silaha za kibalojia.
    UDHAIFU: Hoja hii inadhirisha jinsi upotoshaji huu usivyo na mashiko. Virusi wanaosababisha Covid-19 (yaani SARS-CoV-2), ni kafamilia kamoja tu kati ya familia karibu 60 za ukoo wa Coronavirus. Wana dada yao anaitwa SARS-CoV-1 aliyesababisha mlipuko wa SARS kule China mwaka 2002/2004 lakini ukadhibitiwa. Pia wana binamu naitwa MERS-Cov aliyelipuka kule uarabuni 2012 na kudhibitiwa pia.
Uhalisia uko wapi?
Kuna uwezekano mkubwa wa teknolojia ya mawasiliano kuwa na madhara kiafya kama zilivyo teknolojia nyingi tunazotumia kila siku (magari, simu za mikononi, kompyuta, nk). Kwenye teknolojia ya mawasiliano, madhara yanahusishwa moja kwa moja na mionzi inayotumika kusafirisha data (kwa mfano simu zetu kuwasiliana na minara ya mawasiliano au na kifaa cha kupata mtandao wa intenet kwa njia ya upepo (WiFi)).

Kwa mfano, tafiti kadhaa zilizofanyika nchi kama India, Australia, Marekani, Ufaransa, nk, zimeonesha uwezekano wa madhara yatokanayo na matumizi ya simu za mikononi (sio za 5G). Ziko tafiti zimeonesha mionzi ya simu inaweza kusabanisha kansa, kuharibu mbegu za kiume, nk. Watafiti wanatoa tahadhari na kuwashauri watu kupuunguza mawasiliano ya simu za mikononi na kuzitaka kampuni zinazotengeneza simu kuwa wawazi kwa kuweka tahadhari wazi juu ya madhara mtu anayoweza kuyapata kwa kutumia simu. Wanashauri tuwazuie watoto kutumia simu na vifaa vingine vyenye WiFi ili kuzuia madhara ya mionzi ambayo imeonekana inaweza kusababisha kansa ya ubongo.

Kuna mjadala na mvutano mkubwa kati ya watafiti na watu walio kwenye sekta ya mawasiliano kuhusu ukweli wa madhara vifaa vya mawasiliano. Wanaopinga uwepo wa madhara wanasema hakuna ushahidi wa kutosha kuthibitisha yale yanayodaiwa [Hii ni mada ndefu hivyo kwa sasa niiachie hapa nirudi kwenye 5G].

Hivyo basi, kama simu ambazo tayari tunatumia zenye teknolojia ya 2G, 3G au 4G zimethibitika kwamba zinaweza kua na madhara yatokanayo na mionzi, ni wazi 5G inaweza kuwa na ina hiyohiyo ya madhara. Yanaweza yakawa ama nafuu zaidi kutokana na maendeleo ya teknolojia au makali zaidi kwa sababu hiyohiyo. Manabii wa nadharia njama ya 5G wanajenga hoja kwamba mionzi itokayo kwenye vifaa vya 5G ina nguvu isiyoweza kustahimilika na miili yetu.

Hata hivyo, lazima tutambue kwamba, wagunduzi wa mawasiliano nao ni binadamu na wanapotengeneza teknolojia mpya, wanazifanyia tafiti za kina kupima madhara yake kabla ya kuzipitisha kutumika. Pia, kila nchi (hasa zilizoendelea) zina taasisi za viwango, uratibu na udhibiti kwa lengo la kuthibitisha ubora na usalama wa mitambo ya mawasiliano kabla ya kutumika katika jamii (sisi tuna TCRA). Hakuna taifa/serikali hata moja duniani, iko tayari kufunga mitambo ya mawasiliano ambayo ina madhara kwa watu wake huku wakijua haitachagua nani wa kumdhuru.

Fursa inayotumiwa na wanaohubiri nadharia njama ya 5G
Baadhi ya manabii wa nadharia njama ya 5G ni watu wenye elimu kubwa na ufahamu mpana wa mambo. Wataalamu wengi wa nadharia njama wana akili nyingi na ni wasomi wazuri. Hivyo wanatumia nafasi hiyo kama njia ya kuonesha wanachokiongea kina ukweli. Kunahitajika uwezo mkubwa na uelewa wa mambo kung'amua yaliyo nyuma ya nadharia zao. Hata hivyo, miongoni mwao kuna wengi hawana kabisa uelewa wa teknolojia za mawasiliano na hawana uwezo wa kukuambia 5G ni kitu gani au hizo hatari zinatokeaje katika uhalisia. Ukiwasikiliza vema, wanatumia baadhi ya nadharia za mifumo ya teknolojia ya mawasiliano kwa kuungaunga kama namna ya kuonesha uhatari wa 5G. Wanataja maneno kama artificial intelligence (AI), Internet of Things (IoT) au Machine Leaning (ML) kujazia hoja zao bila kuelewa zinalenga nini hasa. Kwa mtu asiye na eleimu ya mambo haya (na hawa ni wengi kwenye jamii) akitajiwa mambo haya anapata picha inayotisha sana. Kama vile haitoshi, watu hawa hawana uelewa wa kutosha kuhusu epidemilojia ya magonjwa ya mlipuko. Ila, wanafanikiwa kwa kiasi kikubwa kupotosha kwa kua wanajua au kuamini kwamba wanaowasikiliza hawana uelewa wa mambo au elemu yao ni ndogo kuweza kung’amua ukweli au kutafuta usahihi wa wanachokisema.

Hitimisho na Ushauri
Nadharia njama ya 5G na nyingine zina hatarisha watu wengi kuambukizwa na Covid-19 kwani wanaozisambaza wanatoa maelezo yanayokanganya na kuwafanya wengi wasifuate maelekezo ya kisayansi ya ugonjwa huu na namna ya kukabiliana nao. Ndio mana utaelewa ni kwa nini juzi kule Abijan Ivory Coast wananchi wameandama na kwenda kuvunja jengo maalum linaloandaliwa kwa ajili ya kupimia wagonjwa wa Covid-19. Pia utaelewa ni kwa nini, baadhi ya “watumishi” wanahamasisha waumini wao waendelee kufanya ibada za pamoja kwa wingi zaidi wakiamini Covid-19 ni mbinu za mpinga Kristo na wanatakiwa kuamini haitawapata wao. Waliosambaza Covid-19 kwa wingi kule Korea ya Kusini walikua wakristo (walokole) waliopuuzia athari za ugonjwa huu. Waliambukizana kwa wingi na wakafanya karibu mji mzima kulemewa na maambukizi.

Kama nilivyosema kwenye moja ya makala zangu kuhusu janga la Covid-19 na kuziweka
hapa Jamii Forum, mlipuko huu umedhihirisha ni kwa kiasi gani sisi waafrika tulio wengi sio jamii inayoongozwa na elimu, maarifa, sayansi, na teknolojia. Imetuonesha namna tunavyofanya maamuzi yetu bila kutumia taarifa sahihi na tulivyo warahisi kuamini taarifa za uongo, za uzushi, na kutotaka kujishughulisha kutafuta ukweli na maarifa. Pia, imetuonesha namna mfumo wetu wa elimu usivyotuandaa na kutuwezeha kutumia uwezo wetu wa kufikiri, kufanya tafakuri tunduizi, na kuchambua mambo kwa lengo la kutafuta maarifa, ukweli au usahihi wa kile tunachosikia.

Kama vile haitoshi, mlipuko huu umetuonesha namna baadhi ya "watumishi wa dini zetu" wanavyotumia kila fursa wanayoipata kutuweka mbali na ukweli kwa makusudi na kwa manufaa yao binafsi. Hawataki tutumie akili zetu na elimu kutafuta majawabu ya maswali magumu yanatotukabili au suluhisho la changamoto tunazokutana nazo. Kila mara wanataka tutumie fikra za kiimani kama "shortcut" ambayo haitufikishi wanapotuahidi. Ifike mahali, wapendwa hawa wakubali kwamba wao sio miungu na hawana ufunuo wa kila jambo. Wao ni watumishi tu hivyo hawawezi kuwa na maelezo au majawabu ya kila swali au utata unaojitokeza kwenye jamii. Ni sahihi kabisa wakisema hawana maelezo au hawajui au bado wanamwomba wanayemtumikia kupata majawabu. Kukiri hivi hakuwapunguzii kitu katika nafasi yao ya utumishi. Pia kwa mambo ya kitaalamu/kisayansi, ni vema wakatafuta wabobezi wa eneo husika wakawapa mwanga wa kutosha wa kisayansi kabla ya kuyaongelea kwa umma katika muktadha wa kiimani. Hii ina msaada mkuwa sana na inawapa heshima hata nje ya waumini wao. Wana fursa kubwa ya kupata maelezo ya kitaalamu tena bure kutoka kwa makundi yao na hata wasio wa makundi yao.

Moja ya mambo yanayotuchelewesha waafrika kuendelea kwa kasi kama mataifa mengine tuyatazamayo kama vielelezo, ni kuhoji kila kitu kigeni kwa mtizamo wa kukiogopa au kukishuku huku tukiwa hatuna maelezo sahihi wala uthibitisho wa tunachoamini/kuaminishwa/kuwaaminisha wengine. Mbaya zaidi tunakua hatuna mbadala wa kuwapa tunaowajengea hofu. Unawaaminisha watu kuwa 5G ni hatari au ni shetani huku mfukoni una simu ya 4/5G na hotuba au mahubiri unayotoa unayarusha live kwa Youtube inayotumia teknolojia ya 5G kuweza kustahimili wingi wa watu wanayoitumia. Pia una accounts za mitandao ya kijamii ambayo kwa sehemu kubwa zinategemea teknolojia unayopambana nayo. Sasa tukuamini kwa lipi?


Zingatia
  1. Uchambuzi na maoni niliyoyatoa hapa, hayamaanishi kwamba ninaamini hakuna madhara yanayoweza kusababishwa na teknolojia ya 5G. Pia, hayamaanishi ninapinga watu kuhojia, kutafiti, au kuweka mashaka kuhusu usalama wa teknolojia hii. Hapana. Hoja yangu nya msingi ni kutofautina na upotofu unaonezwa na nadharia njama ya kuhusianisha Covid-19 na 5G. Tuhoji na kutafiti madhara ya 5G na mambo mengine (kama ni lazima) kwa kutumia ukweli na ushahidi wa kisayansi badala ya dhana za kufikirika na ndoto za abunuwasi.

    Sehemu kubwa ya Afrika tuko kwenye mkwamo kama jamii na mapokeo tuliyoletewa na waliotutawala (hasa imani) yanatuathiri kifikra na kimitazamo kuliko waliozinzisha. Hivyo tukimaliza hili la Covid-19, tuanze kuweka mikakati ya muda mrefu ya kujikwamua tulipokwama ili kurahisha maendeleo ya watu na vitu. Pamoja na bidii na imani zetu, tunahitaji elimu na maarifa sahihi ili tuweze kupiga hatua na kuleta maendeleo endelevu.


  2. Uchambuzi huu haujalenga kuwashambulia wakristo au "watumishi" kwani nami ni mmoja wao. Nimetaja ukristo (tena kwa tahadhari kubwa) maana ndio kundi nililoko na ninashuhudia jinsi baadhi yetu wanavyokazana kupotosha kuhusu Covid-19 na kinaathiri jamii kubwa.

  3. Neno "Nadharia Njama" sio rasmi katika viunga vya lugha ya Kiswahili bali nimelitohoa mimi mwenyewe baada ya kuketi na kamusi za Kiswahili nikiwa natafuta tafsiri/maana ya "Consipiracy Theory". Sifahamu tafsiri rasmi ya dhana hii kwa Kiswahili.

Mathew Togolani Mndeme (mmtogolani@gmail.com)
Mtafiti wa mifumo ya digitali kwenye ufuatiliaji na udhibiti wa magonjwa

  • Shukrani kwa classmate wangu Dr. Baraka Maiseli (Lecturer in Electronic and Telecommunications Engineering, UDSM) kwa ushauri kwenye ufafanuzi wa teknolojia ya 5G
Asante Dr.Mathew kwa taarifa yako.Ila nina angalizo kidogo.Ndio tuwasomi,na hata mimi ni msomi kama wewe,lakini ni lazima tufikiri "out of the box," not "in the box,"nikiwa na maana tufikirie nje ya vi-degree vyetu nk.nk.

Nimegundua Dr.Mathew kitu kimoja,which is pretty bad.Vi-degree hivi ni tools za kutupigia.Wametupa elimu hizi "fake," which suits their purposes,kututumia kama mouthpieces za kusambaza uongo wao which they have fed us during our school years,especially at Universities.This is aimed at making the rest of the people through us believe in their evil and deadly technologies.Techinology kama 5G,ambayo inatumia the millimetre wave spectrum ni deadly.
Tatizo ni kwamba taarifa yako yote umei
toa kwenye sources ambazo ni za hao hao wenye 5G technology,kwa hiyo hawawezi kukuambia ukweli.Believe me, zile Journals ambazo zilikuwa zinaheshimika sana zamani Kama Nature,Lancet,International Journal of Medical Sciences wameshazi-hijack,wana their fake scientists huko who they pay highly.Hawa paid fake scientists wana-publish fake papers to advance the NWO agenda.So don't believe an inch any mainstream publication straight away these days.

Nina attach taarifa mbali mbali from very independent sources ambazo hazijaghoshiwa kuhusu Covid-19,Covid-Vaccines and 5G and it's relationship to Covid-Vaccines.I repeat,ni independent sources hazijaghoshiwa kabisa,so it is authentic information.Zisome,utapata ukweli halisi.Taarifa nyingi za kwao is fake or bad science,infact mimi naziita udaku.

 
Back
Top Bottom