The Sheriff
JF-Expert Member
- Oct 10, 2019
- 617
- 1,801
Ni kipindi kirefu sasa kumekuwepo aina hii ya utapeli tulioubatiza jina la “TUMA KWA NAMBA HII”. Wapo waliofanikiwa kukwepa na wapo waliolizwa, na bado kuna wahanga watarajiwa.
Haya yanatokea hata baada ya zoezi la usajili wa laini za simu ambao uliaminisha wengi ungekuwa suluhu ya jambo hili. Miaka inapepea na bado tunalijadili.
Baadhi ya watu wanaamini kuwa utapeli huu unaratibiwa na watendaji wa makampuni ya mawasiliano na taasisi za fedha. Wengine wasema lawama zinapaswa kuvishwa kwa wahanga wenyewe kwa uzembe wao uliopitiliza, na wapo wanaonyooshea kidole Mamlaka yenye dhamana ya Mawasiliano nchini (TCRA) kwa kushindwa kudhibiti tatizo hili.
Kuna wakati TCRA ilikiri ongezeko la matapeli hawa, mara baadaye tukataarifiwa kukamatwa kwa baadhi yao. Hata hivyo, bado watu wanalizwa tu. Kila leo wanaibuka na namba mpya na kutekeleza uhalifu wao kwa kujiamini. Tena wakikushindwa wanakuporomoshea matusi kadhaa ukae nayo kwa kutulia.
TCRA nipeni maelezo ya kunishawishi hapa. Mnashindwa kuratibu zoezi la kuwakomesha wahalifu ambao mna taarifa zao? Kukamata kadhaa kwa ajili ya publicity yenu ili muonekane mnatekeleza majukumu yenu bila kukomesha tatizo, ni kutotutendea haki - ni uhuni!
Sasa, tuendelee tu kuvumilia kwa imani ya kwamba jambo hili litafikia ukomo au tutulie tu tukijua “tutaishi nao”?
Haya yanatokea hata baada ya zoezi la usajili wa laini za simu ambao uliaminisha wengi ungekuwa suluhu ya jambo hili. Miaka inapepea na bado tunalijadili.
Baadhi ya watu wanaamini kuwa utapeli huu unaratibiwa na watendaji wa makampuni ya mawasiliano na taasisi za fedha. Wengine wasema lawama zinapaswa kuvishwa kwa wahanga wenyewe kwa uzembe wao uliopitiliza, na wapo wanaonyooshea kidole Mamlaka yenye dhamana ya Mawasiliano nchini (TCRA) kwa kushindwa kudhibiti tatizo hili.
Kuna wakati TCRA ilikiri ongezeko la matapeli hawa, mara baadaye tukataarifiwa kukamatwa kwa baadhi yao. Hata hivyo, bado watu wanalizwa tu. Kila leo wanaibuka na namba mpya na kutekeleza uhalifu wao kwa kujiamini. Tena wakikushindwa wanakuporomoshea matusi kadhaa ukae nayo kwa kutulia.
TCRA nipeni maelezo ya kunishawishi hapa. Mnashindwa kuratibu zoezi la kuwakomesha wahalifu ambao mna taarifa zao? Kukamata kadhaa kwa ajili ya publicity yenu ili muonekane mnatekeleza majukumu yenu bila kukomesha tatizo, ni kutotutendea haki - ni uhuni!
Sasa, tuendelee tu kuvumilia kwa imani ya kwamba jambo hili litafikia ukomo au tutulie tu tukijua “tutaishi nao”?