macho_mdiliko
JF-Expert Member
- Mar 10, 2008
- 21,822
- 39,649
Mkuu asante sana wewe ndiyo umetoa maelezo mazuri. Nilijua tu haya malalamishi yatakuwa yamesbabishwa na short-cut tunazopenda watanzania. Hii sheria ya mteja kukuonyesha kitambulisho ni nzuri sana na ilitakiwa serikali ifuatilie kwa makini ili itekelezwe. Unaona watu hapa wanadai eti kuulizia kitambulisho na kundika jina la mteja kwenye log-book itachukuwa muda! Uvivu gani wabongo huu! Kumbe hata huu utapeli unasabishwa na mawakala kufanya short-cut ya kutouliza utambulisho wa mteja! Serikali ifanye juhudi kwenye hizi case za utapeli au muamala ukiwa na walakini wawe wawe wanawashtaki mawakala kama hawakudai kitambulisho cha mteja na ku-record details zake.Biashara ya fedha ni ngumu sana. Ugumu umekuwa mkubwa zaidi pale line zilipoanzwa kuuzwa kiholela. Kama mtoa mada ungesoma sheria na taratibu za hizi mitandao kabla ya kuwa wakala Leo usingepiga kelele. Unacholalamikia ni issue ambayo wao wamekukataza na wewe kwa ukaidi wako umefanya. Ufahamu kwamba hiyo bypass inawapunguzia circulation na profit?
Najua utaniuliza kuwa we utajuaje kwamba muamala unaenda kwa mtu mwingine? Jibu ni kwamba sisi mawakala ndio tulikiuka taratibu. Wao taratibu zao zinataka mteja akupe kitambulisho hapo ndipo pa kutambua mhusika. Zilipoanza kuzagaa line baadhi ya mawakala wakapuuza kitambulisho, waliodai wakakimbiwa, kwenda na soko kila mmoja akapuuza.
Jambo la kushauri ni kwamba mitandao ifanye mabadiliko katika suala la uwekaji pesa. Iwe kama benki kuweka umwekee mtu yeyote bila kujali uwepo wake, sheria Kali ziwe katika kutoa ni lazima muhusika awepo ili kutoa ulinzi wa wizi.
Kingine hebu fanya research, tigo kila muamala wanakuonyesha commission yake, fanya kujumlisha commission za miamala yote ya siku kisha linganisha na commission watakayo kuonyesha kesho yake, kisha upate majibu halisi.
Sent using Jamii Forums mobile app