Je, wajua Airtel waliamrishwa kurejesha Tsh 1,200,000 kwa mteja aliyetapeliwa Airtel Money?

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,011
9,879
Novemba 5, 2016, Suleiman Hiyari Mtarisi akiwa mteja wa Airtel(T) Limited alikosea kutuma fedha na aliwaomba mtandao wake warudishe fedha aliyotuma kimakosa ambayo ilikuwa ni Tsh 18,000. Mtu wa huduma kwa wateja alimuhakikishia kurejesha muamala ndani ya saa 24. Fedha hizo zilishindwa kurejeshwa ambapo alipiga simu mara kadhaa hadi Novemba 8 ambapo muamala wake ulirejeshwa.

Novemba 9, Suleimani aliokea simu kutoka kwa mtu aliyejitambulisha kuwa mfanyakazi wa Airtel na alikuwa na maelekezo ya kuingua akaunti yake. Kwa kuwa alikuwa amewasiliana na Airtel siku moja nyuma hakumtilia shaka hivyo. Baadae alibaini ameibiwa Tsh 1,200,000 kutoka kwenye akaunti yake kutoka kwenye akaunti ya Airtel.

Suleimani aliripoti polisi na Airtel kuhusu wizi huo lakini kutokana na sintofahamu akaenda Kamati ya Malalamiko ya TCRA ambapo wote walisikiliza malalamiko yake na kuiamuru Airtel irejeshe fedha hizo kwa mteja wao kwa kuwa ilionekana kama ni mtu wa ndani aliyekuwa anafahamu kuhusu Suleiman hadi kufanikisha wizi huo.

Uamuzi wa kamati umerekodiwa katika malalamiko Namba TCRA/02/11/Oktoba/2018.
 

Attachments

  • Uamuzi wa Kamati ya malalamiko ya Mamlaka Ya Mawasiliano Tanzania, Kati ya Suleiman Hiyari Mta...pdf
    3.2 MB · Views: 9
utapeli wa mtandaoni unahusisha Wafanyakazi wa mtandao husika 100%

mimi nilitaka kutapeliwa kupitia till yangu ya m pesa sasa nikajiuliza aliyenipigia simu namba kaipataje ikiwa hata ukimurushia hela mteja inaenda code ya wakala na sio namba ya laini husika ?

nilipojaribu kuwacheck voda tantalila zikawa nyingi mi nikawambia tu siku nikiibiwa kwa njia yoyote ile wajiandae kuja mahakamani kunijibu namba ya simu kwenye till ya wakala hua inapatikanaje.

mpaka leo sijawahi kuona hata sms ya tapeli kwenye hio laini.
 
Juzi nilikuwa naongea na mtu nimtumie fedha akanitumia namba pamoja na jina litakalosomeka.
Cha kushangaza jana kuna mtu kanitumia namba na jina ambapo jina mojawapo linafanana na jina la juzi akitaka nimtumie fedha kupitia jina hilo
Nilishangaa sana
 
Wafanyakazi wa mitandao wanahusika kwa zaidi ya asilimia 90 kwasababu hata ukipoteza SIM card na hukuwa na kitambulisho ukahitaji fedha iliyokuwepo kwenye SIM yako unapata ilimradi uwape posho pia ukisjili laini mpya uwakala mara nyingi unapigiwa simu kupewa maelekezo ambayo yanakuongoza kutapeliwa
 
Back
Top Bottom