TBC journalist Jerry Muro held over alleged graft

TBC journalist Jerry Muro held over alleged graft

Jamaaniiiiiiiiiiiiiiiiiii jerrrrrrrrrrryyy jeryyyyyyyyyyyy
mwacheniiii jerrrryyyy wetu

miss tanzania afumaniwa

miss tanzania 2009 miriam gerald amekumbwa na kashfa ya kufumaniwa na predeshe aliempangia huko masaki

wakiongea kwa huzuni wadau wanasema binti huyo alikuwa amepangishiwa na mzee mmoja mfanya biashara ambae wamekuwa akija na hashim lundenga wakati mwingine hapa



dada wetu tangu alipoletwa hapa hivi karibuni amekuwa akikaingiza ka kijana fulani mida ya usiku sasa nahisi huyu mzee aliweka watu wake hapa ili kumwamngalia nani anaingia,..ndipo majuzi alipowekea mtego akaingia mzee akaitwa akamakuta kijana alichofanya ni kumpa siku 2 awe ameshahamisha vitu vyake vyote ;;mzee aliona aibu kuaibika akamuaa kumwacha kijana aendeleze libeneke huku binti akilia na kijana kushangaa nini kinaendellea je ni mzazi wake kaja kumchukua la hasha kumbe ni hawara wake



pamoja na hayo binti amekuwa akipigiwa simu kuhusu utapeli wa vitu alivyoiba toka kwa muandaji wa mashindano mwanza flora lauwo .,..bibie amekuwa akimtafuta sana miriam na kusema yeye ndie aliemsaidia nguzo za miss tanzania aliposhinda akaingia mititni na simu yangu apokei akipigiwa nyingine anabadilisha namba,...mama huyo ambae amesema ameamua kuachana na swala hilo la urembo amesema huyo dada nina rb yake nasubiri muda wake akikamatwa ama nikimwona aibu lazima imkute



ameondoka south africa nikasema labda anaitaji nikamwacha amerudi amenibadilishia na simu ...mi nasema mwache mungu yupo



hizi ni taarifa mbaya kwa mh hashim lundenga,kwa kushindwa kutengeneza mazingira ya maadili na kuonekana wasichana wote ma miss ni malaya....ama kusihia kwenye kashfa chafu,...



Unajua lundenga anapaswa kulaumiwa amekuwa akiwakutanisha hawa ma miss na wafanyabiashara ambao ni wana tamaa za ngono bila kuajali umri kwamba ni watotot wao;hili ameelezwa siku nyingi na mpaka wengine kuhisi anakula hela kwa mwanamke anaepatikana



hili ni jambo la kukemewa na wana jamii nzima kwani matokeo yake ndiyo haya kufumaniwa kuwekwa kinyumba na kujiingiza katika tamaa za mali wasizoziweza uwezo wao





tukiwa kama watanzania tunalaani vitendo hivi vya wakina hashim lundenga na waandaji wote wanaotumia miss tanzania kama mchezo wa kuwatafuta wanwake wa kuwaaambukiza ukimwi na mwiso kuja kutumaliza sie watotot wadoggo ama ngast....laana hiii aitaishia hapa kama lundenga ataendelea na uchafu huu
 
My take on this controversy ni hii:-
1. Jeshi la Polisi(JLP) baada ya kuwa wameaibishwa mara kadhaa na Jerry Muro(JM) walipanga kumnyamazisha/kulipa kisasi kwa mbinu yeyote.
2. Kapama na Mgasa (matapeli sugu) wametumika na JLP kumtumbukiza Jerry katika mchezo wa kutafuta rushwa kwa Wage. Kwanini nafikiri hivi? Polisi inawataja Kapama na Mgasa kama matapeli sugu na waliona kesi nyingine ghafla baada ya JM kukamatwa na matangazo yote kwenye media zote nchini, jamaa wamekamatwa ''kirahisi'' kinondoni (JIULIZE). Polisi walikuwa wapi siku zote kukamata matapeli hawa sugu?
3.Kapama na Mgassa wamekataliwa dhamana kwa kuwa wana kesi nyingine. Hawa hawataachiwa kwani wanaweza kuropoka wakiwa uraiani.Kwa kuwa hawa ni watuhumiwa na JLP inawajua kama matapeli sugu huenda hapa kuna dili, tusaidieni kumdhalilisha JM tuwape ''ulinzi wa kipolisi'' kama vile kuacha kufuatilia kesi zenu za nyuma n.k
4.Ziko taarifa kuwa JM was on the verge of revealling a shocking corruption scandal. Nani angetajwa? Wage alikuwa nahusika? pamoja na kina nani wengine? Hawa hawawezi ku conspire na JLP (wanayo motive, JM amewaumbua), Kapama na Mgassa (wametishwa na JLP, wanataka kujinasua) Wage (pengine ni mtajwa katika kashfa aliyokuwa anifuatilia JM pamoja na kina nani) duh...ngumu...hii kesi ni ngumu.

Upande wa pili wa shillingi:
1. JM alikuwa mzoefu kweneye huu mchezo(kutisha na kujipatia rushwa)
2. Akaunda urafiki na Mgassa na kapama(matapeli sugu) pengine na baadhi ya polisi ambao wamemgeuka na kumchoma.

Maswali machache.
1. Hivi JLP wamefanya upekuzi wowote nyumbani kwa JM?Au ndio kusema wameridhika ushahidi wote wanaoutaka ulikuwa kwenye gari and that is it? Sijasikia lolote kuhusu JLP kwenda nyumbani kwa JM.
2.Kwanini JLP hawakusubiri JM akutane na WAGE ,pengine hela zitolewe ndipo wafanye arrest?
3. Kama tayari walikuwa na ushahidi wa CCTV na wanaonekana walikuwa na UHAKIKA kuwa vidhibiti vyote vilivyotajwa na mlalamikaji viko kwenye gari kwanini walimuita City Garden aje kufanya nini??????? si wangenkamata mahali popote tu barabarani, AU wangeenda tu ofisini kwake TBC kwani Wage alikuwa najua mtuhumiwa wake ni JM.
4. Hivi kwa mtu kama Wage ni kweli alikuwa hamjui JM kiasi aamini kuwa JM ni mtu wa usalama wa Taifa/mwanajeshi/PCCB kwanini asingemtaarifu tu Tido Mhando kuwa JM aamekuja kwangu na kuiita Polisi??????

Maswali ni mengi...Polisi watahitaji nguvu lubwa sana kushinda hii kesi, wasidhani RISITI YA PINGU PEKEE NDIO ITAWAPA USHINDI, baadhi ya maswali haya yatauliwzwa na DPP, mawakili, Wazee wa baraza n.k!!!!

kazi nzuri - umetupa wigo mpana wa kufikiria.
 
Haya sura mpya hadi BUNGENI kazi kwelikweli..... Tanzania Daima inaripoti


Jerry Muro sasa alipasua Bunge
• Kilango, Mdee wataka uchunguzi huru ufanyike

na Irene Mark Dar na Rahel Chizoza



SAKATA la utapeli linalomwandamana mtangazaji wa kituo cha utangazaji cha TBC1, Jerry Murro, limetua bungeni na kuwagawa wabunge.
Wakati suala hilo likitikisa Bunge mjini Dodoma, jijini Dar es Salaam limeingia katika sura mpya baada ya mtangazaji huyo kuhusishwa na mtandao wa matapeli sugu.
Muro anadaiwa kuwa pamoja na matapeli hao katika jaribio la kutaka kupokea rushwa ya sh milioni kumi kutoka kwa aliyekuwa Mhasibu wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo, Michael Karoli.
Baadhi ya wabunge waliozungumza na Tanzania Daima Jumatano jana, walisema kwa nyakati tofauti kuwa kitendo kilichofanywa na polisi dhidi ya Muro ni cha uonevu, huku wengine wakitaka sheria ichukue mkondo wake.
Mbunge wa Mufindi Kusini, Benito Malangalila (CCM), alisema suala la Muro kukamatwa kwa tuhuma za rushwa ni majungu kwani amekamatwa siku chache baada ya kuibua uovu unaofanywa na Polisi wa Kikosi cha Usalama Barabarani aliowanasa wakipokea rushwa kutoka kwa madereva wa magari makubwa.
"Katika hali ya kawaida, maelezo yanayotolewa na polisi dhidi ya Muro binafsi siyaelewi kwani wanajichanganya sana, hali inayoonyesha kwamba mashitaka ya mwanahabari huyo maarufu nchini kwa sasa yamepikwa kumkomoa," alisema.
Alisema kama ni suala la rushwa, polisi walipaswa kuwasiliana na Taasisi ya Kudhibiti na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ili waweke mtego wa kumnasa na si kama walivyofanya.
"Inauma sana kuona mtu muhimu kama Jerry anatiwa mbaroni wakati amesaidia sana umma wa Tanzania hadi kupewa Tuzo ya Mwanahabari Bora kwa kuibua mambo yaliyokuwa yakitendeka kwa kificho ndani ya Jeshi la Polisi na katika sekta nyingine. Mimi binafsi imeniumiza sana," alisema Malangalila.
Mbunge huyo alimtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Said Mwema kuwawajibisha askari waliohusika kumkamata Muro kama itabainika hana hatia ili kulisafisha jeshi hilo.
Naye Mbunge wa Viti Maalum, Halima Mdee (CHADEMA), alisema hofu imetanda kwa jamii na kwa baadhi ya wanasiasa kuwa Muro anaonewa baada ya kuibua habari za rushwa zilizosababisha baadhi ya askari polisi wa usalama barabarani kuachishwa kazi.
Alisema ili kuondoa utata huo, uchunguzi wa kina unapaswa ufanyike kujiridhisha kwamba tatizo liko wapi na kuiondolea hofu jamii ambayo kwa sasa inalia na Jeshi la Polisi kwamba imemwonea mtangazaji huyo.
Aidha, alisema polisi inapaswa kuweka wazi kama ni kinyume cha utaratibu au sheria kwa raia kukutwa na pingu kwani zinauzwa kihalali.
"Polisi waweke wazi suala hili, siyo wanasema juu juu kwamba wamemkuta na pingu au wamemkuta na bastola, hapa waseme kama ni kinyume kuwa na vitu vya aina hii kwa ajili ya kujikinga," alisema Mdee.
Kuhusu kukamatwa na polisi bila uwepo wa TAKUKURU, mbunge huyo alisema inawezekana kwani wao ni chombo cha usalama, lakini alitahadharisha kuendelea kuzungumziwa kwa jambo hilo bila kuwahusisha kwani Bunge lilikwishapitisha sheria ya kuipa nguvu taasisi hiyo.
Naye Mbunge wa Bububu, Cosmas Masolwa (CCM), alisema Muro amekamatwa katika kipindi kibaya ambacho alikuwa katika vita ya rushwa dhidi polisi na mamlaka nyingine za serikali.
Kwa ukweli huo, alisema sakata lake linaonyesha wazi kwamba polisi wanatumia vibaya madaraka yao kunyanyasa raia na kutaka hatua za haraka zichukuliwe.
Masolwa alilitaka Jeshi la Polisi kumchunguza mtu anayedai kuombwa rushwa na Muro ili kujiridhisha kama tuhuma alizozitoa ni za ukweli au amembambikizia kesi mwanahabari huyo kwa sababu anazozijua.
"Hapa inawezekana upo mchezo uliofanyika, haiwezekani mtu afichue madhambi yao leo, halafu kesho wamkamate katika mazingira yasiyoeleweka," alisema Masolwa.
Kwa upande wake, Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango Malecela (CCM), alisema suala hili liangaliwe kwa undani ili kubaini ukweli.
Alisema ni vema ufanyike uchunguzi huru ambao hautaegemea upande wowote ili haki itendeke.
"Kwa kweli binadamu hatupendani, hilo halina ubishi. Kwa suala hili nashauri liangaliwe kwa undani bila upendeleo ili haki itendeke... Katika hatua hii, sitaki kulizungumzia sana," alisema Kilango.
Aidha, wabunge wengine waliotoa maoni yao walionyesha wasiwasi na kutaka kesi hiyo ipelekwe mahakamani mapema kama ilivyo kwa kesi nyingine badala ya kuendelea kuiweka mikoni mwa polisi kwa muda mrefu.
Wakati wabunge wakitoa kauli hiyo, jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum, Suleiman Kova, amemhusisha Muro na mtandao wa matapeli sugu jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Kamanda Kova aliwataja watu aliodai kuwa ni washirika wa Muro kuwa ni pamoja na Deogratius Mgassa (35) na Edmund Kapama (52) na kuwaonyesha mbele ya wanahabari huku akisisitiza kwamba ni matapeli sugu.
Kamanda Kova alisema watuhumiwa hao waliokuwa wakisakwa na polisi kwa muda mrefu, walikamatwa jana kwenye mgahawa maarufu wa PR Camp uliopo Kinondoni jijini Dar es Salaam baada ya kuwafahamu kupitia picha za elektroniki zilizonaswa kwenye kamera za CCTV katika hoteli mbalimbali za jijini.
"Jeshi la Polisi liliendeleza upelelezi wake na kufanikiwa kuwanasa watuhumiwa hawa ambao ni matapeli sugu sana, wamewaliza watu wengi katika jiji hili. Huyu Kapama anaishi Mwananyamala na Mgassa anaishi Mbezi Beach.
"Wana kesi nyingi katika mahakama mbalimbali hapa jijini, hivyo tumewanyima dhamana na tunawashikilia hadi tutakapokamilisha upelelezi wetu hivi karibuni na kuwapeleka mahakamani.
"Hawa tumewanyima dhamana kwa sababu hawana maadili, wanaweza kutapeli hata dhamana yenyewe, sio waaminifu na tukiwafikisha mahakamani tutapeleka hati ya kiapo ili kuiomba mahakama izuie dhamana zao hadi kesi hii na nyingine zinazowakabili zitakapomalizika.
"Napenda jamii ielewe kwamba kuwanyima dhamana hawa watuhumiwa ni kwa sababu za kiusalama zaidi, hawa ni matapeli sugu sana, wamewaliza watu wengi jijini hapa akiwemo mama mmoja wa BOA bank hivi karibuni," alisisitiza Kamanda Kova.
Kuhusu Muro, mwandishi aliyejizolea sifa lukuki kwa uandishi wa habari za uchunguzi na kufichua rushwa, kamanda huyo alisema upelelezi wa shauri lake bado unaendelea kwa kasi na umakini huku sheria na taratibu zikizingatiwa.
Pamoja na hayo, Kova ambaye ni Kamishna Msaidizi wa Polisi alisema hadi jana, Muro aliyeshinda tuzo ya uandishi bora kwa mwaka 2009, ameshindwa kuwasilisha risiti ya pingu alizodai kununua kihalali, jambo linaloongeza utata katika kesi hiyo.
Kati ya Januari 28 na 31 kwa pamoja watuhumiwa hao akiwemo Muro, wanadaiwa kutumia vitisho kudai rushwa ya sh milioni 10 kutoka kwa Karoli (50) ambaye hivi karibuni alifukuzwa kazi na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
Madai ya fedha hizo yalitokana na kashfa ya ufisadi na umiliki wa majumba na hoteli za kifahari mjini Morogoro waliyomhusisha nayo na kwamba kwa maelezo ya Karoli, fedha hizo zingesaidia kuizima kashfa hiyo.
Kwa mujibu wa maelezo ya mlalamikaji huyo, watuhumiwa hao walijitambulisha kama maofisa wa TAKUKURU wenye vyeo tofauti. Inadaiwa kwamba mmoja wao walijitambulisha kuwa Kaimu Mkurugenzi wa TAKUKURU Dar es Salaam, mwingine alisema ni ofisa wa kawaida kutoka taasisi hiyo nyeti na wa mwisho alijitambulisha kama mwanajeshi wa nyota tatu na ofisa wa TAKUKURU kitengo cha habari. Aidha, sakata hilo linalovuta hisia za watu wengi linatarajiwa kufikishwa mahakamani hivi karibuni sheria ichukue mkondo wake.
 
Jerry Muro alikuwa anamuinvestgate huyo mahasibu aliefukuzwa ndo chanzo, Mhasibu mwenyewe amekula sana na mapolisi hawa thats why they are helping him out, picha etc zilikuwa za kuja kuanika hadharani ufisadi wa huyu mhasibu, ndo maana Pinda alimfyatua!
 
Maggid, you are dam right. "Seek the truth, and the truth will set you free".............................................................................................................. Kwa upande wa Jerry. Jerry bado anao muda to come clean, I doubt if he'll save his job, ila Watanzania, tutamwelewa, jamii itamwelewa, yeye kama binadamu, atakuwa huru and life will go on........................................................................................Kamanda Kova, kashajiaibisha, kachafuka, naye ni vizuri akitulia asizidi kujipaka .....Kitendo cha kuwaparedi watuhumiwa mbele ya waandishi na kusema ni matapeli, ndio tayari ameshawahukumu, hakuna kesi pale................................................................Pamoja na Kamanda Kova kupenda sana kuuza sura kwenye luninga, this time, sura kauza lakini pia nguo kavuliwa, hivyo anaonekana ... wa mnyama, kichani ni hamna kitu, empty kabisa!.
 
SAKATA LA MURO: KESI YA PANYA KAPEWA PAKA.
SAKATA la madai ya kuomba Rushwa ya shilingi Mil.10 linalomkabili mwandishi wa shirika la Habari la TBC, Jerry Muro linahitaji uchanganuzi wa Kina, na fikra yakinifu zitakazokidhi haja za watanzania wanaofuatilia swala hili, na kuondoa utata unaoonekana wazi.

Suala la Muro limejaa utata na halieleweki wazi si tu kwa wananchi wanafuatilia, bali hata yeye nadhani hajui kunachoendelea.

Utata huu unatokana na mambo makuu mawili. Kwanza ni mazingira ya kukamatwa kwa hicho kinachodaiwa “Rushwa” na pili ni wahusikakatika Kesi yake.

Mazingira ya Kesi tangu kukamatwa kwake hadi kufikishwa kituoni yanaibua maswali mengi kwa kila mwenye fikra hai. Murro alikamatwa Jumapili ya tarehe 31/01/2009 akiwa katika gari lake aina ya Cresta GX100 lenye namba za usajili T 545 BEH na kufikishwa katika kituo kikuu cha Polisi Mkoa wa Dar; kwa madai ya kuomba rushwa ya Sh. Million 10 kutoka kwa aliyekuwa Mhasibu wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo. Bw. Michael Wage.

Bw. Wage anadai kwamba aliombwa rushwa hiyo na Muro siku mbili kabla ya kukamatwa, walipokutana na Muro katika Hotel moja jijini Dar. Hivyo Muro alipofikishwa kituoni hapo alitakiwa kutoa maelezo kuhusu tukio la siku mbili zilizopita.

Haingii akilini mtu kuomba rushwa leo halafu eti akamatwe siku mbili baadae; Lazima Umma uelezwe kwanini hakukamatwa siku hiyo hiyo alipoomba rushwa? Au labda makachero wote wa Polisi walikuwa wameenda likizo hivyo ilibidi kusubiri hadi siku mbili baadaye watakaporudi kutoka huko walikokuwa wameenda kula “good time”.

Lakini pia ni kwanini Bw. Wage hakuripoti Sakata hilo TAKUKURU ambao kisheria ndio wanaoshughulikia rushwa? Angeenda TAKUKURU angepewa noti zilizojizolea umaarufu kama “Pesa za moto” ambazo zingetumika kama ushahidi mzuri wa kumtia Murro hatiani. Je, Wage hafamu kuwa TAKUKURU ndio wenye dhamana ya madai yote yanayohusu rushwa? Kama anafahamu hilo, alienda Polisi kufanya nini?

Kwanini alikimbilia Polisi badala ya TAKUKURU? Huko polisi alikuwa anamfuata nani? Lazima swali hili lijibiwe kwa ufasaha na uyakinifu.

Lakini cha kuchekesha ni kwamba alikamatwa bila ushahidi wowote uliohusu Rushwa. Si “noti za moto” za TAKUKURU wala sarafu za Polisi alizokutwa nazo Murro.

Badala yake Polisi waliibua madai ya kukutwa na pingu ambayo hayana uhusiano wowote na kesi ya msingi ya Rushwa.

Lakini hili la pingu nalo linahitaji mjadala mpana. Mjadala huu ni kutokana na mazingira ya kukutwa kwa Pingu hizo. Gazeti la Nipashe la Jumatatu February 1/2010 liliripoti kuwa Murro alipofikishwa Kituoni hapo alipelekwa sehemu ya juu (Ghorofani) ya kituo kwa ajili ya mahojiano. Wakati Murro akiwa kwenye mahojiano gari lake lilikuwa likilindwa na askari kanzu.

Kwa mujibu wa taarifa za Polisi, siku hiyo alipoombwa rushwa Wage alidai kuona Pingu ndani ya gari la Muro. Hivyo Muro alipokamatwa gari yake ikalazimika kupekuliwa. Lakini funguo zikapotea katika mazingira yaliyojaa utata hapohapo kituoni. Hivyo Muro kulazimika kupiga simu nyumbani kuomba funguo za akiba.

Lakini kabla funguo za akiba hazijafika, zile zilizopotea zilipatikana na pingu hizo kukutwa ndani ya gari la Jerry; Je, nani alikuwa na funguo hizo?? Je, nikisema kwamba kuna askari alipoka fungua hizo na kwenda kuweka Pingu kwenye gari la Muro nitakuwa nimekosea?? Au nikisema wale makachero walioachwa kulinda gari wakati Muro akiwa kwenye mahojiano walitumia mbinu zao za “Kimafya” kutumbukiza Pingu katika gari la Muro nitakuwa navunja kifungu gani cha Sheria??

Lakini Wage, (mhasibu aliyesimamishwa kazi na waziri Mkuu kutokana na shutuma za ubadhirifu) akaibua hoja nyingine mufilisi. Eti alipokuwa kwenye gari ya Muro (wakati Muro akimuomba rushwa) alisahau miwani yake ambayo baada ya upekuzi ilikutwa kiti cha mbele wakati wa upekuzi.

Binafsi sidhani kama kukutwa kwa miwani kinahusika na sakata la msingi la Rushwa. Bali kwa kutumia ushahidi wa miwani kwa mbaaali kunaweza kutusadikisha (japo si sana) kuwa Wage alipanda gari ya Muro. Lakini je, kila anayepanda gari ya Muro anaombwa rushwa? Kama kila anayepanda gari ya Muro huombwa rushwa basi madai ya Wage yatakuwa na msingi; vinginevyo hizo ni fikra kurupushi tu.

Katika gari ya Muro kulikutwa vitu kadhaa, vikiwemo vifaa vyake vya kazi. Lakini pia ilikutwa miwani, boksi mbili za tissue na pingu za mkononi.
Viwili kati ya hivyo yaani miwani pamoja na tissue, Wge alidai ni mali zake na alizisahau aliposhuka. Kama amekiri kumiliki miwani na tissue na kwamba alivisahau aliposhuka, basi yawezekana hata hizo pingu yeye ndiye mmiliki wake na alizisahau tu, kama alivyosahau hivyo vingine. Kama aliweza kusahau miwani (anayoitumia kila siku), kwanini tushindwe kuamini kuwa hata hizo pigu alizisahau??.

Baada ya kuona namna MAZINGIRA ya Kesi yalivyojaa utata hebu tuangalie WAHUSIKA katika Kesi hii.

Michael Wage ambaye ndiye mlalamikaji mkuu katika Kesi hii ni “mhanga” katika “bomoabomoa” iliyofanywa na waziri mkuu mhe.Mizengo Pinda ambapo watendaji wa juu wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo walisimamishwa kazi.

Lakini ikumbukwe kuwa hadi waziri mkuu kufikia hatua ya kuwasimamisha watendaji hao kazi inadaiwa Murro ndiye aliyefichua ufisadi uliokuwa umeighubika Halmashauri hiyo. Kwa tafsiri hiyo Muro ndiye “aliyewachomea utambi” watendaji hao, na kwa maana hiyo wana hasira nae. Hivyo nikisema Kesi hii ni ya kupikwa sidhani kama kimantiki itapingika.

Lakini hata jeshi la Polisi nao si marafiki sana wa Muro maana nao walishajeruhiwa na makucha yake.

Akiwa ITV Muro aliwahi kufichua rushwa iliyotolewa kwa trafiki katika maeneo ya barabara ya Dar – Moro. Habari hiyo ilirushwa na kituo cha televition cha ITV kupitia kipindi cha Ripoti maalum haikufurahiwa sana na Polisi maana Askari polisi 13 walisimamishwa kazi kwa tuhuma hizo za rushwa. Lakini pia hivi majuzi Murro alishiriki kuandaa kipindi cha Usiku wa Habari kilichorushwa na TBC -1 ambapo askari wa Usalama barabarani Mkoa wa Iringa walionekana wakipokea Rushwa.

Hili nalo liliongeza idadi ya maadui wa Muro na labda pia liliibua mbinu za namna ya kumzima. Ndio! Hatakiwi kuendelea kuumbua wakubwa kwa kile anachokiita “Habari za Uchunguzi”. Nani ana uhakika wa kupona kama akiachiwa aendelee kufichua? Yeah! Lazima azimwe maana fichua fichua yawezekana akafichua pasipofichulika.

Lakini jumatatu tarehe 1/February/2010 Kamanda wa Polisi wa kanda maalumu ya Dar es Salaam; Selemani Kova aliongea na waandishi wa habari kuelezea tukio la kukamatwa kwa Muro. Pamoja na kuongea sana (kama kawaida yake) alinukuliwa na vyombo vya habari akisema “…..hapa namsaidia Wage kusema; maana haya alipaswa kuyasema yeye”.

Kauli hii inaibua utata kwa kila mwenye akili timamu. Wage ni nani hadi aajiri Jeshi la Polisi kumsemea? Kwa lipi hasa? Na kwa ujira wa shilingi ngapi?

Baadhi ya watu wenye fikra finyu walimsifu RPC Kova kutoa tamko bila kujua kuwa Kova alikuwa anajishtaki mwenyewe. Kwa kukiri kwamba anasema kwa niaba ya Wage; ina maana kuwa Wage ndiye aliyemtuma aseme. Swali. Tangu lini Kamanda Kova amefanyika kuwa Afisa habari/msemaji wa Wage??

Napotafakari kauli ya Kova (Kwamba alimsaidia Wage Kusema) naanza kupata majibu kwanini Wage hakwenda TAKUKURU na badala yake akakimbilia Polisi.

Kutokana na kauli hii uhusiano baina ya Kova na Michael Wage unapaswa uchunguzwe ili tujue msimamo wa RPC wetu. Ikiwezekana achague moja kama ataendelea kuwa RPC au ataacha kazi yake ya upolisi abakie na hiyo mpya ya kuwa Afisa habari wa Wage.

Kwa ujumla mlalamikaji katika Kesi hii Michael Wage pamoja na wanaoendesha kesi hii Jeshi la Polisi wamewahi kuwa “majeruhi” wa Muro kwa nyakati tofauti. Halafu eti leo ndio wanaongoza upande wa mashtaka katika Kesi ya yuleyule “mbaya wao”. Halafu tunategemea haki itendeke. Thubutu!! Hicho ni kichekesho. Tusishangae kuona Muro akipokwa HAKI yake waziwazi maana Kesi ya Panya kapelekewa Paka. Ni uzandiki.

Niachie ujumbe:
0715-187677
 
naona sasa mambo ya muro yamezidi...!
 
Inaonyesha wewe ni mwandishi mzuri wa habari umejitahidi kuunganisha Dot.
Kikubwa Kova amechemsha kwa hili ameshindwa kufanya kazi yake anacho fanya ni kuokoteza ushahidi inabidi tuhoji IGP anatumia vigezo gani kupanga hawa makamanda wa Mikoa kweli Kova kachemka hana budi kukaa kimyaa.
 
naona sasa mambo ya muro yamezidi...!

seriously.......mpaka haina maana tena!!!!!!!!!!!!!!! naanzisha yangu nataka kujua ni mchaga wa wapi na mimi
 
Mmhhhhhhhhhhhhh😱😱😱...Bora nisiseme tu maana nikisema nitatukana I think.....
 
naona sasa mambo ya muro yamezidi...!

Asante malisa kuturushia hii nyeti nyenye michanganuo mingi mingi, umeichambua vilivyo, wengi wetu uwezo wa kutafakari ni mdogo sana na ndiyo maana we just need this details kutusaidia.

let us wait and see what next........
 
Hivi huyu Wage alisema alitishiwa nyumbani kwake Bagamoyo 28/1/2010 sasa iweje aje aripoti Dar? Je! huko kwao hakuna vituo vya polisi?

2. Tangu tarehe 28/01/2010 vituo vya polisi vilikuwa wapi ama alikuwa hajui pahala pa kwenda hadi asafiri toka mkowa wa PWANI kuja Mkoa wa DAR ES SALAAM.

hapa mimi naona kama katuni za tom & jerry
 
For a country passing through transinsition period with big vacuum in leadership like ours people like Jerry Muro(represents Journalist who search for facts and put into light irregularities ) are highly not needed by "Leaders", i won't be surprised if this at the end turns to be "cooked" skandal. but also we should leave a room for doubt as Jerry might also use information he has in a wrong way
 
Jana usiku niliangalia vipande vyote vilivyorekodiwa vye maelezo ya Jerry Muro na yale ya Kamanda Kova. Kwa kuangalia lugha ya mwili, nilimwonea huruma sana Jerry Muro. Yuko katika wakati mgumu, maana, katika yote mazuri aliyoifanyia jamii, kwa sasa yuko katika mtihani mgumu . Swa ni kwa namna gani ataibakisha imani na heshima ya jamii kwake?

Niandikayo hapa hayamhusu Kamanda Kova na Jerry Muro tu, huenda yana manufaa kwa jamii pana. Katika ulimwengu huu kuna waliotembea katika nchi nyingi. Na hufika wakati ukamsikia binadamu mwenzako akitamka kwa kujisifu: “ Mimi nimezunguka karibu dunia nzima!”. Asichokijua binadamu huyo ni ukweli kuwa huko kote alikokwenda ni kipande kidogo sana cha dunia hii. Ukiunganisha sehemu zote alizokanyaga mguu wake na kujionea kwa macho yake yaweza kuwa sawa na kipande ambacho Baba Gile wa kijijini Kalenga , Iringa amekanyaga na kujionea kwa macho yake. Naye atakwambia ametembea kwa miguu au kusafiri kwa baiskeli kwenda vijiji vya mbali sana na Kalenga anakoishi.

Ndivyo maisha yalivyo. Hapa duniani tunayoyajua ni machache sana kuliko tusiyoyajua. Kila mtu ana kipande chake anachokijua. Tukiunganishanganisha vipande hivi, vinakua, tunapata maarifa zaidi. La Jerry Muro limegeuka. Sasa lLinahusianishwa na tuhuma za utapeli, ni tuhuma nzito, ni kashfa. Jana niliandika juu ya kiu ya kutaka kufahamu ukweli. Ukweli mzima.

Na siku zote, ukweli udhihiri, huwa ni suala la wakati tu. Ukweli hauhitaji shahidi, husimama wenyewe. Mapinduzi ya teknolojia nayo yamepelekea wanajamii wengi kufuatilia yanayofanyika Dar na kwengineko. Pale kijijini Kalenga, katika kila wanakijiji kumi, wanne wana simu za mkononi. Katika kila kaya kumi, moja ina televisheni. Kasi hii ya mapinduzi ya upatikanaji wa taarifa inaendelea.

Vivyo hivyo, na hamu pia ya wanajamii kuutafuta na kuupata ukweli imeongezeka. Na maishani, jambo baya linalokuhusu wewe, liseme mwenyewe. Mfano, una mkeo nyumbani. Kazini unatembea na Katibu wako Muhtasi. Kuna siku mfanyakazi mwenzako atamwambia ukweli mkeo juu ya mahusiano yako na Katibu wako. Mkeo atakuweka kikaangoni na ushahidi. Utakiri kosa, utaomba msamaha. Nafasi ya mkeo kukusamehe ni 20/80. Ndio, una nafasi ya asilimia 20 tu ya kusamehewa.

Kinyume chake, kama ungeenda mwenyewe ukamwambia mkeo juu ya dhambi uliyofanya, dhambi ya kuisaliti ndoa yenu. Kisha ukamwomba radhi akusamehe kwa kutoka nje ya reli, nafasi ya mkeo kukusamehe ni 80/20. Ndio, una nafasi ya asilimia 80 ya mkeo kukusamehe.

Macho ya wanajamii yanaliangalia na kulifuatilia kwa karibu sakata hili la Jerry Muro na Jeshi la Polisi. Jerry Muro hapa anawakilisha pia tasnia ya habari na mawasiliano. Kwa wanajamii inahusu imani yao kwa Jeshi la Polisi na Wanahabari. Ikumbukwe, huu ni mwaka wa uchaguzi. Polisi na Wanahabari wana mchango mkubwa katika kufanikisha mchakato huo. Vyombo hivyo viwili havipaswi kugubikwa na wingu kubwa la mashaka. Ya wanajamii juu ya utendaji wao na hususan suala zima la maadili.

Kama sakata zima ni kazi ya ‘ kisanii’ inayofanywa na baadhi ndani ya jeshi la polisi, basi, busara hapa si kusubiri mahakama. Ni kwa polisi kuikabili jamii na kusema ukweli mzima, kukiri mapungufu, maana sote ni binadamu. Polisi iwaombe radhi Jerry Muro na wanajamii. Nafasi ya kusamehewa na kubakisha imani ya jamii kwa jeshi hilo ni 80/20. Ni kubwa. Na kwa Jerry Muro, hivyo hivyo. Ukweli wa jambo zima anaujua, na jamii itakuja kufahamu. Kama amehusika kwa namna moja au nyingine na tuhuma hizi za utapeli, basi, aikabili jamii. Akiri mapungufu, naye ni binadamu. Aliombe radhi jeshi la polisi na wanajamii. Na saa ya kufanya hivyo ni hii.

Maggid

Iringa, Februari, 3, 2010.

Blah blah nyiiingi!!!!!!!!!!!! Hivi Watanzania jamani mbona maneno yetu yanakuwa mareeeeeeefu na yasiyokuwa na mantiki yeyote? Anyway najua waandishi wengi wa habari hawataki kukubali ukweli kuwa: UANDISHI WA HABARI NI MOJA YA TAASISI ZINAZOONGOZA KWA KULA RUSHWA HAPA TANZANIA. Ni ajabu na... rushwa akila polisi mbaya lakini akichukuwa mwandishi mhhh sio kitu. Tuwe serious kama tunataka kuondoa rushwa. Huyu dogo hana pa kutokea hata mkimtetea namna gani. Alitaka kufanya utapeli na wacha sheria ichukue mkondo wake. Msilete longolongo zenu nyie waandishi wala rushwa.... (Samahani sana kwa wale waandishi wachache ambao ni wasafi)
 
For a country passing through transinsition period with big vacuum in leadership like ours people like Jerry Muro(represents Journalist who search for facts and put into light irregularities ) are highly not needed by "Leaders", i won't be surprised if this at the end turns to be "cooked" skandal. but also we should leave a room for doubt as Jerry might also use information he has in a wrong way

mimi nafikiri watu bado wana matatizo kwenye interpretations, yaani tayari RPC amefanya interprete kuwa Muro hana kesi though, make just look mpaka RPC anasema jamaa alikosea kusema, ngoja nimsemee what is that, hii ipo kweli???? just by lil understanding mtu uankuja na interprets kuwa there's no case behind. Huyo Wage anatafuta njia ya kutoka na uzandiki wake, make mfa maji haachi kutapatapa, the guy srewed himself, wala sijui kama anaweza hata kwenda mahakamani, make wakisema lete ushahidi atapeleka miwani, halafu huyo RPC naye ana akili kabisa, ataendesha vipi kesi ambayo haina hata ushahidi, it is non-sense, the whole stuff is out of ascenses.
 
Back
Top Bottom