My take on this controversy ni hii:-
1. Jeshi la Polisi(JLP) baada ya kuwa wameaibishwa mara kadhaa na Jerry Muro(JM) walipanga kumnyamazisha/kulipa kisasi kwa mbinu yeyote.
2. Kapama na Mgasa (matapeli sugu) wametumika na JLP kumtumbukiza Jerry katika mchezo wa kutafuta rushwa kwa Wage. Kwanini nafikiri hivi? Polisi inawataja Kapama na Mgasa kama matapeli sugu na waliona kesi nyingine ghafla baada ya JM kukamatwa na matangazo yote kwenye media zote nchini, jamaa wamekamatwa ''kirahisi'' kinondoni (JIULIZE). Polisi walikuwa wapi siku zote kukamata matapeli hawa sugu?
3.Kapama na Mgassa wamekataliwa dhamana kwa kuwa wana kesi nyingine. Hawa hawataachiwa kwani wanaweza kuropoka wakiwa uraiani.Kwa kuwa hawa ni watuhumiwa na JLP inawajua kama matapeli sugu huenda hapa kuna dili, tusaidieni kumdhalilisha JM tuwape ''ulinzi wa kipolisi'' kama vile kuacha kufuatilia kesi zenu za nyuma n.k
4.Ziko taarifa kuwa JM was on the verge of revealling a shocking corruption scandal. Nani angetajwa? Wage alikuwa nahusika? pamoja na kina nani wengine? Hawa hawawezi ku conspire na JLP (wanayo motive, JM amewaumbua), Kapama na Mgassa (wametishwa na JLP, wanataka kujinasua) Wage (pengine ni mtajwa katika kashfa aliyokuwa anifuatilia JM pamoja na kina nani) duh...ngumu...hii kesi ni ngumu.
Upande wa pili wa shillingi:
1. JM alikuwa mzoefu kweneye huu mchezo(kutisha na kujipatia rushwa)
2. Akaunda urafiki na Mgassa na kapama(matapeli sugu) pengine na baadhi ya polisi ambao wamemgeuka na kumchoma.
Maswali machache.
1. Hivi JLP wamefanya upekuzi wowote nyumbani kwa JM?Au ndio kusema wameridhika ushahidi wote wanaoutaka ulikuwa kwenye gari and that is it? Sijasikia lolote kuhusu JLP kwenda nyumbani kwa JM.
2.Kwanini JLP hawakusubiri JM akutane na WAGE ,pengine hela zitolewe ndipo wafanye arrest?
3. Kama tayari walikuwa na ushahidi wa CCTV na wanaonekana walikuwa na UHAKIKA kuwa vidhibiti vyote vilivyotajwa na mlalamikaji viko kwenye gari kwanini walimuita City Garden aje kufanya nini??????? si wangenkamata mahali popote tu barabarani, AU wangeenda tu ofisini kwake TBC kwani Wage alikuwa najua mtuhumiwa wake ni JM.
4. Hivi kwa mtu kama Wage ni kweli alikuwa hamjui JM kiasi aamini kuwa JM ni mtu wa usalama wa Taifa/mwanajeshi/PCCB kwanini asingemtaarifu tu Tido Mhando kuwa JM aamekuja kwangu na kuiita Polisi??????
Maswali ni mengi...Polisi watahitaji nguvu lubwa sana kushinda hii kesi, wasidhani RISITI YA PINGU PEKEE NDIO ITAWAPA USHINDI, baadhi ya maswali haya yatauliwzwa na DPP, mawakili, Wazee wa baraza n.k!!!!