TBC journalist Jerry Muro held over alleged graft

TBC journalist Jerry Muro held over alleged graft

Jerry Muro anaonekana kabisa hana nidhamu...mdomo wake mkubwa utamponza atapoteza puclic support aliyonayo. Kwa nini asimwachie wakili wake awe anongea kwa niaba yake badala kuongea hovyo kila kukicha. Nenda Kapambane na Kova mahakamani sio humo kwenye Tv utafikiri unagombea Ubunge.
 
mmh, kova anangoja risiti ya pingu! sijui yeye mwenyewe kama anazo risiti
ya kila kitu anachokimiliki.

sitashangaa nikisikia "baada ya uchunguzi makini polisi wamegundua kwamba bastola amilikayo jerry muro ilipata husika na tukio la kijambazi siku za nyuma".

japokuwa jerry muro anasema "kova ni mtu mdogo sana" aelewe kwamba kama
kweli amehusika na rushwa jamaa watamnasa na watamshughulikia upasavyo.

hata hivyo yawezekana naye kova ndio kaanzisha mpambano na waandishi na
wao watamchimba mpaka wapate uchafu wake.

kwangu mimi nasubiri sheria ifuate mkondo wake.
 
Asante Kaitaba kwa analizo, nimerekebisha hilo neno, Pili asante to First Lady kwa maelezo yako fasaha (wenyewe wanasema Short and clear)
 
Jerry kawaletea risiti ya pingu na sasa sinema imeingia part 2. Tunakumbuka Kova alisema ana uhakika Jerry hawezi leta ushahidi huo sijui sasa atakuja na ngonjera gani.
 
Jerry kawaletea risiti ya pingu na sasa sinema imeingia part 2. Tunakumbuka Kova alisema ana uhakika Jerry hawezi leta ushahidi huo sijui sasa atakuja na ngonjera gani.

Lakini naye Jerry hizo pingu ni za nini kwani yeye ni police ????
 
kwani kazi ya pingu ni nini?

kazi ya pingu ni kufunga waharifu Mwanakijiji mie sio afande siwezi kukutana na wewe na kukufunga pingu ..hatuko kwenye mada za ndoa leo😉
Mie siwezi kumiliki pingu nazifanyia nini? kwani mie afande ? na hata kama ninanzo sina ruhusa ya kumfunga mhalifu hivo basi sioni umuhimu wa kuwa nazo ..je yeye alikuwa anazifanyia nini hizo pingu?
 
Muro aongeza utata
• Awasilisha risiti za pingu alizokamatwa nazo

na Martin Malera


amka2.gif
SAKATA la mwandishi wa habari za uchunguzi, Jerry Muro, limeingia katika hatua mpya baada ya kubainika kuwa ana risiti za pingu ambazo polisi walimkamata nazo.
Umiliki huo wa pingu unaongeza utata katika sakata zima linalomhusisha na utapeli, ingawa linajibu swali la Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova aliyetilia shaka zilikotoka pingu hizo.
Juzi alikaririwa akimtaka Muro awapelekee polisi risiti, akisema si rahisi kupata pingu kwa kuwa "haziuzwi hovyo kama njugu."
Kamanda Kova alisema ni marufuku kwa raia kumiliki pingu, na kwamba kupatikana nazo ni kosa la jinai.
Alisisitiza kuwa pingu ni mali ya polisi, magereza na jeshi; hivyo mtu wa kawaida kukutwa nazo ni kosa la jinai. Na alidai kwamba Muro asingeweza kupata risiti.
"Pamoja na kumwambia atuletee risiti, tunajua hatafanikiwa kuzipata kwa kuwa pingu haziuzwi ovyo kwani mwenye mamlaka ya kumuweka nguvuni mtu ni polisi pekee," alisema Kamanda Kova.
Hata hivyo, jana Muro alilithibitishia Tanzania Daima kwamba anamiliki kihalali pingu na bastola aina ya CZ 97B namba A6466 iliyotengenezwa nchini Czechoslovakia.
Risiti hiyo inaonyesha Muro alinunua pingu hizo Mei 20 (mwaka umefutikafutika) katika duka la silaha la Mzinga Corporation lililoko Upanga, jijini Dar es Salaam, akapewa risiti namba 34357310.
Kwa mujibu wa risiti hiyo iliyoandikwa jina kamili la Muro, pingu hizo zilinunuliwa kwa sh 25,000.
Tanzania Daima ilipowasiliana na duka hilo la silaha, mmoja wa wafanyakazi wake ambaye hakutaka kutaja jina, alikataa kuzungumzia risiti hiyo kwa madai kuwa si msemaji.
Mfanyakazi huyo alilitaka Tanzania Daima kuwasiliana na Meneja Mkuu wa Mzinga Corporation, lakini hakupatikana. Ilidaiwa kuwa alikuwa nje ya ofisi.
Muro anayekabiliwa na tuhuma za kudai rushwa kwa vitisho pamoja na kukutwa na pingu isivyo halali, amekuwa gumzo tangu kuanza kwa sakata hili kutokana na utata wa taarifa zinazomhusu, hasa zinolewazo na polisi.
Mwanahabari huyo ambaye yuko nje kwa dhamana, anakabiliwa na tuhuma za kukusudia kutaka kuomba rushwa na kujifanya ofisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (Takukuru).
Juzi, Kamanda Kova alimwingiza Muro katika mtandao wa matapeli sugu.
Kwa mujibu wa Kova, Muro na matapeli wengine wawili, wanadaiwa kushirikiana katika mpango wa kuomba rushwa ya sh milioni 10 kutoka kwa aliyekuwa Mhasibu wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo, Michael Karoli Wage kati ya Januari 28 na 31 mwaka huu.
Watuhumiwa hao ni pamoja na Deogratius Mgassa (35) na Edmund Kapama (52).
Walimhusisha Wage na kashfa ya ufisadi na umiliki wa majumba na hoteli za kifahari mjini Morogoro, wakataka awape pesa ili "wasimlipue".
Kwa mujibu wa maelezo ya mlalamikaji huyo, watuhumiwa hao walijitambulisha kama maofisa wa Takukuru, wenye vyeo tofauti.
Inadaiwa kwamba mmoja wao alijitambulisha kuwa ni Kaimu Mkurugenzi wa Takukuru Dar es Salaam, mwingine akajifanya ofisa wa kawaida kutoka taasisi hiyo, wa tatu alijitambulisha kama mwanajeshi wa nyota tatu na ofisa wa Takukuru Kitengo cha Habari.
Muro alikamatwa mwishoni mwa wiki, majira ya saa 5 asubuhi katika Hoteli ya City Garden katikati ya Jiji la Dar es Salaam baada kuwekewa mtego na Jeshi la Polisi.
Tayari Baraza la Habari Tanzania (MCT) limetoa taarifa kuelezea kusikitishwa kwake na tukio hilo na kulitaka Jeshi la Polisi kuharakisha uchunguzi, kutomnyanyasa na kuhakikisha haki inatendeka ili umma ujue kilichomtokea mshindi huyo wa tuzo ya uandishi bora wa mwaka 2009, katika uchunguzi wa habari za rushwa.
Umma umegawanyika kuhusu sakata la Muro, huku baadhi ya wananchi, wakiwamo wabunge, wakionyesha kumtetea kwa madai kuwa amebambikiwa tuhuma hizo kwa sababu ya kazi zake za kufichua rushwa ya polisi wa usalama barabarani.


Source Tanzania Daima, Feb 4, 2010
 
Imeandikwa wapi, au kifungu gani cha sheria kinasema kuwa na pingu lazima uwe polisi?? wengine wanatumia ktk mapenzi na kadhalika....kuwa na pingu sio issue hapa, msiseme namtetea Jerry, ni ukweli tu.
Polisi wanaleta longolongo bwana, suala la msingi hasa lilikuwa rushwa. Sasa wanatupoteza uelekeo tufikirie suala la pingu badala ya suala la msingi ambalo wanaona wamechemsha.
 
Kazi yake sio tofauti na kufuli, na wengi tunamiliki makufuli.
Mh! Labda kufuli la baiskeli. Hili la Muro kumiliki pingu linaongeza hisia za utapeli. Polisi wangeenda kumpekua nyumbani kwake mengi yangeibuka!
 
.......only in Tanzania.....! badala ya kukomaa na huyo Michael Wage ambaye katimuliwa kwa ubadhilifu, na inajulikana kabisa ana investments za ajabu Morogoro, abanwe aseme aliraise vipi hiyo capital.....polisi wetu wanadeal na kuokoteza ushahidi wa ktiu walichoshindwa kukisuka........!
 
Jamani, hapa tuache kuzungumzia ushabiki!
Lets ask ourselves, hata kama kumiliki pingu si kosa, mwandishi wa habari, pingu inamsaidia nini katika shughuli zake za kila siku?. Nafikiri hili ni swali la msingi zaidi. Na yeye Jerry aulizwe alitarajia kutumia pingu katika mazingira ya aina gani kwenye michakato yake ya kupata habari.

Huu umiliki halali wa pingu wa bwana muro unatufanya tuliangalie hili suala kwa pande zote mbili bila kutoa maelezo au maona ya kiushabiki zaidi. Katika mazingira kama haya, ni uchunguzi ulio huru tu ndio utakaoweza kufichua ukweli wa hili suala zima.
 
Lile sakata la Jerry Muro, limetinga rasmi bungeni asubuhi hii kwenye kipindi cha maswali na majibu ya papo kwa papo.

Sakata hilo limeshushwa bungeni na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Mh. Hamad Rashid Mohamed, Mbunge wa Wawi (Pemba), alimuuliza Waziri Mkuu, katika nchi nyingi, waandishi wa habari wanaokuwa mstari wa mbele kufichuo vitendo viovu dhidi ya dola, dola huwa inawashukia, kama polisi wanavyomshukia Jerry Muro, baada ya kufichua rushwa yaTraffic?

Pinda alijibu, Jerry Muro ni binadamu kama binadamu wengine, hivyo anaweza kufanya makosa, na polisi nao vile vile ni binadamu, hivyo alisema anasikitika jinsi suala hili linavyoshupaliwa kwa kutumia vyombo vya habari, amesema polisi wanatumia vibaya vyombo vya habari, na Jerry nae anatumia vyombo vya habari kuendeleza malumbano.

Pinda amesema anashauri polisi kutimiza wajibu wake kwa kutumia zile zile standard procedures sio kutumia media.Rashid Mohamad akauliza swali la nyongeza, kwa kumtaka Pinda kuingilia mchakato ili kuharakisha na haki, itendeke. Pinda akajibu, hana sababu ya kuingilia uchunguzi wa kipolisi, japo kuna public interest lakini hebu kwanza viachiwe vyombo husika.
 
Lile sakata la Jerry Muro, limetinga rasmi bungeni asubuhi hii kwenye kipindi cha maswali na majibu ya papo kwa papo.more update coming.
LOL!hatari kweli
 
Jamani, hapa tuache kuzungumzia ushabiki!
Lets ask ourselves, hata kama kumiliki pingu si kosa, mwandishi wa habari, pingu inamsaidia nini katika shughuli zake za kila siku?. Nafikiri hili ni swali la msingi zaidi. Na yeye Jerry aulizwe alitarajia kutumia pingu katika mazingira ya aina gani kwenye michakato yake ya kupata habari.

Huu umiliki halali wa pingu wa bwana muro unatufanya tuliangalie hili suala kwa pande zote mbili bila kutoa maelezo au maona ya kiushabiki zaidi. Katika mazingira kama haya, ni uchunguzi ulio huru tu ndio utakaoweza kufichua ukweli wa hili suala zima.

Analysti- sina la zaidi.
 
Back
Top Bottom