Jana usiku niliangalia vipande vyote vilivyorekodiwa vye maelezo ya Jerry Muro na yale ya Kamanda Kova. Kwa kuangalia lugha ya mwili, nilimwonea huruma sana Jerry Muro. Yuko katika wakati mgumu, maana, katika yote mazuri aliyoifanyia jamii, kwa sasa yuko katika mtihani mgumu . Swa ni kwa namna gani ataibakisha imani na heshima ya jamii kwake?
Niandikayo hapa hayamhusu Kamanda Kova na Jerry Muro tu, huenda yana manufaa kwa jamii pana. Katika ulimwengu huu kuna waliotembea katika nchi nyingi. Na hufika wakati ukamsikia binadamu mwenzako akitamka kwa kujisifu: " Mimi nimezunguka karibu dunia nzima!". Asichokijua binadamu huyo ni ukweli kuwa huko kote alikokwenda ni kipande kidogo sana cha dunia hii. Ukiunganisha sehemu zote alizokanyaga mguu wake na kujionea kwa macho yake yaweza kuwa sawa na kipande ambacho Baba Gile wa kijijini Kalenga , Iringa amekanyaga na kujionea kwa macho yake. Naye atakwambia ametembea kwa miguu au kusafiri kwa baiskeli kwenda vijiji vya mbali sana na Kalenga anakoishi.
Ndivyo maisha yalivyo. Hapa duniani tunayoyajua ni machache sana kuliko tusiyoyajua. Kila mtu ana kipande chake anachokijua. Tukiunganishanganisha vipande hivi, vinakua, tunapata maarifa zaidi. La Jerry Muro limegeuka. Sasa lLinahusianishwa na tuhuma za utapeli, ni tuhuma nzito, ni kashfa. Jana niliandika juu ya kiu ya kutaka kufahamu ukweli. Ukweli mzima.
Na siku zote, ukweli udhihiri, huwa ni suala la wakati tu. Ukweli hauhitaji shahidi, husimama wenyewe. Mapinduzi ya teknolojia nayo yamepelekea wanajamii wengi kufuatilia yanayofanyika Dar na kwengineko. Pale kijijini Kalenga, katika kila wanakijiji kumi, wanne wana simu za mkononi. Katika kila kaya kumi, moja ina televisheni. Kasi hii ya mapinduzi ya upatikanaji wa taarifa inaendelea.
Vivyo hivyo, na hamu pia ya wanajamii kuutafuta na kuupata ukweli imeongezeka. Na maishani, jambo baya linalokuhusu wewe, liseme mwenyewe. Mfano, una mkeo nyumbani. Kazini unatembea na Katibu wako Muhtasi. Kuna siku mfanyakazi mwenzako atamwambia ukweli mkeo juu ya mahusiano yako na Katibu wako. Mkeo atakuweka kikaangoni na ushahidi. Utakiri kosa, utaomba msamaha. Nafasi ya mkeo kukusamehe ni 20/80. Ndio, una nafasi ya asilimia 20 tu ya kusamehewa.
Kinyume chake, kama ungeenda mwenyewe ukamwambia mkeo juu ya dhambi uliyofanya, dhambi ya kuisaliti ndoa yenu. Kisha ukamwomba radhi akusamehe kwa kutoka nje ya reli, nafasi ya mkeo kukusamehe ni 80/20. Ndio, una nafasi ya asilimia 80 ya mkeo kukusamehe.
Macho ya wanajamii yanaliangalia na kulifuatilia kwa karibu sakata hili la Jerry Muro na Jeshi la Polisi. Jerry Muro hapa anawakilisha pia tasnia ya habari na mawasiliano. Kwa wanajamii inahusu imani yao kwa Jeshi la Polisi na Wanahabari. Ikumbukwe, huu ni mwaka wa uchaguzi. Polisi na Wanahabari wana mchango mkubwa katika kufanikisha mchakato huo. Vyombo hivyo viwili havipaswi kugubikwa na wingu kubwa la mashaka. Ya wanajamii juu ya utendaji wao na hususan suala zima la maadili.
Kama sakata zima ni kazi ya ' kisanii' inayofanywa na baadhi ndani ya jeshi la polisi, basi, busara hapa si kusubiri mahakama. Ni kwa polisi kuikabili jamii na kusema ukweli mzima, kukiri mapungufu, maana sote ni binadamu. Polisi iwaombe radhi Jerry Muro na wanajamii. Nafasi ya kusamehewa na kubakisha imani ya jamii kwa jeshi hilo ni 80/20. Ni kubwa. Na kwa Jerry Muro, hivyo hivyo. Ukweli wa jambo zima anaujua, na jamii itakuja kufahamu. Kama amehusika kwa namna moja au nyingine na tuhuma hizi za utapeli, basi, aikabili jamii. Akiri mapungufu, naye ni binadamu. Aliombe radhi jeshi la polisi na wanajamii. Na saa ya kufanya hivyo ni hii.
Maggid
Iringa, Februari, 3, 2010.
Niandikayo hapa hayamhusu Kamanda Kova na Jerry Muro tu, huenda yana manufaa kwa jamii pana. Katika ulimwengu huu kuna waliotembea katika nchi nyingi. Na hufika wakati ukamsikia binadamu mwenzako akitamka kwa kujisifu: " Mimi nimezunguka karibu dunia nzima!". Asichokijua binadamu huyo ni ukweli kuwa huko kote alikokwenda ni kipande kidogo sana cha dunia hii. Ukiunganisha sehemu zote alizokanyaga mguu wake na kujionea kwa macho yake yaweza kuwa sawa na kipande ambacho Baba Gile wa kijijini Kalenga , Iringa amekanyaga na kujionea kwa macho yake. Naye atakwambia ametembea kwa miguu au kusafiri kwa baiskeli kwenda vijiji vya mbali sana na Kalenga anakoishi.
Ndivyo maisha yalivyo. Hapa duniani tunayoyajua ni machache sana kuliko tusiyoyajua. Kila mtu ana kipande chake anachokijua. Tukiunganishanganisha vipande hivi, vinakua, tunapata maarifa zaidi. La Jerry Muro limegeuka. Sasa lLinahusianishwa na tuhuma za utapeli, ni tuhuma nzito, ni kashfa. Jana niliandika juu ya kiu ya kutaka kufahamu ukweli. Ukweli mzima.
Na siku zote, ukweli udhihiri, huwa ni suala la wakati tu. Ukweli hauhitaji shahidi, husimama wenyewe. Mapinduzi ya teknolojia nayo yamepelekea wanajamii wengi kufuatilia yanayofanyika Dar na kwengineko. Pale kijijini Kalenga, katika kila wanakijiji kumi, wanne wana simu za mkononi. Katika kila kaya kumi, moja ina televisheni. Kasi hii ya mapinduzi ya upatikanaji wa taarifa inaendelea.
Vivyo hivyo, na hamu pia ya wanajamii kuutafuta na kuupata ukweli imeongezeka. Na maishani, jambo baya linalokuhusu wewe, liseme mwenyewe. Mfano, una mkeo nyumbani. Kazini unatembea na Katibu wako Muhtasi. Kuna siku mfanyakazi mwenzako atamwambia ukweli mkeo juu ya mahusiano yako na Katibu wako. Mkeo atakuweka kikaangoni na ushahidi. Utakiri kosa, utaomba msamaha. Nafasi ya mkeo kukusamehe ni 20/80. Ndio, una nafasi ya asilimia 20 tu ya kusamehewa.
Kinyume chake, kama ungeenda mwenyewe ukamwambia mkeo juu ya dhambi uliyofanya, dhambi ya kuisaliti ndoa yenu. Kisha ukamwomba radhi akusamehe kwa kutoka nje ya reli, nafasi ya mkeo kukusamehe ni 80/20. Ndio, una nafasi ya asilimia 80 ya mkeo kukusamehe.
Macho ya wanajamii yanaliangalia na kulifuatilia kwa karibu sakata hili la Jerry Muro na Jeshi la Polisi. Jerry Muro hapa anawakilisha pia tasnia ya habari na mawasiliano. Kwa wanajamii inahusu imani yao kwa Jeshi la Polisi na Wanahabari. Ikumbukwe, huu ni mwaka wa uchaguzi. Polisi na Wanahabari wana mchango mkubwa katika kufanikisha mchakato huo. Vyombo hivyo viwili havipaswi kugubikwa na wingu kubwa la mashaka. Ya wanajamii juu ya utendaji wao na hususan suala zima la maadili.
Kama sakata zima ni kazi ya ' kisanii' inayofanywa na baadhi ndani ya jeshi la polisi, basi, busara hapa si kusubiri mahakama. Ni kwa polisi kuikabili jamii na kusema ukweli mzima, kukiri mapungufu, maana sote ni binadamu. Polisi iwaombe radhi Jerry Muro na wanajamii. Nafasi ya kusamehewa na kubakisha imani ya jamii kwa jeshi hilo ni 80/20. Ni kubwa. Na kwa Jerry Muro, hivyo hivyo. Ukweli wa jambo zima anaujua, na jamii itakuja kufahamu. Kama amehusika kwa namna moja au nyingine na tuhuma hizi za utapeli, basi, aikabili jamii. Akiri mapungufu, naye ni binadamu. Aliombe radhi jeshi la polisi na wanajamii. Na saa ya kufanya hivyo ni hii.
Maggid
Iringa, Februari, 3, 2010.