Tatizo la kukatika katika umeme kuikosesha kura CCM

Tatizo la kukatika katika umeme kuikosesha kura CCM

"Tanzania ya Magufuli itakuwa ni Tanzania ya viwanda". !!?? Hivi viwanda vitaendeshwa na nishati gani?!!? Umeme hakuna. Na mkurugenzi wa Tanesco ni story-teller mwingine, alituambia mabomba ya gesi yaliyozindliwa TWO WEEKS AGO ni ufumbuzi. Wapi (!!) Mpaka leo mgawo upo palepale, tena ndio mkali zaidi. Zilikuwa hekaya za Abu-Nuwas!
 
Achilia jumapili,sasa hivi wanakata hata saa kumi na moja alfajiri muda tunaojiandaa kutoka kwenda makazini na unarudi saa moja usiku,sasa hata hivyo vitu kwenye mafriji vitapona kweli?Na wale ndugu zetu waliojiajiri wa welding,matofali wanapata shida sana.Inawabidi wakeshe wakifanya kazi,ila tutaambiwa baada ya gesi kuwa kuanza kutumika sasa miundo mbinu imekuwa ya zamani ni chakavu hivyo tunashughulikia hilo,na likiisha hilo utaambiwa kifaa cha kutolea gesi kibovu,kwani hawakosi sababu.
 
Kuongoza hii nchi ni kitu kirahisi sana cha msingi uwe mtu wa mboyoyo tuu basi.
 
CCM:Tuchagueni tena umeme itakuwa wa uhakika,tena utakuwa bure kabisa.
Watanzania tujipime
 
CCM:Tuchagueni tena umeme itakuwa wa uhakika,tena utakuwa bure kabisa.
Watanzania tujipime

Mkuu, kwa hali ya watanzania wengi walivyopofushwa akili za na Ccm, kweli wanaweza kuwachagua tena. Watanzania wengi hawajitambui, mwenge umewapumbaza; ni wakuwaombea.
 
Ndugu zangu wote mliojiandikisha kupiga kura na mnaotegemea umeme katika maisha yenu ya kila siku, NAWAOMBA SANA tuinyime CCM kura zetu kwa sababu ni walaghai kwa kutudanganya kila siku kuhusiana na upatikanaji wa umeme. Hapa Mwanza umeme unazimwa saa 11.30 za asubuhi mpaka saa mbili za usiku. TUIKATAE CCM sababu siyo wakweli.
 
Tatizo la watanzania wanasumbuliwa na ushabiki bila pasipokujali hali halisi inayolikumba taifa

hivi kwa mateso wananchi waliosababishiwa na ccm
hakuna sababu kabisa ya kuichagua ccm mwaka huu wapumzishwe kwanza ili wapate adabu ya kuheshimu wananchi
 
Inasikitisha sana siku Magufuli ukisikia anafanya Kampeni Dar umeme haukatwi. Ila Lowassa akifanya
bas fitna, CCM mnashinikiza kukata umeme ili watu wasiate nafasi ya kusikiza Sara. Tambueni
kuwa watu wamechoka na kwa uonevu huu kwa pamoja mtatoka..!!! Inshallla!!!!
 
Inakatisha tamaa sanaa aisee.!! Nakuwa sielewi tofauti ya Chama na CCM na Serikali. Mpaka tunafikia hapa wakati Tanesco ni serikali na haitakiwi kupendelea au kukomesha upande mwingine.
 
Kwa hali ilivyo ni aibu kubwa kwa ccm, haiwezekani kuanzia mwezi wa sita nchi iko kwenye mgao wa umeme wakutisha alafu bado waziri na viongozi wa tanesko kwao ni business as ussual.

Umeme umeathiri uchumi kwa taifa hili kwa kiwango kikubwa sana kuna viwanda vimepunguza wafanyakazi mpaka hivi sasa, na ajira za watu zimepotea kwa uzembe huu.

CCM msahau kupata kura za watanzania, napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa rais Kikwete kwa kufanikisha zoezi hili kwa jitihada zake kubwa alizotumia kuhakikisha taifa halina umeme na kushindwa kuwachukulia hatua za haraka wahusika huku viwanda vikiendelea kupunguza wafanyakazi na hizi ndio zile dalili ambazo Mungu anatukumbusha watanzania ili tujuwe CCM hawafadhiliki kura tulizowapa na bado wanaendelea kutudanganya ebu fikirini.

Umeme wakuwasha matumizi tu yakawaida haupo huo anaoongelea Magufuli wa viwanda utatoka wapi?

CCM mmelikoroga na sasa October 25/2015 lazima mtalinywa.

Asanteni
 
Kila kitu kimeharibika kwa kukosa umeme. siku zisogee tu haraka tumuingize Rais wetu Lowassa Madarakani
 
Halafu wanazidi kudanganya kwenye Kampeni kuwa serikali ya Maguli itakuwa ya viwanda! Kwa umeme upi? Miaka 10 iliyopita JK alipoingia madarakani tatizo la kwanza alilokutana nalo ni mgao wa umeme! Anaondoka kukiwa na mgao wa umeme ikiwa ishara kuwa Ari mpya, Kasi mpya na Nguvu mpya ilikuwa kama moshi tu! Geresha tupu. Sina sababu ya kuamini ahadi yoyote ya CCM! Hapakuwa na maisha bora kwa kila Mtanzania badala yake ni kinyume chake!
 
Huu ndio mwisho wa waongo. Jitihada zetu tulio elimika na kutambua wakati wa kuiondoa ccm ni huu tunapaswa kujitahidi kuwashawishi watu wasio na uelewa juu ya mambo haya na namna ccm alivyo kiungo cha shetwani. Nawaomba tupige simu kwa ndg na jamaa vijijini au kuwatembelea tukawashawishi umhimu wa kuiondoa ccm na tukifahamisha namna inavyotuumiza na kukwamisha maendeleo yetu huku mijini na yao huko vijijini.
 
UKAWA mtawapata wapumbavu na malofa wenzenu. Wenye akili wanajua nini kinaendelea
 
Back
Top Bottom