Tatizo la kukatika katika umeme kuikosesha kura CCM

Tatizo la kukatika katika umeme kuikosesha kura CCM

kuna rafiki yangu anafanya kazi tanesco wakati tunapata kilaji nilimuuliza sababu za kukata umeme wakati mwingine zaidi ya masaa 36 wakati ijumaa ya wiki iliyopita mlitamba kuwa mmewasha mitambo mingi na sasa hakutakuwa na kukatikakatika kwa umeme tena lakini hali ndo imekuwa mbaya kuliko, si afadhari watujulishe kama kuna mgao tujipange .majibu yake yalikuwa kama ifuatavyo:-
" mgao wa umeme hakuna ila tumechoka kabisa na serikali ya ccm kwani shirika letu ndilo limekuwa kichwa cha mwendawazimu . We jaribu kuona kashifa zote kubwakubwa utazikuta tanesco, kuanzia iptl, richmond, escrow n.k., pia kuna kashfa ndogondoga zinazohusu ununuzi wa mafuta mazito , nguzo, ununuzi wa misumari badala ya spea n.k. Tuna muda sasa hatujaongezwa mishahara ukilinganisha na baadhi ya wakala wa serikali tukiomba nyongeza tunaambiwa shirika linajiendesha kwa hasara, tumeona adui yetu ni ccm hivyo tunakata makusudi hasa kipindi hiki cha kampein ili kuwachonganisha ccm na wapiga kura ili wasiichague oktoba 25" . Je hii inaweza kuwa kweli au kuna tatizo jingine la kiufundi.
endelea kupiga posho za ukawa lakn hapa hatudanganyiki ng'oooo hapa ni kazi tu
 
Huo ni uongo. Kwa issue ya shirika kujiendesha kihasara ni kweli waweza ingia hata google na ufungue TANESCO utakuta habari kibao mojawapo ikiwa ni hasara ya zaidi ya Tsh 460 Bilioni.
Kuhusu kukata umeme kwasababu za kisiasa ni uongo kwakuwa TANESCO ipo chini ya Wizara ya Nishati na Madini. Kumbuka CCM ndio inayounda serikali.
Hapa kwa taarifa yako tu na wengine pia ni kwamba siasa haiwezi kuingilia technical issues hata kama watalazimika wanasiasa kuweka siasa kwenye masuala ya ufundi nchi inaweza kaa gizani kwa muda mrefu.

Duh umejibu utadhani huishi Tanzania!
 
Huo ni uongo. Kwa issue ya shirika kujiendesha kihasara ni kweli waweza ingia hata google na ufungue TANESCO utakuta habari kibao mojawapo ikiwa ni hasara ya zaidi ya Tsh 460 Bilioni.
Kuhusu kukata umeme kwasababu za kisiasa ni uongo kwakuwa TANESCO ipo chini ya Wizara ya Nishati na Madini. Kumbuka CCM ndio inayounda serikali.
Hapa kwa taarifa yako tu na wengine pia ni kwamba siasa haiwezi kuingilia technical issues hata kama watalazimika wanasiasa kuweka siasa kwenye masuala ya ufundi nchi inaweza kaa gizani kwa muda mrefu.
Mkuu labda hujanipata vizuri hii inaonekana ni internal sabotage dhidi ya CCM ili ishindwe uchaguzi.
 
Mkuu labda hujanipata vizuri hii inaonekana ni internal sabotage dhidi ya CCM ili ishindwe uchaguzi.

Unafikiri wizarani hakuna wataalam. Wapo sana na wanariport kwa wakubwa. Issue ni kwamba Demand na supply haviendani.. ndio maana nakwambia technical issues ni vigumu kuweka politics.
 
Unafikiri wizarani hakuna wataalam. Wapo sana na wanariport kwa wakubwa. Issue ni kwamba Demand na supply haviendani.. ndio maana nakwambia technical issues ni vigumu kuweka politics.
Mimi sijakubishia mkuu lakini kwa nini TANESCO wanakwepa kutangaza mgao na awali walitangaza tatizo litaisha tarehe 14/9 baadae tarehe 19 wakatangaza kwa mbwembwe mbeke ya waziri wa nishati kuwa sasa hakutakuwa na upungufu wa umeme tena lakini ndo tatizo limekuwa worse.
 
Mgao wa umeme pamoja sehemu kubwa ya inchi kutokufikiwa na miundombinu ya umeme ni sababu moja tosha ya kuivurumisha CCM ipotee kabisa katika ya macho ya watanzania.

CCM wana sema hapa kazi tu, je kazi bila umeme itatoka wapi??? Watanzania tuwache walaghai ccm na maneno ya mengi ambayo ni ya kilaghai. Sasa hivi wanatuomba kura kwa heshima na nidhamu iliyotukuka. Wakipata tunarudi katika manyanyaso yao kama kawaida.

Tusiogope mabadiliko, sehemu zote walizo fanya mabadiliko wamepata majibu chanya.
 
Mgao huu wa Umeme usioisha bila hata taarifa yoyote,tuliambiwa kuwa ni siku 7 tu lakini cha ajabu mpaka Leo mgao unaendelea, tuliambiwa ni kwa sababu mitambo ya gesi lakini mgao unaendlea! Yaani ni karaha mwanzo mwisho!

Prof. Muhongo alitudanganya kuwa ndani ya mwaka moja Mgao wa umeme utakua historia lakini mpaka leo ni kilio.HIVI WANAOMBA KURA ZA NINI HAWA?
 
Kama unakereka Na kukatika Kwa Umeme, suluhisho ni tar. 25 October 2015, kapige kura Na kuikataa ccm, bila hivyo tutalalamika miaka nenda rudi, usipofanya hivyo ccm hawana majibu ya kumaliza tatizo la Umeme , rejea ahadi walizotoa hakuna ahadi iliyoleta suluhisho ya tatizo la Umeme, huku kwetu tumefunga ofisi tunamsubiri tar25. Tukaikatae ccm, tumalize tatizo la Umeme.
 
Ccm ya kikwete imewachinja watanzania kwa umeme na hapana shaka umeme unawachinja ccm Mwaka huu.ccm out ni lazima 2015
 
Walitutangazia kuwa ni katizo LA umeme sasa limegeuka kuwa tatizo la umeme,wamewahi kusema kuwa taitizo la umeme litakuwa historia sasa limekuwa janga la taifa
 
oct 25 tusifanye makosa, tuhakikishe tunamwondoa huyu mkolono wa kijani
 
jamani hili tatizo linanikera sana sana,cha kushangaza zaidi wanasema ni mitambo inafungwa ,hiyo mitambo inafungwa mpaka jumapili?ukawa mko wapi mfanye uchunguzi tujue tatizo ni nini.yaani mtu anaye ishabikia ccm anashida kwenye akili yake.tunateseka sana na umeme
 
Mgao huu wa Umeme usioisha bila hata taarifa yoyote,tuliambiwa kuwa ni siku 7 tu lakini cha ajabu mpaka Leo mgao unaendelea, tuliambiwa ni kwa sababu mitambo ya gesi lakini mgao unaendlea! Yaani ni karaha mwanzo mwisho!

Prof. Muhongo alitudanganya kuwa ndani ya mwaka moja Mgao wa umeme utakua historia lakini mpaka leo ni kilio.HIVI WANAOMBA KURA ZA NINI HAWA?
wenzio wamestuka kuwa serikali ya UKAWA hakutakuwa na mgao na vijiji vyote vitapelekewa umeme sasa majenereta yao watamuuzia nani?
 
Back
Top Bottom