Ulukolokwitanga
JF-Expert Member
- Sep 18, 2010
- 8,397
- 7,979
Mko Dodoma mnajadili namna ya kuendelea kutawala badala ya kujadili namna ya kutatua kero za wananchi. Muda mrefu sasa mgao wa umeme unaendelea na hapa ninavyoandika hii kitu umeme umekatika na ulikatika jana, juzi na wiki yote hii na mwezi wote huu umeme umekuwa ukikatika kwa vipindi tofauti, either siku nzima au masaa. Pia toka mwaka umeanza umeme unakatika na Ni miaka 53 sasa ya Uhuru umeme unakatika.
Nimefuatilia katika hotuna ya mwenezi Nape Nnauye sijasikia neno UMEME likitamkwa. Rasimu ya katiba haionyeshi kama kupata umeme ni haki za msingi za mtanzania na mnataka tuipigie kura za ndiyo, je kwa miaka 50 ijayo umeme utaendelea kuwa sio haki yetu ya msingi? Mh Rais anazunguka dunia kutafuta wawekezaji, je watawekeza nini bila kuwa na umeme wa uhakika? Ajira zitapatikana wapi wakati kila siku giza na viwanda havifanyi kazi muda wote.
Je CCM ina maslahi gani na mgao wa umeme?
Nimefuatilia katika hotuna ya mwenezi Nape Nnauye sijasikia neno UMEME likitamkwa. Rasimu ya katiba haionyeshi kama kupata umeme ni haki za msingi za mtanzania na mnataka tuipigie kura za ndiyo, je kwa miaka 50 ijayo umeme utaendelea kuwa sio haki yetu ya msingi? Mh Rais anazunguka dunia kutafuta wawekezaji, je watawekeza nini bila kuwa na umeme wa uhakika? Ajira zitapatikana wapi wakati kila siku giza na viwanda havifanyi kazi muda wote.
Je CCM ina maslahi gani na mgao wa umeme?