Tatizo la kuchanganya mafuta

teac kapex

JF-Expert Member
Jan 23, 2011
470
136
Habari za leo wadau wa jukwaa hili, leo kwa bahati mbaya nimechanganya mafuta, nina gari aina ya hiace ambayo inatumia Petroli, nimekwenda kituo cha mafuta muuzaji bila kuuliza akashindilia diesel kama lita 4 hivi na ndani ya tank kulikuwa kama na lita 7 za petroli nilipoondoka tu umbali usiozidi mita 50 gari ikaanza kuwa na miss na kwa kweli imenigharimu sana maana nimelazimika kutumia mafuta mengi kwa umbali mfupi, na hadi sasa miss ni kubwa sana, sasa naomba ushauri wenu nifanye nini kuiondoa? Nb kumbuka kwa nimejitahidi kuongeza mafuta mengine kama ya sh 40,000 lakini hakuna mafanikio. MSAADA TAFADHALI
 
Hiyo hiace ina engine gani? Next time bandika sticker ya petrol kwenye kifuniko cha mafuta , huwa inasaidia kumkumbusha pump attendant..
 
Badala ya kumwaga hayo mafuta ww unaongezea mengine...akili za wapi hizi!
Ukiendelea kukaza fuvu utaua plug zote!
 
Habari za leo wadau wa jukwaa hili, leo kwa bahati mbaya nimechanganya mafuta, nina gari aina ya hiace ambayo inatumia Petroli, nimekwenda kituo cha mafuta muuzaji bila kuuliza akashindilia diesel kama lita 4 hivi na ndani ya tank kulikuwa kama na lita 7 za petroli nilipoondoka tu umbali usiozidi mita 50 gari ikaanza kuwa na miss na kwa kweli imenigharimu sana maana nimelazimika kutumia mafuta mengi kwa umbali mfupi, na hadi sasa miss ni kubwa sana, sasa naomba ushauri wenu nifanye nini kuiondoa? Nb kumbuka kwa nimejitahidi kuongeza mafuta mengine kama ya sh 40,000 lakini hakuna mafanikio. MSAADA TAFADHALI
Yaani ukaona dawa ni kuongeza mengine???

Baada ya kuongeza ndo unakuja kuuliza????

Pole sana
 
Endeleakuendesha mpaka yaishe, afu weka mengine miss itaisha.
 
Kama ina Engine ya 2Y,3Y hiyo haina shida itakata miss taratibu na kuwa sawa, ila kama ni 1TR au 2TR mwaga mafuta kwenye Tank usafishe au peleka gereji mapema hizo ni mayai ya kisasa angalau 2RZ ikipata mafuta machafu inahimili
 
Back
Top Bottom