Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,809
- 218,463
Baada ya kufanya Tathmini kabambe huku D'Salaam na Mkoani Mbeya , kwa kweli tumegundua kwamba Sherehe za Christmas ni kama hazipo kabisa kutokana na dhiki kuu iliyosababisha Ugumu mkubwa wa Maisha ambao Wazee wengi wanadai haujawahi kuwepo kwenye nchi tangu wapate akili.
Mishahara duni ya Wafanyakazi, pamoja na kuanguka kwa uchumi kulikosabisha pia kuanguka kwa biashara kumewafanya watu wengi kula Matembele na Sembe au Dagaa mchele na Ugali wa dona. Bei ya Nyama na Mchele hazishikiki ambako kilo 1 ya nyama imefikia hadi elfu 12 huku mchele wa kuridhisha ukifikia hadi tsh 3500 kwa kilo moja.
Hata kwenye vinywaji nako ni balaa , Pombe pekee iliyong"ara kwenye mauzo inajulikana kama "Kisungura" sifahamu hasa inaitwaje , ila ni kijipombe kilicho kwenye vichupa vidogo vya plastic , mwanzoni kipombe hiki walikuwa wanakunywa vijana makapuku , lakini kwa sasa hata maofisa wanakunywa kutokana na ugumu wa maisha , hakuna Mtanzania anayeitwa Mnyonge anayeweza kununua bia angalau 5 tu , hii ni balaa !
Sababu kubwa ya mambo haya imetajwa kuwa ni Kushindwa kwa serikali ya Tanzania kuinua Uchumi wa nchi na hata uchumi wa mtu mmojammoja, dhiki inayowakabili wananchi wa Tanzania kwa sasa imezidi hata ya enzi zile za kuvaa viraka kwenye makalio na kama hali itaendelea kubaki hivi kuna hatari Watanzania kuanza kula mizizi.