TANZIA: Mtambuzi Apata Msiba

TANZIA: Mtambuzi Apata Msiba

pole sana mtambuzi! mungu awape faraja katika kipindi hiki.
 
Mkuu Pasco nimekupata shemeji.

Kwa wale ambao wangependa kuuungana na familia ya mzee Mtambuzi katika msiba huu kwa njia ya rambirambi, tafadhali tumieni namba zifuatazo; Tigo-Pesa 0715 729292 na M-Pesa 0752 729292.
Mkuu Mwita Maranya, asante nimekupata, namuandalia pole yake na kuahidi pia nitaheshimu name calling maana ukutuma tuu jina linakuja!.

Ila huu ushemeji ni wa upande upi?, maana sisi kanda ya Ziwa huwa tuna misururu!, na utajiri wa madada sii haba!, familia zenye watoto wachache ni zile za watoto 8!.
Pasco
 
Mkuu Pasco nimekupata shemeji.

Kwa wale ambao wangependa kuuungana na familia ya mzee Mtambuzi katika msiba huu kwa njia ya rambirambi, tafadhali tumieni namba zifuatazo; Tigo-Pesa 0715 729292 na M-Pesa 0752 729292.
hizi namba ni kwa ajili ya kutuma pesa tu?
kama unataka kumpigia na kumpa pole pia inaruhusiwa?
 
poleni sana wafiwa ... Mtambuzi Mwenyezi Mungu wape faraja na nguvu katika kipindi kigumu cha msiba.....Raha ya milele umpe eehh bwana na mwanga wa milele umwangazie apumzike kwa amani Amina
 
Last edited by a moderator:
hizi namba ni kwa ajili ya kutuma pesa tu?
kama unataka kumpigia na kumpa pole pia inaruhusiwa?

Hahaha FP mbona unanichekesha msibabi!?
Rambirambi si lazima iwe fedha taslimu, hata kumpigia simu na kumpa maneno mazuri ya faraja na kumpa moyo ni rambirambi tosha.

NB: hairuhusiwi na haikubaliki ku-''deep''!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mwita Maranya, asante nimekupata, namuandalia pole yake na kuahidi pia nitaheshimu name calling maana ukutuma tuu jina linakuja!.

Ila huu ushemeji ni wa upande upi?, maana sisi kanda ya Ziwa huwa tuna misururu!, na utajiri wa madada sii haba!, familia zenye watoto wachache ni zile za watoto 8!.
Pasco

Mkuu shemeji Pasco wala huna sababu ya kuutilia shaka ushemeji wetu.

Mke wangu, Mama Rhobi ni msukuma mzaliwa wa Bukoli Geita, tena nilifanikiwa kumg'oa huko kwa mbinde sana, siunajua tena wazee wa Bukoli walikuwa wana wasiwasi na kipigo kwa binti yao! Lakini after some years wamekuja kubaini kwamba binti yao amependeza na ana furaha zaidi ya alivyokuwa nyumbani kwao.

Btw, turudi msibani kwanza haya yetu tutayatafutia mahali pake muafaka.
 
Last edited by a moderator:
Pole Sana Mtambuzi Kwa Kufiwa Na Mama Mkwe! msiba huu ni wetu sote maana ww ni baba,kaka,mshauri,mfariji na mwalimu wa maisha yetu humu JF!
 
Hahaha FP mbona unanichekesha msibabi!?
Rambirambi si lazima iwe fedha taslimu, hata kumpigia simu na kumpa maneno mazuri ya faraja na kumpa moyo ni rambirambi tosha.

NB: hairuhusiwi na haikubaliki ku-''deep''!
hapo kwenye NB tafadhali naomba unitake radhi...... yaani mimi kabisa ni-deep? tafadhali....
sawa nimekupata mkuu,
kweli mimi naamini maneno ya faraja ndo muhimu zaidi ya mpesa
 
Jambo la muhimu la kukumbuka ni kuwa kazi ya Mungu haina makosa, ila kibinadamu haizoeleki na inauma sana, pole sana kaka Mtambuzi na familia yote, tupo pamoja ktk kipindi hiki kigumu na Mungu awape nguvu na ujasiri mkuu.
 
may her soul rest in eternal peace. Pray that you can be strong together with your family
 
Back
Top Bottom