TANZIA: Kamanda James Kombe afariki dunia

TANZIA: Kamanda James Kombe afariki dunia

KAMANDA KOMBE AFARIKI: Aliyekuwa Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, ACP James Kombe amefariki leo katika Hospitali ya Ocean Road alipokuwa akitibiwa.
 
RIP Kamanda KOMBE.

Nitakukumbuka kwa jinsi ulivyofanya kazi kwa uadilifu mkubwa.

Nakumbuka kipindi akiwa RPC Arusha nilikuwa na tatizo la umiliki wa shamba maeneo ya USA mkuu wa kituo cha Polisi USA wakati huo alikuwa Msangi sasa hivi ni RCO wa Dar.Mvamizi alikuwa mwanamke wakati huo huo alikuwa kimada wa Msangi kila nikipeleka malalamiko hakuna kinachofanyika nikaamua kumwona RPC baada ya kumweleza tatizo langu alimwita Msangi mbele yangu akamgombeza kama house boy wake kisha akamwamuru afungue jalada upya na apeleke kesi mahakamani.

Pumzika kwa amani kamanda Kombe.
 
watu mmekuwa na roho kavu kiasi hcho?? Nimesoma michango ya wengi hapa hata pole tu imekuwa ngumu, zaid zaid wanaonekana kufurah. Dah! Kifo kweli kimekuwa chepesi...upumzke kwa amani Kamanda
 
Kila mwanadamu ni mdhambi, usimhukumu mtu usije ukahakumiwa, kila dhambi inasamehewa na Mungu kama utaitubu na kuiacha, dhambi isiyosamehewa ni kumkufuru roho mtakatifu...
TUSIMHUKUMU, MUNGU NDIYE ATAMHUKUMU.. R.i.p kamanda kombe... Mungu akurehemu.

Sasa unapomuambia R.i.p,wewe ndiye mungu??
 
R.I.P kombe tutakukumbuka kwa kazi
uliyoifanya ukiwa Rpc Arusha.
 
Jamani wale walio katika madaraka fanyeni lile lililo bora kwa wanadamu wote angalia hii chuki inavyojionyesha kwa wachangia ni dhahiri kuwa watawaliwa hawakubaliana na mnavyofanya, PLEASE BADILIKENI!!!!!!!!!!
 
Pumzika kwa amani Kamanda Kombe
Arusha watakukumbuka kwa ulivyoutuliza mji kipindi kukiwa na ujambazi wa kutisha wa silaha
 
Alikuwa anaingia field kabisa........hapa ni pale junction ya Kenyatta.....hu ho haaa (kung-fu)

images
niliposoma tu huu uzi wa Kifo cha Kombe, hii ndio picha iliyoniingia akilini. Kamanda miezi michache kabla ya kustaffu kwake. Just died at early Sixties!
 
Mbona wanakufa wazalendo wengi vijijini na haitangazwi?Huyu nae ni wa kawaida tu kwani kila nafsi itaonja mauti.Aliwaibia sana watanganyika kwa kula na kupokea rushwa.
maskin weee! siku za Udika Mremi (Dar Express) zinahesabika sasa
 
Back
Top Bottom