Kwa kweli ni mapema sana wakuu. Ngoja niishie hapo tu nisije nikakufuru, maana MUNGU huyu kama haoni watu wa kuchukua mapema!! Mzee huyu kazi alikuwa anaimudu. Huyu si ndo alikuwa mkuu wa operesheni pale makao makuu ya polisi? Mzee aliendesha operesheni kali sana kwenye mapori ya Geita, Bi'muro, Kibondo na Kasulu huku yeye mwenyewe akiwa msitari wa mbele. Pia baada ya kustaafu alipata shavu pale TANAPA kama mkuu wa operesheni, majangili walikiona cha mtema kuni! Poleni wafiwa, pole TANZANIA. Tumempoteza shujaa!!
Duhh!ama kweli hii ni kama jamaa aliyekwenda msibani akaanza kuangua kilio huku akidai marehenu walisoma wote.Kumbe aliyefariki ni mtoto wa mwaka mmoja!