TANZIA: Kamanda James Kombe afariki dunia

TANZIA: Kamanda James Kombe afariki dunia

Kwa kweli ni mapema sana wakuu. Ngoja niishie hapo tu nisije nikakufuru, maana MUNGU huyu kama haoni watu wa kuchukua mapema!! Mzee huyu kazi alikuwa anaimudu. Huyu si ndo alikuwa mkuu wa operesheni pale makao makuu ya polisi? Mzee aliendesha operesheni kali sana kwenye mapori ya Geita, Bi'muro, Kibondo na Kasulu huku yeye mwenyewe akiwa msitari wa mbele. Pia baada ya kustaafu alipata shavu pale TANAPA kama mkuu wa operesheni, majangili walikiona cha mtema kuni! Poleni wafiwa, pole TANZANIA. Tumempoteza shujaa!!
 
Kamanda Kombe namkumbuka kwa tukio la uchaguzi mkuu wa 2020. Mkurugenzi wa Manispaa ya Arusha alikuwa anasuasua kumtangaza mshindi wa Ubunge wa Arusha Mjini kati ya Baltida Buriani na Godbless Lema wakati wananchi wameshajua mshindi na wako Ofisi ya Manispaa tangu mapema asubuhi baada ya uchaguzi. Nakumbuka wananchi walikuwa wakiimba nyimbo za kushinikiza mshindi atangazwe, FFU, 'washawasha' na Polisi wakiwa wametanda eneo hilo.

Kamanda Kombe alipoona Mkurugenzi anajizungusha kutangaza matokeo, alimwambia Mkurugenzi kuwa ifikapo saa kumi atawaondoa Maaskari wake waliokuwa wanalinda amani, ndipo Mkurugenzi akasalimu amri na kumtangaza Godbless Lema kuwa mshindi.

Hapana Mkuu!
Umemfananisha na Basilio Matei!
 
Pumzika kwa amani kamanda Kombe.Kwa kweli kazi yako uliimudu sana.Hata kama ulikuwa na mapungufu ni ya kibinadamu.Nakumbuka Serengeti uliendesha operation kali sana mpaka ukamnasa Jambazi hatari sana(Isengere) aliyeua mlinzi wako.Pole sana Dada Eva.

Dah pole sana kwa familia ya kamanda mstaafu Kombe.

Kijana wa kazi Isengele akiwa na umri mdogo sana wa miaka ishirini hivi alikuwa ni tishio sana kwa wananchi na hata vyombo vya dola vilikuwa vinamgwaya sana,alikuwa akiiba ng'ombe hadi umasaini na hakuwahi kutiwa nguvuni kwasababu ya umahiri wake wa kutimia bunduki-alikuwa tishio sana Isengere.

Nakumbuka siku alipouawa ni baada ya kamanda Kombe akiwa OCD Serengeti, kuamua kuingia frontline yeye mwenyewe ili kukabiliana na kijana wa kijiji cha Machochwe. Alifanikiwa kumuua Isengere Huku akimpoteza mlinzi(msaidizi) wake katika makabiliano hayo.

Kiujumla kamanda Kombe alikuwa mwadilifu na mchapakazi asiyependa dhulma na uonevu kwa kadri nilivyomfahamu.

Pole kwa familia ndugu jamaa marafiki na watanzania wote.
 
Kwa kweli ni mapema sana wakuu. Ngoja niishie hapo tu nisije nikakufuru, maana MUNGU huyu kama haoni watu wa kuchukua mapema!! Mzee huyu kazi alikuwa anaimudu. Huyu si ndo alikuwa mkuu wa operesheni pale makao makuu ya polisi? Mzee aliendesha operesheni kali sana kwenye mapori ya Geita, Bi'muro, Kibondo na Kasulu huku yeye mwenyewe akiwa msitari wa mbele. Pia baada ya kustaafu alipata shavu pale TANAPA kama mkuu wa operesheni, majangili walikiona cha mtema kuni! Poleni wafiwa, pole TANZANIA. Tumempoteza shujaa!!

Mkuu umechanganya "madesa",huyo unayemtaja ni kamanda mstaafu Venance Tossi, bado anaendelea kupiga kazi na Tanapa baada ya kustaafu polisi.

Namkumbuka kamanda Tossi mojawapo ya vituko vyake akiwa mkuu wa operation wa jeshi la polisi aliruka na helikopta ya jeshi la polisi kwenda rufiji kulabiliana na wapika gongo!
 
Wanakufa waliokuwa na nafuu katika utendaji kama akina Siro, yale mangunguli yenye roho mbaya kwa watanzania hayafi kama akina Mahita na Kamhanda! RIP kamanda!
 
Yule mu uaji wa wale wafanyabiashara wa morogoro ni Abdalla Zombe sio Kombe.

Hata hivyo mi ningefurahi sana kama ningesikia ni Kamhanda, alipo muua Mwangosi akapandishwa cheo.
This is only in Tanzania.

Waziri Celina Kombani naye yupo kimya wakati wale wafanyabiashara wa Madini wa morogoro
walikuwa wanamfadhili kila uuchaguzi tena kwa asilimia kubwa sana. Huyu naye hana shukrani kabisa.

hahahahaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!!!!!!!!!!!!
 
Mkuu umechanganya "madesa",huyo unayemtaja ni kamanda mstaafu Venance Tossi, bado anaendelea kupiga kazi na Tanapa baada ya kustaafu polisi.

Namkumbuka kamanda Tossi mojawapo ya vituko vyake akiwa mkuu wa operation wa jeshi la polisi aliruka na helikopta ya jeshi la polisi kwenda rufiji kulabiliana na wapika gongo!

Aaaah MKuu Mwita Maranya, ni kweli mkuu! Hawa jamaa wanafanana kwa uchapa kazi ndo maana wengi tunayachanganya haya majembe! ASANTE KWA KUNISAHIHISHA MKUU!
 
kila nafsi itaonja mauti na malipo ni hapahapa duniani, liwe somo kwa wanaobaki roho mbaya haisaidii wote tutakufa tu.
 
Alikuwa akijituma sana, lakini hakuacha kusali.
Miaka ya mwanzoni mwa 80's kama sisahau, alikuwa Mkuu wa Kituo Oysterbay.

Siku ya jumapili nilipokuwa tunasali Msasani ZKKKT,nikasikia nyuma yangu jamaa kapiga mwayo, baada ya muda mfupi akawa anasua kwa usingizi.

Ikabidi niulize, huyu jamaa nani?
Kuna jamaa walikuwa wanamfaghamu, akasema ni Kombe huyo Mkuu wa Kituo Oystebay.
Jamaa akaendelea, nawasikitikia sana hawa jamaa maana hawalali kuwasaka majambazi!!

Hiyo ndiyo picha ya Kamanda Kombe iliyobaki kichwani.

RIP Kamanda Kombe.
 
Akaribishwe vyema na malaika wa mbinguni. Huyo mzee binafsi atabaki sana moyoni mwangu kwa mambo aliyonifanyia personally nilipokuwa nakaribia kudhulumiwa na wazungu fulani ambapo baada ya kunisaidia alikataa japo pesa ya vocha.

RIP Kamanda Kombe.


Noted Kamanda wangu! Hakika J. Kombe tutamkumbuka daima!

Alale kwa Amani yake Bwana wetu!
 
MYSRIH(may your soul roast in hell) mshirika wa majambazi!ulitanguliza sana pesa kuliko usalama wa raia na mali zao.,kudadadek.
 
Dah pole sana kwa familia ya kamanda mstaafu Kombe.

Kijana wa kazi Isengele akiwa na umri mdogo sana wa miaka ishirini hivi alikuwa ni tishio sana kwa wananchi na hata vyombo vya dola vilikuwa vinamgwaya sana,alikuwa akiiba ng'ombe hadi umasaini na hakuwahi kutiwa nguvuni kwasababu ya umahiri wake wa kutimia bunduki-alikuwa tishio sana Isengere.

Nakumbuka siku alipouawa ni baada ya kamanda Kombe akiwa OCD Serengeti, kuamua kuingia frontline yeye mwenyewe ili kukabiliana na kijana wa kijiji cha Machochwe. Alifanikiwa kumuua Isengere Huku akimpoteza mlinzi(msaidizi) wake katika makabiliano hayo.

Kiujumla kamanda Kombe alikuwa mwadilifu na mchapakazi asiyependa dhulma na uonevu kwa kadri nilivyomfahamu.

Pole kwa familia ndugu jamaa marafiki na watanzania wote.

Ngombe wote waliokuwa wanachukuliwa kama fidia kwa walioibiwa mifugo katika vijiji vya tarafa ya Ngoreme na vijiji vya mbaribari, machochwe na kebanchebanche waliishia mfukoni mwa Kombe hakuna fidia iliyomfikia mlengwa!Kwa unafiki wetu tusubiri siku ya Zombe risala kibao za kumsifia na unafiki kibao!
 
Back
Top Bottom