TANZIA: Kamanda James Kombe afariki dunia

TANZIA: Kamanda James Kombe afariki dunia

maskin kombe R.I.P. mbona mapema au kakosa posho za kila siku ndio kaded
 
umekosea kidogo mkuu, aliyekuwa RPC wakati ule alikuwa ni Basilio Matei.

Ni kweli mkuu, nimekosea. Nakumbuka ule uamuzi wa Matei ulimfanya ahamishiwe Makao Makuu ya Polisi. Siasa za nchi hii ni vituko vitupu!
 
Arusha ilikuwa salama chini ya huyu mtu,alinitendea wema ambao sitausahau.R.I.P kombe.
 
Akaribishwe vyema na malaika wa mbinguni. Huyo mzee binafsi atabaki sana moyoni mwangu kwa mambo aliyonifanyia personally nilipokuwa nakaribia kudhulumiwa na wazungu fulani ambapo baada ya kunisaidia alikataa japo pesa ya vocha.

RIP Kamanda Kombe.
 
RIP Kamanda KOMBE.

Nitakukumbuka kwa jinsi ulivyofanya kazi kwa uadilifu mkubwa.

Nakumbuka kipindi akiwa RPC Arusha nilikuwa na tatizo la umiliki wa shamba maeneo ya USA mkuu wa kituo cha Polisi USA wakati huo alikuwa Msangi sasa hivi ni RCO wa Dar.Mvamizi alikuwa mwanamke wakati huo huo alikuwa kimada wa Msangi kila nikipeleka malalamiko hakuna kinachofanyika nikaamua kumwona RPC baada ya kumweleza tatizo langu alimwita Msangi mbele yangu akamgombeza kama house boy wake kisha akamwamuru afungue jalada upya na apeleke kesi mahakamani.

Pumzika kwa amani kamanda Kombe.

Kweli kabisa Mkuu, huyu jamaa alikuwa hapendi kuonea, utendaji wake kidogo unashabihiana na Basilio Matei. Kuna kipindi nilikuwa ikulu ndogo, nikatoroka kwenda kusikiliza kesi ya Dr. Slaa ya kupiga uchaguzi wa ubunge karatu, niliporudi polisi wawili waliokuwa pale ikulu ndogo wakawa wananitukana, Kombe alipotokezea ghafla akawasikia wakiniporomoshea matusi. Walirushwa kichura nikarudishiwa amani yangu.

R.I.P. Kamanda

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Nakubaliana na wewe asilimi kubwa hata lema aliona sio dili tena akatoka huko na kule kwa wakurya wanamjua huyu bwana na ukorofi wao hapo walifunga brack.
ni yule aliyewahi kuwa RPC Arusha?kama ni yeye alisaidia sana kupunguza ujambazi arusha,Rip bwana komandoo.
 
Mungu awape moyo wa uvumilivu wafiwa wote

RIP Kamanda

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Namkumbuka akiwa RPC wa Arusha,alipambana na ujambazi na Mapolisi wala rushwa! Alikua kipenzi cha wana Arusha. Poleni wafiwa,alale mahali pema peponi. Amen.
 
Pumzika kwa amani kamanda Kombe.Kwa kweli kazi yako uliimudu sana.Hata kama ulikuwa na mapungufu ni ya kibinadamu.Nakumbuka Serengeti uliendesha operation kali sana mpaka ukamnasa Jambazi hatari sana(Isengere) aliyeua mlinzi wako.Pole sana Dada Eva.
 
RIP Kamanda KOMBE.

Nitakukumbuka kwa jinsi ulivyofanya kazi kwa uadilifu mkubwa.

Nakumbuka kipindi akiwa RPC Arusha nilikuwa na tatizo la umiliki wa shamba maeneo ya USA mkuu wa kituo cha Polisi USA wakati huo alikuwa Msangi sasa hivi ni RCO wa Dar.Mvamizi alikuwa mwanamke wakati huo huo alikuwa kimada wa Msangi kila nikipeleka malalamiko hakuna kinachofanyika nikaamua kumwona RPC baada ya kumweleza tatizo langu alimwita Msangi mbele yangu akamgombeza kama house boy wake kisha akamwamuru afungue jalada upya na apeleke kesi mahakamani.

Pumzika kwa amani kamanda Kombe.

Amina" Pumzika kwa amani kamanda Jemes Kombe mzee wangu kombe imeniuma sana daaah tulishiriki wote mazishi ya babu pale mwika mwezi 6 leo mzee umetangulia mbona mapema sana aaaaaah.lala
usingizi wenye ushindi dhidi ya kaburi.
 
Pumzika kwa amani kamanda Kombe.Kwa kweli kazi yako uliimudu sana.Hata kama ulikuwa na mapungufu ni ya kibinadamu.Nakumbuka Serengeti uliendesha operation kali sana mpaka ukamnasa Jambazi hatari sana(Isengere) aliyeua mlinzi wako.Pole sana Dada Eva.

Amina...Eva,frid wamempotza baba muhimu sana kwao Imeniuma sana.
 
Unapotoa post tafakari usikurupuke tu,hadhi yamabasi ya Dar ex niyakubebwa kweli?Au unamaanisha ilikuwa nikapuni ya Kamanda Kombe!Naweka wazi kuwa mmiliki wa Dar ex na Kombe nindugu na Mmiliki huyu hakutegemea kabisa nafasi ya Kombe ili kuendesha Kampuni yake hili nakuhakikishia mimi.

Asante Mkuu kwa kumjibu kwa busara na hekima, huyu mtu ...tukampumzishe mzee bwana.
 
Back
Top Bottom