Nchi tajiri kabisa dunia ya Marekani inayomiliki zaidi ya asilimia 20 ya Uchumi wote wa dunia inashuhudia mfumuko mkubwa na mbaya wa bei kuwahi kutokea katika nchi hio unaofikia asilimia 6.8, huku Tanzania sisi tukisalia kwenye mfumuko wa asilimia kati ya 3 & 5.
Mfumuko huu wa bei wa nchi ya Marekani haujawahi kutokea kwa miaka 40 iliyopita kwani kwa mara ya mwisho ulishuhudiwa mwaka 1982,Si Marekani tu UK, Uturuki, Ujerumani nako hali ni mbaya,
Wakati watanzania wengi tunalalamika kwamba vitu vimepanda bei nchini hali ni tofauti sana kwa majirani zetu na duniani kwa ujumla wake kwa bei ya vitu huko ni juu zaidi, Watanzania tufanye bidii kuelewa yanayoendelea duniani sio kulalamika pekee ,
Kwa mujibu wa World Population Review Tanzania ilikuwa na Inflation ya asilimia 3.4 mwaka 2021 wakati Kenya ikiwa na asilimia 6.06,Rwanda asilimia 13.16 na Uganda ni asilimia 3.0 japo inflation imeendelea kupanda maeneo mengi,
Wakati huo huo huko duniani Venezuela wao wakishika mkia kwa kuwa na inflation rate ( CPI ) ya asilimia 9,986 na Zimbabwe wakifikia asilimia 56.8 na kuifanya SADC kuwa na ongezeko la inflation kwa mwaka 2020|21 linalofikia asilimia 3.5 na kuifanya SADC kuwa na annual inflation ya asilimia 46.9,
Inflation inachangiwa na mambo makubwa matatu ambayo ni Demand|Mahitaji ya bidhaa na huduma , Gharama za Uzalishaji|Cost of Production na Nguvu kazi au built in inflation
Tanzania kinachotusumbua ni "Cost Push Inflation " yaani mfumuko wa bei unaosababishwa na gharama za uzalishaji hasa baada ya kuongezeka kwa bei za "mafuta" na kukosekana kwa Umeme wa uhakika wakati flani,
Mpaka naandika makala hii mfumuko wa bei Tanzania kwa bidhaa na huduma kwa Vipimo vyote vya CPI,PPI na WPI unakisiwa kufikia kati ya asilimia 3 & 5 hii ni kwa mujibu wa ripoti ya mwisho ya BOT,
Tunaposema Tanzania ipo salama sana chini ya Mhe Samia Suluhu Hassan tunamaana hii na lazima Watanzania watambue kuwa kupanda kwa bei ya bidhaa na huduma Tanzania ni "JAMBO LA DUNIA NZIMA" wala si jambo la Mama Samia Suluhu Hassan CCM,ACT-Wazalendo,NCCR-Mageuza wala CHADEMA ni jambo la dunia nzima.
View attachment 2070586
VIVA TANZANIA VIVA || VIVA SAMIA VIVA