Tanzania: Utawala bora vs Rushwa

Tanzania: Utawala bora vs Rushwa

Halisi heshima kwako Mkuu,
Ni kweli magazeti ya Tanzania yanashangaza sana,yaani katika magazeti yote,gazeti lisiloogopa kitu ni MwanaHalisi pekee!!!Hao jamaa walichapisha orodha yote ya mafisadi huku wengine wakikunja mbawa zao kama kunguru na kisha baadae na wao wakaanza kuwaandika waliokuwa wakikanusha.Mbona hayo hayo magazeti yaliandika kauli za mafisadi kuwa Slaa ni mwongo?je walimkonsalti na kuthibitisha uongo wake kabla ya kuandika?au kwa vile wapinzani hawana serikali ndo maana wanaandika tu?

kweli magazeti na TV za Tanzania viashangaza sana.At least kuna kile kipindi cha asubuhi cha "Power Breakfast" pale Radio Clouds cha kina Masudi Kipanya,Fina Mango na Gerald Hando,vijana hawa kwa kweli ni wa kupongezwa kutokana na ujasiri wao wa kuwa critical na kujadili longo longo za wasanii wetu zinazoathri maisha na ustawi wa nchi yetu...laiti kama vyombo vyote vingekuwa free...
 
Mambo yaiva

2007-10-12 16:42:14
Na Mwandishi Wetu, Dodoma


Mambo yameiva! Siku moja tu baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bwana Jakaya Kikwete kueleza kuwa kila tuhuma ya rushwa iliyoibuliwa ingali ikifanyiwa kazi na vyombo vya usalama, hatimaye utekelezaji wa vitendo umeanza.
Taarifa zilizolifikia gazeti hili zinadai kuwa tayari baadhi ya vigogo wameanza kushughulikiwa.

Imedaiwa kuwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini, TAKUKURU imeshaandaa orodha ndefuu!

Taarifa hiyo imekuja wakati ni leo tu imeripotiwa kuwa tayari Mkurugenzi wa Wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma, Bi. Mary Qorro na Kaimu Mweka Hazina, Bw. Jeremia Kusimula wamewekwa kati.

Wawili hao inadaiwa tayari wamepandishwa kizimbani ili kujibu tuhuma za kutafuna mamilioni kadhaa ya walipa kodi wa wilaya hiyo.

Taarifa zinafafanua zaidi kuwa mbali na vigogo hao, wengine walionaswa na TAKUKURU na kuburuzwa kortini ni Mtunza Bohari, Bw. Pius Mgessa na Mhasibu Msaidizi, Bi. Bertha Augustino.

Inaelezwa kuwa wote hao wanatuhumiwa kuuhujumu uchumi wa nchi kwa kufanya udanganyifu na hivyo kutafuna Sh. Milioni 12, mali ya halmashauri hiyo.

Mapema, Kamanda wa TAKUKURU mkoani Dodoma, Bw. Leonard Mtalai, alikaririwa akisema kuwa watuhumiwa hao walishirikina na mfanyabiashara mmoja, kati ya Desemba 2006 na January 2007, katika kula njama na kufanya udanganyifu wa malipo hewa ya Sh. Milioni 12.

Juzi wakati akizungumza katika hafla ya kuchangia ujenzi wa hosteli ya kanisa la KKKT mjini Arusha, Rais Kikwete alisema Serikali yake itawashughulikia ipasavyo wala rushwa, bila kujali majina wala nyadhifa zao.

Hata hivyo, alionya watu wanaojipa mamlaka ya kujifanya polisi, waendesha mashtaka, wapelelezi na pia mahakimu wa kuwahukumu watuhumiwa bila kufuata sheria za nchi.

SOURCE: Alasiri
 
Inaelezwa kuwa wote hao wanatuhumiwa kuuhujumu uchumi wa nchi kwa kufanya udanganyifu na hivyo kutafuna Sh. Milioni 12, mali ya halmashauri hiyo.

hawa ndio wahujumu uchumi?mbona tunatania?
wako wapi kina balali,
wako wapi kina Karamagi?
wako wapi kina EL?

mbona PCCB mnatufanya sie vipofu,au nyie ni tawi la wanamtandao?
 
Hii ndio bongo...wanaokula rushwa ndogo ndogo sabau ya ukata ndio wanaodakwa...wanaokula rushwa nene nene wanakingiwa kifua na President....Unafikiri atawakamatia wapi wakati na yeye ndio mtuhumiwa na captain katika JK Eleven ya Dr. Slaa?
 
Kwa nini hakuna tamko Rasmi la Ikulu kuhusu ufisadi?

Nashindwa kushawishika kuwa JeiKei ni msafi. Haiwezekani mtu msafi akaishi kwenye nyumba chafu kisha akaendelea kufurahia tu pasipokuchukua hatua za kuisafisha. Anachoweza kukifanya, ni kujifanya mtanashati akiwa nje ya nyumba yake, lakini akirudi ndani anakuwa katika hali yake aliyoizoea ya kuwa mchafu.

JeiKei hajatoa tamko lolote la maana kuhusiana na ufisadi na mafisadi. Badala yake anatoa kauli zinazokinzana. Baba wa Taifa alisema ''Ukimwangalia usoni mtu mwenye dhamira ya dhati ya kupambana na Rushwa utamtambua'' Ni kweli, alichosema Nyerere. Sioni hali hiyo usoni Kwa JeiKei.

Nadhani ni kwakuwa na yeye yupo kwenye orodha ya Mafisadi! Kwa nini kakaa kimya? Kuna kitu kinachomzunguka, akitaka kuongea kinamkwama kooni? Wana JF hebu tuujadili ukimya wa JeiKei katika hili suala nyeti linalogusa maisha ya kila mTZ.
 
..na inastahili ifanyiwe mabadiliko makubwa haraka sana

Posted Date::10/20/2007
Tuhuma: Mkapa analindwa na katiba ya Tanzania
* Inasema wazi hawezi kushtakiwa milele
* Aweza tu kujibu tuhuma kama akipenda

* Ni zile za ufisadi, kufanya biashara Ikulu

Na Andrew Msechu
Mwananchi

KATIBA ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndiyo inayompa jeuri Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa, kukataa kujibu tuhuma za ufisadi na kufanya biashara akiwa Ikulu zinazomkabili kwa kuwa hawezi kushtakiwa milele.

Rais huyo mstaafu tayari amewaeleza wanaomtuhumu wasitarajie majibu yoyote kutoka kwake kwa kuwa tayari yeye ameshastaafu masuala ya kisiasa, hivyo asingependa kujihusisha na malumbano yoyote ya aina hiyo kwa sasa.

Mkapa alitoa kauli hiyo Alhamisi iliyopita alipokuwa akihutubia katika mkutano wa tathmini ya mwaka ya Taasisi ya Mkapa inayoshughulikia masuala ya Ukimwi (Benjamin William Mkapa HIV/AIDS Foundation), uliofanyika katika Hoteli ya Kunduchi Beach, jijini Dar es Salaam.

Tuhuma zinazoelekezwa kwa Mkapa ambazo zimekuwa zikichapishwa katika magazeti na pia kuzungumzwa na wanasiasa wa upinzani na wengine, akiwamo Katibu Mtendaji wa Mfuko wa Mwalimu Nyerere (MNF), Joseph Butiku zinaeleza kuwa, rais huyo mstaafu alikiuka taratibu za uongozi kwa kutumia nafasi yake kama kiongozi wa nchi katika kujitafutia mali.

Suala hilo linatafsiriwa kuwa ni matumizi mabaya ya madaraka sambamba na ukiukaji wa maadili ya uongozi wa umma.

Lakini Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 inatoa ulinzi dhidi ya mashtaka kwa rais aliyepo madarakani na aliyestaafu katika Ibara ya 46(3) ya katiba.

Ibara hiyo inasema; "Isipokuwa kama hataacha kushika madaraka ya rais kutokana na masharti ya ibara ya 46A (10), itakuwa ni marufuku kumshtaki au kufungua mahakamani shauri lolote la jinai au kumdai mtu aliyekuwa anashika madaraka ya rais baada ya kuacha madaraka hayo kutokana na jambo lolote alilofanya yeye kama rais wakati alipokuwa bado anashika madaraka ya rais kwa mujibu wa Katiba hii".

Ufafanuzi unaopatikana katika kifungu cha 46A (10), unasema kuwa rais mstaafu anayeweza kushtakiwa kwa kosa la jinai au madai ni yule aliyeondolewa madarakani kwa azimio la bunge baada ya mashtaka dhidi yake (bungeni) kuthibitika, jambo ambalo halikumtokea Mkapa.

Kifungu hicho kinasema, "Endapo Bunge litapitisha azimio kuwa mashtaka dhidi ya rais yamethibitika na kwamba hastahili kuendelea kushika kiti cha rais, spika atawafahamisha rais na mwenyekiti wa tume ya uchaguzi juu ya azimio la bunge, na hapo rais atawajibika kujiuzulu kabla ya siku ya tatu tangu bunge lilipopitisha azimio hilo."

Kwa mujibu wa vifungu hivyo, Rais Mkapa hakuondolewa madarakani na bunge, hivyo anabakia na sifa ya kutoshtakiwa milele hadi Katiba itakapozungumza vinginevyo.

Hali hiyo inaonyesha wazi kuwa, majibu ya Mkapa aliyoyatoa siku za hivi karibuni yalijikita katika kinga aliyonayo kikatiba, jambo ambalo inaonekana wanaomtaka kujibu tuhuma walikuwa hawajalitazama, au wanataka ajibu tu kwa misingi ya kuonyesha ustaarabu na uadilifu.

Hata hivyo, miongoni mwa wanaomtaka Mkapa kujibu tuhuma ni Mhadhiri wa Sheria katika Kitivo cha Sheria, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Sengondo Mvungi, ambaye alikaririwa na gazeti dada la Mwananchi jana akisema kuwa; kauli ya Mkapa kwamba hataki kujibu tuhuma hizo kwa kuwa ni za kisiasa siyo ya uwajibikaji na uungwana.

Mvungi alisema, Mkapa hawezi kukwepa kujibu tuhuma hizo kwa kuwa hana kinga kisheria kuwajibika kwa mambo aliyofanya kwa utashi wake wakati wa utawala wake.

Alisema sheria inampa kinga rais kwa mambo aliyofanya kama rais na siyo aliyofanya kwa utashi wake, hivyo Mkapa anapaswa kujibu tuhuma hizo endapo zimemlenga yeye binafsi.

Kwa kuzingatia tafsiri ya Dk Mvungi, yapo baadhi ya mambo ambayo Mkapa anaweza kushtakiwa, hasa aliyoyafanya binafsi kama vile kufanya biashara akiwa Ikulu, lakini

kwa tuhuma za Wapinzani kuwa anahusika na ufisadi kwa kuwa ulifanyika yeye akiwa rais, zinalindwa na Katiba.

Mwingine aliyeeleza nia ya kumtaka Mkapa kujibu tuhuma ni Mhadhiri wa Siasa katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Mwesiga Baregu, ambaye alisema kauli ya Mkapa inaleta hisia kuwa amesahau kuwa aliingia Ikulu kwa ridhaa ya wananchi na aliahidi kuwatumikia wananchi hao kwa ukweli na uwazi.

"Nafikiri mheshimiwa Mkapa amesahau kwamba aliomba kazi ya Urais kwa hiari yake na akaahidi kulitumikia taifa kwa ukweli na uwazi. Sasa ni busara zaidi akimaliza vizuri kwa kujisafisha tuhuma hizo," alisema Profesa Baregu.

Profesa huyo aliongeza kuwa ni muhimu sasa kwa serikali kuanzisha utaratibu wa viongozi wa umma kutangaza mali zao kabla na baada ya kuingia madarakani, ili jamii ifahamu uwezo wao kimapato na kuwaamini katika kila jambo wanalofanya.

Alisema kitendo cha Rais Mstaafu Mkapa kujibu tuhuma hizo sio tu kitamaliza mjadala unaoendelea kuhusu tuhuma za ufisadi dhidi yake, bali pia kitamjengea heshima na imani zaidi kwa wananchi.

Hata hivyo, wachambuzi wa masuala ya kisiasa, wanasema kutaja tu mali za viongozi haitoshi, bali wanatakiwa kueleza na jinsi walivyopata mali hizo, ili uadilifu wao uweze kujidhihirisha.
 
Hapa tutawaomba wataalamu wa Sheria wa compare na contrast katiba yetu na ya Malawi na ya Zambia ambapo maraisi wastaafu wameweza kushtakiwa.
na Je wenzatu wamefanikiwa kwa kifungu kipi?
Na tukiona tuna mapungufu basi mapendekezo ya kubadili hivyo vifungu yafanyike.
 
Katiba ya Tanzania siyi kitanu cha Mwenyezi Mungu. Katiba imeandikwa na Watanzania, hivyo kama kuna mapungufu yoyote ikiwemo la kuwashtaki Marais wala rushwa, mafisadi, wanaosaini mikataba mibovu na wanaojilimbikizia mali basi Watanzania bila shaka yoyote wangependa yafanywe mabadiliko haraka sana ili wahusika wafunguliwe mashtaka kwa maslahi ya Watanzania. Tumechoka kuwa na katiba inayowalinda watenda maovu.
 
Wow!
Naona kuna watu wanakuja hapa JF na kusoma tumeandika nini na kufanya news nadhani nilishaelezea hili swala hapa.
Katiba inatakiwa iandikwe upya, kumshtaki rais siyo jambo muhimu sana kwenye katiba ila katiba iwe hamuwezeshi rais kula rushwa au kuwa fisadi. Lazima tutambue kuwa sheria na haki ni vitu viwili tofauti, kama rais akiwa na uwezo wa kula rushwa na akimaliza uongozi wake mkampeleka mahakamani haimaanishi kuwa mtamfunga au atarudisha kitu chochote anaweza kushinda kesi vilevile.
 
Wow!
Naona kuna watu wanakuja hapa JF na kusoma tumeandika nini na kufanya news nadhani nilishaelezea hili swala hapa.
Katiba inatakiwa iandikwe upya, kumshtaki rais siyo jambo muhimu sana kwenye katiba ila katiba iwe hamuwezeshi rais kula rushwa au kuwa fisadi. Lazima tutambue kuwa sheria na haki ni vitu viwili tofauti, kama rais akiwa na uwezo wa kula rushwa na akimaliza uongozi wake mkampeleka mahakamani haimaanishi kuwa mtamfunga au atarudisha kitu chochote anaweza kushinda kesi vilevile.

Sio vibaya waandishi kuja kuchukua hapa habari lakini wanatakiwa watoe credit kwa JF kuwa ndio source yao.
 
Posted Date::11/2/2007
Wahisani kuisaidia kukabili rushwa Tanzania
Na Ramadhan Semtawa
Mwananchi

NCHI 14 wahisani wa Tanzania, zimekubali kuijengea nguvu Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), ili iweze kupambana vema na ufisadi nchini.

Tamko la nchi hizo lililotolewa jijini Dar es Salaam jana, pamoja na kukubali kusaidia Takukuru, lakini kwa pamoja na serikali zimekubaliana kwamba taarifa zote kuhusu ufisadi nchini ambazo zimefanyiwa kazi na taasisi hiyo kuanzia mwaka jana na huu, zianikwe hadharani.

Tamko hilo lilisomwa jana katika majumuisho ya mkutano kati ya serikali na wafadhili kuhusu mapitio ya Fedha za Misaada ya Wafadhili katika Bajeti (GBS.

GBS ni mpango wa nchi na mashirika 14 wafadhili kusaidia bajeti ya serikali moja kwa moja, hivyo kulifanya bunge kuwa na maamuzi ya usimamizi wa matumizi na mapato ya serikali.


Katika bajeti ya serikali ya mwaka 2007/08, nchi hizo ziliweza kuchangia asilimia 38 ya bajeti ambayo ni sawa na kiasi cha sh 881, 320.00 milioni.

Katika tamko hilo lililosomwa na Mwenyekiti wa vikao vya GBS, David Stanton, nchi hizo zimeukaribisha vema uamuzi huo wa kuanika taarifa za ufisadi (si majina) ambao ni mkakati wa serikali na kwamba iko tayari kuisadia Takukuru kiufundi na taarifa hizo kuanikwa katika tovuti.

"Tuko tayari kusaidia PCCB katika kuijengea uwezo wa rasiliamali za kiufundi na kitaalamu," linasema tamko hilo.

"Uongozi na mapambano ya rushwa, PCCB (Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa), itachapisha taarifa za rushwa kwa ngazi tofauti nchini, kuanzia mwaka uliopita na mwaka huu kisha kuziweka katika tovuti yao," ilisema tamko hilo.

"Tuko tayari kusaidia misaada ya kiufundi kwa PCCB, tunakaribisha juhudi za ripoti maalumu ya kuangalia usafirishaji wa rasilimali, kama wanyama pori, mazao ya misitu na samaki".

"Kuna umuhimu mkubwa wa kuangalia na kusimamia vema rasilimali na miundombinu, ili ziweze kukuza uchumi," linasema tamko hilo.

Stanton katika tamko hilo, alisema nchi hizo zimeweka bayana kwamba uchunguzi huru ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na ushiriki wa kikamilifu wa serikali, utatoa mwelekeo wa jinsi gani zitaweza kuongeza ushirikiano na Tanzania katika misaada kwa bajeti ya mwaka 2008/09.

Tamko hilo ambalo sehemu inataja mambo matano ya msingi ambayo yalijadiliwa kwa pamoja kati ya pande zote mbili, linasisitiza haja ya serikali kuendeleza mapambano ya dhati dhidi ya rushwa ili kuleta mafanikio katika juhudi za sasa.

Ndani ya tamko hilo, Stanton alisema jambo jingine lililojadiliwa kati ya hayo matano, ni usimamizi madhubuti wa rasilimali za nchi na miundombinu, kama hatua ya kukuza uchumi.

Tamko hilo limeongeza kwamba, jambo la tatu lililojadiliwa na kukubaliwa na pande zote mbili, ni kuhakikisha kunakuwepo uwazi kwa fedha zinazopelekwa wilayani ambako matokeo ya GBS yanapaswa kuonekana.

Katika tamko hilo, wahisani hao pia waliweka bayana haja ya kupatiwa ufumbuzi kwa migogoro ya kazini katika sekta muhimu za maendeleo.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Gray Mgonja, alisema serikali imejipanga vema kuweza kushirikiana na nchi wahisani.

Mkutano huo ambao ulianza Oktoba 29, pamoja na mambo mengine ulitawaliwa na mjadala mkali kuhusu tuhuma za ufisadi ikiwemo ndani ya BoT huku serikali ikieleza hatua ilizochukua lakini wafadhili wakizidi kuhoji na kutaka msimamo madhubuti zaidi katika suala hilo.
 
its been a decade sasa tokea nianze kusikia kuhusu hao wahisani ! kulikoni ?
 
You have to wait for another 3 decades in order to see promising results....🙂Oh! Bongo!
 
mie binafsi i have no problem waiting even if it takes forever, lakini hao je wanaotaka maendeleo overnight ? si ndio hawatoisha kulalama kila siku !
 
Mie naona mwangaza mdooogo upande mwingine mwa tunnel hili la ubadhilifu na ufisadi. Labda hawa wahisani wataweza kufanya mambo mazuri kurekebisha hali ya rushwa TZ.

Tukipata watu wa nje kama hawa watakuwa wanafanya mambo bila bias, wala personal interests. Inaweza nd'o ikawa solution tunayohitaji Tanzania.

I see hope.....Mungu Ibariki Tanzania.
 
Mie naona mwangaza mdooogo upande mwingine mwa tunnel hili la ubadhilifu na ufisadi. Labda hawa wahisani wataweza kufanya mambo mazuri kurekebisha hali ya rushwa TZ.

Tukipata watu wa nje kama hawa watakuwa wanafanya mambo bila bias, wala personal interests. Inaweza nd'o ikawa solution tunayohitaji Tanzania.

I see hope.....Mungu Ibariki Tanzania.

yaani waje kutuongoza or i misunderstood something here??
 
Ni hadi pale Wahisani na serikali watapoona kuwa maendeleo siyo kujenga nyumba ya ghorofa sita, kuipatia jenereta la umeme, kutengeneza kisima cha maji hapo na kuweka pampu, na kununua setilaiti na kuiwezesha kupata matangazo ya kimataifa na ya ndani pamoja mtandao; wakati nyumba yenyewe imejengwa kwenye kijiji cha Chuya ambako hata kwenye ramani hakipo!..na cha kuudhi kijiji kizima hakina hata barabara..!
 
Wahisani wa nchi za magharibi siku zote wana agenda zao. Tanzania ya leo tukitaka kuondoa na kupunguza rushwa tunaweza bila wao. Viongozi wetu watekeleze kwa vitendo kero za wananchi na sheria kali zitumike. Takukuru kiwe ni chombo huru ambacho kinatakiwa kupewa meno kisheria hata ikibidi kumshughulikia rais ambaye yuko madarakani. IT CAN BE DONE.
 
Back
Top Bottom