Tanzania tumepigika tena, safari hii 3-0, Uganda haooooo wamefuzu CHAN 2023

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,460
Safari ya timu ya taifa ya Tanzania kufuzu kucheza Kombe la Afrika kwa Wachezaji wa Ligi za Ndani (CHAN 2023) imefikia tamati baada ya kupata kipigo cha magoli 3-0 dhidi ya Uganda, leo Jumamosi Septemba 3, 2022.

Kwa matokeo ya mechi hiyo iliyochezwa Uganda, Tanzania imetolewa kwa jumla ya magoli 4-0 kwa kuwa mchezo wa kwanza baina ya timu hizo uliochezwa Dar es Salaam wageni walishinda 1-0.

Hivyo, Uganda imefanikiwa kufuzu michuano hiyo kwa mara ya 6 mfululizo wakati Tanzania ikiwa na rekodi ya kushiriki mara mbili pekee.
 
Safari ya timu ya taifa ya Tanzania kufuzu kucheza Kombe la Afrika kwa Wachezaji wa Ligi za Ndani (CHAN 2023) imefikia tamati baada ya kupata kipigo cha magoli 3-0 dhidi ya Uganda, leo Jumamosi Septemba 3, 2022.

Kwa matokeo ya mechi hiyo iliyochezwa Uganda, Tanzania imetolewa kwa jumla ya magoli 4-0 kwa kuwa mchezo wa kwanza baina ya timu hizo uliochezwa Dar es Salaam wageni walishinda 1-0.

Hivyo, Uganda imefanikiwa kufuzu michuano hiyo kwa mara ya 6 mfululizo wakati Tanzania ikiwa na rekodi ya kushiriki mara mbili pekee.
Kocha mpya hawezi ata kushindana na 🦁 ndo Kocha wa Taifa.
 
Nilisema hapa hapa kupanga ni kuchagua

Tumepanga kuwa na ligi bora hivyo timu ya taifa lazima tu iwe mbovu automatic.

Nikatoa mifano ni lini england au south africa walichukua kikombe chochote watu waliishia kunitukana.

Angalia ligi ya Brazil, Argentina, Belgium ambazo zinafanya vizuri kwenye timu za taifa ligi zao za ndani vipi jibu ni kuwa wanazalisha wachezaji wengi kwenda kushindana nje ya nchi yao.

Sisi, South Africa na English ni wachezaji wangapi tunao wanaocheza ligi za nje? Utakuta ni 1% tu ya wachezaji

Hivyo lazima tukubali kuwa na ligi Bora tushindane kwenye club competitions Africa.

Au tuweke sheria tuwe na wachezaji wengi wa ndani tuue ligi ili tuwe na timu ya taifa angalau ya kwenda chani maana hata kombe la Africa tutaenda ila kwa tabu.

Ziacheni timu za Tanzania zisajili wachezaji quality wa nje Ili tuenjoy ligue mambo ya timu ya taifa mwachie Karia maana alishasema mawazo yake kwa sasa ndio yanatawala ukitaka usubiri wakati wako ukiwa Rais TFF.😀
 
tukiacha usimba na uyanga pamoja na timu mpya ya tozo kutoka kwa defao tutafika mbali na jinga moja zungu jeusi linalo ogopa jua
 
Nilisema hapa hapa kupanga ni kuchagua

Tumepanga kuwa na ligi bora hivyo timu ya taifa lazima tu iwe mbovu automatic.

Nikatoa mifano ni lini england au south africa walichukua kikombe chochote watu waliishia kunitukana.

Angalia ligi ya Brazil, Argentina, Belgium ambazo zinafanya vizuri kwenye timu za taifa ligi zao za ndani vipi jibu ni kuwa wanazalisha wachezaji wengi kwenda kushindana nje ya nchi yao.

Sisi, South Africa na English ni wachezaji wangapi tunao wanaocheza ligi za nje? Utakuta ni 1% tu ya wachezaji

Hivyo lazima tukubali kuwa na ligi Bora tushindane kwenye club competitions Africa.

Au tuweke sheria tuwe na wachezaji wengi wa ndani tuue ligi ili tuwe na timu ya taifa angalau ya kwenda chani maana hata kombe la Africa tutaenda ila kwa tabu.

Ziacheni timu za Tanzania zisajili wachezaji quality wa nje Ili tuenjoy ligue mambo ya timu ya taifa mwachie Karia maana alishasema mawazo yake kwa sasa ndio yanatawala ukitaka usubiri wakati wako ukiwa Rais TFF.
Tatizo la Tanzania cha kwanza kabisa ni uwezo wetu kua chini tatizo la pili ni mazingira mabovu ya nchi kufanya uwekezaji kwenye sekta ya michezo.kwasababu sio mpira wa miguu tu ndio tunaofanya vibaya.Kila mchezo tuko vibaya.hiyo ligi unaiona nzuri kwasababu timu zinasimamiwa na watu binafsi ila ingekua niswala linalosimamiwa kitaifa isingekua hivyo ilivyo.Hizo nchi ulizosema inawezekana haziko vizuri kwenye soka ila angalau kuna michezo wanayofanya vizuri tofauti na sisi ambao hata kuogelea kumetushinda wakati tumezungukwa na mito,maziwa kila mahali.
 
Nilisema hapa hapa kupanga ni kuchagua

Tumepanga kuwa na ligi bora hivyo timu ya taifa lazima tu iwe mbovu automatic.

Nikatoa mifano ni lini england au south africa walichukua kikombe chochote watu waliishia kunitukana.

Angalia ligi ya Brazil, Argentina, Belgium ambazo zinafanya vizuri kwenye timu za taifa ligi zao za ndani vipi jibu ni kuwa wanazalisha wachezaji wengi kwenda kushindana nje ya nchi yao.

Sisi, South Africa na English ni wachezaji wangapi tunao wanaocheza ligi za nje? Utakuta ni 1% tu ya wachezaji

Hivyo lazima tukubali kuwa na ligi Bora tushindane kwenye club competitions Africa.

Au tuweke sheria tuwe na wachezaji wengi wa ndani tuue ligi ili tuwe na timu ya taifa angalau ya kwenda chani maana hata kombe la Africa tutaenda ila kwa tabu.

Ziacheni timu za Tanzania zisajili wachezaji quality wa nje Ili tuenjoy ligue mambo ya timu ya taifa mwachie Karia maana alishasema mawazo yake kwa sasa ndio yanatawala ukitaka usubiri wakati wako ukiwa Rais TFF.
Hizi ni akili za ma.vi kabisa
 
IMG-20220904-WA0012.jpg
 
Back
Top Bottom