Tanzania inahitaji Rais Fyatu?

Tanzania inahitaji Rais Fyatu?

Zipo njia nyingi za kutoa taarifa za kuliokoa TAIFA letu hili. Ipo hii JF na baadhi ya watu humu ambao sio waoga, wapo WABUNGE wasiri na JASIRI sana.

Unaamini vyombo hivyo (JF & Bunge) havijafanya kazi hiyo mpaka sasa? Na kama vimeshatoa msaada mkubwa sana, je? unaona kunamwitikio wowote kutoka kwa watoa maamuzi wa kushughulikia taarifa hizo kwa moyo moja? au ni nani hasa anatakiwa apewe hizo taarifa ambaye haja pata hadi sasa? kama sio tutarudi kny mzunguko ule ule......hakuna panya wakumfunga kengele paka hapo!
 
Utawala wa kijeshi siyo suluhisho kamwe la matatizo ya kidemokrasia; ni uthibitisho wa uwepo wake
 
Ok humo (EPA, RICHMONDULI et al) decision makers wametafuniwa kila kitu at the end nini kimetokea? wamemeet your expectations?
Ndio. EL hakuwa mtu wa kuachia Uwaziri Mkuu mapema hivyo na kwa staili ile; JEETU PATEL hakufikiria hata siku moja angepanda karandinga la Magereza. Angalau tumeanza.
 
Utawala wa kijeshi siyo suluhisho kamwe la matatizo ya kidemokrasia; ni uthibitisho wa uwepo wake

Mwanakijiji,
Maadamu tupo hapa tunaandika maana yake ni kuwa tatizo lipo. Tumeona Thailand jamaa wakimwaga kinyesi nyumbani kwa PM ingawa jamaa alishinda uchaguzi ila jamaa wanasema kuwa "PM alihonga/Kugawa khanga na tshirt kwa Thailand sijui kukoje?"

Kila mtu anafahamu kuwa ukitaka kupasua jipu mapema, unasema hapana linauma. Ila likikubana sawasawa basi mwenye utalilia wakupasue. Mama mmoja alikataa kumyooosha mwanae mkono baada ya kuvunjika. Alikuwa akichemsha maji na kuweka chumvi, akianza kuunyoosha, mtoto analia na yeye analia na mechi inakuwa imekwisha. Sasa hivi yule kijana kawa kilema kwa sababu mkono umepinga kama minazi ya ufukweni mwa bahari kiasi kwamba hawezi kushika wala kunyenyua kitu...... hiyo ni huruma au unyama?
Tukubali tu kuwa tuna jipu na inabidi lipasuliwe
 
Ndio. EL hakuwa mtu wa kuachia Uwaziri Mkuu mapema hivyo na kwa staili ile; JEETU PATEL hakufikiria hata siku moja angepanda karandinga la Magereza. Angalau tumeanza.

Mkuu, huyo EL is like Nyati aliyekwaparuliwa sikio vile....is not finished as many of us do think mkuu! El is still in action, tena anaweza kuwa dangerous more than ever!

Hayo ya kina Jeetul mkuu ni ngonjera tu......hakuna hata hukumu mmoja ilishatolewa kny hayo maskandal mkuu......! hata JK anaweza pandishwa kny Karandinga bt just for show off tu, they don't mean real business mkuu!
 
Mijitu hapa inapiga kelele weeee lakini mwisho wa siku inaipigia kura CCM. Na matatizo ya Tanzania na Afrika sio viongozi wabovu tu. Matatizo yako deeper zaidi ya hilo.
 
Unaamini vyombo hivyo (JF & Bunge) havijafanya kazi hiyo mpaka sasa? Na kama vimeshatoa msaada mkubwa sana, je? unaona kunamwitikio wowote kutoka kwa watoa maamuzi wa kushughulikia taarifa hizo kwa moyo moja? au ni nani hasa anatakiwa apewe hizo taarifa ambaye haja pata hadi sasa? kama sio tutarudi kny mzunguko ule ule......hakuna panya wakumfunga kengele paka hapo!
Mipanya imekuwa mikubwa Paka wamenywea! mipaka...EL and etal. tihi tihi!!
 
Hatuhitaji mwehu wala mjeshi! Tunahitaji mtu mwenye akili timamu kabisa! anayejua na kuona aibu juu ya makosa yake. Lakini cha msingi zaidi, tunahitaji organizesheni ya watu ambao wanaamini katika nguvu ya umma, ambao wao kukucha kukiingia giza wanafikiria kuwakimbiza viongozi mchakamchaka kupitia wananchi na kuwaweka viongozi tumbo joto! Sio zama, za udikteta hizi, ni nafasi za kuangalia majoto ya wananchi yako wapi na kujengea juu yake!
 
Ndiyo, rais mwepesi wa kuchukua hatua pale inapobidi. Tunahitaji yule asiyependa vikao vingi ktk kuyakabili mambo magumu. Yule ambaye kichwa chake ni baraza lake kuu la ushari.Vile vile mwenye jicho la huruma kwa watu wakipato cha chini, na asie pendelea uso wa matajiri bali mtu wa watu na usawa.
 
hapa kijeshi jeshi tu, nashangaa hadi sasa hili jeshi letu bado halijachukua hatua wakati nchi inateketea na mafisadi

Watu waliokuwa wanaenda jeshini i wale waliofeli, ndiyo maana utakuta wanajeshi wetu wanapiga raia kabla ya kupewa nchi, mkuu wakipewa si ndio basi tutapigwa bila sababu.

NAKUBALIANA NA Idea ya jeshi,ila hawa wetu, sijui hata kamawanajua kuna internet , ili wasome JF.

Yaani sijawa convincede bado na uwezo wa jeshi letu katika vitu vingi sana
 
Watu waliokuwa wanaenda jeshini i wale waliofeli, ndiyo maana utakuta wanajeshi wetu wanapiga raia kabla ya kupewa nchi, mkuu wakipewa si ndio basi tutapigwa bila sababu.

NAKUBALIANA NA Idea ya jeshi,ila hawa wetu, sijui hata kamawanajua kuna internet , ili wasome JF.

Yaani sijawa convincede bado na uwezo wa jeshi letu katika vitu vingi sana

Webby,

........hebu rekebisha hilo Mkuu........please
 
Rais mwenye maono ya kuthubutu kama Obama tulishampata, Nyerere, whats more daring and visionary than "Azimio la Arusha"
Mbishi na mbwatukaji kama Ahmedinajad, tushampata, Benjamin William Mkapa ambaye aliwapiga vijembe kina Tony Blair kwenye CHOGM Australia 2001 na kumsifia Mugabe mpaka Blair akampoza kwa kumpa position katika team yake ya Afrika.

Asiyetishiwa na wawekezaji kama Hugo Chavez, Huyu Nyerere, aliyepiga beat kwamba kama wawekezaji hawawezi kufikisha offer ya royalties tunayoitaka tutakaa na madini yetu.

Mwenye kuzungukwa na watu wenye uwezo kama Lula - Yaani wewe hawa corrupt bunch wa Brazil ndio umewaona watu wenye uwezo?

Na mwenye mvuto kwa watu wa kawaida kama Zuma -Huyo babako JK tunaye lakini charisma yake haisaidii chochote, sanasana inatulostisha tu maana watu wanashindwa ku focus kwenye issues wanamuonea haya rais akitabasamu, Nyerere anakwambia kama unamchagua rais kwa haiba nenda kanywe naye chai.

Rais ambaye amefyatuka kidogo (au sana kutegemea na kipimo) ambaye hakupiga magoti kwa kila mtu anayejiita "mwekezaji" na tulikuwa naye, Nyerere alikuwa chizi, literary, na alisema nchi inahitaji "mwehu" ili iendelee.Lakini hata baada ya kuwa na mwehu huyu kama rais kwa miaka ishirini na kitu bado tunasota.

Kufyatuka si tija, tushakuwa na rais fyatu na hakusaidia that much kiuchumi.
 
Mtikila akiwa Raisi nitakuwa wa kwanza kuingia msituni!
 
Ni kwa bahati mbaya sana.

Kwamba Rais kama huyo hatapatikana si tu hapa Tanzania bali popote Duniani!

Mzee Mwanakijiji kweli umekarisika umefika mahali unataka kuumba Rais wako.
 
EH,..........kwani huyu tulienae sasa ni "RAIS" au "RAHISI" au "RICE(kwa maana ya "Ubwabwa" kwa lugha ya ughaibuni)????".......... sijaelewa mjadala huu unaelekea wapi!.......NAOMBA MWONGOZO......
 
Back
Top Bottom