Tanzania inahitaji Rais Fyatu?

Tanzania inahitaji Rais Fyatu?

Wakuu tuache kufikiria tawala za kijeshi.Mimi nadhani tupate raia mmoja tu mzalendo mwenye vision na uchungu wa kweli na maendeleo ya nchi hii.Hawa watu wapo isipokuwa bado hawajapewa nafasi au wanabaniwa au wanavurugwa na system isiyoitakia mema nchi.
Embu tuchukulie mfano tumpe urais Pombe Magufuli leo hii,hivi hatutaweza kusonga kweli?
Utampenyezea wapi Magufuli hadi aupate hata huo UGOMBEA tu? Angalia JK alivyohangaika hata kumpa wizara afanye kazi! Tatizo kubwa tulilonalo ni MFUMO wetu wa jinsi tunavyowapata VIONGOZI wetu. Nani ATAUFUMUA?
 
nadhani iendeshwe kijeshi kwanza ili tuiipate habari yake

Mbona hata sasa ni kama inaendeshwa kijeshi tu! Ona mifano michache hapa :
1. JK (Rais).... Captain wa Jeshi
2. Makamba( Katibu)...Luten wa jeshi
3. Chiligati ( Mwenezi)...Captain wa jeshi
4. Mkuchika ( Naibu Katibu)...Luteni wa jeshi
5.
6.
Na wakuu wa Mikoa na Wilaya kibao!
 
Ndahani

Umenena vyema hapa ni kijeshi jeshi tu ndio tutaenda

Viongozi wetu siku hz sijui wamekuwaje, yaani utadhani hawakwenda Shule

Kila siku huwa nawashauri wawe wanasikiliza zile hotuba za Baba waTaifa mara kwani watajifunza kile alichokuwa akikisema
 
Tunachohitaji ni Chama mbadala wa CCM, haijalishi kitaongozwa na nani!
 
Mbona mnasahau kuwa raisi anawekwa na Watanzania wenye umri wa miaka 18 , ambao wamejiandikisha kupiga kura na wanaojitokeza siku ya uchaguzi kupiga kura. Na vile vile haki hiyo ya kuchagua iwe ya mtu yoyote kugombea bila kujali chama.Hivyo basi mawazo yote mazuri yalitolewa humu yasubiri mwaka kesho siku ambayo nafasi hiyo itatangazwa na tume kuwa wazi na kuruhusu watu wagombee bila kujali chama, hiki ndio kitu cha kushinikiza serikali imesema haigopi wagombea binafsi kama ndivyo waweke ngoma kati sio kukimbilia mahakakani.Tuhimize mgombea binafsi na kururhusu watanzania wote popote walipo wawe na fursa ya kuchagua viongozi wao.
 
Tunahitaji Rais mwenye maono ya kuthubutu kama Obama, mbishi na mbwatukaji kama Ahmedinajad, asiyetishiwa na wawekezaji kama Hugo Chavez, mwenye kuzungukwa na watu wenye uwezo kama Lula na mwenye mvuto kwa watu wa kawaida kama Zuma. Tunahitaji Rais ambaye amefyatuka kidogo (au sana kutegemea na kipimo) ambaye hatopiga magoti kwa kila mtu anayejiita "mwekezaji" na ambaye hatozungukwa na wenye kuimba sifa zake.

Tunahitaji Rais ambaye amefyatuka kama Mrema!!!!!!

Ni katika kuongezea: kati ya hawa nani anaeza imudu nchi yetu hii Sitta au Pinda au Zitto au Mbowe irudi kwenye mstari ulioonyooka?
 
Utampenyezea wapi Magufuli hadi aupate hata huo UGOMBEA tu? Angalia JK alivyohangaika hata kumpa wizara afanye kazi! Tatizo kubwa tulilonalo ni MFUMO wetu wa jinsi tunavyowapata VIONGOZI wetu. Nani ATAUFUMUA?


Ndiyo hapo sasa.Ndiyo mana nikasema wachapakazi wapo sema bado hawajapewa nafasi na wanabaniwa na kuvurugwa kwa sababu za kisiasa.
Magufuli pamoja na mapungufu yake lakini leo hii angepewa wizara ya nishati tu basi mabadiliko tungeanza kuyaona.Kikwete angetaka kauli mbiu yake ya kasi mpya itekelezeke kivitendo basi angempa uwaziri mkuu Magufuli.Wallah miaka hii 5 ya mwanzo tungeona mengi.
 
Sidhani kama tunahitaji mapinduzi ya mabomu. Hayo yameshapitwa na wakati. Tunahitaji mapinduzi ya kiuongozi na kimtazamo. Tunahitaji Rais ambaye ataendeleza vision na mission za taifa letu kwa kasi kubwa. Tunahitaji rais ambaye atayaangalia matatizo ya watanzania na kuyafanyia kazi. Tunahitaji rais anayeweza kuwakemea mawaziri wake wanapofanya upumbavu. rais ambaye anaweza kwenda kwa wananchi na kuomba radhi pale serikali inapokosea na akatekeleza matakwa ya watanzania
 
Sikonge,

Hao wako hoi baada ya kuvimbiwa vibaya! Hakuna tofauti kati ya UWT na Government hapa. Hao UWT wakiona issue unafikiri wanatakiwa kuiripoti wapi?Serikalini kwa JK or kwa MKPP or wapi? unafikir wanapenda kutwanga maji kwenye kinu? nao ni binadamu kama sisi, they got needs vile vile....so nao wanajoin the battle kuwakandamiza wanyonge na kutii kiu ya mabwana na yao pia!

Tena FYI, hivi vijamaa ukikutana navyo huku uswaz vinasumbua sana, vikinywa bia eti vinatoa EUROs au Pound.....! wapi na wapi?

Inasikitisha. Kama wanalipwa bila kazi nayo inazidi kusikitisha. Ila inabidi wakae mkao wa kula na wao maana huwa wakifukuzwa kazi, kazi pekee ni kufungua biashara zake au kufungua Mpelelezi wa kujitegemea ambayo kwa Tz bado ngumu. Hiyo kazi huwa inaisha vibaya kama hukujiandaa mapema. Na kwa hali ilivyo, kama akija kichaa basi hao jama wote watapanguliwa na kuanza upya maana huwezi anza na watu ambao wameshanogewa na visenti vya CCM. Ila ubaya mmoja ni kuwa, wale wenye moyo na ari ya kuifanyia kazi nchi yao, ndiyo wanakuwa frustrated. Unakusanya habari nzuri kuliokoa taifa, ukiipeleka kwa boss unapigwa warning USIRUDIE kuipeleleza hiyo scandal maana ni ya Kigogo fulani.....
 
Hapana! c lazima awe fyatu au mwendawazimu. Awe ni mtu aliye na utashi wa kuthubutu ( kushughulikia mtu yeyote kwa haraka pindi anapofanya uzembe au ubadhirifu bila woga ila kwa kuwekeana mikataba wakati wa kukabidhiwa majukumu), wote mliowataja ni watu walio na misimamo na c fyatu.
 
Tusisahau kwamba ufisadi umeingia hadi JESHINI pia. Akina Mboma, Waitara,...ni matajiri kwelikweli. Labda tuwatafute akina Thomas Sankara mle.....
The guy was my favorite. He did not live long! Blaise Compaore aliyemuua eti leo anaenda kumshawishi Kapten camara wa guinea aachie madaraka. Sijui itawezekanaje
 
Tusisahau kwamba ufisadi umeingia hadi JESHINI pia. Akina Mboma, Waitara,...ni matajiri kwelikweli. Labda tuwatafute akina Thomas Sankara mle.....

Watatumalizaaa. Ni mafisadi wa kupindukia, tena ndio watakua wanaiba waziwazi kwa kisingizio cha amri ya jeshi.
 
Tunahitaji Rais mwenye maono ya kuthubutu kama Obama, mbishi na mbwatukaji kama Ahmedinajad, asiyetishiwa na wawekezaji kama Hugo Chavez, mwenye kuzungukwa na watu wenye uwezo kama Lula na mwenye mvuto kwa watu wa kawaida kama Zuma.

A recipe for disastor
 
......... Ila ubaya mmoja ni kuwa, wale wenye moyo na ari ya kuifanyia kazi nchi yao, ndiyo wanakuwa frustrated. Unakusanya habari nzuri kuliokoa taifa, ukiipeleka kwa boss unapigwa warning USIRUDIE kuipeleleza hiyo scandal maana ni ya Kigogo fulani.....

Sikonge,

Hapo ndio kwenye utata hasa! Tunaolaumu na kujiuliza UWT/TISS wapo wapi ndo tuelewe wazi hapo kny blue, ndio wanapoishia na mishemishe zao zote......! na zaidi waliendelea kuzifuatilia skendal za namna hiyo report inatakiwa waione kwanza vigogo wahusika, kabla ya kuipa go ahead kny hatua zinazofuata kama wataona inawafaa......! tutafika?
 
Inasikitisha. Kama wanalipwa bila kazi nayo inazidi kusikitisha. Ila inabidi wakae mkao wa kula na wao maana huwa wakifukuzwa kazi, kazi pekee ni kufungua biashara zake au kufungua Mpelelezi wa kujitegemea ambayo kwa Tz bado ngumu. Hiyo kazi huwa inaisha vibaya kama hukujiandaa mapema. Na kwa hali ilivyo, kama akija kichaa basi hao jama wote watapanguliwa na kuanza upya maana huwezi anza na watu ambao wameshanogewa na visenti vya CCM. Ila ubaya mmoja ni kuwa, wale wenye moyo na ari ya kuifanyia kazi nchi yao, ndiyo wanakuwa frustrated. Unakusanya habari nzuri kuliokoa taifa, ukiipeleka kwa boss unapigwa warning USIRUDIE kuipeleleza hiyo scandal maana ni ya Kigogo fulani.....
Zipo njia nyingi za kutoa taarifa za kuliokoa TAIFA letu hili. Ipo hii JF na baadhi ya watu humu ambao sio waoga, wapo WABUNGE wasiri na JASIRI sana.
 
Mzee Mwanakijiji,
Taabu ya nini mbona watu Fyatu hao tunao isipokuwa tu tunashindwa kuwaunganisha!...Amini maneno yangu Upinzani wakiungana jeshi hilo linapatikana kabisa - Chadema + CUF + TLP = umepata uongozi huo tatizo ni kwamba wasomi wanaogopa na wanajaribu kutumia vitabu na mzani wa elimu kuwa ndio kipimo halali cha uongozi.... ni Makosa makubwa!
Viongozi tulokuwa nao Chadema, CUF na TLP ndio reflection hasa ya uongozi bora wa Kiafrika. Wanafahamu tulikotoka (Chadema), wanayafahamu matatizo yetu (TLP), wana wivu wa maendeleo (Chadema/CUF) na mwisho UZAWA ni pambano lao la kwanza (CUF)..
Ukiweka vichaa hawa madarakani pamoja, mwaka mmoja tu nchi itanyoooka!
 
Back
Top Bottom