Tanzania Iko Mashakani

Tanzania Iko Mashakani

"Wazee Wa LAWAMA"Dunia nzima inawajua "Reciprocated and brainless MUDY Followers"Dunia nzima hakuna kama ninyi.KUDOS
 
Hivi ni kweli tunataka kuendekeza udini ili tusahau mshikamano wetu kama watanzania.

Kumbukeni silaha ya mnyonge ni umoja(Mwl. Nyerere). Umoja wetu unatakiwa sana ili tupigane bega kwa bega dhidi ya haya matatizo makubwa yanayoikumba nchi yetu kama ufisadi.

Tukianza kua na matabaka mara ooh yule ni muislam ameteuliwa wakiristo wameachwa, au yule mkiristo kwanini amepata?
Sioni kama ni sahihi kuwaza udini maana namna unavyompa cheo shetani ndivyo unavyozidi kumpa nafasi ya kutawala.

Wengine mnaweza kuniona mimi nimepitwa na wakati(outdated) ila kiukweli dini hua hainisumbui kabisaa wala hua sihitaji kujua dini ya mtu wala kuchagua rafiki wa dini flani.

Kama watu watapoteza mshikamano kwa kujadili udini miaka michache ijayo Tanzania itakua imechakaa kama Somalia ilivyokua imechakaa miaka mitatu nyuma.
 
Wapi RASTAFARIANS,HINDUS,BUDHA,KINGUNGE Amkeni MDAI HAKI ZENU NA NINYI.
 
Huyu bibi kila akipanda kwenye " mwezi" network inakata. Msameheni tu anakaribia menopozi.
 
That is st.upid...
Mimi ni Christian lakini nimeangalia CV at least ya CAG huyo mwingine simjui sikuwa na cha kulalamika zaidi ya ku doubt kama ata apply uwezo wake (professionalism) kwenye rotten system...

Mtu akiingiza udini wakati mtu ana CV inasomeka, ni mj.inga tu...na hatutafika mbali tukiwa tumefikia kuwa na hii tabia chafu...

Ndio maana nimesema 'some'
tatizo hao few wanaweza kuwa na influence kwa wengine
labda ni viongozi wa dini au wanasiasa njaa
wewe umeona ni stupid sababu una 'uelewa mkubwa'
sasa jiulize wangapi wanaweza tazama mambo independently...
tatizo la nchii ni 'mass ignorance'...sio hata udini

usisahau hata Marekani kuna ubaguzi wa rangi na dini but mwisho wa siku watu wanajua nini maana ya kuheshimu
maamuzi ya kura..
 
Inakuwa hivyo sababu aliyeko madarakani ni wa dini hiyo...so ukiongea udini huna haja ya kuuliza...kesho akiwa Mkristo kibao kinageuka...kama baadhi ya watu wanavyoandika kuhusu Nyerere...
Kwa hiyo nadhani ni kuwa neutral kwenye ku discuss hili na si kusema kuwa ni dini hii ndio inakuwa victimized ...bali ni tumekosa kuaminiana...sababu hata akiwa mpagani mwisho wa siku tunataka maendeleo kwani hatutakula kwa kuetegemea mshahara wa CAG au AG...

Solution ni kupunguza madaraka ya Rais, na kufanya post nyeti ziwe competitive...am just thinking...
AU tuwe kama wa Malaysia ambao ni taboo kuongelea upendeleo kwa wa Malay hata magazetini...ukiongea hilo tu unatiwa ndani...te te te

Solution mi hilo tu nafasi ziwe za kuchaguliwa
mfano waakuu wa mikoa na wilaya ama zifutwe au zichaguliwe
that way mtu hatatazama Rais kachagua mtu wa dini gani
maamuzi ya wananchi yataheshimiwa
 
Na wanasiasa ni watu selfish sana ...kadi zikiwaishia wanatumia kadi za kigaidi...udini na ukabila...yani hii ni silaa mbaya sana angalia Kenya na Rwanda (Ukabila) Nigeria (udini) these people will never see peace...maana hii sumu ni ngumu kuitoa hata kwa maziwa ya punda...

Wananchi wa kawaida wa hizi nchi ni very innocent ila kwa kutokuwa na ufahamu wanatumiwa na wanasiasa kujinufaisha wao kwa kubaki madarakani au kupata madaraka

Fuatlia kesi ya Kenya the Hague utagundua hao watu wachache wanavyoweza sababisha mauaji makubwa
wananchi hawana udini but what if ukiingia kanisani au msikitini ukute mnaelekezwa nani wa kumchagua?
watu wachache wanaweza nunua media kama Kenya na Rwanda
au kununua viongozi wa dini.....halafu the rest ikawa history.....

so hata kama general population hakuna udini...the threat is very real
sababu general population linaweza kuvurugwa na media au watu wengine wenye influence....

mimi uchaguzi uliopita nilimpigia kura DK Slaa but nawajua watu ambao 'walitishwa' kumchagua kwa kuwa tu alikuwa padri zamani....go figure......
 
Mkuu haya mambo tunayakuza tu bila sababu yoyote.... Sijaona kwa Kikwete kuwa Rais amewafaidisha nini waislam mpaka wamtete. Kikwete yupo kwa maslahi yake binafsi , familia yake,maswahiba zake na chama chake CCM.
Hapa tutatoana ngeu lakini hamna cha maana tunachokipata.
Sijaona ni kwa namna gani CAG au AG kuwa mkristo au muislam kunawafaidisha vipi wakristo au waislam.
Anyway kwani naona ndiyo njia tunayoichagua watanzania.

tazama vizuri nimesema 'some people'
mfano wewe ni CHADEMA i am sure umewahi soma post za Yerricko Nyerere humu
akitukana waislam waziwazi...kuna post aliwahi sema humu Kikwete ndo Rais wa mwisho muislam
sijaona hata nyinyi CHADEMA wenzie mkilaani post hizo badala yake atajibiwa na wale wanaonekana ni kuwa
ni waislam...wakati kisiasa mtu akiwa wrong tunapaswa kumkataa wote regardless ya dini zetu..
 
Kwa mtaji huo, ina maana uchaguzi wa mwakani mgombea wa CCM lazima awe Mkristo la sivyo kitanuka?

*Nimetaja mgombea wa CCM kwa sababu huyo ndo atakayeshinda uchaguzi*

kuna watu wengi including Pasco wameshawahi kusema CCM wana 'unwritten rule'
ya kubadili Rais kwa kuangalia Dini.......akitoka muislam anakuja mkristo hivyo hivyo
sasa this time ikitokea akaja tena muislam no one knows reaction itakuaje...
hata kama ndie wananchi wanamtaka..
 
Last edited by a moderator:
Nimesoma hii post na kujikuta napatwa na Ghadhabu juu yako, lakini ngoja nitulize presaha ili nisiharibu hali ya hewa. Faiza wewe ni Celeb hapa JF unajulikana Kuanzia chama chako dini yako mpka wengine wanajua unapoishi, napata shaka sana na kile unacho kitafuta unapoanzisha mada za kuwachokonoa watu watoe hoja kuwa waislamu na uislamu ndio chanzo cha udini.

Samahani kama nitakuwa nakutusi lakini kama nitakuwa nimeeleweshwa vizuri hizi ndio Ashki zenyewe, tena tunaweza kuziita Ashki majinun za udini. Faiza umeona wiki inataka kukatika watu hawajafungua thread za kibaguzi, za kuchochea udini wala hawajafungua thread za kusema Waislamu magaidi, waislamu wadini, mtoto wa kike Ashki zimekushika unaanza kuleta tafakuri gombanishi.

Hii post yako inataka watu waseme Uislamu ndio Udini, Je wakina kahatan watakaa kimya na kukuacha uichafue imani yao? Leo umeamua kuandika post kwa intelijence ya primary, so sorry. Na Watu hapa JF Wameamka hakuna jinsi ya kupata unacho kitaka kwenye mjadala wako huu.

Kama unatamani kuona watu wakitupiana maneno, kwamba waislamu wadini na wengine warushe maneno waislamu wadini basi umeula wa chuya. Nenda Kenya au Nigeria Hapa Bongo Hizo Ashki zitakuua.

Mods nawaomba huyu dada apigwe Ban kila atakapokuwa analeta mada za aina hii na kila atakapo kuwa anapost coments za kidini ili tupunguze hili tatizo hapa jukwaani JF isijekutumika vibaya kuharibu Taifa letu.

Mwisho nasema Ashki ni kilema. ukiwa ashki majnun wa kupigana, basi utatafuta mtu na kumwambia, "wewe huna nguvu za kupigana na mimi", akipanik na kukuvaa. basi umetibiwa Ashki.
 
Last edited by a moderator:
Weka "context" hiyo ni aya nzuri sana kwa mwenye kufikiri. Ngoja nikusaidia kuiweka kama ilivyo halafu uisome vizuri.

Qur'an 5:51. Enyi mlio amini! Msiwafanye Mayahudi na Wakristo kuwa ni marafiki. Wao ni marafiki wao kwa wao. Na miongoni mwenu mwenye kufanya urafiki nao, basi huyo ni katika wao. Hakika Mwenyezi Mungu hawaongoi watu wenye kudhulumu. ***


Qur'an 5:52. Utawaona wale wenye maradhi nyoyoni mwao wanakimbilia kwao wakisema: Tunakhofu yasitusibu mabadiliko. Huenda Mwenyezi Mungu akaleta ushindi au jambo jingine litokalo kwake wakawa wenye kujuta kwa waliyo yaficha katika nafsi zao. ***

Hiyo context iko wapi ? Zipo aya nyingi ambazo ni za udini perse na ndizo IS, Alshabaab ,Alqaeda et al. Wanazitumia lakini dunia kwa unafiki inalaumu IS et al. Na kujifanya hawajui IS wanamtumikia mungu wao ....
 
Kusema kweli waisilamu tuseme kweli tu dini yetu inatufundisha kuwa wakristo ni makafiri tu na awapaswi kuongoza waslamu. Tazama yanayofanywa na kundi la ISis huko iraq ndio utajua. Mimi kweli naogopa sana kama tutajikuta kama nchi tumeanza kugwanyika kidini balaa lake ni kubwa.

Yeyote anaekufuru ni kafir.
 
Nimesoma hii post na kujikuta napatwa na Ghadhabu juu yako, lakini ngoja nitulize presaha ili nisiharibu hali ya hewa. Faiza wewe ni Celeb hapa JF unajulikana Kuanzia chama chako dini yako mpka wengine wanajua unapoishi, napata shaka sana na kile unacho kitafuta unapoanzisha mada za kuwachokonoa watu watoe hoja kuwa waislamu na uislamu ndio chanzo cha udini.

Samahani kama nitakuwa nakutusi lakini kama nitakuwa nimeeleweshwa vizuri hizi ndio Ashki zenyewe, tena tunaweza kuziita Ashki majinun za udini. Faiza umeona wiki inataka kukatika watu hawajafungua thread za kibaguzi, za kuchochea udini wala hawajafungua thread za kusema Waislamu magaidi, waislamu wadini, mtoto wa kike Ashki zimekushika unaanza kuleta tafakuri gombanishi.

Hii post yako inataka watu waseme Uislamu ndio Udini, Je wakina kahatan watakaa kimya na kukuacha uichafue imani yao? Leo umeamua kuandika post kwa intelijence ya primary, so sorry. Na Watu hapa JF Wameamka hakuna jinsi ya kupata unacho kitaka kwenye mjadala wako huu.

Kama unatamani kuona watu wakitupiana maneno, kwamba waislamu wadini na wengine warushe maneno waislamu wadini basi umeula wa chuya. Nenda Kenya au Nigeria Hapa Bongo Hizo Ashki zitakuua.

Mods nawaomba huyu dada apigwe Ban kila atakapokuwa analeta mada za aina hii na kila atakapo kuwa anapost coments za kidini ili tupunguze hili tatizo hapa jukwaani JF isijekutumika vibaya kuharibu Taifa letu.

Mwisho nasema Ashki ni kilema. ukiwa ashki majnun wa kupigana, basi utatafuta mtu na kumwambia, "wewe huna nguvu za kupigana na mimi", akipanik na kukuvaa. basi umetibiwa Ashki.


Yale yale sasa unayafanya
swali je hizi issue za udini zipo au hazipo?
je akiongelea mtu mwingine mfano Pasco....hakuna shida?
but akiongelea Faizafoxy zinakuwa ni tatizo?
naona unapinga udini kwa kutumia udini.....
 
Last edited by a moderator:
Kete ya udini ilikuwa muhimu sana kwa CCM mwaka 2010 ili waweze kushinda uchaguzi. Iliwahi kutumiwa kabla dhidi ya CUF, lakin 2010 ikawa reloaded! Ikumbukwe kwamba, ukiacha Nyerere; hakuna rais mwingine ambaye amewahi kuingia madarakani kwa mtaji mkubwa wa kisiasa kama Kikwete (80% ya kura). Watu wote walimpenda, waweza kusema wakristo walimpenda zaidi-hata Kilaini akasema ni chaguo la Mungu.

Shida ikaj baada ya kuiuzulu kwa Lowassa. Kwa maoni yangu, Lowassa alikuwa ngao ya udhaifu wa Kikwete. Lowassa alikuwa na nguvu kisiasa tofautia Pinda. Pinda mtu wa kutumwa. Baada ya kupwaya kwa serikali, wananchi wakawa wanatafuta mbadala. Slaa akajitokeza kugombea urais and the rest is history!

Uchochezi wa kidin umetumika makusudi kumbakiza Kikwete madarakan. Binafsi naamin angeweza kushinda bila hili, japo kwa asilimia chache zaid. Udin umeanzishwa, umelelewa na kukuzwa na vyombo vya dola na CCM. Ktk suala la kuchinja ng'ombe na kukojolea Quran, lilikuwa lilikuwa limeshabalehe. Kabla ya hapo, wakristo hawajawah kuwa wamoja ktk maslahi yao. Mazingira yamewaunganisha na sasa ni wamoja zaid. Nao wamejifunza kulialia, kulalamika na kushuku mambo (wakati mwingne bila sababu ya msingi). Waislam wamejifunza kuwa wakristo nao wana grievances zao japo hawakuwa kudai hapo kabla(wangependa na wao wachinje wanyama).

Funzo: Hakuna mshind kwenye chuki na uchochezi wa kidini. Serikali iache kutumia dini ktk masuala ya utawala na uongozi. Pia Islamization na Christianization zisitumie resources za serikali. Dini ziikabe serikal, zisikabane.
 
Weka "context" hiyo ni aya nzuri sana kwa mwenye kufikiri. Ngoja nikusaidia kuiweka kama ilivyo halafu uisome vizuri.

Qur'an 5:51. Enyi mlio amini! Msiwafanye Mayahudi na Wakristo kuwa ni marafiki. Wao ni marafiki wao kwa wao. Na miongoni mwenu mwenye kufanya urafiki nao, basi huyo ni katika wao. Hakika Mwenyezi Mungu hawaongoi watu wenye kudhulumu. ***


Qur'an 5:52. Utawaona wale wenye maradhi nyoyoni mwao wanakimbilia kwao wakisema: Tunakhofu yasitusibu mabadiliko. Huenda Mwenyezi Mungu akaleta ushindi au jambo jingine litokalo kwake wakawa wenye kujuta kwa waliyo yaficha katika nafsi zao. ***

Hiyo context iko wapi ? Zipo aya nyingi ambazo ni za udini perse na ndizo IS, Alshabaab ,Alqaeda et al. Wanazitumia lakini dunia kwa unafiki inalaumu IS et al. Na kujifanya hawajui IS wanamtumikia mungu wao ....

Faiza Watanzania tumekuwa na amani miaka yote kwasababu Hiyo Aya Imetafsiriwa kama ifatavyo:

Muislamu hatakiwi kumfanya rafiki mkristo kwa maana ya kumshirikiana naye kwenye mambo ambayo kwenye uislamu ni dhambi, Mkristo akila nguluwe usimfanye rafiki, mkristo akijihusisha na ushoga usimfanye rafiki kwenye ushoga wake usiungane naye. Hivi we usisaidiwe kufikiria na Al-shabaab, we hujiulizi kama ukimtenga mkristo utamsaidiaje kuijua haki, utamfundishaje ili aijue Batil, Tuache Imani za kibaguzi zitabomoa taifa letu. tusibomoe nyumba tunayoishi wote
 
kuna watu wengi including Pasco wameshawahi kusema CCM wana 'unwritten rule'
ya kubadili Rais kwa kuangalia Dini.......akitoka muislam anakuja mkristo hivyo hivyo
sasa this time ikitokea akaja tena muislam no one knows reaction itakuaje...
hata kama ndie wananchi wanamtaka..
Sumu ya Siasa za Udini, Ukanda na Ukabila, "Is It Real? au ni Dhana tuu?!.
Wanabodi nauliza, hii sumu ya siasa za udini, ukabila na ukanda are they real au ni dhana tuu?!.

Jee Watanzania si wana dini zao?, jee kuna ubishi kuwa alipoanza rais Mkristu, JK Nyerere, alipoondoka Mwinyi aliingia tuu by chance?. No miongoni mwa sababu za Mwinyi kuingia ni pamoja na dini yake, this is a fact!. Alipoondoka Mwinyi sialiingia Ben, inamaana aliingia tuu by a mare chance and by chance akawa ni Mkiristu na alipotoka JK nae akaingia by mare chance, na by chance akawa ni Mwislam?. Tutake tusitake, kuna kupokezana hata kama ni by chance, then tuendelee ku play by chance?. Kwenye uchaguzi uliopita kuna vyama vilipata kura nyingi maeneo ya dini fulani, and this is a fact!. Kuna taasisi na makundi ya watu wali waendorse wagombea fulani kutokana na dini zao!. This is fact!. Jee hii ni dhana ya udini tuu au ndio ukweli wenyewe?

Hii dhambi ya mbegu ya sumu ya siasa za udini, ukabila na ukanda, zimepandwa na CCM, zimelelewa na CCM na hatimaye 2015, CCM itavuna ilichopanda!.

Jee mbegu hii ya sumu kaipanda nani?, jee tunaweza kuipiga vita kwa kuikanusha tuu (denial) au tunatakiwa kuubali ukweli mchungu na kukabiliana nao (facing the problem)!.

Nauliza tuu?

Pasco

Pia nilishauri mahali, kuwa we have to break this thing!.
Japo hakuna kupokezana: Kiukweli, kihaki, kihalali na kimuungano, 2015 ni zamu ya Mzanzibari!!.
Wanabodi,

Nauliza, Jee CCM itawatendea haki Watanzania kwa kuwasimamishia mgombea kutoka Zanzibar?! au itaendelea kupandikiza sumu ya udini kwa ku bow down kwenye the fact and fallacy ya zamu za kupokezana kwa dini?!.

Is in not
Kiukweli kabisa, Kihaki kabisa, Kihalali kabisa na kwa lengo la kudumisha, Muungano, 2015 ni Zamu halali ya Zanzibar kutupatia Rais wa JMT?!.

Pasco

 
Back
Top Bottom