Tanzania Iko Mashakani

Tanzania Iko Mashakani

Mkuu Kikwete aliyasikia yaliyosemwa na Lukuvi na huyu muanzisha huu alianzisha uzi hapa kumtaka Kikwete amwajibishe Lukuvi lakini hakufanya hivyo. MACCM ni wanafiki wakubwa wanatumia "Divide and conquer" ili kuendelea kubaki madarakani huku wakijua fika kwamba wanapotoa kauli kwamba CUF ni chama cha waislamu hivyo wakristo wengi hawatakuwa tayari kuwapigia wagombea wa CUF, vivyo hivyo wanaposema Chadema ni chama cha wakristo basi waislamu wengi hawatakuwa tayari kuwapigia kura wagombea wa Chadema na hii ndo sababu kubwa kuna MACCM yanahangaika sana kutafuta namna ya kuleta mtafaruku ndani ya UKAWA kwa sababu unafiki wao wa udini waliokuwa wakiutumia dhidi ya vyama hivi viwili hawataweza kuutumia tena.



https://www.jamiiforums.com/katiba-...lliam-lukuvi-ameutia-dosari-utawala-wako.html

Mkuu tukijadili mtu mmmoja mmoja itakuwa taabu sana. Muhimu ni kuwa wakristo na waislamu wameendelea kuishi kwa pamoja kwa maelfu ya miaka pamoja na changamoto zilizowahi kutokea. Mfano chama kinachotuhumiwa kwa kuingiza na kuulea mfumokristo sio chadema ni ccm. Dhulma wanaothibitisha kufanyiwa waislamu ni toka CCM na sio chadema. Hivyo maneno ya mtu mmoja au kikundi cha watu hayawezi kuwa generalized vinginevyo utajibu vipi maneno ya waziri na kiongozi mwenye dhamana ya uwaziri kama lukuvi na maneno alotoa kanisani? Je ndio msimamo wa ccm na kanisa?
 
Naam, Tanzania iko mashakani.

Kwa nini?

Ni ukweli usiopingika, leo hii Tanzania tuko mashakani kama nchi.

Ukweli usemwe na ubaki kuwa ukweli.

Tanzania tuko mashakani kwa sababu moja tu. Udini.

Nini maana ya "udini", jibu ni sahali sana. Kwa hakika hakuna zaidi, hakuna asiye Muislaam ambae ni mdini. Udini ni Uislam na Wadini ni Waislaam.

Aje mmoja kupinga hilo.

Mengi tutayaongea wakati mjadala unaendelea na yatabainika.

FaizaFoxy ustake kukuza mambo hizi ishu za udini mnaziongelea kinadharia tu huku mtaani watu hawana mpango na hawajui tu kama kuna hayo mambo ya udini tuna shirikiana kwa 100%.
 
Last edited by a moderator:
The boss mimi nadhani hoja ni vigezo, kama wamekidhi vigezo hakuna haja ya majungu. Sema watu wanataka kutumia hii kwa maslahi yao binafsi.

Tushaanza kubaguana wenyewe kwa wenyewe.ndo mana Mimi mtu akiniuliza kuwa mm dini au kabila langu huwa namjibu kuwa Mimi ni Mtanzania.
 
Last edited by a moderator:
.. FaizaFoxy nakuja kuweka sawa mada yako hiyo ya udini.......loading
 
Last edited by a moderator:
Mimi nilijua baada ya Kikwete kuteua waislam wawili mfululizo tu italeta shida
tulipokuwa na CAG na AG wakristo haikuwa shida.....now hizo pisition zimekuwa replaced na waislam...
some people cant hide their unhappiness......

Mkuu haya mambo tunayakuza tu bila sababu yoyote.... Sijaona kwa Kikwete kuwa Rais amewafaidisha nini waislam mpaka wamtete. Kikwete yupo kwa maslahi yake binafsi , familia yake,maswahiba zake na chama chake CCM.
Hapa tutatoana ngeu lakini hamna cha maana tunachokipata.
Sijaona ni kwa namna gani CAG au AG kuwa mkristo au muislam kunawafaidisha vipi wakristo au waislam.
Anyway kwani naona ndiyo njia tunayoichagua watanzania.
 
Kuna wale Boko Haram pia kule Nigeria kuna Al Shabab kule Somalia ambao wamefanya mauaji ya kutisha Kenya kwa kuwalenga wale ambao si Waislamu.
Mkuu na wewe usiniangushe kwa kuingia kwenye huo mtego wa kuhubiri udini na kuwaacha maadui ujinga, umasikini , maradhi na baba yao ccm.
Hayo makundi uliyoyataja ni ya kigaidi, yakifanya mashambulizi yao hayaulizi mkristo nani au muislam nani.
Halafu hata hao viongozi wa ccm awe mkristo , awe muislam lao moja tu kuangalia maslahi yao binafsi na chama chao cha kifisadi.
Hao watu nafsi zao kwanza na chama hakuna cha dini wala nini.
Just think.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Mimi nilijua baada ya Kikwete kuteua waislam wawili mfululizo tu italeta shida
tulipokuwa na CAG na AG wakristo haikuwa shida.....now hizo pisition zimekuwa replaced na waislam...
some people cant hide their unhappiness......
That is st.upid...
Mimi ni Christian lakini nimeangalia CV at least ya CAG huyo mwingine simjui sikuwa na cha kulalamika zaidi ya ku doubt kama ata apply uwezo wake (professionalism) kwenye rotten system...

Mtu akiingiza udini wakati mtu ana CV inasomeka, ni mj.inga tu...na hatutafika mbali tukiwa tumefikia kuwa na hii tabia chafu...
 
Tanzania iko mashakani kweli.

Tanzania iko mashakani kwa kuwa haina uongozi mathubuti. Haina uongozi unaoeleweka na wenye msimamo.

Tanzania iko mashakani kwa kuwa inaendeshwa na genge la wevi wanaojiita serikali. Genge la wauaji wanaojiita serikali. Genge la watu wasio na maadili wala soni wanaojiita serikali.

Tatizo la Tanzania siyo dini, kwa kuwa dini haina mwenyewe. Tatizo la Tanzania ni wizi, ufisadi, kukosa maadili na kushindwa kuwajibika.

Wizi hauna dini. Andrew na Mrisho wanashirikiana kuiba. Edward na Aziz pia, bila kusahau Anna, Sospeter, James na Sethi wakisaidiwa na Frederick na Mrisho. Urais hauna ubia lakini wizi na ufisadi una ubia kiasi kwamba mfanyabiashara Seth/PAP anakuwa na nguvu ya kuaimbia Mahakama nini iseme kwa Bunge La Jamhuri na hata kwa Raisi wa Jamhuri katika kufanya kazi zake.

Tanzania iko mashakani na ni mashaka makubwa. Mungu wa dini yo yote na aisaidie Tanzania katika mashaka hayo.
 
Kweli kabisa huo udini ndiyo mada iliyopo, na mimi naamini, ukitajwa "udini" basi ni Uislam, na wakitajwa "wadini" basi bila shaka ni Waislaam.

Naomba nipinge katika hilo au nieleimishe na unioneshe ni nani "mdini" Tanzania hii zaidi ya Muislam.

Inakuwa hivyo sababu aliyeko madarakani ni wa dini hiyo...so ukiongea udini huna haja ya kuuliza...kesho akiwa Mkristo kibao kinageuka...kama baadhi ya watu wanavyoandika kuhusu Nyerere...
Kwa hiyo nadhani ni kuwa neutral kwenye ku discuss hili na si kusema kuwa ni dini hii ndio inakuwa victimized ...bali ni tumekosa kuaminiana...sababu hata akiwa mpagani mwisho wa siku tunataka maendeleo kwani hatutakula kwa kuetegemea mshahara wa CAG au AG...

Solution ni kupunguza madaraka ya Rais, na kufanya post nyeti ziwe competitive...am just thinking...
AU tuwe kama wa Malaysia ambao ni taboo kuongelea upendeleo kwa wa Malay hata magazetini...ukiongea hilo tu unatiwa ndani...te te te
 
.. FaizaFoxy wizara nyeti zote zineshikiliwa na waislam ujue......fedha, usalama wa taifa, elimu, afya..... etc
tatizo nn kwani?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu kamwe siwezi kuingia kwenye huu upumbavu wa kutaka kutumia tofauti ya dini zetu kupandikiza chuki miongoni mwetu, lakini Mkuu pale penye kasoro tusikae kimya. Utamwitaje mwenzio kafiri kwa sababu tu ya tofauti za kidini? Huyu ni binadamu mwenzio ambaye ukianguka anaweza kukusitiri na kukupa msaada wa kila aina ili akusaidie binadamu mwenzie. Napinga kwa nguvu zote jitihada za wachache ambao wanataka kupandikiza udini nchini ili wanufaike nao na hivyo kuendelea kubaki madarakani. Adui wetu mkubwa Tanzania ambaye anasababisha Watanzania wengi kuishi katika maisha ya ufukara mkubwa ni MACCM hawa ndio adui zetu ambao inabidi tupambane nao kwa kila hali na ili kufanikiwa dhidi ya adui huyu mkubwa wa Watanzania. Waumini wa dini zote hizi kubwa mbili inabidi kusimama bega kwa bega kupambana kwa dhati dhidi ya hawa wahuni, mafisadi, wauza unga, majangili na magaidi.

Tunaona maafa makubwa yanayotokea Nigeria yanayosababishwa na udini, kamwe tusiwape nafasi wale wenye nia mbaya ya kutaka kuleta chuki nchini kwa kutumia tofauti zetu za kidini nchi yetu ikawa kama Nigeria.


Mkuu na wewe usiniangushe kwa kuingia kwenye huo mtego wa kuhubiri udini na kuwaacha maadui ujinga, umasikini , maradhi na baba yao ccm.
Hayo makundi uliyoyataja ni ya kigaidi, yakifanya mashambulizi yao hayaulizi mkristo nani au muislam nani.
Halafu hata hao viongozi wa ccm awe mkristo , awe muislam lao moja tu kuangalia maslahi yao binafsi na chama chao cha kifisadi.
Hao watu nafsi zao kwanza na chama hakuna cha dini wala nini.
Just think.
 
:yo: :yo: :yo: THANK YOU nyumba kubwa

Inakuwa hivyo sababu aliyeko madarakani ni wa dini hiyo...so ukiongea udini huna haja ya kuuliza...kesho akiwa Mkristo kibao kinageuka...kama baadhi ya watu wanavyoandika kuhusu Nyerere...
Kwa hiyo nadhani ni kuwa neutral kwenye ku discuss hili na si kusema kuwa ni dini hii ndio inakuwa victimized ...bali ni tumekosa kuaminiana...sababu hata akiwa mpagani mwisho wa siku tunataka maendeleo kwani hatutakula kwa kuetegemea mshahara wa CAG au AG...

Solution ni kupunguza madaraka ya Rais, na kufanya post nyeti ziwe competitive...am just thinking...
AU tuwe kama wa Malaysia ambao ni taboo kuongelea upendeleo kwa wa Malay hata magazetini...ukiongea hilo tu unatiwa ndani...te te te
 
Last edited by a moderator:
Mkuu kamwe siwezi kuingia kwenye huu upumbavu wa kutaka kutumia tofauti ya dini zetu kupandikiza chuki miongoni mwetu, lakini Mkuu pale penye kasoro tusikae kimya. Utamwitaje mwenzio kafiri kwa sababu tu ya tofauti za kidini? Huyu ni binadamu mwenzio ambaye ukianguka anaweza kukusitiri na kukupa msaada wa kila aina ili akusaidie binadamu mwenzie. Napinga kwa nguvu zote jitihada za wachache ambao wanataka kupandikiza udini nchini ili wanufaike nao na hivyo kuendelea kubaki madarakani. Adui wetu mkubwa Tanzania ambaye anasababisha Watanzania wengi kuishi katika maisha ya ufukara mkubwa ni MACCM hawa ndio adui zetu ambao inabidi tupambane nao kwa kila hali na ili kufanikiwa dhidi ya adui huyu mkubwa wa Watanzania. Waumini wa dini zote hizi kubwa mbili inabidi kusimama bega kwa bega kupambana kwa dhati dhidi ya hawa wahuni, mafisadi, wauza unga, majangili na magaidi.

Tunaona maafa makubwa yanayotokea Nigeria yanayosababishwa na udini, kamwe tusiwape nafasi wale wenye nia mbaya ya kutaka kuleta chuki nchini kwa kutumia tofauti zetu za kidini nchi yetu ikawa kama Nigeria.

Na wanasiasa ni watu selfish sana ...kadi zikiwaishia wanatumia kadi za kigaidi...udini na ukabila...yani hii ni silaa mbaya sana angalia Kenya na Rwanda (Ukabila) Nigeria (udini) these people will never see peace...maana hii sumu ni ngumu kuitoa hata kwa maziwa ya punda...

Wananchi wa kawaida wa hizi nchi ni very innocent ila kwa kutokuwa na ufahamu wanatumiwa na wanasiasa kujinufaisha wao kwa kubaki madarakani au kupata madaraka
 
nashangaa mnaotoleana roho kwa dini zilozokuja na mashua na viboko mkachapwa.

Hakuna aja ya kuvutana kwa dini kila mtu ataubeba mzigo wake mwenyewe na utaukumiwa kwa matendo si dini
 
pamoja na hayo bado waislamu wanategemea kupata mahakama yao ya kazi mwezi wa pili kama ilivyohadiwa na waziri mkuu Pinda,la sivyo watalinukisha
 
nashangaa mnaotoleana roho kwa dini zilozokuja na mashua na viboko mkachapwa.

Hakuna aja ya kuvutana kwa dini kila mtu ataubeba mzigo wake mwenyewe na utaukumiwa kwa matendo si dini

humu jamvini magaidi ni wengi sana.
 
Back
Top Bottom