Kete ya udini ilikuwa muhimu sana kwa CCM mwaka 2010 ili waweze kushinda uchaguzi. Iliwahi kutumiwa kabla dhidi ya CUF, lakin 2010 ikawa reloaded! Ikumbukwe kwamba, ukiacha Nyerere; hakuna rais mwingine ambaye amewahi kuingia madarakani kwa mtaji mkubwa wa kisiasa kama Kikwete (80% ya kura). Watu wote walimpenda, waweza kusema wakristo walimpenda zaidi-hata Kilaini akasema ni chaguo la Mungu.
Shida ikaj baada ya kuiuzulu kwa Lowassa. Kwa maoni yangu, Lowassa alikuwa ngao ya udhaifu wa Kikwete. Lowassa alikuwa na nguvu kisiasa tofautia Pinda. Pinda mtu wa kutumwa. Baada ya kupwaya kwa serikali, wananchi wakawa wanatafuta mbadala. Slaa akajitokeza kugombea urais and the rest is history!
Uchochezi wa kidin umetumika makusudi kumbakiza Kikwete madarakan. Binafsi naamin angeweza kushinda bila hili, japo kwa asilimia chache zaid. Udin umeanzishwa, umelelewa na kukuzwa na vyombo vya dola na CCM. Ktk suala la kuchinja ng'ombe na kukojolea Quran, lilikuwa lilikuwa limeshabalehe. Kabla ya hapo, wakristo hawajawah kuwa wamoja ktk maslahi yao. Mazingira yamewaunganisha na sasa ni wamoja zaid. Nao wamejifunza kulialia, kulalamika na kushuku mambo (wakati mwingne bila sababu ya msingi). Waislam wamejifunza kuwa wakristo nao wana grievances zao japo hawakuwa kudai hapo kabla(wangependa na wao wachinje wanyama).
Funzo: Hakuna mshind kwenye chuki na uchochezi wa kidini. Serikali iache kutumia dini ktk masuala ya utawala na uongozi. Pia Islamization na Christianization zisitumie resources za serikali. Dini ziikabe serikal, zisikabane.