Mwana wa Mungu
JF-Expert Member
- Aug 14, 2008
- 1,003
- 83
Kitu cha kuelewa hapa, ni kwamba, sio kwamba Mengi kawasha Moto. unajua watanzania wengi hatujui ni nani hasa mafisadi na nani sio mafisadi. kitu ambacho napenda kuwahakikishia leo hii ni kwamba, kilio cha watanzania kimefika mbele za Mungu, machozi yao yamesikiwa, na Mungu atatumia mtu yoyote yule hata kama sio mengi au kama ni mengi sisi hatujui, Mungu atawafichua mafisadi wote ili nchi yetu iwe na haki.
Masikini mara nyingi huwa hawana mtetezi hapa duniani, mtetezi wetu ni Mungu peke yetu. tunaposema mafisadi ni wabaya, huo ubaya anaeuona zaidi ni masikini, wagonjwa, watu wa kipato cha chini nk. hawa ndo wanajua kinachoongelewa kwasababu maisha kwao ni magumu sana, HELA ZINAZOIBWA ZINGEWEZA KUWAPUNGUZIA MACHUNGU HAYO YOTE.
Mungu ameinuka kuwatetea watanzania, na muda si mrefu, Mungu atawafichua mafisadi wote tanzania, na hata kama wengine wanaonekana kama ni mafisadi marafiki wanaoungana kupambana na wapigania haki, Mungu atawagombanisha walane wao kwa wao muda si mrefu. macho ni yetu tutakapouona wokovu wa Mungu kwa macho yetu ya nyama. Mungu ibariki Tanzania. amin.
Masikini mara nyingi huwa hawana mtetezi hapa duniani, mtetezi wetu ni Mungu peke yetu. tunaposema mafisadi ni wabaya, huo ubaya anaeuona zaidi ni masikini, wagonjwa, watu wa kipato cha chini nk. hawa ndo wanajua kinachoongelewa kwasababu maisha kwao ni magumu sana, HELA ZINAZOIBWA ZINGEWEZA KUWAPUNGUZIA MACHUNGU HAYO YOTE.
Mungu ameinuka kuwatetea watanzania, na muda si mrefu, Mungu atawafichua mafisadi wote tanzania, na hata kama wengine wanaonekana kama ni mafisadi marafiki wanaoungana kupambana na wapigania haki, Mungu atawagombanisha walane wao kwa wao muda si mrefu. macho ni yetu tutakapouona wokovu wa Mungu kwa macho yetu ya nyama. Mungu ibariki Tanzania. amin.