Mbeya: Wakili Mwabukusi, Nyagali Mdude na Waandishi wa Habari wakamatwa na Polisi

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,978
141,994
Wakili Boniface Mwabukusi na mwanaharakati Mdude_Nyagali ambao walikuwa na mkutano na waandishi wa habari leo jijini Mbeya wamekamatwa na jeshi la polisi.

Wawili hao walikuwa wakizungumzia maandalizi ya maandamano ya kupinga mkataba wa bandari na madai ya kupatikana kwa katiba mpya. ambapo mara baada ya mkutano na waandishi wa habari, jeshi la polisi lilifika na kuwakamata wazungumzaji hao pamoja na waandishi wa habari wanne.

Habari za hivi sasa zinaeleza, hao wote waliokamafwa wamefikishwa katika kituo kikuu cha polisi Mbeya ofisi ya Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa wa Mbeya.

Wakili Boniface Mwabukusi na mwanaharakati Mdude_Nyagali wamekuwa wakipinga mkataba wa bandari na kufikia hatua ya kuitisha maandamano kupinga mkataba huo.

Waandishi wa habari waliokamatwa ni Ipyana Samson, Ahadi Mtweve, Isack Kyando nami Josea Sinkala.

Itakumbukwa Oktoba 22, 2023 katika Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma mikataba mitatu ya uwekezaji na uendelezaji wa bandari ya Dar es Salaam lisainiwa kati ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) na Kampuni ya DP World mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Rais Samia Suluhu Hassan

Chanzo: Jambo TV
 
Vijana wanakosa ajira,wamama wajawazito wanakufa kwa kukosa huduma bora za afya,umeme tatizo,miundombinu hovyo,kodi wahuni wanatafuna kila siku.

Vijana wa nchi msiwachekee hawa wahuni.
 
Mwabukusi alifanya kazi nzuri kwenye kesi ya bandari. Ila naona alinogewa na publicity hadi amenza kuharibu.
Ameharibu wapi?

Zile demand zao tatu kwanini wanaandamana umeziona?

Kama umeziona, umeona yoyote isiyo na maana pale? Kama ndio tuambie ni ipi, na kwanini unaona haina maana?

Ukishindwa kujibu kwa ufasaha hayo maswali, ukubali ulichoandika pale juu hakina maana.
 
Hao akina Mdude na dr. slaa hawana intelligensia ya kujua kuwa hamna mtu ata andamana?

naona wana subiri polisi waje sehemu za maandamani halafu waje waseme polisi wame andamana kwa niaba yao.

nchi hii ni ngumu ku organise maandamani bila platform either dini au chama cha siasa.
 
Hao akina Mdude na dr. slaa hawana intelligensia ya kujua kuwa hamna mtu ata andamana?

naona wana subiri polisi waje sehemu za maandamani halafu waje waseme polisi wame andamana kwa niaba yao.

nchi hii ni ngumu ku organise maandamani bila platform either dini au chama cha siasa.
Wewe unayo intelijensia iliyokwambia hayupo atakayeandamana nao, au ni mpiga ramli?
 
Back
Top Bottom