TANGAZO: Maandamano dhidi ya malipo ya DOWANS

Msanii

Platinum Member
Jul 4, 2007
22,592
29,712
Wakuu, Nawakilisha....
LEGAL AND HUMAN RIGHTS CENTRE
Justice Lugakingira House, Kijitonyama, P. O. Box 75254, Dar Es Salaam, TANZANIA
Telephone: 2773048, 2773038, Fax: 2773037, E-mail: lhrc@humanrights.or.tz
Website www.humanrights.or.tz



TANGAZO


Maandamano ya Amani Dhidi ya UFISADI na Malipo kwa Kampuni ya Dowans Jumamosi 29/10/2011

Kituo Cha Sheria na Haki za Binadamu kwa ushirikiano na mashirika mengine ya kutetea haki za binadamu nchini wameandaa maandamano ya amani Dar es salaam siku ya Jumamosi hii tarehe 29 Oktoba 2011 kupinga ufisadi na malipo TATA ya kifisadi kwa kampuni ya Dowans kama njia mojawapo ya kumuenzi baba wa Taifa. Maandamano haya yataanzia Ubungo nje ya ofisi za TANESCO mpaka viwanja vya Jangwani kuanzia saa 2.30 asubuhi.

WATANZANIA WAZALENDO SHIME TUUNGANE NA TUJITOKEZE KWA UMOJA WETU KUPINGA UFISADI HUU NA MATUMIZI MABAYA YA FEDHA NA MALI ZETU.

Imetolewa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu



Francis Kiwanga (Adv.)
Mkurugenzi Mtendaji.

=============
UPDATE
=============
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI:
MAANDAMANO YA KUPINGA SERIKALI KUILIPA DOWANS Sh. BILIONI 111
Novemba, 2010 Mahakama ya usuluhishi ya kimataifa ilitoa tuzo dhidi ya Tanesco kuilipa Dowans shillingi billion 94. Jambo hili liliibua hisia na hasira miongoni mwa wananchi kwa kulalamika na kupinga ulipaji huo wa fedha za umma kwa kampuni tata - kutokana na taarifa za kamati teule ya Bunge.

Baada ya tuzo hiyo watu binafsi, mashirika yasiyo ya kiserikali na mawakili wa Tanesco walipinga mahakama kuu kusajili tuzo hiyo. October 2011 Mahakama kuu ilitoa uamuzi wa kusajili tuzo hiyo na kuamuru Tanesco ilipe shillingi billion 94 na asilimia 7.5 ya gharama hizo. Hata hivyo kabla ya usajili wa tuzo hiyo, Dowans iliuza mitambo husika kwa kampuni ya Symbion Powers kinyume cha taratibu kwa kuwa kulikuwa na amri ya mahakama ya kuacha hali ya mitambo ibaki kama ilivyo. Cha kushangaza ni jinsi ambavyo Serikali ilikuwa mstari wa mbele katika kuingia mkataba wa uzalishaji wa umeme na Symbion Powers kwa gharama ya watanzania hali ikijua mitambo hiyo iko kwenye mgogoro uliopo mahakamani.
Kwa kuzingatia haya, Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kwa kushirikiana na Asasi kadhaa za Kiraia na Wanaharakati wa Haki za binadamu tulitoa tamko tarehe 11 Oktoba 2011 kuitaka serikali kuchukua hatua ikiwa ni sehemu ya kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa bila mafanikio.

Kwa kuwa serikali imeamua kudharau maoni yetu, na kwa kuwa kuna kila dalili kwa serikali kuilipa Dowans fedha za wananchi, sisi, asasi za kiraia, vyama vya wafanyakazi, serikali wakilishi za wanafunzi na raia wa kawaida wa Dar es salaam tunaitisha maandamano kwa uratibu wa kituo cha Sheria na Haki za Binadamu siku ya Jumamosi tarehe 29/10/2011. Kwa hapa Dar es salaam, maandamano yataanzia Ubungo, mbele ya zilipo ofisi za Makao makuu ya TANESCO hadi Viwanja vya Jangwani kuanzia saa 2:30 asubuhi.

Maandamano haya yanalenga kuitaka serikali kufanya yafuatayo:-

  1. Kutokuilipa kabisa Dowans kwa kutumia hela za walipa kodi wa Tanzania.
  2. Itoe maelezo ya kina kwanini ilipuuza ushauri wa kisheria wa kuvunja mkataba na Richmond toka awali kwani kwa mujibu wa washauri wa kimarekani Hunton & Williams LLP wakati Tanesco inaingia mkataba na Richmond Dev’t Co. Kampuni hiyo haikuwa imeshasajiliwa achilia mbali kuwa haikuwa na uwezo wa kutekeleza majukumu yake chini ya mkataba huo.
  3. Itekeleze kwa dhati maazimio 23 yaliyotolewa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania juu ya mlolongo mzima unaopelekea mpaka sasa tutakiwe kulipa bilioni 111. Kwa kufanya hili Serikali pia ituthibitishie kuwa itaacha kabisa kukikosea heshima chombo ambacho ni kisemaji na wakilishi cha wananchi kupitia wabunge.
  4. Kama sheria za kimataifa zinatubana kulipa deni hili basi malipo haya yafanyike kwa kuuza mali za wale waliotusababishia kadhia hii na kwamba malipo ya kuilipa dowans yafanyike pale tu serikali itakuwa imeshawachukulia hatua kali wahusika wa kadhia hii. Umma ni lazima ujiridhishe kwa kuona hatua hizo zinachukuliwa.
  5. Kuchukuwa hatua ya kinidhamu kwa wale wote walioshiriki katika kuingiza serikali katika mkataba huu hata mawakili waliotoa ushauri huu.
  6. Serikali ipeleke Bungeni muswada wa utaratibu mzuri na sahihi wa kushirikisha wananchi na hata wabunge katika kuingia mikataba ya kimataifa na serikali ili kuepusha hali kama hii kutokea.

Kwa hiyo tunatoa wito kwa watanzania wote tuadhimishe kumbukumbu ya miaka 12 ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, kwa kutenda yafuatayo:-

  1. Tujitokeze kwenye maandamano ya amani na kupinga ufisadi na malipo ya kifisadi ya Dowans siku ya Jumamosi, tarehe 29 Oktoba 2011.
  2. Kuvaa nguo za maombolezo, nyeusi, kama ishara ya maombolezo tukikumbuka msimamo wake wa kupinga ufisadi na matumizi mabaya ya rasilimali za taifa,
  3. Tuzitumie siku za ibada za Ijumaa, Jumamosi na Jumapili zote ndani ya muda huu, kumuomba Mungu atujalie Uzalendo na Ujasiri wa kuitetea nchi yetu, kama alivyofanya Mwalimu Nyerere,
  4. Kuwasiliana na wanaharakati nchi nzima mahali walipo, ili kupanga na kuandaa mahali pa kukutania siku ya maandamano haya ya amani.

Mwisho, tunaomba walipa kodi (wananchi) wote ambao hawajapendezwa na mlolongo huu unaopelekea ulipaji wa deni hilo la Dowans na ufisadi mwingine wote kuwa na uthubutu na kujitokeza kwa wingi kusimamia kile ambacho wanaona ni haki na stahili ya wananchi wote na taifa letu kwa ujumla.

Kwa niaba ya asasi za kiraia ncini Tanzania zinazopigania haki na kupinga ufisadi na matumizi mabaya ya rasilimali za Umma.
 

Attachments

  • Dowans Maandamano J2.docx
    40.7 KB · Views: 127
  • Press Release DOWANS Oct 2011 - 5.docx
    590.9 KB · Views: 64
Tungesubiri matokeo ya rufaa ambayo serikali imekata.....hakuna mtu anaependa nchi ilipe fedha hizo kwa dowans...pili lile ni suala la kisheria linapaswa kupingwa kisheria mahakamani sio barabarani na mitaani kwa maandamano.wanasheria wanajua watusaidie katika hili.
 
Kwa kweli kusema tusubiri serekali imekata rufaa ni kukosea maana serekali ndio imetufikisha hapa na kwa mtiririko wa tangu Richmond inaanza mpaka hapa hakuna zaidi ya usanii tuu unafanywa na serekali na mwisho wa siku tutarudi hapahapa tulipo kwamba kisheria serekali ina makosa, sasa kuandamana ni kuiambia serekali inalazimika kuwajibika kikamilifu na hili na sio porojo za danadana hizi wanazofanya, hivi sisi watanzania tunachoogopa haswa ni nini? hizi hela zitakazolipwa tufahamu kwamba ni sisi ndio tutagharamika na sio hao viongozi wazembe ambao zaidi wataambulia lawama za mitaani pembenipembeni kama tulivyozoea kama makondoo, kweli tunahitaji kuwa serious zaidi ya maneno, tunahitaji vitendo jamani. OHOOOOOO!!!!!!!!!
 
limepitwe na wakati
serikali imekata rufaa

Jeykey na Inauma acheni ujuha au ndo mnatimiza wajibu kwa kazi mlotumwa jamvini? Kwa mujibu wa utapeli mliofanya kwenye mkataba ni kuwa mkataba hauruhusu suala hilo kupekwa nje ya Mahakama ya hao waliowapa Dowans ushindi.

Mnatufanya WaTz wote majuha. Shuhudieni hayo maandamano, labda yatawapa kujua kama sisi bado majuha au tumeerevuka.
 
Wakuu, Nawakilisha....

Naomba utuhakikishie authenticity ya hili Tangaza maana nashindwa kukuamini kwa sababu jina lako hapa JF ni msanii...kwa tafsiri ya kawaida kabisa kwa mtanzania wa kawaida, msanii ni laghai, asiyeaminika, mtu wa "SOUND" na tafsiri nyingi za aina hiyo. Je, utatuhakikishiaje kuwa hiki ulichokiweka siyo usaniii?

USHAURI WANGU: kwa vitu ambavyo ni serious kama hiki, we need to have a serious tone, ikianzia na mtoa habari mwenyewe.


That's my concern
 
limepitwe na wakati
serikali imekata rufaa
Rufaa ya serikali hiyo hiyo iliyoingia katika mkataba huo....
Najua ni sanaa tu zinatengenezwa ili kufuta kelele za wananchi...najua mwisho wa siku watalipa tu, tena with penalty!!
 
Naomba utuhakikishie authenticity ya hili Tangaza maana nashindwa kukuamini kwa sababu jina lako hapa JF ni msanii...kwa tafsiri ya kawaida kabisa kwa mtanzania wa kawaida, msanii ni laghai, asiyeaminika, mtu wa "SOUND" na tafsiri nyingi za aina hiyo. Je, utatuhakikishiaje kuwa hiki ulichokiweka siyo usaniii?

USHAURI WANGU: kwa vitu ambavyo ni serious kama hiki, we need to have a serious tone, ikianzia na mtoa habari mwenyewe.


That's my concern
Mkuu, Mimi ni msanii kwa fani yangu wala sibabaishi ktk ninachokifanya ama kufikiria kufanya.
Hii taarifa ni wito wa kweli na hakuna blahblah ndani yake. Naamini media nyingi hili tangazo litawekwa.
Kwa uhakika zaidi wasiliana na anuani inayojionesha kwenye hilo Tangazo kwa uhakika zaidi.
Hii tabia yetu ya kupuuzia mambo kwa sababu ya uchaguzi ama ubaguzi ndo inatuletea janga kila kukicha.

Neno Msanii mmelikuza wenyewe maana hapo zamani mtu mwizi, laghai na bandidu alikuwa anaitwa PROFESA (Mfa. Prof Ndumilakuwili), Mjifunze kuheshimu fani za watu mkuu...


limepitwe na wakati
serikali imekata rufaa
...Labda kwa maslahi yako mkuuu....
 
Kwa kweli kusema tusubiri serekali imekata rufaa ni kukosea maana serekali ndio imetufikisha hapa na kwa mtiririko wa tangu Richmond inaanza mpaka hapa hakuna zaidi ya usanii tuu unafanywa na serekali na mwisho wa siku tutarudi hapahapa tulipo kwamba kisheria serekali ina makosa, sasa kuandamana ni kuiambia serekali inalazimika kuwajibika kikamilifu na hili na sio porojo za danadana hizi wanazofanya, hivi sisi watanzania tunachoogopa haswa ni nini? hizi hela zitakazolipwa tufahamu kwamba ni sisi ndio tutagharamika na sio hao viongozi wazembe ambao zaidi wataambulia lawama za mitaani pembenipembeni kama tulivyozoea kama makondoo, kweli tunahitaji kuwa serious zaidi ya maneno, tunahitaji vitendo jamani. OHOOOOOO!!!!!!!!!

Kwa hapa umelonga, nakumbuka waisilamu nchi nzima waliandamana dhidi ya hukumu ya mwisilam mwenzao kufungwa kwa kukashifu dini nyingine za kikiristo. hukumu hiyo ilitolewa morogoro.hawakusubiri rufaa.Hapa baada ya waislimu kuandamana, serikali na mahakama waliaingilia na ilitengua hukumu hiyo na kuachiwa huru huyo mwislam aliyekuwa amefungwa.Kwa hapa hakuna rufaa, itakayo kubalika.Swali ni kwanini serikali ilishindwa kenye mahakama ya ICC? na pia ni hatua gani zilichukuliwa tangu hawa mabwana walivyoanza kuonyesha jeuri ya kukimbilia mahakamani?Hapa watanzania hili limepangwa na mafisadi kuwa lazima walipwe , serikali kukata rufaa ni kiini macho ingekuwa madhubuti tusingeshindwa tangu kwenye kesi ya icc .maandamano ni hoja ya msingi kuonyesha watanzania si watu legelege wa kuendekeza tamithilia za mahakamani
 
Mkuu, Mimi ni msanii kwa fani yangu wala sibabaishi ktk ninachokifanya ama kufikiria kufanya.
Hii taarifa ni wito wa kweli na hakuna blahblah ndani yake. Naamini media nyingi hili tangazo litawekwa.
Kwa uhakika zaidi wasiliana na anuani inayojionesha kwenye hilo Tangazo kwa uhakika zaidi.
Hii tabia yetu ya kupuuzia mambo kwa sababu ya uchaguzi ama ubaguzi ndo inatuletea janga kila kukicha.

Neno Msanii mmelikuza wenyewe maana hapo zamani mtu mwizi, laghai na bandidu alikuwa anaitwa PROFESA (Mfa. Prof Ndumilakuwili), Mjifunze kuheshimu fani za watu mkuu...


...Labda kwa maslahi yako mkuuu....

Kwa hapa umelonga, nakumbuka waisilamu nchi nzima waliandamana dhidi ya hukumu ya mwisilam mwenzao kufungwa kwa kukashifu dini nyingine za kikiristo. hukumu hiyo ilitolewa morogoro.hawakusubiri rufaa.Hapa baada ya waislimu kuandamana, serikali na mahakama waliaingilia na ilitengua hukumu hiyo na kuachiwa huru huyo mwislam aliyekuwa amefungwa.Kwa hapa hakuna rufaa, itakayo kubalika.Swali ni kwanini serikali ilishindwa kenye mahakama ya ICC? na pia ni hatua gani zilichukuliwa tangu hawa mabwana walivyoanza kuonyesha jeuri ya kukimbilia mahakamani?Hapa watanzania hili limepangwa na mafisadi kuwa lazima walipwe , serikali kukata rufaa ni kiini macho ingekuwa madhubuti tusingeshindwa tangu kwenye kesi ya icc .maandamano ni hoja ya msingi kuonyesha watanzania si watu legelege wa kuendekeza tamithilia za mahakamani
 
Rufaa ya serikali hiyo hiyo iliyoingia katika mkataba huo....
Najua ni sanaa tu zinatengenezwa ili kufuta kelele za wananchi...najua mwisho wa siku watalipa tu, tena with penalty!!
maandamano ndo hoja ya msingi, nakumbuka waisilamu nchi nzima waliandamana dhidi ya hukumu ya mwisilam mwenzao kufungwa kwa kukashifu dini nyingine za kikiristo. hukumu hiyo ilitolewa morogoro.hawakusubiri rufaa.Hapa baada ya waislimu kuandamana, serikali na mahakama waliaingilia na ilitengua hukumu hiyo na kuachiwa huru huyo mwislam aliyekuwa amefungwa.Kwa hapa hakuna rufaa, itakayo kubalika.Swali ni kwanini serikali ilishindwa kenye mahakama ya ICC? na pia ni hatua gani zilichukuliwa tangu hawa mabwana walivyoanza kuonyesha jeuri ya kukimbilia mahakamani?Hapa watanzania hili limepangwa na mafisadi kuwa lazima walipwe , serikali kukata rufaa ni kiini macho ingekuwa madhubuti tusingeshindwa tangu kwenye kesi ya icc .maandamano ni hoja ya msingi kuonyesha watanzania si watu legelege wa kuendekeza tamithilia za mahakamani
 
Ole wake niskie mtu anaingiza mambo ya udini hapa, hii haina dini wala kabila msijemkadanganywa kwenye ibada zenu kuwa msiandamane ni maandamano ya dini fulani hayo, utakua ni ujinga wa hali ya juu. Kaeni kimya kabisa kama unaenda twende, kama huendi kaa kimya mie ntavaa kashati kangu ka JF
 
Hivi yale maandamano ya 14 October yaliishia wapi?? Au ndiyo kupima kina cha maji kupitia JF!!
 
Kuanzia TANESCO Ubungo mpaka Jangwani siyo kilometer kama 10!!! Haiwezekani wakakubali maandamano ya distance ndefu kiasi hicho!!
 
Ole wake niskie mtu anaingiza mambo ya udini hapa, hii haina dini wala kabila msije mkadanganywa kwenye ibada zenu kuwa msiandamane ni maandamano ya dini fulani hayo, utakua ni ujinga wa hali ya juu. Kaeni kimya kabisa kama unaenda twende, kama huendi kaa kimya mie ntavaa kashati kangu ka JF

Lazima kieleweka, nilikua nisafiri lakini siendi lazima niwepo na Mimi pia, ntakua mbele kabisa, najua kibali kimepatikana
 
Back
Top Bottom