Ratiba ya maandamano 2026

Ratiba ya maandamano 2026

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
368,278
Reaction score
851,918
Ya sabasaba yamepita bila watu wengi kuandamana kutokana na nguvu kubwa ya ulinzi iliyotumika kudhibiti maandamano
Siku ya 7/7 ilitawaliwa na ukimya wa kutisha
Barabara zilikuwa tupu
Biashara asilimia 99 zilikuwa zimefungwa
Watanganyika kwa asilimia 90 hawakutoka majumbani, kitu ambacho si kawaida kwa siku kama hiyo

Serikali pengine itaona aibu kutoa tathmini ya hasara iliyopata kwa hiyo siku moja tuu
Kuanzia maenesho ya miaka 50 ya 7/7 kudoda na kudorora vibaya sana, gharama kubwa iliyomika kuvileta barabarani vyombo vya ulinzi na usalama, posho, mafuta, vifaa, silaha, nknk..

Biashara zote ambazo zilifungwa serikali pia ilikosa mapato
Ukimya ule wa jana haukuwa utulivu wa amani bali ulikuwa utulivu uliojaa fukuto la chini
Hilo fukuto la chini kwa chini linaendelea kufukuta chini kwa chini na hili na hili ndio linatengeneza ratiba endelevu ya maandamano kwa kila tukio kubwa la kitaifa kwa siku zijazo

1. Maadhimisho ya 8/8
2. Ufunguzi wa AFCON
3. Maadhimisho ya kumbukumbu ya kifo cha Baba wa taifa 14. Oct
4. Maadhimisho ya kumbukumbu ya mauaji ya October 29
5. Maadhimisho ya sikukuu za mwisho wa mwaka X-mas na Mwaka mpya!

Kuna madai ya wananchi wa Tanganyika.. Hayafanyiwi kazi yanaendelea kupuuzwa.. Yakiendelea kupuuzwa tena na tena hizi ratiba za maandamano hazitakoma
 
Hivi Tanganyika ni Ziwa au nchi?
Minaona ni Titi sio Ziwa...
IMG-20260703-WA0019.jpg
 
Hivi Tanganyika ni Ziwa au nchi?
Neno Tanganyika linawakilisha mambo mawili tofauti:
ni jina la ziwa na pia lilikuwa jina la nchi kabla ya kuungana na Zanzibar kuunda Tanzania.
 
Ya sabasaba yamepita bila watu wengi kuandamana kutokana na nguvu kubwa ya ulinzi iliyotumika kudhibiti maandamano
Siku ya 7/7 ilitawaliwa na ukimya wa kutisha
Barabara zilikuwa tupu
Biashara asilimia 99 zilikuwa zimefungwa
Watanganyika kwa asilimia 90 hawakoka majumbani, kitu ambacho si kawaida kwa siku kama hiyo

Serikali pengine itaona aibu kutoa tathmini ya hasara iliyopata kwa hiyo siku moja tuu
Kuanzia maenesho ya miaka 50 ya 7/7 kudoda na kudorora vibaya sana, gharama kubwa iliyomika kuvileta barabarani vyombo vya ulinzi na usalama, posho, mafuta, vifaa, silaha, nknk..

Biashara zote ambazo zilifungwa serikali pia ilikosa mapato
Ukimya ule wa jana haukuwa utulivu wa amani bali ulikuwa utulivu uliojaa fukuto la chini
Hilo fukuto la chini kwa chini linaendelea kufukuta chini kwa chini na hili na hili ndio linatengeneza ratiba endelevu ya maandamano kwa kila tukio kubwa la kitaifa kwa siku zijazo

1. Maadhimisho ya 8/8
2. Ufunguzi wa AFCON
3. Maadhimisho ya kumbukumbu ya kifo cha Baba wa taifa 14. Oct
4. Maadhimisho ya kumbukumbu ya mauaji ya October 29
5. Maadhimisho ya sikukuu za mwisho wa mwaka X-mas na Mwaka mpya!

Kuna madai ya wananchi wa Tanganyika.. Hayafanyiwi kazi yanaendelea kupuuzwa.. Yakiendelea kupuuzwa tena na tena hizi ratiba za maandamano hazitakoma
This is obvious !!!!
 
This is obvious !!!!
Maadhimisho ya mwaka mmoja ya matukio na mauaji ya MO29 (Oktoba 29) yanatarajiwa kufanyika mnamo Oktoba 29, 2026 nchini Tanzania.

Harakati na maandalizi haya yanatokana na kumbukumbu ya machafuko, maandamano makubwa, na vifo vilivyotokea wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa tarehe 29 Oktoba 2025.

Raia na wanaharakati mbalimbali, ikiwemo makundi ya vijana (GenZ) na vyama vya siasa, wamekuwa wakihamasishana kutumia siku hii kama alama ya kuwakumbuka na kuwaenzi wahanga waliopoteza maisha au kujeruhiwa katika matukio hayo.
 
Back
Top Bottom