Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 359,879
- 828,434
Tunadhalilika duniani
Tunadhalilika mitandaoni
Tunadhalilika Afrika
Tunadhalilika ndani ya jumuiya ya Afrika mashariki mashariki
Hakuna haja ya kurudia chanzo cha haya yote.. Haisaidii tena.. Maana maji yameshamwagika.. Tukitaka kuzoa tutazoa tope
Kazi hiyo ya udhalilishaji inafanywa na makundi mbalimbali hapo nchi jirani ya Kenya yakiongozwa na vijana wao maarufu kama Gen-Z.. Hawafanyi haya kama uchokozi la hasha ipo sababu ya wazi kabisa
Sasa basi kuna vikundi vingi vilibuka hapa bongo vikiongozwa na kile maarufu kama CHAWA WA MAMA! Hivi vilijiapiza kuwa vitakula sahani moja na yeyote yule atakayemzogoa mama kwa lolote like
Ni wiki sasa inaisha Gen-Z kila uchao wanakuja na kituko kipya cha udhalilishaji, matusi, kejeli, kashfa.. Nknk.. Sijaona hata kikundi kimoja kikitoa walau waraka wa sentence moja ya kukemea.. Je vinafurahia haya yanayoendelea?
Hebu tuvitaje vile vikundi vyote hapa.. Tuvitengenezee petition ya kufutwa na kuadhibiwa maana vimeshindwa kazi
Udhalilishaji unaoendelea hauishii kwa mhusika tuu Bali mpaka kwetu sisi tusio na kosa lolote... Wakianza kutukana hawana breki aisee .. Inaumiza sana
Tunadhalilika mitandaoni
Tunadhalilika Afrika
Tunadhalilika ndani ya jumuiya ya Afrika mashariki mashariki
Hakuna haja ya kurudia chanzo cha haya yote.. Haisaidii tena.. Maana maji yameshamwagika.. Tukitaka kuzoa tutazoa tope
Kazi hiyo ya udhalilishaji inafanywa na makundi mbalimbali hapo nchi jirani ya Kenya yakiongozwa na vijana wao maarufu kama Gen-Z.. Hawafanyi haya kama uchokozi la hasha ipo sababu ya wazi kabisa
Sasa basi kuna vikundi vingi vilibuka hapa bongo vikiongozwa na kile maarufu kama CHAWA WA MAMA! Hivi vilijiapiza kuwa vitakula sahani moja na yeyote yule atakayemzogoa mama kwa lolote like
Ni wiki sasa inaisha Gen-Z kila uchao wanakuja na kituko kipya cha udhalilishaji, matusi, kejeli, kashfa.. Nknk.. Sijaona hata kikundi kimoja kikitoa walau waraka wa sentence moja ya kukemea.. Je vinafurahia haya yanayoendelea?
Hebu tuvitaje vile vikundi vyote hapa.. Tuvitengenezee petition ya kufutwa na kuadhibiwa maana vimeshindwa kazi
Udhalilishaji unaoendelea hauishii kwa mhusika tuu Bali mpaka kwetu sisi tusio na kosa lolote... Wakianza kutukana hawana breki aisee .. Inaumiza sana