TANESCO wanataka ninunue transformer

TANESCO wanataka ninunue transformer

Ulipiga namba gani? Tatizo ni nini? Wilaya na namba ya simu tafadhali
Nilipiga namba hizi 0222194400/ 0768985100,NIkaongea ni muhudumu wenu ambaye baada ya kushindwa kunipa huduma bora akamuita boss wake ambaye naye alishindwa kunipa huduma bora na wakanipa namba ya ofisi yao nikapiga wakashindwa kunipa huduma bora na bado nikaenda katika ofisi yao wakashindwa kunipa huduma bora.


Unajua waliniambia nini?ETI KIASI NILICHOKUWA NADAI ni kidgo sana nilipe tu kuepuka usumbufu.
 
Kama utakumbuka Maelekezo ya Serikali hapo awali hakuna mteja anayepaswa kununua kifaa chochote cha kumfungia umeme bali ni jukumu la TANESCO kusogeza miundombinu ya umeme kwa wateja wake, tafadhali tusaidie taarifa zifauatazo

Jina

Namba ya Simu

Wilaya

Na kiasi ulichodai kuambiwa ulipie ili tukujipatie ufafanuzi kwa taarifa kamili

TANESCO HUDUMA KWA WATEJA

MAKAO MAKUU
Safi
 
Nilipiga namba hizi 0222194400/ 0768985100,NIkaongea ni muhudumu wenu ambaye baada ya kushindwa kunipa huduma bora akamuita boss wake ambaye naye alishindwa kunipa huduma bora na wakanipa namba ya ofisi yao nikapiga wakashindwa kunipa huduma bora na bado nikaenda katika ofisi yao wakashindwa kunipa huduma bora.


Unajua waliniambia nini?ETI KIASI NILICHOKUWA NADAI ni kidgo sana nilipe tu kuepuka usumbufu.
Tunaomba namba yako na tatizo tulifanyie kazi tafadhali
 
mkuu una options 2 tu:

- toa chapaa ununue iyo 'transfoma'

- au usubiri miaka 5(hmm au zaidi) mingine tanesiko waendelee wakufikie na transfoma ya 'bure'
Na hapo ndo kiota chao cha RUSHWA KIPO.Mimi nilijua ukiamua kununua Transforma basi umeliwa.Bora Utengeneze umeme wako mwenyewe ama wa SOLA au UPEPO au mwingine kuliko uwape TANESCO pesa yako wakati hawana shukrani.
 
Taarifa

Mteja hapaswi kulipia kifaa chochote kwa ajili ya kuunganishiwa umeme

Nb

Kwa mujibu wa kanuni za umeme mteja anaweza kufata taratibu na kujengewe line au transfoma kwenye eneo lake,
Fuatilieni managers wenu wa wilayani na usambazaji wa umeme vijijini ,labda makao makuu hamjui hilo lakini ni watu tunapigwa kalenda kuletewa umeme mpaka utoe chochote,anayetoa chochote manager anaagiza tu haraka ,umeme ni haki ya kila mtu hasa kwa sehemu ambazo utaratibu wa kugawa umeme umeanza fuatilieni managers wenu mambo wanayofanya
 
Na hapo ndo kiota chao cha RUSHWA KIPO.Mimi nilijua ukiamua kununua Transforma basi umeliwa.Bora Utengeneze umeme wako mwenyewe ama wa SOLA au UPEPO au mwingine kuliko uwape TANESCO pesa yako wakati hawana shukrani.
tanesiko wa humu JF yupo kinadharia (kimakaratasi) zaidi, uhalisia upo kwa tanesiko branchini
 
Nilipiga namba hizi 0222194400/ 0768985100,NIkaongea ni muhudumu wenu ambaye baada ya kushindwa kunipa huduma bora akamuita boss wake ambaye naye alishindwa kunipa huduma bora na wakanipa namba ya ofisi yao nikapiga wakashindwa kunipa huduma bora na bado nikaenda katika ofisi yao wakashindwa kunipa huduma bora.


Unajua waliniambia nini?ETI KIASI NILICHOKUWA NADAI ni kidgo sana nilipe tu kuepuka usumbufu.
Ndogo kivipi wakati ni haki yako ,kwenye social media wako vizuri kwenye field ni kero tupu
 
Tunaomba namba yako na tatizo tulifanyie kazi tafadhali
Namba yangu ya sim siwezi kuwapa tena maana nilishawapatia zaidi ya Mara moja.Nilidai sana mnipe incident tracking number ambayo rekodi kama hizo mngeweka hapo na kwenu ingekuwa rahisi zaidi ila kwa sababu mtapoteza ulaji ndo inabidi sasa mjifanye kuuliza namba za simu kila mahali.Kama information nilizowapa bado haziwapi mwanga basi ni ushahidi kuwa bado mko incompetent.

Mnawezaji kuhudumia wateja zaidi ya 60M na bado hamana mfumo wa kusimamia matukio ambao ni wa kikampuni.Iko mifumo ya bei chee kabisa ambayo inaweza unganisha ofisi zote za TANESCO .Au hata kuunganisha ofisi za mikoa tu?
 
Namba yangu ya sim siwezi kuwapa tena maana nilishawapatia zaidi ya Mara moja.Nilidai sana mnipe incident tracking number ambayo rekodi kama hizo mngeweka hapo na kwenu ingekuwa rahisi zaidi ila kwa sababu mtapoteza ulaji ndo inabidi sasa mjifanye kuuliza namba za simu kila mahali.Kama information nilizowapa bado haziwapi mwanga basi ni ushahidi kuwa bado mko incompetent.

Mnawezaji kuhudumia wateja zaidi ya 60M na bado hamana mfumo wa kusimamia matukio ambao ni wa kikampuni.Iko mifumo ya bei chee kabisa ambayo inaweza unganisha ofisi zote za TANESCO .Au hata kuunganisha ofisi za mikoa tu?
Mfumo upo tafadhalo toa ushirikiano
 
Ndogo kivipi wakati ni haki yako ,kwenye social media wako vizuri kwenye field ni kero tupu
Hapa yenyewe bado hawako vizuri ila ni kwa sababu ni JF,aliyepewa hii kazi anapata na muda wa kusoma nyuzi zingine za kula tunda kimasihara kwa gharama za bundle la tanesco wakati siku hizi mifumo ya CRM ipo mingi sana ambayo TANESCO wanaweza kuitumia kutoa huduma bora na mitandao ya kijamii na simu zikawa ni listening points tu.
 
Hapa yenyewe bado hawako vizuri ila ni kwa sababu ni JF,aliyepewa hii kazi anapata na muda wa kusoma nyuzi zingine za kula tunda kimasihara kwa gharama za bundle la tanesco wakati siku hizi mifumo ya CRM ipo mingi sana ambayo TANESCO wanaweza kuitumia kutoa huduma bora na mitandao ya kijamii na simu zikawa ni listening points tu.
Mfumo upo na njia za.mitandao ya kijamii ni.kuwafata wateja wetu walipo.Tunashukuru sana
 
Mfumo upo tafadhalo toa ushirikiano
Ila humuutumii?Vinginevyo taarifa yangu niliyoleta kwenu ningepewa incident namba hapa ningekupa tu hio namba na mengine ungejua pa kuanzia.SO bado tunarudi kule kule kufundishana ABC wakati ile tarehe 19 niliwapa darasa la bure na mkasema mmejifunza ila naona bado sana
 
Ila humuutumii?Vinginevyo taarifa yangu niliyoleta kwenu ningepewa incident namba hapa ningekupa tu hio namba na mengine ungejua pa kuanzia.SO bado tunarudi kule kule kufundishana ABC wakati ile tarehe 19 niliwapa darasa la bure na mkasema mmejifunza ila naona bado sana
Ndio maana tumeomba ushirikiano wako tukusikilize, tunaamini kwa hekima na uungwana wako utakuwa mzalendo kwetu ili kazi hii iwe rahisi
 
Ukiwa na matumizi makubwa ya umeme unalazimika kununua transformer yako ambayo unaweza fungiwa ndani ya uzio wako na gharama ya kuhudumia ni zako. Hii sio tz hata nchi nyingine iko hivyo. Chukua mfano uwe na mota 4 za hp50 ambazo zina kv 37 kwa kila mota ambazo in total matumiz yako yatadondokea kwenye 148 na mara nyingi mtaan ni kva 200, yaan unajikuta wewe ndo unawaunyonya mtaa maana watabakiwa na kama kva 50 wewe ukiwa unebeba nusu na robo.
Kwa milion kumu ni bei ndogo maana bado kuna vifaa vyake. Kuna faida nyingi za kuwa na transformer yako. Moja ikiwa kupata umeme wa kutosha kwenye kiwanda chako.
Ukiona kazi nenda tanalec ulizia bei ya kva 50 tu ambayo kwa mota za hp 50 huwez washa mbili kwa wakati mmoja halafu urejee tena hapa
 
Ndio maana tumeomba ushirikiano wako tukusikilize, tunaamini kwa hekima na uungwana wako utakuwa mzalendo kwetu ili kazi hii iwe rahisi
Mkuu,Lengo langu leo ni kufanya kazi yenu iwe ngumu ili mjifunze kuifanya iwe rahisi.Mteja anapopiga simu ni lazima mumpe incident namba regardless tatizo lake ni nini.Pile mteja akileta taarifa kwenu ni jukumu lenu kulifanyia kazi kwa kuwasiliana na wahusika.Hii tabia yenu ya kuona raha kuwapigisha watu foleni katika ofisi za TANESCO kwa issues ndogo ndogo ni dalili ya kujenga mazingira ya wizi,rushwa na utapeli.Watu tupige mistari shuleni,jeshini na tanesco nako tupige mstari tena hata viti vya kukaa wateja hamna yaani mnakuwa kama wajima wakati tupo karne ya ishirini na moja?

Huku mitandaoni mnatusikiliza lakini mnaonekana bado hamjajua suluhu ya changamoto yenu ni nini.

Kama kweli mnataka kusolve issue yangu nipatieni namba ya simu ya Mkuu wa kitengo cha HUDUMA kwa wateja hapo makao makuu niwasiliane naye.
 
Mkuu,Lengo langu leo ni kufanya kazi yenu iwe ngumu ili mjifunze kuifanya iwe rahisi.Mteja anapopiga simu ni lazima mumpe incident namba regardless tatizo lake ni nini.Pile mteja akileta taarifa kwenu ni jukumu lenu kulifanyia kazi kwa kuwasiliana na wahusika.Hii tabia yenu ya kuona raha kuwapigisha watu foleni katika ofisi za TANESCO kwa issues ndogo ndogo ni dalili ya kujenga mazingira ya wizi,rushwa na utapeli.Watu tupige mistari shuleni,jeshini na tanesco nako tupige mstari tena hata viti vya kukaa wateja hamna yaani mnakuwa kama wajima wakati tupo karne ya ishirini na moja?

Huku mitandaoni mnatusikiliza lakini mnaonekana bado hamjajua suluhu ya changamoto yenu ni nini.

Kama kweli mnataka kusolve issue yangu nipatieni namba ya simu ya Mkuu wa kitengo cha HUDUMA kwa wateja hapo makao makuu niwasiliane naye.
Mpaka sasa haujafanya wajibu wako wa msingi wa kutoa taarifa ili tujue undani wa swala lako, tunasikitika sana pale ambapo tunaomba taarifa kamili na wewe unajibu kwa ujumla, hakuna huduma bora bila taarifa zako, toa hata namba ya simu tutaona kila kitu kupitia mifumo yetu
 
Back
Top Bottom