TANESCO wanataka ninunue transformer

Ndugu mpendwa Mteja wetu

Tunafurahia kukuhudumia kupitia kurasa zetu za mitandao ya kijamii, tafadhali onesha taarifa kamili kwa huduma bora.

Jina

Eneo

Wilaya

Namba ya simu

Tatizo

Toka lini

Namba ya taarifa

Ahsante sana

TANESCO Huduma kwa Wateja
baadhi ya watumishi wenu wana kauli mbovu sana na za kukatisha tamaa kabisa na ndio maana wengine wanaona bora hata wafunge solar system tu
 
  • Thanks
Reactions: Lee
baadhi ya watumishi wenu wana kauli mbovu sana na za kukatisha tamaa kabisa na ndio maana wengine wanaona bora hata wafunge solar system tu
Tunaomba tukusikilize,

Je ni kauli gani ulijibiwa

Ulipiga simu tarehe ngapi na muda gani?

Namba yako ya simu tafadhali
 
Hebu twende taratibu...

Let's say ninapoishi ni 5km kutoka eneo ambalo lina miundombinu ya TANESCO...

Je, nikitaka huduma yenu mtaniletea umbali wa 5 KM kwa gharama zenu?
Swali zuri sana.
Ni wachache sana watakaoelewa mantiki ya hili swali.
 
na ukishanunua ni mali yao .... huu mchezo upo sana hasa maeneo ya vijijini
 
Ila humuutumii?Vinginevyo taarifa yangu niliyoleta kwenu ningepewa incident namba hapa ningekupa tu hio namba na mengine ungejua pa kuanzia.SO bado tunarudi kule kule kufundishana ABC wakati ile tarehe 19 niliwapa darasa la bure na mkasema mmejifunza ila naona bado sana
Taja number usaidike mkuu, usikate tamaa bongo ukitaka huduma mpaka utoe rushwa au uwe unajuana na mtu sehemu husika
 
baadhi ya watumishi wenu wana kauli mbovu sana na za kukatisha tamaa kabisa na ndio maana wengine wanaona bora hata wafunge solar system tu
lakini imezoelekaa watu wenye matusi ni mafundi/ watu wa tanesco ...hii wana tuzo miaka yote yao
 
Ukiwa na matumizi makubwa ya umeme unalazimika kununua transformer yako ambayo unaweza fungiwa ndani ya uzio wako na gharama ya kuhudumia ni zako. Hii sio tz hata nchi nyingine iko hivyo. Chukua mfano uwe na mota 4 za hp50 ambazo zina kv 37 kwa kila mota ambazo in total matumiz yako yatadondokea kwenye 148 na mara nyingi mtaan ni kva 200, yaan unajikuta wewe ndo unawaunyonya mtaa maana watabakiwa na kama kva 50 wewe ukiwa unebeba nusu na robo.
Kwa milion kumu ni bei ndogo maana bado kuna vifaa vyake. Kuna faida nyingi za kuwa na transformer yako. Moja ikiwa kupata umeme wa kutosha kwenye kiwanda chako.
Ukiona kazi nenda tanalec ulizia bei ya kva 50 tu ambayo kwa mota za hp 50 huwez washa mbili kwa wakati mmoja halafu urejee tena hapa
Mbona Tanesco mwenyewe amesema hapa transforma hainunuliwi vitu vyote ni bure Sasa wewe unalinganishaje Tanzania na wengine?
 
Tafadhali pitia tena maelezo yetu ukiyasoma vizuri utaelewa tulichomaanisha, mteja aliyelalamika tumeshawasiliana naye Dm Na tumefikia pazuri
Safi kikubwa mteja changamoto yake itatuliwe na nyie humu hongereni kufatilia changamoto za wananchi, ningependa na taasisi zingine zijiunge humu JF Ili ziweze kupata changamoto zetu wateja na kuboresha nchi yetu
 
Taja number usaidike mkuu, usikate tamaa bongo ukitaka huduma mpaka utoe rushwa au uwe unajuana na mtu sehemu husika
Mkuu,hawa huduma yao ni mbovu sana.Tukiendelea kuwaendekeza tutazidi kuchoka na kuumia
 
E
Kama utakumbuka Maelekezo ya Serikali hapo awali hakuna mteja anayepaswa kununua kifaa chochote cha kumfungia umeme bali ni jukumu la TANESCO kusogeza miundombinu ya umeme kwa wateja wake, tafadhali tusaidie taarifa zifuatazo

Jina

Namba ya Simu

Wilaya

Na kiasi ulichodai kuambiwa ulipie ili tukupatie ufafanuzi kwa taarifa kamili

TANESCO HUDUMA KWA WATEJA

MAKAO MAKUU
Nyie jamaa kuweni makini sana vpi kuhusu kununua nguzo maana umeme maskan kwa maza hakuna kisa nguzo moja, na tunaambiwa tununue, pia nliwahi enda tanesco kufatilia umeme nyumba ya baba nkamkuta mzee mmoja analalamika analalamika tanesco kuwa mlimtoza hela ya nguzo tatu pale makambako Sasa shida ikawa watu wanakuja wanaingiziwa umeme Bure kupitia yeye na tanesco walimtoz hela ya nguzo tat Kama laki sita hiv... Jaman haya mambo yapo sana Ila shida mnalindana huko juu, umeme tunapenda sana t
 
E

Nyie jamaa kuweni makini sana vpi kuhusu kununua nguzo maana umeme maskan kwa maza hakuna kisa nguzo moja, na tunaambiwa tununue, pia nliwahi enda tanesco kufatilia umeme nyumba ya baba nkamkuta mzee mmoja analalamika analalamika tanesco kuwa mlimtoza hela ya nguzo tatu pale makambako Sasa shida ikawa watu wanakuja wanaingiziwa umeme Bure kupitia yeye na tanesco walimtoz hela ya nguzo tat Kama laki sita hiv... Jaman haya mambo yapo sana Ila shida mnalindana huko juu, umeme tunapenda sana t
Ndugu mpendwa Mteja wetu

Tunafurahia kukuhudumia kupitia kurasa zetu za mitandao ya kijamii, tafadhali onesha taarifa kamili kwa huduma bora.

Jina

Eneo

Wilaya

Namba ya simu

Tatizo

Toka lini

Namba ya taarifa

Ahsante sana

TANESCO Huduma kwa Wateja
 
Habari, Mimi ni mkazi wa Morogoro vijijini. Biashara yangu ni ya kukoboa zao(silitaji kwa sababu binafsi) ni mwaka wa tatu sasa nafuatilia kuwekewa umeme katika kiwanda hichi kidogo maana natumia diesel lakini gharama nnazopewa ni zaidi ya milioni kumi, ikiwemo na kununua transform.

Wataalam hili suala limekaaje maana nashindwa kuelewa. NINUNUE transformer kivipi wakati ni wajibu wa TANESCO kutupatia huduma kwa malipo husika ya huduma hi.. na ugumu wa kuwekewa umeme unakuja wapi jamani. MSAADA
one sided story
weka barua ya TANESCO
 
Wanataka hela ya ku brashia kiatu hao
Jamaa wananata knyama nguzo inaweza ikawa dirishan kwak tu ila kukushushia umeme kama hujawapa kitu utasubiri Sana alaf wanakula rushwa kizembe sana sema tu ndo vle wa tz weng hatupendi kuharibiana kazi
 
one sided story
weka barua ya TANESCO
Maelezo ya mleta uzi yana walakini.
Eti aliambiwa kwa mdomo. Hakuna ushahidi wa kutosha wa kuweza kuthibitisha maelezo ya huyu mleta uzi.
Kimashine cha kusaga/kukoboa kinahitahitaji kweli kufungiwa transformer? Je Load ya hizo mashine ikoje?
Ukiacha transformer bado kuna issue ya ujenzi wa line kubwa ya umeme ili transformer ifungwe mwisho wa line hiyo. Haya yote mleta uzi hajafafanua.
 
Tunaomba tukusikilize,

Je ni kauli gani ulijibiwa

Ulipiga simu tarehe ngapi na muda gani?

Namba yako ya simu tafadhali
Mtaalam wa TANESCO uliopo ndani ya jukwa huru hili. .
Awali ya yote nakupa gongole kwa kulikabili hili jukwa na tena nakupa shukran zangu za dhati kwa uvumilivu na lugha unaotumia ndani ya jukwa hili.ila nashindwa kukuelewa kwa misimamo yako tukupe (Majina yetu halisi - Nambari zetu za simu halisi- na wilaya zetu tunaolalamikia halisi?...) Kweli unatutakia mazuri kwa mingu watu? Kama ww sio roboti unaekariri majibu baci elewa kua hapa JF kila mchangiaji anatumia JINA BANDIA....
 
Ndugu mpendwa Mteja wetu

Tunafurahia kukuhudumia kupitia kurasa zetu za mitandao ya kijamii, tafadhali onesha taarifa kamili kwa huduma bora.

Jina

Eneo

Wilaya

Namba ya simu

Tatizo

Toka lini

Namba ya taarifa

Ahsante sana

TANESCO Huduma kwa Wateja
Can't give you my credentials... Infact hamuaminiki, naomba mpokee tu Kama maoni, mjirekebishe, mtu unalipia gharama za kuingiziwa umeme vizur lakn hata kuja kuchek raman ya mtaa lazma uuwatoe, ukitaka kuingiziwa umeme mapema pesa ... Aisee ni balaa
 
Back
Top Bottom