TANESCO wanataka ninunue transformer

TANESCO wanataka ninunue transformer

Twenda kwenye swala la msingi tafadhali kwani unapata changamoto gani?

Eneo

Wilaya

Simu

Mteja anatusaidia sisi kumuhudumia kwa kutoa ushirikiano
Changamoto yangu ni juu ya utendaji wenu wa kazi kama help desk na kama kampuni.Je hilo nalo linahitaji namba yangu ya simu na jina langu?
 
Changamoto yangu ni juu ya utendaji wenu wa kazi kama help desk na kama kampuni.Je hilo nalo linahitaji namba yangu ya simu na jina langu?
Changamoto gani haswa? Ulitoa taarifa lini na kwa namba ipi tufatilie?
 
Mlishinwa nilipowapigia simu na kutembelea ofisi zenu.Mtawezaje leo
Tafadhali tupatie taarifa hapa tunakuahidi kukupatia huduma au ufafanuzi

Hii ni TANESCO mpya iliyojipanga kukuhudumia
 
Tunaamini kabla ya kutuhumu tungepata taarifa kamili.kwanza nasisi tutoe ufafanizi sahihi hakuna mteja anayepaswa kuteseka nasisi TANESCO tupo
Msaidieni apate umeme sio mumpe ufafanuzi la sivyo hili mnalijua sasa mnataka mumfafanulie vizur alipe
 
Msaidieni apate umeme sio mumpe ufafanuzi la sivyo hili mnalijua sasa mnataka mumfafanulie vizur alipe
Kuna mambo mawili ya kuzingatia

1.Je kafikiwa na miundombinu? Kama ndio anapata huduma

2 Je hajafikiwa na miundombinu? Kama ndio anapaswa kusubiri tuendelee kuisogeza
 
Mimi pia naona hawataki. Ila kwanini wakatae ikiwa ni jukumu lao na Mimi ni haki yangu kupewa huduma hiyo.
Halafu ikitokea ukalipia baadaye watawasambazia watu umeme kwa kutumia transformer uliyolipia bila kurudishiwa chochote, kuna maeneno mtu anaambiwa anunue nguzo akitaka umeme, we umenunua nguzo baadaye wanatumie nguzo hiyo kuvuta umeme kwa wengine wakati we uliyelipia nguzo hupewi chochote, utaratibu wa hovyo sana.
 
Halafu ikitokea ukalipia baadaye watawasambazia watu umeme kwa kutumia transformer uliyolipia bila kurudishiwa chochote ,kuna maeneno mtu anaambiwa anunue nguzo akitaka umeme ,we umenunua nguzo baadaye wanatumie nguzo hiyo kuvuta umeme kwa wengine wakati we uliyelipia nguzo hupewi chochote ,utaratibu wa hovyo sana
Taarifa

Mteja hapaswi kulipia kifaa chochote kwa ajili ya kuunganishiwa umeme

Nb

Kwa mujibu wa kanuni za umeme mteja anaweza kufata taratibu na kujengewe line au transfoma kwenye eneo lake,
 
Mko smart Sana wakuu,
Mungu awazidishie Moyo huu wa kizalendo.

Hii ndo tanesco mpya sasa tulokua tukiiota miaka na miaka.
Ila bado hawajafikia kiwango cha usmart.Niliwapigia simu tarehe 19 nikaongea na kwa masaa 3.Nikawapa maelekezo wawasiliana na Muhasibu wao wa Mkoa wa Arusha na wakasema hawana mawasiliano yake wala hawana namna ya kuweza kuwasiliana nae bali inabidi nimtafute mwenyewe.
 
Ila bado hawajafikia kiwango cha usmart.Niliwapigia simu tarehe 19 nikaongea na kwa masaa 3.Nikawapa maelekezo wawasiliana na Muhasibu wao wa Mkoa wa Arusha na wakasema hawana mawasiliano yake wala hawana namna ya kuweza kuwasiliana nae bali inabidi nimtafute mwenyewe.
Ulipiga namba gani? Tatizo ni nini? Wilaya na namba ya simu tafadhali
 
mkuu una options 2 tu:

- toa chapaa ununue iyo 'transfoma'

- au usubiri miaka 5(hmm au zaidi) mingine tanesiko waendelee wakufikie na transfoma ya 'bure'
 
Back
Top Bottom